Saturday, June 21, 2008

JUNI 21, 2008 UBAGUZI WA RANGI

Bado sielewi kwa nini binadamu tunabaguana, Kwa nini wazungu wanaona wao ni bara zaidi kuliko watu weusi. Wakati wote tukiumia au kujikata maumivu ni yale yale, pia wote damu inatoka. Wakati mwingine unaweza kufikiri ya kuwa kuna mungu wawili au niseme wao wanafikiri hivyo mungu mzungu na mungu mwafrika. Kwani zamani nilikuwa nasikia tu ya kwamba kuna ubaguzi nilikuwa sielewi, lakini sasa naelewa kwani naona mwenyewe kwa macho yangu. Halafu sasa sio wanwabugua watu weusi tu hapana wote ambao si wazungu kwa mfano waarabu, wahindi, wachina n.k.. Yaani wanaogopa hata kukua jirani wakati mpo kwenye basi anakubali kusimama kuliko kukaa siti moja na mwafrika. Wao wanasema wanaogopa wakikaa siti moja basi wao pia watabadilika na kuwa weusi. Wakati mwingine hata kusalia wanaogopa, yaani kushikana mikono. Nasema tena kwa uchungu mwingi sana inaumiza sana tena sana kuona watu wana roho mbaya kiasi hiki. Kwa hali hiyo mtu kila siku unaishi tu yaani siku ikiisha shukuru mungu. Natamani ile ndoto ya Mrtin Luther King ingekuwa kweli, kwamba siku moja mtoto mzungu na mtoto mwafrika watashikana mikono na watacheza pamoja. Je? wasomaji ni kweli sisi waafrika tupo nyumba sana kwa kila hali(jinsi)? Sababu gani wao wanasema waafrika ni wajinga wanakaa tu wanasubiri kupewa wao ni wajinga HAKUNA MTU ANAWAAMBIA WAAFRIKA WANGU WAJINGA. Kwa kweli naumia sana

Na; Yasinta Ngonyani

Wednesday, June 18, 2008

JUNI 18,2008 mziki wa kale


Hapa jamani mnaona akina mama na akina baba katika mavazi maalum. Hapo zamani haya ndio yalikuwa mavazi ya hapa sweden. Na hapo ndo walikuwa wanapiga huo mziki wa asili kama ville Lizombe, zeze au kama umewahi kumsikia Marehemu ZAWOSE yule mgogo alikuwa akiimba na kupiga malimba nk. hiyo instument inaitwa FIOL.
Na; Yasinta Ngonyani

JUNI 18,2008 MIDSUMMER EVE






















Sasa nadhani mtashangaa na kusema ametuletea nini sasa sawa ngoja niwaambie:- Imekuwa ni mila na desturi hapa Sweden. Yaani wakati huu ni katikati kabisa ya mwaka: Na siku hii hapa watu wanasema hivi uchume maua na uweke chini ya mto kisha ulala na usiku ule utaota nani atakuwa mchumba wako. sasa ngoja nikuambia chakula kinacholiwa siku hii, ni samaki wabichi yaani waiopikwa au kuchomwa. Samaki wabichi ambao wamewekwa kwenye maji na viungo maalum kama mwaka hivi. Bila kusahau viazi mviringo (matosani) vya kushemsha na vyakula vingine vingi. Na halafu siku hii watu wanakunywa sana pombe na hasa pombe kali, na pia nisisahau kunakuwa midsummerdance kama mnavyoona katika picha, wanatengeneza (msalaba) huuu kwa majani na maua kidogo. Maana ya huu msalaba kwa lugha ya hapa unaitwa (STÅNG) nitakuelezeni siku nyingine.Baadaya kupeleleza nimeambiwa sababu kubwa ya kuadhimisha au nisema kukumbuka mila hii ni kuwaomba miungu ili mazao (mavuno ) yapatikane kwa wingi . Lakini cha kushangaza ni kwamba wao(waswidi) hawaamini kuna mungu Je? sasa watapataje mazao mengi kama hawaamini? Wanasema hata kama hawaamini lakini hii siku ni safi kwani wanakula chakula na kingi na kunywa mpaka kulewa. Sijui wasomaji mmeelewa kama hamjaelewa basi nitadadisi na kuwaeleza kwa kirefu zaidi siku nyingine.


Na ; Yasinta Ngonyani

Juni 18, 2008 SHAIRI (KWA NINI?)

Kwa nini vitu kama hivi vinazaliwa,
Yaani ambavyo havihitaji kuishi.

