Wednesday, August 2, 2017

HIVI NDIVYO VYAKULA AVIPENDAVYO KAPULYA WENU

Ugali wa ulezi na nyama ya kuku, na sio ugali tu ugali na mlima wake juu ukiisha huu ni lazima usingizi mnono utapatikana iwe mchana au usiku:-)
Samaki waliokaangwa kwa ustadi haswaaaa
Au tu chips MIHOGO...nimekula sana mlo huu wakati nipo chuo kwanza naupenda pia ilikuwa bei rahisi  na unashibisha . Ukipata na kachumbali yako mmmhhh utajiuma kidole au pia ulimi:-) Haya niwatakieni mlo mwema siku ya leo chochote utakachokula kiwe kitamu.....PANAPO MAJALIWA

No comments: