Friday, April 15, 2011

IJUMAA YA LEO: HEBU FIKIRIA MILO YETU HII YA ASILI, WANAODHARAU VYAKULA KAMA HIVI HAO WANA HASARA HASWA!!!

Najaribu kufikiria naamka asubuhi. Naingia shambani kuchuma boga, nalichemsha na halafu tayari kwa Chakula cha asubuhi. Yaani boga kwa chai ya rangi. Kwa mimi chai yangu kama kawaida bila sukari hapo nitafaidi na kulamba mikono. Na mchana ni ugali, samaki, mboga majani kidogo, mchuzi, maharagwe kinywaji maji. Mmmm!! yam yam yam!!utamu jamani ...karibuni tujumuike basi.... Jioni naona tubadili mboga, tutakula KISAMVU ..yaani hapa mimate hadi inanidondoka si mchezo ..karibuni sana jamani tufaidi uhondo huu... Picha hizi kutoka kwa kaka Mjengwa . IJUMAA NJEMA WANDUGU!!!

14 comments:

ADELA KAVISHE said...

nawe pia ijumaa njema kipenzi ubarikiwe,,nimependa sana vyakula hivyo vya asili.

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

Ijumaa njema Da Yasinta!

Ila utawarusha roho watu wengi kwa mamisosi kedekede!

Unknown said...

dah mlo uko kamili kabisaaaa.

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

eat only the living food, will give u life. but dead food will give u death!!!!

Anonymous said...

Nipo job lakini umenikumbusha kitu, jana nimepokea zawadi kutoka kwa mama. Kanutumia mahindi mabichi, viazi mviringo,maharage na boga. Yani nikirudi tu nalichemsha halafu nalila kwa kijiko tartiib, nna kama miaka minne hivi sijakula hii kitu.

PASSION4FASHION.TZ said...

Na wewe pia,njaa inaniuma naingia humu nakutana na vitu kama hivi...we mchokozi sana.
xx

Simon Kitururu said...

Ijumaa njema kwako pia Mrembo!

Rachel Siwa said...

weweeeee dada Yasinta usifunge malango wangu,mimi leo mgeni wako!!!!!mambo iko huko!

Ijumaa njema nawe na familiya!.

Upepo Mwanana said...

weekend njema kwako

Unknown said...

Hiyo picha ya chini imenikumbusha makumbusho ya taifa DSM.

Anonymous said...

hivi kwanini watu wngi hawaupendi ugali?kwanini watuwengi hawyapendi maharage/we.? kwa nini siku ukipikwa wali katika familia zetu nikama sikukuu? kwanini ukikosa sukari nyumbani unasononeka je asali siyo tamu ?.dagaa nazo je niza watu wa hali ya chini.?mchicha nao unatatizo gani? kaka s

Sara Chitunda said...

Yaani dada hapo umenikumbusha kijijini kwa chai ya asubuhi mpaka mate yananitoka natamani ningeipata sasa hivi ningefurahi sana.

Mija Shija Sayi said...

Haya watu wa diet semeni sasa..

Simon Kitururu said...

@Mwanamke wa SHOKA:Ki-diet HASA ,...



....labda umezidisha kula kama ndani ya siku umekula vyote hivyo pichani!:-(