Saturday, June 13, 2015

TUANZE JUMAMOSI HII KWA KIFUNGUA KINYWA HIKI HAPA CHAI KWA MIHOGO...KARIBUNI!!

 Mihogo ya kuchemsha  na hii chai hapa chini basi siku itakuwa njemaaaa. Karibuni tujumuike
Kwa wale waliozaliwa miaka ya uhuru watakubaliana na mimi kuwa vyombo hivi vilikuwa vya heshima sebuleni, kwenye kabati, halafu unakunywa chai kwa adabu maana yake kikombe cha moto, chai ya moto basi hapo chai inatelemka polepole...

4 comments:

Penina Simon said...

Umenikumbusha mbaliii,
navitamani hivyo vikombe lkn havipo ss na masinia yake kama siyaoni oni sku hzi!!!! nadhani vinapotea hivyo vyombo sasa

Nakutakia ibada njema

Yasinta Ngonyani said...

Dada P. Usikate tamaa vifaa kama hivi vipo wewe endelea kutafuta tu.

ray njau said...

Mlo wenye ladha maridhawa bila madhara!

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray! Hivi ndivyo vyakula avipendavyo Kapulya:-)