Wednesday, May 11, 2011

WANAMITINDO WA WIKI HII NI HAWA HAPA!!

Huwa nafurahi sana nionapo utamaduni wetu wa KIAFRIKA unaendelezwa yaani kuvaa kama vile kanga na vitenge. Na sasa naona KANGA zinakuja juu kwa kushona magauni, mashati, mikoba nk. UTAMADUNI WA KIAFRIKA UDUMU!!!

Ebu angalia hapa, yaani kuangalia tu unaona jinsi UAFRIKA HALISI na mavazi yako unavyopendeza. BINAFSI NIMEPENDA/NINAYAPENDA SANA MAVAZI KAMA HAYA. Je? wewe unapenda mavazi ya aina gani?



4 comments:

Anonymous said...

katika kipengere, cha mvazi ya kiafrika hupata shida sana kuamini au kujua hasa nilipi vazi la kiafrika.ila kwapicha hizi ulizo weka jamaa wamependeza,na ndo jambo la muhimu kwangu linapo tokea swala la mavazi.kupendeza inategemea na chaguo la mtu, na aina ya nguo ulio vaa.labda kajiswali kidogo nguo zenye asili ya kiafrika ,nijinsi zinavyo onekana kuwa na marangirangi mengi,au kuwana michoro mbalimbali kama vile wanyama,mimea,nk au batiki,kanga vitenge? sijuwi ,Da, Mija,na Yasinta hebu tafuteni,unajuwa 'tunafika mahali tunakuwa waonga hata kuvaa 'suti' wengine kusema nivazi la kizungu kwa upande wangu si shabikii sana!.ila wakati wa harusi yangu nilivaa tena niliwekelea kanyau kwelikweli ! .baada ya harusi sijaigusa mpakaleo hii.kaka s

John Mwaipopo said...

sidhani swali la awali la anon linahitaji kumsumbua hivyo. afrika kama ilivyo kubwa katu haiwezi kuwa na vazi moja eti tukaliita 'vazi la afrika'. vivyo hivyo tanzania ilivyokubwa sidhani kuna vazi la kitanzania/kitaifa. ila kuna UJANJA wa/MASLAI wat watu fulani kutaka kuwalazimisha watu woote watambue na kuvaa vazi fulani, aghalabu wanalolipendekeza wao, eti liwe vazi la taifa. hamtupati ng'o. katu vazi la asili la wahaya si lile la wachagga, la wagogo si la wanyaki, la wamasai si la wafipa nk, nk, nk ...

kuhusu picha hizi za yanayoitwa mavazi ya kiafrika/kitaifa ni mambo hayo hayo ya kutaka kuwawazimisha wengi waige mavazi ya wachache kwa kisingizio cha 'vazi la taifa'. nyuma ya pazia kuna dhima na hila ya kibiashara zaidi. hamnipati ng'o kwa kisingizio cha 'vazi la taifa'. mtanipata kwa nia yangu ya kutaka kuvaa vazi la asili ya watu fulani ama lililoshonwa kwa namna fulani. kwa chambo cha 'vazi la taifa' narundia hamnipati n'go.

kwanza hata hao waliopigwa picha huvaa mavazi haya kwenye maonyesho tu, aghalabu usiku. sijawahi kuwaona kwa uwingi huu wamevaa mavazi haya kariakoo, kwenye daladala, darasani nk

Salehe Msanda said...

Habari
Nami nayapenda mavazi yetu ya asili na hasa muonekano wetu wa asili.

Ila du tumeathiriwa na utamaduni wa kimagaharibi

Kinachotokea ni kujirudia kwa historia maana mavazi haya yalikuwa yanavaliwa na babu na baba zetu miaka hiyo na walikuwa wanapendeze na kuvutia na yalikuwa ya gharamu ndogo.

Ifike mahali tujivunie vitu vyetu maana vita hadhi na thamani kubwa si mavazi tu hata vyakula na utamaduni wa maisha ya kaifrika kwa ujumla

Kila la kheri.

Unknown said...

Kuna suala huwa linasahaulika sana,na hii imekuwa ni desturi kama sio tabia ya wengi afrika na kwingineko.Tamaduni zetu tumezitekeleza, yaani kwamba kila kabila lilikuwa na aina yao ya mavazi, tukirejea katika historia ya kila kabila.

Yumkini wewe ukawa ni miongoni mwa wale ambao hawajui historia ya kabila lako. Laiti kama tungekuwa na utamaduni wa kutaka kufahamu historia za makabila yetu hili suala la kusema vazi la tanzania au afrika ni ngumu kupatikana lisingekuwa linazungumzwa kama hivi leo.

Nasema hivi kwa sababu tamaduni za magaharibi zimeshika hatamu na asili yetu kupotea, mtizamo wangu nauunganisha pia na katika muziki. Mfano Tanzania tuna makabila meeengi sana, waimbaji ama wanamuziki kama wangejikita kutafiti ama kujifunza muziki asilia wa makabila yetu na kuuboresha nadhani tusingekuwa na manyimbo yanayofanana fanana.

Leo hii kuna ambao wamejikita katika vyakula, kwamba hapa wanauza na kutengeneza vvyakula vya asili toka katika makabila mbalimbali ila sijawahi kuona ama kusikia kuwa kuna sehemu wanadesign mavazi yaliyotoka katika makabila mbalimbali.

KWA HIYO NI SISI KATIKA VISIVYO VYETU.