Saturday, June 25, 2011

KUADIMIKA KWA MUDA KWA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO/KAPULYA!!!

Blog ya MAISHA NA MAFANIKIO inapenda kuwataarifu wasomaji wake kwamba haitakuwa hewani kwa muda.
Sababu kubwa ya kutokuwa hewani, nadhani wengi mmeona/soma/sikiliza posti ya 22/6 kuwa KAPULYA atakuwa SAFARINI na posti ya 22/6 ilikuwa kama kionjo tu yaani akifikiri jinsi safari itakavyoanza ....Sio safari nyingine bali ya NYUMBANI-TANZANIA.

Nitajitahidi kuwataafu mawili matatu. TUKUTANE TENA WAKATI MWINGINE PAMOJA DAIMA. NAWATAKIENI WOTE KILA JEMA. TUTAONANA.
NGOJA DR. Remmy amalizie kwa wimbo huu......

KARIBUNI SANA SONGEA-RUHUWIKO:-(-----:-)

21 comments:

Masangu Matondo Nzuzullima said...

Safiri salama Da Yasinta. Salama zao na usikose kutujulisha yanayoendelea huko kwa Wangoni....

Najua pia kwamba utakuwa na huzuni kwani Asifiwe hatakuwepo kukulaki. Natumaini kwamba Mungu Atakutia nguvu na moyo wa matumaini....

Anonymous said...

safari njema ufike salama da yasinta

Simon Kitururu said...

Safari njema Nangonyani!

Mija Shija Sayi said...

Safirini salama Dada, msiache kutuletea zawadi ya karanga.

Tutakumiss sana.

MARKUS MPANGALA said...

Shibe shibe shibe, haina bei
aenda kula nyumbani,
haina bei,
kwani nyumbani ni nyumbani
hata kama ni kichakani,
nyumbani kwetu, nyumbani,

Muungwana ni vitendo, karibu sana,
NIMEANDAA NDEGE YA LUPALU A.K.A UNGO

Mwanasosholojia said...

Safari njema da'Yasinta!

Raymond Mkandawile said...

Kila la kheri dada Yasinta na wasalimie wote hapo nyumbani....

Unknown said...

Karibu Tized

Faith S Hilary said...

Safari njema dada...enjoy nyumbani :-)

raynjawa said...

"JASIRI HAACHI ASILI NA MUACHA ASILI NI HASIDI NA HANA AKILI"
Safari njema mdau wetu Yasinta.
Nakutakia kila la kheri afya njema,baraka tele la kila jema liandamane na michirizi ya nyayo zako njema sana.

Rachel Siwa said...

Safari njema mama Erik! usile sana huko maana unahamu na kila kitu!!!!

emu-three said...

Karibu bongo, natumai utakuwa umejiandaa, maana macho yalizoea mwanga, huku usiku ni giza kwakwenda mbele...lakinii usijali ndio nchi yetu ...KARIBU SANA MPENDWA, UKIFIKA UJARIBU KUTUTAFUTA...

John Mwaipopo said...

hivi mtu hukaribishwa kwao? kama ndivyo yasinta ngonyani KARIBU NYUMBANI

Goodman Manyanya Phiri said...

Safari njema, Dada! Hatimaye, KILA MTU KWAO TU! (Sikua na muda wa kusoma taarifa yako ya kwanza juu ya safari yako na hayo ni tukokana na pilika-pilika za kwangu hapa, lakini naamini unakuja nao kabisa 'wajomba' zetu akina-Erik tukacheze nao mpira nasi: huenda tutaweza kusahau kidogo mambo mazito yanaotuathili daima eti!)

mumyhery said...

Safari Njema Mama Erick!!!

Anonymous said...

karibu nyumbani usikose kutembelea vijiwe vyetu vya manzase

Nampangala said...

Mlongo husisahau kuludi na mangatungu, chikandi, na mdonyolela. Safari njema kwako na familia yako. Mmbarikiwe sana. tutaonana ukiludi.

Mwanasosholojia said...

Dada'ngu Yasinta, bado hujarudi tu? Kweli hii ni likizo, tumekumiss sana sana!Ukipata ka-upenyo turushie mawili matatu!

Rik Kilasi said...

Ni matumaini tu ulifika salama dada Yasinta.Kila lakheri huko bombiyumbi lol

Anonymous said...

Da Yasinta Kama upo Songea Call 0755448177 au 0655448177 au fika Ofisi ya Waandishi wa habari jengo la Saccos ya walimu mtaa wa Zanzibar uliza Nyumayo. Karibu sana nyumbani.

Yasinta Ngonyani said...

Ahsanteni wooote nilisafiri salama namshukuru Mungu. Samahanini kwa kutowataarifu mapema. Muda ulibana mno.