Sunday, November 4, 2012

JUMAPILI YA LEO NAPENDA KUSALI SALA HII KWA MAREHEMU WOTE AKIWEPO MAMA MKWE WANGU AMBAYE KATUACHA JANA!!!

Na tuwaombee marehemu
Ewe Baba Mwenyezi, Mpaji wa maisha na afya, twakuomba uwaangalie kwa rehema marehemu pia wagonjwa wote, hasa wao wanaotakiwa maombi yetu, ili kwa baraka yako juu yao, na juu ya wao wawatumikiao, ikiwa mapenzi yako warudishiwe afya yao ya -mwili na ya roho,na pia marehemu wote wastarehe kwa amani, nao wakutolee shukrani katika kanisa lako takatifu; kwa Yesu Kristo, Bwana wetu. Amina.
JUMAPILI NJEMA KWA WOTE NA UPENDO UTAWALE NDANI YA MIOYO YENU.

14 comments:

Anonymous said...

Pole sana Dada Yasinta na familia yako. Bwana Yesu awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu cha msiba wa mama mkwe. Bwana ametoa, bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

Anonymous said...

Pole sana Dada Yasinta na familia yako. Bwana Yesu awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu cha msiba wa mama mkwe. Bwana ametoa, bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

Anonymous said...

Pole dada Yasinta. Mwenyezi Mungu awalaze mahali pema Ameen.

Rachel Siwa said...

Ameen!!!! na Poleni sana sana wapendwa na Muwe na j'pili njema nanyi na watu wooote.

Rafiko wa hiari said...

Oh rafiki pole sana kuondokewa na mama mkwe, tuko pamoja kwa maombezi. Raha ya milele umpe ee Bwana, na mwanga wa milele umwangazie, astarehe kwa amani. Amina

emuthree said...

Poleni sana, na duwa yako ipokelewe, kwani wao wametangulia na siye ni watarajiwa. Wao wameshatangulia kuyarisha makao,bado zamu yetu! Twamuomba mola awarehemu!

John Mwaipopo said...

poleni sana na msiba huu wa familia. Mungu Awatie nguvu na ustahimilivu

Emmanuel Mhagama said...

Ni habari ya huzuni lakini ni ukweli usioweza kupingwa na mwanadamu awaye yote. Kwa bahati mbaya sana kifo ni tukio ambalo halizoeleki na hakuna atakayekuja kulizoea, labda kama "fuse" za kichwa haziko sawa sawa. Hata hivyo tunalo tumaini kama yasemavyo maandiko matakatifu, "Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtarajia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo; atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyoe" Fil 3:20-21.
Mungu awatie nguvu na faraja katika kipindi hiki kigumu. Rest In Peace Our Lovely Mama.

Mija Shija Sayi said...

Poleni sana, Mungu awatie nguvu.

RIP Mama Mkwe..

ray njau said...