Kwa nini vitu kama hivi vinaota
ambavyo havitakiwi kuvunwa

Kwa nini mimi kila wakati nakuwa nimeshiba
wakati wengine wengi hawana chakula

Kwa nini zinatengenezwa silaha nyingi sana
kwa ajili ya kuua?

Kwa nini hatuwezi kufunzana
vipi kupokea shida za wengine

Kwa nini hatuwezi kujifunza kuwa waangalifu
kwa yetu wetu ulimwengu na yetu paradiso

Kuna maswali mengi,
ambayo hayana majibu, duniani hapa na yenye ahadi za uongo


Na; Yasinta Ngonyani

Monday, June 16, 2008

Juni 15,2008 MAHITAJI/CHAKULA/ USAFIRI

Tumwombe mungu ili hali hii isiendelee; Yaani Bei ya chakula imepanda, bei ya mafuta imepanda pia. Usafiri umekuwa ghali eeh jamani mbano tutakufa sasa kwani hatutaweza kwenda hospitali. Na je? tutalalaje bila mafuta ya taa? Na je tutapikaje bila mkaa angalia pia ada za shule kweli tutaweza kusoma? Kama nakumbuka vizuri watu wa zamani walisema ukiishiwa sana usikose chumvi ndani ya nyumba lakini sasa hiyo chumvi itapatikanaje? Je? hizo bajeti haziwezi kurudiwa kupangwa tena kwani watu tunaumia.


Na; Yasinta Ngonyani

Sunday, June 15, 2008

JUNI 15,2008 AKILI NYINGI HUONDOA MAARIFA

Sijui mngekuwa wenzangu mngesema /fanya nini? Ni hivi kuna rafiki yangu mmoja ameniomba msaada/ ushauri ya kuwa katika familia yake hakuna mawasiliano. Kila mmoja anafanya kama anavyotaka. Na hivi leo ninavyosema ameniambia amepatwa na mshtuko kusikia kanisani wanatangaza tangazo la kwanaza la ndoa kati ya baba yake na mwanamke ambaye hajapokelewa katika familia. Labda, sijasema tangia mwanzo huyu rafiki yangu mama yake mzazi alishafariki na sasa baba yake anataka kufunga ndoa na mwanamke mwingine baada ya miaka mitatu tu na huyu mwanamke hajakubalika na watoto wa huyu baba. Je? ungekuwa /mngekuwa wewe /ninyi u/mngemshaurije ili nimpe jibu huyu rafiki yangu?


Na; Yasinta Ngonyani

Juni 15, 2008 TANGAZO: Vitabu Vinauzwa

Habari za leo ndugu wasomaji, ndio najua mtasema huyu mtu vipi. Sio kitu hapa ni baadhi ya vitabu yaani vya hadithi;-


1. Upeo wa mapenzi kimetungwa na; Nyehana Justin
2. Maisha ni safari ndefu na; J.D Ukason na B.G. Mbele
3. Hasusa ya shetani na; Manfred Chr. Mahundi
4. Mdundiko wa maisha na; Joachim Gatahwa
5. Anasa hunasa na; Deusi .C. Masunzu
6. Nakulaumu wewe na Frederick Mbabagu Titi
7. Lazima unioe na; H. Kusare Mboya
8. Nambie Nikuambie na; S.A. Mpinga
9. Salome maskini na; Bernard Mapalala
10. Talaka siku ya ndoa na; S. F. Shija
11. Hadith za wangoni cha kwanza mpaka cha nne na: Angela Amandus Haule
12. Nimekugundua! na; Anania Mbawala
13. Tamaa mbaya na; Kayafa H. Mwangoka
14. Penzi Chungu na; C. Abdul Ntandu
15. Kwa nini iwe jumapili na; Marco Malilo Kaluma
16. Kizazi gani hiki na; Patrick M. Kija
17. Wimbi la aibu na; Amina S. Mlele
18. Simba wa Tunduru na; B.Z. Mkirya

Na vingine vingi vingi ambavyo havipi kwenye orodha haya sasa wahi usichelewa kwani nadhani kuna wengi ambao wana hamu sana yakusoma. Kwa hiyo chukua nafasi kabla sijabadili mawazo. Bei ya kitabu kimoja ni euro 9,99. Kazi kwako sasa.


