Tuesday, August 6, 2013

UJUMBE WA LEO JUMANNE NI KAMA UFUATAVYO!

Wakati mwingine ni bora kuwa mpweke ili kukwepa kuumizwa!!! Nawatakieni wote jioni/mchana au asubuhi na pengine usiku njema/mwema. Pia IDD NJEMA. KAPULYA

4 comments:

Anonymous said...

Kuwa mpweke mara moja-moja si mbaya, kwa sababu unapata fursa ya kuchambua matatizo yako bila bughdha. Idd njema Kapulya na wadau wote.Tunasubiri pilao ya mbuzi. By Salumu.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Salumu! Ulichosema ni kweli huwa napenda kuwa peke yangu na dawa nzuri pia ni kuwa kwenye sehemu ya ukimya. Ila kama ikija ya kuumizana na wenza wetu hakika inauma hasa kama umeachwa au rafiki wa karibu sabna .

Unknown said...

Kweli kbs Da yasinta bora kuwa peke yako unajiepusha na mengi. Idd njema na kwako pia karibu

Mija Shija Sayi said...

Big Nooooo!!
Duniani huwezi kukwepa kuumizwa / kuumiza! Mimi naamini kabisa kwamba ni kwa kupitia kuumizwa ndio tunaimarika..
Sipendi kuumizwa lakini siogopi kuumizwa....na maumivu yaje tu tutapambana. Ila upweke haufai, binadamu tumeumbwa kutegemeana..
Ni hayo tu Head Girl..!!