Wednesday, November 21, 2012

MARA YA MWISHO KULA CHAKULA/MAGIMBI ILIKUWA KIHESA -NJOMBE KWA CHAI YA RANGI

Hapa ni magimbi kabla hajamenywa na ....

....hapa tayari yamemenywa na kuchemshwa tayari kwa kula. Magimbi unaweza kula kama chakula cha asubuhi, mchana au jioni. Ila mimi nimeyatamani sana leo na ningeyale kama chakula cha asubuhi hii ya leo kwa....
.

......kikombe hiki cha chai ya rangi  ila sasa.... haya ngoja nile kwa macho. Je? wewe mara ya mwisho ni lini umekula magimbi?

9 comments:

emu-three said...

Napenda sana magimbi kwa chai asubuhi, tupo pamoja ndugu wangu

batamwa said...

mimi nimeyala mwezi wa sita nilipokuwa likizo nyumbani Bukoba maana nayalima shambani kwangu,mengine tulienda porini kuwinda tukachoma hukohuko wacha utamu wake ulivyokuwa mtamu maana chakula cha porini kinakuwaga kitamu yaani hapo mate yananitoka

Yasinta Ngonyani said...

Ndugu wangu emu-3! tena chai yenyewe isiwe na sukari hapa ndiyo utauona utamu wake. Pamoja daima.

batwama! wewe unajua kweli kutamanisha mtu...ngoja nije huko Bukoba ...ulipotea au ndo ulikuwa unayafaidi magimbi nini?

batamwa said...

hapana nipo ila mishughuli ya kila siku karibu Bukoba ukayafaidi

ray njau said...

Magimbi ya BK na ya kule kwetu KILI sijui ladha ni ile ile Mshaija?

Anonymous said...

Good post. I learn something new and challenging on websites I stumbleupon every
day. It will always be helpful to read content from other writers and practice something from
other web sites.
Here is my webpage - how to get your ex back

batamwa said...

waitu Ray ladha ni ileile tu maana udongo unafanana kwa kiasifulani hivyo hayakuwa na tofauti kubwa sana

ray njau said...

Infwakiti yesi!!

Penina Simon said...

Duh watu mnajua kutamanisha wenzenu, sasa unafanyaje huko au hv vitu vipo huko?
mie leo ntapita sokoni Buguruni nikajinunulie kwa ajili ya mlo wa usiku.