Na ; Yasinta Ngonyani

Saturday, June 14, 2008

Juni14,2008 Gari


Ya nini kupoteza pesa kuwanunulia watoto vifaa vya kuchezea wakati inawezekana kutengeneza. Yaani hapo vitu vinavyohitajika ni dungu baada ya mafuta ya kula kwisha, mwanzi, ndala zilizochoka kwa ajili ya matairi bila kusahau ufundi. Haya basi kimbia gari halingoji mtu.............tena bei nafuu kabisa.
Na; Yasinta Ngonyani

Friday, June 13, 2008

jun i 13 2008 Picha


Juni 13,2008 LIKIZO

Leo ni siku ile ambayo shule zote ulimwenguni zimefungwa. Ila sasa sikiliza, wanafunzi hapa wao wanalikizo ndefu sana wiki kumi. Yaani mpaka mwezi wa nane tarehe 19. Sababu kubwa ni kwamba hakuna kipindi kingine watu wanaweza kufurahia joto, kuonana, kula na kunywa na marafiki. Ooh nilitaka kusahau kitu muhimu sana kuogelea kwani si mnajua tena, baridi yaani kuanzia mwezi wa tisa mpka wa nne(tano) ni baridi tu nadhani nimeandika kuhusu Hali ya hewa kwa hiyo rudi nyuma na usome tena kama umesahau. Yaani hapa watu wanaona jua (joto) miezi mitano(sita) kama hivi. Sasa labda watu wataonekana nje, kwani hatuonani kabisa wakati wa baridi kila mtu ndani tu. Maisha ya Ughaibuni ndugu zanguni mmmmmmh ..........tuache hivyo hivyo kwani waswahili wanasema ukikuta wanyeji wanatembea uchi basi nawe tembea.

Na; Yasinta Ngonyani

Friday, June 6, 2008

Wimbo wa Taifa

Bila kusahau kumshukuru mungu

Mu ngu ibariki Tanzania,
Dumisha Uhuru na Umoja,
Wake kwa waume ume na watoto,
Mungu ibariki,
Tanzania na watu wake,
Ibariki Tanzania,
Ibariki Tanzania,
Tubariki Watoto wa Tanzania.

najua mtasema nimechanganyikiwa kwani kila mtu TZ anaweza kuimba wimbo wa taifa sawa lakini mimi leo nimekumbuka sana Tanzania yengu. Naipenda sana nchi yangu Tanzania.



Na; Yasinta Ngonyani

Nembo ya Taifa


1. Mwenge huwapa tumaini waliokufa moyo, heshima kwa wale wanaonyanyaswa na amani pale palipo na chuki.
2. Bendera ni alama ya Tanzania huru,
3. Silaha,; mkuki, mshale na shoka ni silaha za kilinda na kujenga Taifa.
4. Mlima Kilimanjaro ambao ni mrefu kuliko yote katika Afrika upo Tanzania
5. Mazao ya pamba na kahawa kuonysha utajiri wa kilimo kama uti wa mgongo wa uchumi
6. Pembe huonyesha utajiri wa wanyama wa asili katika Tanzania.
7. Mume na mke huonysha usawa, ushirikiano na umoja wa watu katika kujenga Taifa
8. Na mwisho ni Uhuru na Umoja ndiyo wito maalum wa Taifa.
Na; Yasinta Ngonyani

CCM

hapa ni bendera ya CCM








Na; Yasinta Ngonyani

Juni 6, 2008 Nchi Yetu Tanzania




Jamani nyumbani ni nyumani leo nimekumbuka kweli nyumbani yaani Tanzania. kama mlikuwa mmesahau maana ya rangi basi nawakumbusha:
1. Nyeusi - huonysha watu na Jamhuri ya Tanzania.
2. Kijani - huonyesha mimea na ardhi ya Tanzania
3. Njano - huonysha utajiri wa mali na asili
4. Bluu - huonyesha bahari inayoziunganisha sehemu za Jamhuri ya Muungano
Na; Yasinta Ngonyani














