Tuesday, December 6, 2016

MANGATUNGU (VELVET BEANS AU COWITCH BEANS) NI CHAKULA KWETU UNGONINI

KWETU UNGONINI TUNAITA MANGATUNGU. Chakula hiki inabidi upike kwa makini sana. Kwanza unachemsha kisha unamenya. Na hapo kazi inaanza unachemsha na kumwaga maji zaidi ya mara kumi. Sababu ni kwamba inasemekana kuna sumu ndio maana maji ya mwanzo huwa meusi sana . Kwa lugha ya kiingereza huitwa "velvet beans au cowitch beans"...pia inasemekana:- Mangatungu ni dawa kama viagra, ni kahawa, na ni dawa ya kutibu magonjwa ya nerves kama vile Parkinson disease. Kwa habari zaidi soma http://en.wikipedia.org/wiki/Mucuna_pruriens#Uses
N a baada ya kuchemsha na kumwaga maji zaidi ya mara kumi na mwisho wake matokeo yake huwa hivi  tayari kwa kula...ni chakula kizuri cha asili...

No comments: