Monday, February 7, 2011

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAPATA MKURUGENZI MPYA WA IDARA YA UTALII


Na Tulizo Kilaga wa Wizara ya Maliasili na Utalii
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii amemteua Bw. Ibarahim Mussa kuwa
kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Utalii kuanzia tarehe 01 February 2011.

Uteuzi huo ameufanya kwa mujibu wa kifungu cha 6 (1) (b) cha Sheria ya
Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002.

Ibrahim A. Mussa (53) ni mtumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii tangu
mwaka 1982 hadi sasa ambapo alifanya kazi katika ngazi mbalimbali, katika
Idara ya Misitu na Idara ya Utalii.

Kabla ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Utalii, Ibrahim A. Mussa alikuwa
Mkurugenzi Msaidizi anaesimamia Utafiti, Takwimu na Mafunzo katika Idara
ya Utalii.

Bw. Mussa ana Shahada ya Uzamili (International Tourism Management)
aliyoipata mwaka 2005 kutoka chuo cha Sheffield nchini Uingereza

Bw. Mussa anachukua nafasi ya Mkurugenzi wa Idara ya Utalii kutoka kwa Bi.
Maria Mmari ambaye amepangiwa kazi nyingine.