Wednesday, June 8, 2011

USAFIRI WA NDEGE TOKA DAR ES SALAAM KWENDA SONGEA UMEANZA LEO

Habari hii imenipa furaha sana kwa kweli. Na nikaona si mbaya kama ikiwa katika kipengele chetu cha MARUDIO YA JUMATANO. Katika utembezi wangu pia kama wengine waniitavyo KAPULYA basi nimeipata habari hii JIFUNZE KUSINI.


Ndege ndogo zinatua katika kiwanja hiki cha Ruhuwiko Songea Ruvuma

Na ndege kubwa pia zinatua katika uwanja huu,Songea ina uwanja mzuri wa ndege,ila bahati mbaya ni ndege za viongozi ndizo zinazo tua hapo,sasa imekuwa bahati kampuni hii imeamua kuanzisha huduma hiyo ya usafiri.


Maneja wa uwanja wa ndege Songea Bwana Valentine Fasha mwenye tai nyeusi akiwa na mfanyakazi mwenzake wakati Rais Kikwete akiwasili uwanjani hapo juzi.
KAMPUNI ya ndege ya Air Indigo imeanza safari zake Leo,toka Dar es salaam kwenda Songea,ambapo toka juzi abiria kutoka Dar es salaam kwenda Songea walikwisha jaza ndege inayoweza kuchukua abiria 25.
Meneja wa uwanja wa ndege wa Songea Bwana Valentine Fasha aliiambia blog hii uwanajani hapo kuwa nauli ya kwenda na kurudi ni Tanzania shilingi 400,000/=,pia alisema usafiri wa ndege utakuwa wa siku mbili Juma tatu na Ijumaa.
Alisema kuwa booking ya safari inafanyika hapo hapo Air port kwani kwa muda huu hawana na ofisi ya kukatia tiketi mjini Songea.Hizo ndizo habari njema kwa wakazi wa Songe,na wilaya zake.

12 comments:

emu-three said...

MAMBO MAZURI HAYO, NDIO MAENDELEO...TUTAKALIA FOLENI ZA BARABARANI MPAKA LINI, UKIWA NAZO SHUUU, CHAPU UMESHAFIKA AU VIPI DADA YANGU

Yasinta Ngonyani said...

Yaani we acha tu nikiwa Dar mara moja nipo kunyumba. Ama kweli maendelea haswaaaa. KARIBUNI SANA RUHUWIKO:-)

Anonymous said...

Nikwambie kitu Da Yasinta,nimejaribu kujifanya mimi ndo wewe,na hakika nimejikuta rohoyangu/nafsi vikiburudika kwa kuwepo na ndege kutoka Dr- Songea.wewe mtu wa ulaya kweli ukufika Dar unataka upate usafiri wa haraka na wakuaminika ili uwawahi nduguzako songea.kwanzia sasa nakuona ukipanga kabajeti ka nauli ya ndege kutoka huko majuu uliko na ukifika Tz, naulikwenda songea.safi sana .Kaka S.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka S. Ahsante kwa kuifanya wewe ndo mimi na kuwa na furaha kama hiyo. Ni kweli uliyosema maana huwa nikifika Dar huwa nakuwa na shauku kweli ya kufika Ku-Songeya.. Nawe wala usisite kuja Ruhuwiko Karibu sana.

Mija Shija Sayi said...

Yasinta hongereni sana wenzetu...

Raymond Mkandawile said...

Wanaosema Tanzania hatuna maendeleo sasa wakati umefika kufunga vinywa vyao na kukubaliana nasisi kufurahia mabadiliko haya.Dada Yasinta i can imagine how happy ure...tupo pamoja sana kufurahia swala hilo.
Si Songea tu sasa hivi hata mbeya tuna usafirikama huo mara tatu kwa wiki na kama sikosei hata Iringa nako pia wanao...JE HAYO SI BAADHI YA MAENDELEO YA KUJIVUNIA?

Anonymous said...

Da yasinta, ku-songeya, nitafika tu japo yamebaki manyoya kuku washakula!.wangoni nyinyi niwatani zangu, songea nimuhimu kunahistoria yake ambayo nataka kuja kuona hasa huko waliko jenga wajerumani. Napia kama alivyodokeza ndugu Mkandawile,maendeleo yana kuja taratibu, leo kandege kesho chuo kikuu nk. Da mija we ulie tu garimoshi nawewe mpaka kieleweke(natania mwanza ndege kibao) Kaka S.

John Mwaipopo said...

Nakubaliana na wote hapo juu (na waliojirudia. ha! ha! ha!). Juzi nilikuwa namtazama ITV waziri wa uchukuzi Eng. Nundu kuhusu mpango mkakati wa kuhuisha usafiri wa ndege hapa nchini. kama aliyoyasema yanatekelezeka basi mambo yatakuwa safi. ana upeo mkubwa katika biashara ya ndege.

Rachel Siwa said...

SONGEA OYEEEEEEEE!!!!!

Anonymous said...

Safi sana mlongo maana wametusogezea mpaka mlangoni tushindwe wenyewe tu. Ni habari njema kwetu.

Anonymous said...

daaah! saaafi mara moja tu shuuu nipo songea

Anonymous said...

safiiiii ruhuwiko oyeeeee