Wednesday, November 2, 2016

JE WAKULIMA WA VIJININI WANATHAMINIWA?

Tanzania Iringa:- Ndugu zanguni! katika picha tunamwona bibi kikongwe akiwa na mzigo mkubwa wa kuni huku katika mkono wake wa kulia uliopata kufanya mamia ya shughuli ukiwa umeshika jembe, ni dhahiri kuwa bibi huyu ni mtu anayejali kazi zinazompatia riziki yake kwa kuwa dhana ya jembe ni kilimo na kuni ni chakula lakini serikali inawapa nguvu gani akina bibi kama hawa ili kuboresha kilimo chao mfano nyenzo za kilimo au mikopo.

wakulima wengi maeneo ya vijijini hulalamika kuwa serikali haiwapi msaada na matokeo yake wakulima hao hujikuta wakifanya kilimo duni, kila mwaka huwa hivyo tu. Je? mwaka mpya ujao (2017) inaweza kuwa ndo fursa ya serikali kuwainua wakulima.?

No comments: