Wednesday, May 27, 2009

MLIMA WETU KILIMANJARO+JIOGRAFIA


Mlima Kilimanjaro ni mrefu kuliko yote Afrika mita 5895. Ni mlima wa asili ya volkeno. Kilele chake kimefunikwa na theluji.

12 comments:

chib said...

Wakenya zamani walipokuwa wanajitangaza kimataifa katika sekta ya utalii walikuwa wanadai upo kwao, watanzania tulikuwa tumelala usingizi. Sasa tumezinduka, lakini wakenya walishafaidi sana.

Naona umeamua kuutangaza kabisa, tunashukuru

Yasinta Ngonyani said...

Wakenya wao wachokozi kila kitu wanasema cha kwao na pia hata kiSwahili wanasema cha kwao. Na sasa wanasema waTanzania hatujui kiingereza. Naona hao wana kisa nasi. Ila huu mlima ni wetu kabisa wala wasilete maneno kama walifaidi basi. Lakini sasa tumeamka!!!

Mzee wa Changamoto said...

Hapa ingependeza kama tugesema kuwa kilele chake kilifunikwa na theluji maana sasa hivi theluji iliypo hata lori dogo la Mitsubishi Canter halijai.
Inasikitisha

www.tanzaniasports.com said...

Mpaka leo wakenya wanautumia Mlima wetu katika vivutio vya Nchi yao...Ni muhimu viongozi wetu wakawa wabunifu.

Ivo Serenthà said...

When I was a child, a giraffe at the zoo in my city, I was spit in the face, he had not liked the leaf that was offered, I cried desperately, but was a response dictated by the non-approval.

A hug, Yasinta

Marlow

Bennet said...

Sio mlima tu hata Serengeti pia wanaitangaza yao kwa kutumia masai mara.
Viongozi wetu wamelala sana ndio maana hata wakati wa mkutano wa Sulivan walitumia maji ya DASANI badala ya maji KILIMANJARO ambayo yangesaidia kuutangaza mlima wetu

Anonymous said...

Wakenya!!! wefi wa kila kitu, wanaongoza kwa ku export tanzanite wakati wao hawana

PASSION4FASHION.TZ said...

Wakenya wana umimi sana,mimi wala siwashangai hata kidogo ndio maana bado wana ukabila sana,yote hiyo ni sababu ya umimi.

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

kwani ukiwa nchini kenye huuni mlima huu?

Anonymous said...

Do you know that Tanzania the Warm Heart of Africa?.

Yasinta Ngonyani said...

Naona hapa wote mnasema ni kosa la viongozi wetu kuwa Wakenya wamefaidika na wanafaidika. Basi ngoja awamu ijayo niende kufanya kampeni niwe mtu fulani na nibadilishe kila kitu. Maana sasa ni wakati wa kuamka.
Asante wote kwa maoni yenu na naona wote mna uchungu na nchi yetu.

Kamala nadhani ukiwa Kenya unauona mlima huo.

Israel Saria said...

Sawa Bi Maisha, endapo utafanikiwa kupata nafasi katika awamu ijayo, basi tukumbukane katika ufalme wako. Hata ukinipa nafasi ya kuwa Mlinzi wako tu....