Saturday, August 17, 2013

KUMBUKUMBU YA MAMA ALANA NGONYANI!

MAREHEMU MAMA ALANA NGONYANI 1952-2004
Imetimia miaka 9 tangu ututoke ghafla usiku wa tarehe 17 Agosti 2004 wakati bado  tulikuwa tunakuhitaji. Ingawaje kimwili umetutoka, kiroho bado tunakukumbuka. Tunakukumbuka siku zote kwa upendo wako, mawazo yako yaliyojaa busara , ukarimu/ucheshi na malezi bora. Tulikupenda lakini Mungu alikupenda zaidi.
Tunamwomba Mwenyezi Mungu aiweke roho yako mahali pema peponi. AMINA
Na tumkumbuke mama yetu kwa wimbo huu

+TUTAKUKUMBUKA MILELE MAMA YETU MPENDWA ALANA NGONYANI+


5 comments:

ray njau said...

Poleni kwa ndugu,jamaa na marafiki.

Anonymous said...

Mungu azidi kukupa amani na faraja wakati huu unapomkumbuka mama yako mzazi.

Rachel Siwa said...

Ulale kwa Amani mama Ngonyani,,Poleni sana familia ya Ngonyani.

Interestedtips said...

Poleni sana dada, Ulale kwa amani Mama

Yasinta Ngonyani said...

Ahsanteni wote kwa kuwa nasi katika kumkumbuka nama yetu mpwbswa Alana.