Monday, January 12, 2015

HODI..HODIII....NAPENDA KUMSHUKURU MUNGU NIMESAFIRI SALAMA NA NIMERUDI TENA SALAMA

KAPULYA KIZIZINI PERAMIHO 2/1/2015
Nachukua nafasi hii kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutulinda katika safari yetu na pia sasa tumerudi salama tena. Pia ahsanteni kwa  sala zenu. Nilikuwa natamani kula nyama ya ngómbe nikaona ngoja nitembelea kizizini  Peramiho kwa wale wanaotokea Songea wanajua ni wapi. Na wewe usiyejua ni njia ya kwenda Peramiho upande wa kushoto kama unatokea Songea.
TUPO PAMOJA ....

5 comments:

Anonymous said...

Tunafurahi kukuona tena baaada ya kupotea zaidi ya siku saba. Usitusahau na sie nyama choma kwa kachumbari.By Salumu.

Anonymous said...

Nikuulize kitu Kadala, hivi uliondoka na picha gani na umerudi na picha gani kuhusu Peramiho? Nakuonea huruma Peramiho ya zamani sio ya sasa! Mengi yamebaki historia. Bustani na mashamba mazuri yote yamekufa, zizi linajikongoja tu, majengo waliyotuachia wamisionari yanaanguka, wale ma-father wa kizungu na mabruda wengi wameshakufa. Bila shaka ata Rafiki zako uliokuwa unacheza nao wapo sio kama ulivyowaacha. Maisha ni ajabu sana tunatamani enzi zetu zile zirudi tena!

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Mdada ulivyomechisha vazi na mjengo sina hamu! Umefunika ile mbaya na karibu tena kwenye baridi baada ya kufaidi vinono vya nyumbani.

Penina Simon said...

Nakupenda the ulivyo simple, hujikuzi, unajishusha hasa unapokuja huku nyumbani, Mungu akuzidishie huo moyo

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Salum!Unajua kublog ni raha mimi sikuwa mtandaoni tangu tarehe 13/12 mwaka jana :-) ni ujanja tu...Ila usihofu nyama choma na kachumbali utapata.

Usiye na Jina! Kwa vile huwa sikai sana..lakini hata hivyo kuna mabadiliko yake...Ndiyo bustani na mashamba yamekufa na zizi linajikongoja. Ni mambo mengi kuhusu Peramiho yanapotea.

Mwalimu Mhango! haikuwa makusudi kumechisha:-) Ahsante nimerudi salama na baridi nimeipokea na mafuta yote yashakauka:-)

Dada P. Ahsante sana.