Juni 6, 2008 Afrika inahamaia Ughabuni

Sasa hali ya hewa hapa Sweden kama nyumbani Afrika. Kusema kweli sijui wapi ni nyumbani kwangu nikiwa hapa nasema nakwenda nyumbani na nikiwa TZ (Ruhuwiko) nasema nakwenda nyumbani yaani hapa sweden. Ebu nisiwachoshe na hayo ya kutojua wapi ni nyumbani kwangu. niwasimulie ambacho nataka kuandika, ni kwamba leo nimefurahi sana, kwanza kabisa ni kwamba nimekula samaki najua mtashanga ni nini cha ajabu kula samaki hapana sio hivyo ni samaki wa kutoka ziwa nyasa amesafiri mpaka huku. Pia furaha imeongezeka kwani nimenunua majani ya viazi yaani matembele(kilugha nabwaka) Najua wengu wanaona nimepungukiwa hapana nina zangu timamu kabisa. Ni hivi mwanzoni nilipata sana shida yaani nilikuwa natamani sana vyakula vya nyumbani TZ hasa samaki na ugali. Lakini sasa naweza kununua hadi majani ya viazi, karanga, mihogo, ila bado sijaona njugu au mboga ya mabogo(kilugha likolo la nanyungu) na kisamvu hivi navitamani sana. Kwa hiyi ninaweza kupata karibu kila aina ya chakula. Lakini hata hivyo havinogi kama vya nyumbani(TZ) kwa sababu ni safiri ndefu mno mpaka kufika huku pia kama samaki sio moja kwa moja toka ziwani. ukitaka kujua ukweli nenda hapo lundunysa.blogspot.com atakuambia utamu wa vyakula hivi.

Na; Yasinta Ngonyani

Juni, 6, 2008

Kama ulikukuwa hujui basi leo utajua. Ni kwamba hapa sweden leo ni sikukuu ya Taifa. Watu wengi wanapumzika tu leo na pia bendera zinapepea. Kwa bahati imeangukia siku nzuri yaani hakuna baridi jua linawaka sana kwa hiyo watu ambao wana mapumziko wamejianika kama mihogo tayari kwa kuota jua ili wapate rangi.

Na; Yasinta Ngonyani

Friday, May 30, 2008

Mei 30, 2008 Haraka Haraka Haina Baraka (Stress)

Kwa muda mrefu nimekuwa ninajiuliza kwa nini watu Ughaibuni wanakuwa na haraka. Maana utakuta mtu ana kitabu napia kalamu, humu ndani ya kitabu ameandika kila kitu nani atakutana naye leo au atafanya nini siku hii, yaani kuanzia asubuhi mpaka jioni. Nimejaribu kuwauliza kwa nini wanafanya hivi? wengine wanasema bila kufanya hivi basi hawawezi kuishi. Pia nimejaribu kuwaambia nitakako mie hakuna mambo haya yaani kwa mfano, naenda kumsalimia mtu/jamaa au rafiki ni kwenda tu na pia wakati huu nakwenda naweza nikakutana na rafiki /mtu mwingine na hapo gumzo litaanza. Lakini hapa haiwezekani kwani safari imepangwa kwenda kwa (Anna). basi ni kwa "Anna". Kwa hiyo sasa utakuta hata watoto wadogo wanasema hawana hali nzuri kwa vile wana mambo mengi. Mambo mengi kiasi kwamba wengine wanashindwa kuendelea na masomo vizuri. Kwa ajili ya (Stress) KILA KITU NI MUDA HATA KULA CHAKULA. Pia hata kutembea. Ammmh kwa kweli naipenda Afrika yangu hakuna haraka afrika au mie mwongo semeni mwenyewe basi kama kweli au vipi.

Na ; Yasinta Ngonyani

Sunday, May 18, 2008

Mei 18, 2008 Litumbandyosi

Haya sasa wasomaji leo nimekumbuka Geografia kidogo.

Litumbandyosi ni kijiji ambacho kipo katika kata ya Litumbandyosi. Tarafa ya Namswea. Wilaya ya Mbinga na mkoa wa Ruvuma. Kijiji hiki kipo kusini magharibi mwa Tanzania. Mashariki kinapakana na kijiji cha Mgazini ,Magharibi kinapakana na kijiji cha Rwanda, Kaskazini kimepakana na kijiji kiitwacho Kingoli na kusini kimepakana na kijiji cha Luhagala. Litumbandyosi ni maarufu kwa kilimo cha mpunga, karanga na mihogo. Kijiji cha Litumbandyosi kina jumla ya watu 7,318 na idadi ya kaya ni 1,449 na kila kaya kwa wastani wanaishi watu watano.
Kijiji hiki ndipo alipozaliwa baba yangu.

