Thursday, January 19, 2017

SWALI LA LEO: SISI BINADAMU NI KITU GANI HASA?

Tunajitahidi sana katika kuvaa vizuri, kula vizuri, kujenga nyumba bora, kendesha magari makubwa na kufanya mengine ambayo yanaweza kuipa raha miili yetu na kutupatia  umaarufu ikibidi. Moja ya sababu za kufanya kwetu hivyo, ni ile imani yetu kwamba sisi ni miili yetu. Lakini ajabu ni kwamba, pamoja na kufanya hivyo, bado tunajikuta haturidhiki. Wengi hatujui kwamba, kutoridhika kwetu huko ni taarifa kwamba sisi ni kitu kingine, siyo miili hii tuliyonayo. Je, tumeshawahi kujiuliza sisi ni akina nani hasa? Kama bado, tumepata nafasi ya kujiuliza sasa na bila shaka tutapata jibu litakaloturidhisha.
Chanzo:- kitabu cha MAISHA NA MAFANIKIO

No comments: