Sunday, February 10, 2013

JUMAPILI NJEMA NDUGU ZANGU:- LEO NA UJUMBE HUU!!!!

Elimu ni ufunguo wa maisha. Tuwaelimishe watoto wetu tangu wangali wadogo ili tuwajengee maisha bora. Wapate kupendwa na kila mmoja wetu na pia Mungu.
UNAJUA UKIAMBIWA KRISTU NAWE UTAJIBU NINI?.............YEYOTE ATAKAYEPITA HAPA LEO AWE NA JUMAPILI NJEMA SANA.

4 comments:

sam mbogo said...

kristu tumaini letu. kaka s

Yasinta Ngonyani said...

Haya kaka Sam! umepatia kabisa ..Uwe na Dominika njema sana na familia yako.

ray njau said...

Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
==================================
“Mambo yenu yote na yatendeke kwa upendo.”—1 WAKORINTHO 16:14
WAZAZI wengi wanakubali kwamba kumzaa mtoto kunaweza kuwa moja ya mambo yenye kufurahisha sana maishani. Mama mmoja anayeitwa Aleah anasema hivi: “Nilifurahi sana nilipomtazama kwa mara ya kwanza binti yangu mchanga. Sijawahi kamwe kuona mtoto mrembo kama huyo.” Hata hivyo, jambo kama hilo lenye kufurahisha linaweza pia kuwaletea wazazi mahangaiko. Mume wa Aleah anasema: “Jambo ambalo lilinihangaisha ni ikiwa ningeweza kumzoeza inavyofaa binti yangu ili apambane kwa mafanikio na matatizo ya maisha.” Wazazi wengi wana mahangaiko kama hayo na wanatambua uhitaji wa kuwazoeza watoto wao kwa upendo. Lakini, wazazi Wakristo ambao wanatamani kuwazoeza watoto wao kwa upendo wanakabili magumu. Magumu gani?
Sasa tunaishi siku za mwisho kabisa za mfumo huu. Kama ilivyotabiriwa, watu wengi ulimwenguni hawaonyeshi upendo. Hata katika familia, watu ‘hawana upendo wa asili,’ na wamekuwa “wasio na shukrani, wasio washikamanifu, . . . wasiojizuia, wakali.” (2 Timotheo 3:1-5) Kushughulika kila siku na watu wenye sifa hizo mbaya kunaweza kuwa na matokeo mabaya juu ya namna washiriki wa familia za Kikristo wanavyotendeana. Kwa kuongezea, wazazi wanapambana na mielekeo waliyorithi ya kutojizuia, kusema mambo bila kufikiri, na kufanya maamuzi yasiyo ya busara katika mambo mengine.—Waroma 3:23
Hata ingawa kuna magumu hayo, wazazi wanaweza kulea watoto wenye furaha ambao wanampenda Mungu. Jinsi gani? Kwa kufuata shauri hili la Biblia: “Mambo yenu yote na yatendeke kwa upendo.” (1 Wakorintho 16:14) Kwa kweli, upendo ni “kifungo kikamilifu cha muungano.” (Wakolosai 3:14)Na tuchunguze sifa tatu za upendo ambazo zinaelezwa na mtume Paulo katika barua yake ya kwanza kwa Wakorintho na tuzungumzie njia fulani hususa ambazo wazazi wanaweza kuonyesha sifa hizo wanapowazoeza watoto wao.—1 Wakorintho 13:4-8)

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray! ahsante kwa neno..na naamini nawe ulikuwa na j´p njema sana .