Tuesday, December 8, 2015

TUNDA LA PERA SIO TUNDA TU ISIPOKUWA :- MAJANI YA MPERA KWA NYWELE ZINAZOKATIKA NA KUPUNGUA

Wanawake wengi wanaopenda urembo wa nywele wamekuwa wakihangaika hata  kama bei mbaya kisa tu kujaza nywele kichwani na kuzifanya zisikatike.
Wasiokuwa na muda wa saluni na wasiokuwa na hela hizi ni habari njema kwao kwamba majani ya mpera ni mazuri kwa kukuza nywele na kuzitibu zile zinazokatika.
Jinsi ya kuyatengeneza kama dawa
Chukua majani yanayotosha kwenye kiganja chako kisha weka kwenye sufuria yenye lita moja ya maji, chemsha kwa muda wa dakika 15 mpaka 20.
Baada ya hapo, yaache yapoe kisha paka kwenye nywele zako kuanzia kwenye mzizi wa nywele mpaka mwisho.
Ukimaliza fanyia masaji nywele zako kama mtu anayepaka mafuta nywele zote.
Baada ya hapo unaweza kuacha kwa muda  kisha ukaosha.
Fanya hivi mara kwa mara, naamini utaona mabadiliko.

2 comments:

Penina Simon said...

Ahsante kwa dawa hii!

Yasinta Ngonyani said...

Dada Penina Tupo pamoja elimu yoyote ni lazima tugawane.