Tuesday, December 31, 2013

SALAMU ZA MWAKA MPYA KUTOKA KWA MAMA MAISHA NA MAFANIKIO NA FAMILIA YAKE !!!

Marafiki,ndugu, na wasomaji  wapendwa!
Ukaribisheni mwaka mpya uwe wa Mafanikio, Amani, Mwanga na Furaha katika maisha yetu.
Nakutakieni wote, wewe na familia yako kila jema na furaha tele katika mwaka mpya 2014.
KHERI KWA MWAKA MPYA 2014. KUMBUKENI WOTE MNAPENDWA!!!!
Nimeona si mbaya kama tukiuvuka mwaka huu kwa kipande hiki cha mziki si mnajua mziki na kazi au mziki,sherehe aaahh ngoja tuserebuke!!.....
TUMWOMBE MUNGU TUONANE NA KUSEMA TENA MWAKA 2014..NA UWE MWAKA WA MATUMAINI----NANGONYANI/KAPULYA

4 comments:

Anonymous said...

Tunakutakia Heri ya maisha na mafanikio 2014. By Salumu!

Salehe Msanda said...

Habari!
Nawe pia tukitakie mwaka mpya mwema.
Tukumbuke kuwa hicho kinachoitwa mwaka mpya ni zaidi ya kile tunachosherehekea.
Kikubwa na kwa kila mmoja wetu kujitathimini na kufanya mabadiliko katika Nyanja zote za maisha yetu na hapo ndipo tutakua tunaendana na hicho kinachoitwa mwaka mpya. Mabadiliko yawe chanya na yenye kutuwezesha kuona uwepo wetu hapa duniani unafaida kwetu na kwa wanaotuzunguka.
Swali la kujiuliza ni hili kwa kuingia mwaka mpya je unaandaa mark gani utakayoicha baada ya kuondoka kwako hapo duniani?
Kila la kheri.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Salum! Ahsante sana..nawe pia iwe hivyo.

Kaka Salehe!Ahsante sana ...Nimelipenda swali lako...

myslot said...

หนังออนไลน์ UglyDolls ผจญแดนตุ๊กตามหัศจรรย์ (2019) ที่นี่ดูฟรีนะครับ ดูหนังออนไลน์ฟรีครับ สนุกแน่นอน

https://www.doonung1234.com/