Monday, March 26, 2018

USITAFUTE PESA TAFUTA FURAHA

Katika maisha kitu kigumu kuliko vyote kukitafuta sio pesa bali ni furaha. Pesa ni ngumu kuitafuta kwasababu kila siku tunaipoteza katika kuitafuta furaha. Pesa humaliza matatizo na matatizo humaliza pesa. Inawezekana hata aliyezigundua  alikufa na madeni, sioni sababu ya kufa kwa sababu ya kutafuta maisha, bora uzima.  Pesa sio kila kitu. Inaweza kununua nyumba lakini haiwezi kununua familia, inaweza kununua  kitanda lakini haiwezi kununua usingizi, inaweza kunuua saa lakini haiwezi kununua muda. Pesa inaweza kununua vitabu lakini haiwezi kununua akili. Na maskini sio yule tu ambaye hana bali hata yule aliyenazo lakini anazitaka zaidi. Tafuta furaha kila siku usisubiri mpaka muda maalumu ndio uwe na furaha. Kila siku hapa duniani ni siku  maalumu. Na kwa taarifa yako sio mwenye pesa tu anayeweza kuhamisha milima hata fukara kapuku kama wewe na mimi. Pesa sio kila kitu bora furaha, inaweza kununua madaraka lakini haiwezi kununua heshima. Inaweza kununua damu lakini haiwezi kununua uhai, inaweza kununua dawa lakini haiwezi kununua afya. Pesa  haiwezi kununua mapezi.
CHANZO.- NILITUMIA NA RAFIKI KMA VIDEO/SIMULIZI NAMI NIMEUGEUZA KAMA MADA..

2 comments:

ray njau said...

Ni Nini Kinachohitajiwa ili Kuwa na Furaha?

Kwa ufupi: Epuka “matendo ya mwili,” na usitawishe “matunda ya roho ya [Mungu].” Ili kuwa na furaha, mtu anapaswa kutamani kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Mungu. Mtu anayejitahidi kutimiza jambo hilo atakuwa mwenye furaha kama Yesu alivyosema.

Kwa hiyo, usikate kauli kimakosa kwamba huwezi kuwa na furaha. Ni kweli kwamba afya yako inaweza kuwa si nzuri kwa sasa au labda una matatizo katika ndoa yako. Labda sasa huwezi kupata watoto au unajitahidi kutafuta kazi nzuri. Labda huna pesa nyingi kama zamani. Hata hivyo, jipe moyo; hupaswi kukata tamaa! Ufalme wa Mungu utatatua matatizo hayo na mengine mengi. Kwa kweli, hivi karibuni, Yehova Mungu atatimiza ahadi iliyotajwa na mtunga-zaburi: “Ufalme wako ni ufalme kwa nyakati zote zisizo na kipimo . . . Unaufumbua mkono wako na kutosheleza tamaa ya kila kitu kilicho hai.” (Zaburi 145:13, 16) Kama vile mamilioni ya watumishi wa Yehova ulimwenguni pote wanavyoweza kushuhudia, kukumbuka ahadi hiyo ya Yehova yenye kufariji kutakusaidia sana kuwa mwenye furaha leo.—Ufunuo 21:3.(Chanzo;jw.org/sw)

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray! Nakushukuru sana kwa kutochoka kupita hapa kila wakati na kuacha lako la moyoni. ajsante sana kwa maelezo na pia neno.