Sunday, May 17, 2009

JE? TUNAZINGATIA HAYA KATIKA MAISHA YETU YA NDOA

PICHA NA MAKALA KUTOKA KWA http://mbilinyi.blogspot.com/


Kumpata mwenza au mke au mume ambaye utaishi naye maisha yako yaliyobaki hapa duniani ni jambo la msingi sana katika maisha ya binadamu.
Na kwa kupenda wenyewe hupelekana hadi kwa viongozi wa dini na kutangaza hadharani kwamba mimi na mwenzangu tunataka kuwa mke na mume na ulimwengu ujue.
Huwa tunakuwa tumejawa na mioyo yenye furaha na kutaka siku ifike upesi ili nianza kuishi na mwenzangu haraka iwezekanavyo.

Mungu bariki mioyo ya maharusi wapya maana hawajui kazi halisi wwanayoenda kuianza kazi halisi maisha ya kweli na kuachana na maisha ya uchumba ambayo mengi ni tambarare kama nyikani.
Baada ya honeymoon tu wengine siku ya pili tu, wengine mwezi wa kwanza tu na wengine mwaka wa kwanza tu wa ndoa huanza kujiuliza hili swali;
Lakini hakuna aliyeniambia itakuwa kama hivi?

Alikuwa anaacha mialiko ya watu kwa ajili yako lakini baada ya kukuoa si hivyo tena, unadhani kwa kuwa alikuwa ana cancel futa mialiko ya kwenda kufanya mambo yake kwa ajili yako kabla hamjaona na mkioana itakuwa sawa?
You are wrong! Unakosea

Ili usipoteze matarajio ya mahusiano yako ya ndoa jaribu kuzingatia mambo yafuatayo (kama unategemea kuoa au kuolewa please print na kafiche haya unaenda kuyasoma na baada ya kuanza ndoa soma tena na pia ukiyaweka moyoni na ukizingatia utakuwa candidate mzuri sana)

Hakuna binadamu anaweza kutimiza mahitaji yako yote:
Mtu ambaye anaweza kutimiza mahitaji yako yote ni BWANA, na ilimpasa kufa ili aweze kukutimizia yote.
Usitegemee ndoa au uliyeoana naye atakutimizia mahitaji yako yote au ahadi zake zote alizoahidi kabla hamjaoana.

Kiwango cha mapenzi hakiwezi kuwa juu kama ilivyo mwanzo wa ndoa.
Jinsi anavyokwambia "nakupenda” huweza kupungua hadi ukashangaa kadri ziku zinaenda ingawa neno ”nakupenda” huleta raha sana kwa mwanamke akisikia kutoka kwa mumewe hata hivyo siku zinavyoenda mwanaume hujisahau na kuanza kula jiwe kusema “nakupenda”
je, utadai?
Pia wanawake nao (wachache sana) akishazaa huanza kujisahau na kujiona mama na si mrembo bado. Huku ni kukosa ustaarabu na kinyume cha maadali.
shame on you! Muona aibu!

Mwanaume anaweza kuwa anakupenda mno lakini bado hatajua unahitaji kitu gani.
Wanawake wengi huja na sentensi ‘ Kama ananipenda angefanya kile napenda afanye” kumbuka usiposema na kumwambia ujue hawezi kujua unataka kitu gani au nini kinakusumbua.
Kama huulizi basi jibu litakua HAPANA
Men read newspapers not minds! Wanaume wanasoma magazeti sio mawazo

Si mara zote uliyeoana naye atapenda kuimarisha mahusiano.
Katika mazingira ya kawaida wanawake hupenda hata kuimarisha kitu kizuri (mfano ndoa ambayo hata haina mgogoro) hata hivyo wanaume wana msemo wao
“ kama haijakatika , isitengenezwe”
Hivyo tumia hekima na kuomba Mungu ili Mungu awape moyo wa umoja na juhudi ya kuishi kwa amani.

Ndoa haiwezi kukufanya uwe umekamilika.
Si mara zote ukiongeza nusu na nusu unapata kitu kizima.
Wengi ambao ni “hawajaoa” hudhani wakioa au kuolewa watakamilika na kujiona kamili na kuwa na furaha ya kweli.
Na wengine hufika mbali zaidi kwa kujinyima vacation, kununua vitu vizuri wakisubiri kufanya hivyo wakioa au kuolewa.
Unapoteza muda wako anza kukamilika kwanza kabla ya kuolewa au kuoa na ingia ukiwa si tegemezi kwamba mwenzako atakukamilisha hadi kukupa furaha.
Ndoa ni kuunganisha uwezo na ku-balance udhaifu siyo kukaa tu kutegemea mwenzako akukamilishie furaha yako.

Usitegemee kufanya kila kitu pamoja
Kufanya kazi pamoja, kupanga mipango pamoja, kuweka malengo pamoja ni suala zuri sana hata hivyo kila mmoja huhitaji kupumzika/pumua.
Usitegemee kila kile unapenda basi na mwenzio atakuwa excited nacho si kweli hivyo kuna wakati utahitaji kuwa mwenye na yeye kuwa mwenyewe.
Nakwambia mapema ili siku ikifika usiseme hakuna aliyeniambia, mimi nimekwambia!

Mtu ambaye anaweza kumbadilisha ni yeye mwenyewe si wewe.
Kama unategemea ukioa au kuolewa utambadilisha mpenzi wako basi utakuwa very much disappointed. Umesikitishwa sana
Kama kuna vitu vinasumbua kwa mpenzi wako kabla humjaona viangalia vizuri, kutegemea kwamba utamsaidia kubadilika baada ya honeymoon ni kujidanganya kulikokithiri.
Ndoa si mahali pa kulaumiana, kukefyakefya (nagging), hasira na kukosoana.
Kama mpenzi wako hajui UCHAFU ni kitu gani hakikisha anafahamu kabla hamjaoana, na kama unategemea utambadilisha aache ulevi, kuvuta sigara, kuwa mwongo nk shauri yako!

Maswali ya kujadili
Wewe ambaye upo kwenye ndoa sasa je, unaona maratajio yako yote ya ndoa yalitimia?
Je, una matarajio yoyote ambayo unahisi yalikusumbua zaidi?
Je, una ushauri gani kwa wanandoa wapya?

4 comments:

Fita Lutonja said...

Hakika nimefurahi sana dada yangu kwa somo kama hilo la ndoa. Hili ni somo makini sana kwakweli wanandoa wanatakiwa kuzingatia mambo kama hayo na ndoa yao itadumu milele na milele hakika penzi hudumishwa kwa upendo na amani.

Yasinta Ngonyani said...

Ni kweli ukizingatia haya mambo ndoa itadumu milele.

Anonymous said...

nitatoa mawazo siku nyingine. Nina swali moja, haya mawazo ni yako binafsi au umesoma mahali?

NURU THE LIGHT said...

YASINTA..jag är inte gift ännu so jag tackar so mycket för dessa råd för jag e säket att de kommer att vara ett stort verktyg för både mig och min man..inshallah