Sunday, February 13, 2011

Jumapili ya leo, Mke: Furaha ya mume wake!!! na ni jumapili ya saba ya mwaka!!


Mwanamke ni furaha ya nyumba!!

Kitabu cha Mithali kinaeleza jinsi mwanamke mkamilifu alivyo, mwanamke aliye furaha na fahari ya mume wake. Mwanamke huyu anafanya kazi zake kwa bidii, ana hekima ni mwaminifu na hutunza kwa uangalifu watu na vitu vya nyumbani. (Mit. 31:10-31)

Kitabu kingine, Hakima ya Yoshua bin Sira, kinamsifu mume mwenye mke wa namna hiyo:-

Apataye mke hujipatia mali iliyo bora, msaidia wa kufaa, na nguzo ya kumtemeza. (Y. b. s. 36: 24).

Yu heri mume aliye na mke mwema kweli,

Mwanamke mwema ni furaha ya mume wake,

Ataishi miaka ya maisha yake katika amani.
Mwanamke mwema ni tunu bora,
Mcha Mungu atatunukiwa huyo watajaa furaraha moyoni hata kama ni maskini au tajiri,
Watakuwa na nyuso zilizochangamka wakati wowote. (Bin Sira 26: 1-4)
Hivi ndivyo mwanamke anavyokusudiwa kuwa kwa mwanaume. Katika maneno yake Mungu kwa nabii Ezekieli, mwanamke huwa; "Furaha ya macho". (Ez. 24-16).

Lakini kwa nabii Hosea, mke huyu aliyekusidiwa kuwa furaha yake, amekuwa chanzo cha mateso ya uchungu wake. (Hos. 2: 4-9) mke huyu hana uaminifu naye huenda kwa wanaume wengine. Amina!!


NAWATAKIENI WOTEEE JUMAPILI HII IWE NJEMA NA PIA BARAKA ZA MUNGU ZITAWALE NYUMBANI MWAKO/MWENU NA POPOTE PALE U/MTAKAPOKUWA.!!!!

8 comments:

EDNA said...

Jumapili njema kwako pia Yasinta.

Goodman Manyanya Phiri said...

Bila wake zetu, sisi hatunathamani yoyote! Tumekwisha!


Asante kwa kutukumbusha wale wa umuhimu maishani mwetu.

MARKUS MPANGALA said...

mmmmmmh jamani mnafanana hadi pua na meno? hata hivyo mke mwema humwumba mume mwema. hongera binti nakutakia upate libambu la bwina

Baraka Chibiriti said...

Asante sana, nawe pia dada Yasinta. J2 njema sana.

Ila ni Jumapili ya sita si ya saba.

Anonymous said...

Asante kwa ujumbe mzuri dada yngu

Simon Kitururu said...

Mmmmh!

Penina Simon said...

kama aonekanavyo ndivyo alivyo aliempata kabarikiwa hakika, ila wengine huwa hivyo hivyo hata ukifika nyumbani mwao unafarijika kumbe huku nyuma moto unawaka

Yasinta Ngonyani said...

Duh! mwenzenu jumapili yangu ilikuwa taiti kidogo. Ila bado nipo na nawashukuruni wote kwa michango yenu mizuri. Mungu awalinde waote ili tuzidi kuwa pamoja. UPENDO DAIMA.