Saturday, July 26, 2008

JULAI 26, 2008 TANZANIA NDOGO

Leo nimefikiwa na wageni/marafiki ambao tuliishi pamoja TZ. Yaani raha sana, kama mnanielewa yaani ule urafiki umepita sasa ni ndugu. Nimeptwa na furaha ya pekee kuongea mambo ya zamani pia kuongea kiswahili lugha yangu. Sijui kama mtu unaweza kuona /jisikia raha japo kukumbuka nyumbani tu. kwani mara nyingi nakumukapo huwa natamani sana nyumbani.

Najua wengu mtashangaa na kuona nimechanganyikiwa. Sawa lakini kama mnavyoelewa utamaduni wa waafrika na wazungu basi mtaelewa naongoa nini. Nina maana kuishi pamoja, kushirikiana, kuishi pamoja kusaidiana hii napenda mimi kwani huondoa upweke. Hii yote nataka kusema leo nimejisikia nipo nyumbani TZ kweli nyumbani ni nyumbani.

No comments: