Friday, September 10, 2010

Jamani sisi kama watoto safari zetu huanzia mbali sana!

Tumetoka mbali jamani!!

Basi ngoja tumsikilize Dada Lady Jay Dee na wimbo wake natamani kuwa malaika, natamani tena kurudi nyuma, natamani kuwa kama zamani na natamani kuwa kama mtoto.!!!!!!!!!!!!!!

Basi ngoja niwatakieni IJUMAA NJEMA pia EID MUBARAK!!! AKIPENDA TUTAONANA !!

4 comments:

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Na hiyo picha haionyeshi ukweli halisi. Ukitaka kuupata ukweli halisi ni pale tunapozaliwa. Tunakuwa hoi bin taabani na tegemezi kwa asilimia 100. Na tunakuwa hivi kwa karibu miaka miwili mizima ya mwanzo.

Halafu jilinganishe na mtoto wa pundamilia au swala ambaye inabidi asimame na kuanza kutimua mbio saa moja tu baada ya kuzaliwa vinginevyo anaweza kuishia katika midomo ya fisi, simba na wanyama wengine.

Binadamu!

Simon Kitururu said...

Kweli kabisa safari zetu huanzia mbali sana kama tu Mkuu Masangu Matondo Nzuzullima alivyo ainisha.

Ijumaa na EID Mubarak njema Mdada Mrembo Binti Ngonyani!

chib said...

Big Up Matondo. Da Yasinta .. Minal Faidhina, kila la heri, japo si wote wanaoisheherekea!

Yasinta Ngonyani said...

Ahsante sana kaka matondo, mt.Simon na kaka Chib. Ila jueni ni kwamba natamani kweli kuwa malaika au mtoto tena...lol