Tuesday, May 20, 2014

KUMBUKUMBU YA MAREHEMU BIBI YETU VALERIANA NGONYANI!!!

ILIKUWA MARA YANGU YA MWISHO

KUONANA NA BIBI 2005 MWEZI WA NNE
Leo ni tarehe 20/5 ni miaka tisa imepita tangu bibi yetu mpendwa Valeriana Ngonyani atutoke.  Kwangu ni kama vile jana tu. Alifariki 20/5/2005 katika hospitali ya Liuli. Sisi wajukuu wako wote, watoto wako ndugu na marafiki wote wanakukumbuka daima. Bibi Valeriana ni huyo aliyejifunika kitenge, katikati nadhani mnajua au basi ni mimi na mwishoni ni mama yangu mdogo, mdogo wake mama. TUTAKUKUMBUKA DAIMA KWA NJIA YA SALA ZETU. USTAREHE KWA AMANI AMINA.

6 comments:

Interestedtips said...

pumzika kwa amani bibi yetu

Nicky Mwangoka said...

Tunamwomba Mungu amweke pema mbinguni Bibi yetu. Amen.
Pole Dada kwa kumbukumbu ya Bibi najua yarudisha machungu ya kupotelewa na kipenzi chetu.

Yasinta Ngonyani said...

Mama Alvin na kaka Nicky Ahsante sana kwa kuungana nami katika siku hii ya kumbukumbu ya wajina wangu mpendwa.

sam mbogo said...

pole sana,nijambo la kumshuru mungu.kaka s

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Sam! Ahsante kwa kuwa nasi katika siku hii ya kumbukumbu!!

obat vimax said...

vimax thanks gan infonya vimax asli di tunggu info selanjutnya gan obat klg