Na; Yasinta Ngonyani

Saturday, May 17, 2008

Mei 17,2008 GETO ZA AFRIKA KUSINI ZINAUNGUA

Gazeti la mwananchi hapa sweden limeandika hivi:.
Johannesburg: Siku chache zilizopita mageto mengi ya huko Johannesburg yameongua moto kwa fujo kali, kwa sababu ya kufukuza wakimbizi, hasa wakimbizi wa kutoka Zimbabwe. Ma mia ya mapolisi wameitwa huko getoni Alexandra, ili kujaribu kuwatuliza watu ambao wanatoka nyumba hadi nyumba. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kuwasaka wakimbizi. Majambazi wanapowakuta waamiaji hao wanawaibia mali zao, wanaunguza nyumba zao na kuwapiga wananchi. Kesi nyingi za vifo na ubakaji (mzito) mbaya umeripotiwa lakini hata hivyo haijulikani wangapi wamekufa.
Wanazimbabwe mamia kwa mamia wamekimbia na kutafuta njia ya kwenda katika vituo vya polisi ili kuepuka uwingi wa watu.

Na; Yasinta Ngonyani

Friday, May 16, 2008

Mei, 16,2008 BABA

Naona hapo http://www.lundnyasa.blogspot.com/ ananilaumu kwa nini sijampa baba sifa. Hapana kwani bila baba basi basi tusingezaliwa. Kwani lazima tukumbuke Mungu alimuumba Eva lakini baadaye aliona si haki Eva awe peke yake alimletea mume Adam. Nadhani wote mmenielewa. Kwa maana hiyo baba naye ana sifa zake, ambazo hazifanani na mama kwani, Kama mmewahi kumsikiliza Dr Remmy Ongala anavyoimba kwa kweli unaweza kulia. (baba amepata mke mwingine na wangoni kwa ugimbi). Hii ndio sababu niliandika kwanza mama na ukizingatia kwa sasa mama yangu mpendwa hayupo nami. Pia mama ana majukumu makubwa zaidi yaani ana kazi ya kuzaa, kulea, na kazi za aina mbalimbali za nyumbani. Inawezekana labda nilikuwa namtamani mama. Kwa hiyo msidhani ya kwamba simthamini/ sina upendo na baba HAPANA. Si unajua father and dotter. natumai nimewapa wasomaji jibu la kuwapendeza.

Na; Yasinta Ngonyani

Monday, May 12, 2008

Mei, 12, 2008 Dini/wakoloni

Hii habari nimetaka muda mrefu kuieleza lakini nilikuwa nashindwa vipi nitawaeleza watu sasa nimepata njia ya kuelezea kwa kifupi. Ni hivi;. Hapo kale Waafrika tulikuwa na nchi pia dini zetu yaani tulikuwa tunajitawala pia tulikuwa na dini zetu. Lakini baadaye wazungu wakaja na kutawala afrika, kwa unyonge wetu tukakubali kutawaliwa. Pia walipokuja wakaja na dini zao. Wakatuambia tuache dini zetu za kuamini mizimu na wakaanza kujenga makanisa na kuanza kuhubiri. Hapo ilikuwa mwaka 1898-1998 kama umesoma (UJIO WA WAMISIONARI WABENEDIKTINI TANZANIA - UNGONI) Na sisi kwa unyonge na upole wetu tukawaamini. Nadhani tangu hapo akili zetu zinaamini wazungu wanaweza kufanya kila kitu tunawaheshimu wao kama mungu. Jambo ambalo si kweli. Ninachotaka kusema ni kwamba wazungu /wamisionari walipoingia afrika waliingia kwa kasi na kuanza aina ya vita yaani kuonyesha wao ndio wenye nchi. Pia wao waliona ni jukumu lao kutusaidia waafrika. Hii ndio sababu mpaka leo tuna kaa tu na kusubiri kupewa ( asante baba) yaani kupata miasaada. Bado inanitatanisha sana, Kwani waafrika bado tunaamini yote tuliyofunzwa na wazungu. Hususani dini, wakati wao wenyewe wameacha kabisa kuamini kuwa kuna MUNGU wanaamini miungu wengine kama miti n.k. Je? kwa nini wao walitukataza sisi tusiamini miungu/mizimu wetu?

Na; Yasinta Ngonyani

Sunday, May 11, 2008

Mei 11, 2008 Hali ya hewa inaendelea..........

Kama ulisoma blogg ya hali ya hewa ya kwamba kulikuwa na baridi kiasi kwamba mtu hukuweza kutoka nje. Sasa ni kinyume kabisa watu wamefufuka. Kiasi kwamba unashikwa na butwaa kuona watu jinsi wanavyojianika kama mihogo. Kwa kweli mila na desturi ni kitu muhimu sana. Siku ya kwanza nilishikwa na butwaa kuona baba, mama, mtoto, mamamkwe, babamkwe wote wamejianika kama mihogo au mamba. utakuta wtu wanatembea na hizi nguo za kuogelea siku nzima. Kisa wanataka kupata rangi yaani sisi binadamu hakuna anayeridhika na kile mungu alichompa. Mwafrika anataka kuwa mzungu na mzungu anataka kuwa mwafrika.

Na; Yasinta Ngonyani

Saturday, May 10, 2008

Mei 10, 2008 kazi bila mshahara

Hakuna mtu apendaye kufanya kazi bila kulipwa,kama si utumwa. Kwani nimesoma na pia nimesikia hapa na pale ya kuwa kwa sasa kuna utata wa walimu Afrika(tanzania) kuna shule moja ipo hapo Songea inaitwa Taifa foundation sec. school. wao hawana walimu. Inawezekana wakawa siku nzima bila kupata hata kipindi kimoja. Walimu wamekula mgomo hawapati mshahara. Ni vizuri kwa wao na ni hasara kwa wanafunzi. Kwani ukizingatia kuna wanafunzi ambao wanahitimu yaani kidato cha nne . Inaonekana watu wanadharau sana kazi ya ualimu na wanasahau ya kwamba hatuwezi kupata elimu bila ya walimu na walimu hawawezi kufanya kazi bila kupata ridhiki yao. Cha kushangaza zaidi ni kwamba wanafunzi wakifanya maandamano/kulalamika, hakuna anayewasikiliza isipokuwa wanapigwa marungu na wengine hata kuwekwa ndani je? Wanafunzi hao hawana haki? Na ukizingatia hiyo elimu si bule, kwa hiyo sio walimu tu ambao inabidi walipwe. Kwani hata wazazi wanaumia wanatoa ada ili watoto wao wapete elimu. Kama itaendelea hivi basi hakutakuwa na taifa la kesho. Je? wasomaji mnasemaje labda inawezekana Waziri wa Elimu halifahamu suala hili au vipi. wani inabidi lichukuliwa majukumu haraka sana tunapoteza maraisi, mawaziri na maprofesa wa baadaye.

Na; Yasinta Ngonyani

Tuesday, May 6, 2008

Mei 6, 2008 Furaha ni kitu adimu

Mara nyingi napatwa na hasira sana na pia uchungu.Yaani ninaposikia watu wanasema, fulani yule anaishi maisha mazuri mwenzetu. Yaani watu wanafikiri kuwa ma gari nzuri, nyumba nzuri nguo nzuri basi akili zao zinawatuma ya kuwa huyu mtu/mwenzetu sio mwenzetu ana furaha na pia raha sana. Kwa kweli sio hivi:- unaweza ukawa na vitu vyote hivyo na ikawezekana maisha yako hayana furaha. Kwani FURAHA sio vitu.
1. Furaha ni kuwa na marafiki/rafiki wenye/mwenye furaha.
2. kuwa na furaha unaweza ukawa na furaha hata kama huna mali yaani vitu vizuri. Nina maana FURAHA NI MUHIMU KOLIKO PESA.
3. Pia furaha ni kuamka kila asubuhi na kujua kuwa ni mzima wa afya pia kuwa na familia ambayo inakujali na kukupenda wewe kama wewe.

Mtu /watu mwenye/wenye furaha huishi maisha marefu.

Na; Yasinta Ngonyani

Thursday, May 1, 2008

Mei 1, 2008 Elimu

Hili jambo limekuwa likinikereketa sana akilini mwangu. ELIMU je? ni nani ana haki ya kupata elimu hapa duniani. Kwa mfano afrika yetu,wazazi wengi wanasema hakuna haja ya kusomesha watoto/mtoto wa kike kwani wanaogopa watapoteza bure pesa kumsomesha mtoto wakati wanajua baada ya muda atarudi nyumbani tu. Lakini kitu ambach mimi bado sijaelewa kwa nini hao wasichana wanaokatishwa masomo baada ya kulea mtoto wake asiendelee na masomo? kwani kwa akili yangu sioni kama kuna tatizo wao wasiendelee na masomo yaani yote ya shule ya msingi na pia sekondary. Au kwa nini basi kusiwe na shule maalum kwa wale wasichana waliopata watoto. Kwani inasemekana kuwa Elimu ni ufunguo wa maisha , Sasa je? kama sisi wasichana hatupati elimu tutakuaje na ufunguo wa maisha?

Na; Yasinta Ngonyani