Wednesday, March 9, 2016

AFYA:- KAMA UANATAKA KUACHANA NA POMBE ZINGATIA HAYA.....

Kama ni mlevi  na unahisi huwezi kuacha kunywa  kwa siku moja, anza kwa kupunguza kiwango cha kunywa, yaaani kama unakunywa bia tatu kwa siku , anza kunywa moja,  baadae  moja kwa siku mbili mpaka utakapozoea kuishi bila pombe/kileo.
Epuka kuweka kilevi au pambe nyumbani au sehemu ya kazi ili kuepuka majaribu.
Usipende kuruka mlo, kula chakula mara tatu (3) mpaka mara nne (4) kwa siku ili kuupatia mwili virutubisho vyote muhimu.
Ondoa dhamira potofu kwamba huwezi kuishi pasipo kunywa pombe. Kumbuka mwili wako umeumbwa kikamilifu kukabili hali zote za maisha, hivyo usihisi kuwa pombe ndio kichochea chako kila unapotaka kufanya jambo fulani.
Zingatia mlo kamili, na jifunze kula matunda kwa mwingi. Hasa kama ulikuwa huli.
Anza kufanya mazoezi na upange ratiba yako ule muda ambao ulikuwa ukitumia kunywa pombe.
Kumbuka mambo mabaya yaliyokutokea kutokana na pombe katika maisha yako. Hii itakusaidia kutothubutu tena  kunywa pombe.
Ongeza unywaji wa maji, jiwekee mazoea ya kunywa maji angalao glasi tano (5)  kwa siku.
Kuwa na tabia ya kujizawadia/kujipongeza kutokana na uamuzi wako mzuri wa kutokunywa pombe.
Ni muhimu kuwashirikisha ndugu, jamaa na marafiki wa karibu kuhusu uamuzi wako wa kuacha pombe/kileo na pia usijione mjinga kwa wale watakao kucheka.
PANAPO MAJALIWA.KAPULYA WENU!

6 comments:

ray njau said...

Kuacha Ulevi

Si kila mtu anayekunywa pombe kupita kiasi anayekuwa mlevi sugu. Lakini baadhi ya watu wanaokunywa kwa ukawaida pombe nyingi, wanakuwa walevi sugu. Kwa kuwa mwili na akili za walevi sugu zimezoea sana pombe, watu hao hawawezi kuacha ulevi kwa kujidhibiti tu au kwa kupata msaada wa kiroho. Allen anasema: “Nilipokuwa nikijitahidi kuacha pombe, nilipatwa na maumivu makali sana. Ndipo nilipotambua kwamba ingawa nilikuwa nikipata msaada wa kiroho, nilihitaji pia matibabu.”

Walevi wengi wanahitaji matibabu ili kuwasaidia katika pigano lao la kiroho la kuacha ulevi na kuepuka kuurudia.* Baadhi yao wanahitaji kulazwa hospitalini ili waweze kupambana na maumivu makali yanayowapata wanapoacha kunywa pombe, au ili wapate dawa za kupunguza tamaa ya pombe na kuwasaidia wasirudie ulevi tena. Mwana wa Mungu aliye na nguvu za kufanya miujiza alisema hivi: “Wale walio na nguvu hawahitaji tabibu, bali wale walio wagonjwa wanamhitaji.”—Marko 2:17.

ray njau said...

Manufaa ya Kufuata Mwongozo wa Mungu

Mashauri ya Biblia yenye hekima kuhusu pombe yanatoka kwa Mungu wa kweli, anayetaka tufurahie maisha sasa na milele. Miaka 24 baada ya kuacha pombe, Allen anasema hivi: “Nilifurahi sana nilipojua kwamba ninaweza kubadilika, na kujua kwamba Yehova alitaka kunisaidia kurekebisha mambo yaliyokuwa yameenda kombo maishani mwangu, na kwamba yeye . . . ” Allen anatua ili kuzuia machozi yanayotaka kububujika anapokumbuka mambo ya zamani. “Yaani, . . . ni jambo zuri sana kujua kwamba Yehova anaelewa, anajali, na anasaidia.”

Kwa hiyo, ikiwa unakunywa pombe kupita kiasi au wewe ni mlevi sugu, usikate tamaa haraka, wala usiamue kwamba hakuna tumaini. Allen pamoja na wengine wengi wamekuwa katika hali ambayo unakabili sasa, nao wamefaulu kupunguza kiasi cha pombe wanachokunywa au wameacha kunywa kabisa. Hawajuti hata kidogo; nawe hutajuta.

Iwe unaamua kunywa pombe kwa kiasi au la, fanya kama Mungu anavyohimiza kwa upendo: “Laiti ungesikiliza amri zangu! Ndipo amani yako ingekuwa kama mto, na uadilifu wako kama mawimbi ya bahari.”—Isaya 48:18.

[Maelezo ya Chini]

Ona sanduku “Je, Pombe Inanitawala?” kwenye ukurasa wa 8.

Kuna vituo vingi vya tiba, hospitali, na mipango mingine ya msaada. Mnara wa Mlinzi halipendekezi matibabu yoyote hususa. Kila mtu anapaswa kuchunguza matibabu mbalimbali na kufanya uamuzi unaopatana na kanuni za Biblia.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 8]

Je, Pombe Inanitawala?

Jiulize:

• Je, ninakunywa pombe nyingi sasa kuliko hapo awali?

• Je, ninakunywa mara nyingi sasa kuliko hapo awali?

• Je, ninakunywa pombe kali sasa kuliko hapo awali?

• Je, ninakunywa ili kutuliza mfadhaiko au kusahau matatizo?

• Je, rafiki au mtu wa familia yangu ametaja kwamba ana wasiwasi kuhusu zoea langu la kunywa?

