Thursday, August 1, 2013

UTAMU WA KULIMA BUSTANI NI SASA: VIAZI VYA KULIMA KWA MIKONO YANGU MWENYEWE LEO TWALA....MLO WA JANA JIONI

 Hivi ni vile viazi angalia hapa na jana jioni ndiyo ikafikia muda wa kuangalia kama vyaweza kuliwa na matokeo yako yakawa kweli vyaweza kwa hiyo jana jioni tumekula viazi vya kulima Nangonyani.......kama
....uonavyo kwenye sahani hapa ni viazi , broccoli, nyanya kidogo, limao na samaki aina ya salmon(kiswahili ) nisaidieni ......kilikuwa kitamu mno....nawashauri wote mlio  na nafasi ya kulima bustani kulima viazi mviringo....NAWATAKIENI ALHAMIS NJEMA NA MWANZO MWEMA WA MWEZI AGOSTI:-)

5 comments:

Anonymous said...

Da Yasinta! yaani mwezi umoja tuu toka ulime hizo viazi na ndio imezaa kwa wingi. kweli weye mtoto ya mkulima. By Salumu.

ray njau said...

Mkulima na jembe lake na mazao yake na mlo wake.

Rachel Siwa said...

Duuhh Hongera sana sana KADALA wa mimi..

Anonymous said...

yani mlo unaonekana ulikuwa mtamu hatari.... mimi mginjwa sana wa mbogamboga, hapa nishatokwa na udenda hatari. nachungliaga bustani ya dada Yasinta...nikiangalia majani ya maboga nawaza mlenda (bamia, majani ya maboga yamechanganywa pamoja yakawekwa magadi, kijaniiiiiiiii..tupia na nyanya chungu kidogo...then upate kitu kama nyama au huyo samaki wako da Yasinta, na ugali...acha kabisa...hongera.

Anonymous said...

Mlo ulikuwa kabambe sana, hongera kwa kula viazi ulivyolima mwenyewe. Nimekula kwa macho dada. Siku nyingine nishtue mapema ili nishiriki mlo pamoja nawe.