Msaada Kutoka kwa “Mungu Anayetoa
---------------------------------
Uvumilivu na Faraja”
-------------------------
MIAKA 2,000 hivi iliyopita, Paulo, mwandikaji wa Biblia alimfafanua Yehova kuwa “Mungu anayetoa uvumilivu na faraja.” (Waroma 15:5)Kwa kuwa Biblia inatuhakikishia kwamba Yehova habadiliki kadiri wakati unavyopita, tunaweza kuwa na hakika kwamba bado Mungu anawafariji wale wanaomtumikia. (Yakobo 1:17)Kwa kweli, Biblia inafunua kwamba Yehova anawafariji kwa njia mbalimbali wale walio na uhitaji. Ni njia gani hizo? Mungu anawatia nguvu wale wanaomwomba msaada kupitia sala. Pia, Mungu anawachochea Wakristo wa kweli kuwafariji waamini wenzao. Na Yehova ameweka katika Neno lake, Biblia, masimulizi yenye kutia moyo ambayo yanawatia nguvu hasa wale wanaoomboleza kifo cha mtoto. Acheni tuchunguze aina hizo tatu za faraja, moja baada ya nyingine.
“Yehova Mwenyewe Akasikia”
Mfalme Daudi aliandika hivi kuhusu Muumba wetu, Yehova: “Mtegemeeni nyakati zote. Mimineni moyo wenu mbele zake. Mungu ni kimbilio letu.” (Zaburi 62:8) Kwa nini Daudi alikuwa na uhakika huo katika Yehova? Daudi aliandika hivi kujihusu: “Huyu mwenye kuteseka aliita, na Yehova mwenyewe akasikia. Na Yeye akamwokoa kutoka katika taabu zake zote.” (Zaburi 34:6)Katika taabu zote zilizompata maishani, sikuzote Daudi alimwomba Mungu msaada, na sikuzote Yehova alimsaidia. Daudi alijua kutokana na mambo yaliyompata kwamba Mungu angemtegemeza na kumsaidia kuvumilia.
Wazazi wanaoomboleza wanahitaji kujua kwamba Yehova atawategemeza wakati wa huzuni nyingi, kama tu alivyomtegemeza Daudi. Wanaweza kumkaribia ‘Msikiaji mkuu wa sala,’ wakiwa na hakika kwamba atawasaidia. (Zaburi 65:2)William, aliyetajwa katika habari iliyotangulia, alisema hivi: “Mara nyingi, nimehisi kwamba singeweza kuvumilia kuishi tena bila mwana wangu, na nimemwomba Yehova anitulize. Sikuzote amenipa nguvu na uhodari wa kuendelea kuishi.” Wewe pia ukisali kwa Yehova kwa imani, Mungu mkuu wa mbinguni atakutegemeza. Mwishowe, Yehova Mungu anawaahidi hivi wale wanaojitahidi kumtumikia: “Mimi, Yehova Mungu wako, ninaushika mkono wako wa kuume, Mwenye kukuambia, ‘Usiogope. Mimi mwenyewe nitakusaidia.’”—Isaya 41:13.
Msaada Kutoka kwa Marafiki wa Kweli
Wale waliofiwa na mtoto mara nyingi wanahitaji wakati wa kuomboleza na kukabiliana na hisia zao wakiwa peke yao. Hata hivyo, halingekuwa jambo la hekima kwao kujitenga na wengine kwa muda mrefu. Kulingana na Methali 18:1. “mtu anayejitenga” anaweza kuumia. Kwa hiyo, wale wanaoomboleza wanapaswa kuwa waangalifu wasianguke katika mtego wa kujitenga.
Marafiki wanaomwogopa Mungu wanaweza kuwasaidia sana wale wanaotaabika. Andiko la Methali 17:17 linasema hivi: “Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote, naye ni ndugu aliyezaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.” Lucy, ambaye pia alitajwa katika habari iliyotangulia, alifarijiwa na marafiki wa kweli baada ya kufiwa na mwana wake. Alisema hivi kuhusu waamini wenzake kutanikoni: “Walitusaidia sana walipotutembelea, hata ingawa nyakati nyingine walisema machache. Rafiki mmoja alinitembelea siku ambazo nilikuwa peke yangu. Alijua kwamba ningekuwa nyumbani nikilia, na mara nyingi alikuja na kulia pamoja nami. Mwingine alinipigia simu kila siku ili kunitia moyo. Wengine walitualika nyumbani kwao kwa ajili ya chakula, na waliendelea kufanya hivyo.”
Ingawa uchungu mwingi ambao wazazi wanahisi wanapofiwa na mtoto hautoweki kwa urahisi, kusali kwa Mungu na kushirikiana na marafiki Wakristo kunaweza kuleta faraja ya kweli kwa wale wanaoomboleza. Wazazi wengi Wakristo ambao wamefiwa na mtoto wanatambua kwamba Yehova yuko pamoja nao. Ndiyo, Yehova “anawaponya wenye mioyo iliyovunjika, naye anafunga sehemu zao zenye maumivu.”—Zaburi 147:3.
Masimulizi ya Biblia Yanayofariji
Zaidi ya sala na ushirika unaojenga, Neno la Mungu lililoandikwa ni chanzo cha faraja kwa wale wanaoomboleza. Masimulizi ya Biblia yanaonyesha kwamba Yesu anatamani sana na ana uwezo wa kuondoa uchungu wa wazazi waliofiwa kwa kuwafufua wafu. Masimulizi kama hayo yanawafariji kikweli wale wanaoomboleza.

Yasinta Ngonyani said...

Shukranai zetu za dhati kwa wale wote waliounga nasi katika kipindi hiki na Mwenyezi Mungu azidi kuwaongezea upendo. Ahsanteni sana kwa kutufariji.

gadiel mgonja said...

pole

Mtani said...

Poleni sana kwa msiba huo, Mungu awape moyo subira katika kipindi hiki kigumu.

Yasinta Ngonyani said...

gadiel! Ahsante.
Mtani! Ahsante sana kwa pole Pamoja daima.