• Je, nimepata matatizo nyumbani, kazini, au safarini kwa sababu ya zoea langu la kunywa?

• Je, ni vigumu kwangu kukaa juma moja bila kunywa pombe?

• Je, ninaona vibaya wengine wasipokunywa pombe?

• Je, ninakunywa kisiri ili wengine wasijue kiasi cha pombe ninachokunywa?

Ukijibu ndiyo kwa swali moja au zaidi kati ya hayo, unahitaji kuchukua hatua ya kupunguza au kuacha kunywa pombe.

ray njau said...

Neno la Mungu Lamsaidia Mtu Aliyekuwa Mlevi

Supot anayeishi nchini Thailand alikuwa mlevi. Mwanzoni alikuwa akinywa jioni tu. Hatimaye alianza kunywa asubuhi na pia wakati wa pumziko la mchana. Mara nyingi alikunywa kusudi tu alewe. Kisha, akaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Supot aliacha kunywa alipojifunza kwamba Yehova Mungu hakubali ulevi. Lakini, baada ya muda akarudia ulevi. Watu wa familia yake walihuzunika sana.

Hata hivyo, Supot bado alimpenda Yehova na alitaka kumwabudu ifaavyo. Marafiki wa Supot waliendelea kumsaidia na kuwatia moyo watu wa familia yake watumie wakati mwingi zaidi pamoja naye, na wasiache kumsaidia. Wakati huo, andiko la 1 Wakorintho 6:10 linalosema wazi kwamba ‘walevi hawataurithi ufalme wa Mungu,’ lilimsaidia Supot kuona umuhimu wa kuacha ulevi. Alitambua kwamba alihitaji kufanya jitihada ya kufa na kupona ili kuacha ulevi.

Supot aliazimia kuacha kabisa kunywa pombe. Hatimaye, kwa nguvu za roho takatifu ya Mungu, mwongozo wa Neno la Mungu, na msaada wa watu wa familia na ndugu kutanikoni, Supot alipata nguvu za kiroho na akashinda tamaa ya pombe. Watu wa familia yake walifurahi sana alipobatizwa ili kuonyesha kwamba alikuwa amejiweka wakfu kwa Mungu. Sasa Supot ana ule uhusiano wa karibu pamoja na Mungu ambao alitamani kuwa nao tangu zamani, na anatumia wakati wake kuwasaidia wengine kiroho. (Madokezo yote kwa hisani ya www.jw.org)

ray njau said...

INAMAANISHA nini kunywa kupindukia? Wengine husema ni kunywa kwa kusudi la kulewa. Ripoti moja iliyotayarishwa na Taasisi ya Kitaifa ya Marekani ya Matumizi Mabaya ya Pombe (NIAAA) ilitoa maelezo hususa zaidi. Ilisema kwamba kunywa kupindukia ni “kunywa mfululizo gilasi tano au zaidi za pombe kwa wanaume, au gilasi nne au zaidi kwa wanawake.”

Ikiwa umeshawishiwa kunywa kupita kiasi au kunywa nawe hujafikia umri unaokubalika kisheria, huko peke yako. Vijana wengi wanatumia pombe vibaya.* Hata hivyo, jiulize, ‘Ni nini ninachojua hasa kuhusu sababu inayonifanya nitake kunywa, nayo pombe inaweza kuwa na madhara gani kwangu?’ Kwa mfano, ungejibu namna gani maswali yanayofuata? Tia alama ya ✔ katika kisanduku kilicho kando ya jibu lako, kisha ufikirie ukweli wa mambo.

a. Vijana hunywa kwa sababu tu wanapenda ladha ya pombe.

□ Kweli □ Si kweli

b. Kwa kuwa vijana wana umri mdogo na afya nzuri, hawaathiriwi sana na ulevi kama watu wazima.

□ Kweli □ Si kweli

c. Kunywa kupindukia hakuwezi kukuua.

□ Kweli □ Si kweli

d. Biblia inakataza pombe

□ Kweli □ Si kweli

e. Matokeo pekee ya kunywa kupindukia ni afya mbaya.

□ Kweli □ Si kweli

ray njau said...

Utachukua Hatua Gani?

Utaamua tu kuwafuata vijana wenzako wanaotumia pombe vibaya? Biblia inasema: “Je, hamjui kwamba ikiwa mnaendelea kujitoa wenyewe kwa yeyote kuwa watumwa ili kumtii yeye, ninyi ni watumwa wake kwa sababu mnamtii yeye?” (Waroma 6:16) Je, kweli unataka kuwa mtumwa wa vijana wenzako au wa pombe?

Unaweza kufanya nini ikiwa umenaswa na mazoea ya kunywa kupindukia? Tafuta msaada upesi kwa kuzungumza na mzazi au rafiki mkomavu. Zungumza na Yehova Mungu katika sala, na umwombe akusaidie. Yehova ni “msaada unaopatikana kwa utayari wakati wa taabu.” (Zaburi 46:1) Kwa kuwa mara nyingi watu hunywa kupindukia au kunywa kabla ya kufikisha umri unaoruhusiwa kisheria kwa sababu ya kuchochewa na marafiki, unahitaji kufanya mabadiliko makubwa kuhusu uchaguzi wa marafiki.* Si rahisi kufanya mabadiliko hayo, lakini kwa msaada wa Yehova unaweza kufanikiwa.(Chanzo.www.jw.org/sw)

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray Ahsante kwa mchango wako mzuri Kama huwa nisemavyo tusinyimane elimu. Hili hambo huwa ngumu sana kwa wengi walilolipitia na pia nimesikia wengi wanasimulia kuwa kuacha kuvuta sigara nako ni shida sana kama umeanza...