Friday, April 22, 2011

IJUMAA KUU HII IWE NJEMA KWA WAUMINI WOTE!!



Ni ijumaa ambayo Bwana Yesu Kristu atapata mateso kwa ajili yetu. Sijui kama kuna mtu angeweza kujitoa roho yake kwa ajili ya mwingine kama Bwana wetu Yesu anavyofanya kwa ajili yetu?..Na nawaombeni usisahau leo ni ile siku ambayo ni siku moja tu kwa mwaka ambayo tunaombwa kuacha kula vyakula vya damudamu hasa nyama ....Mwenyezi
ungu na atawala Nyumbani mwenu. Amina. IJUMAA KUU IWE NJEMA KWA WOTE....

5 comments:

nyahbingi worrior. said...

Mimi siamini katika hayo ya nyama wala nini.Wengi wanaamini kwasababu hatujui tunakotoka na tunakokwenda.


Sifa na utukufu kwake Haile.

Simon Kitururu said...

Mmmmh!

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Da, mi naona nshaharibu tayari kwani nimeshakunywa supu ya mbuzi leo asubuhi. Nitasamehewa bila shaka.

Ijumaa Kuu Njema kwako pamoja na familia yako D'Yasinta!!!

Evarist Chahali said...

Ijumaa Kuu njema nawe kwako dada Yasinta na familia yako.

Goodman Manyanya Phiri said...

Mimi nasubiri mwujiza kutoka Kwake; tena natarajia kabisa!

Asante kwa kutukumbusha Dada Yasinta!