Friday, November 14, 2008

BAADHI YA METHALI NA MAFUNDISHO KUTOKA KATIKA VITABU VYA WANGONI

1) Methali:- Kweli ikidhihirika uongo hujitenga.


Fundisho:- Kesema ukweli kunatusaidia katika kuweza kuishi na watu vizuri bila
kuelemewa na soni na kujifichaficha ambayo ni madhara ya kusema
uwongo.

2) Methali:- Mkataa pema pabaya panamwita

Fundisho:- Usikubali kufunga ndoa na mtu usiyemfahamu barabara.


3) Methali:- Majuto ni mjukuu

Fundisho:- Kila tunapofanya mipango ya mambo makubwa tuchukue tahadhari yote ili
kukwepa matokeo mabaya.


4) Methali:- Anayejua joto la jiwe ni mjusi
Fundisho:- Tusilete vitu majumbani mwetu bila kujali athari zinazoweza kutupata
sisi wenyewe au jirani zetu kutokana na vitu hivyo.


5) Methali:- Kila ngoma ina wimbo wake
Fundisho:- Wazazi tusiyapuuze matatizo ya watoto wetu hata kama wamekuwa ni watu
wazima. Tuwape misaada au ushauri.


6) Methali:- Aliyekataa ukoo alikuwa mchawi.
Fundisho:- Dumisha ukoo kwani ndugu atakufaa siku ya dhiki.


7) Methali:- Mwenda usiku amesifiwa kulipokucha
Fundisho:- Wewe usumdharau mtu kwa kuwa huielewi shughuli anayofanya kwa sababu
penngine shughuli yake italeta mafanikio na wenzako watamsifu.


8) Methali:- Mwanamume sio ndevu.
Fundisho:- Kila mwanamume anao uwezo. Kwa hiyo ni wajibu kwa wanaume wote kushika
moyo wa kiume.


9) Methali:- Mdomo ukila oua haitaki.
Fundisho:- Watu wengine hawafurahii mafanikio ya wenzao.



10) Methali:- Hasira ya mkizi furaha ya mvuvi.
Fundisho:- Unapokuwa na hasira usifanye jambo lenye umuhimu mkubwa ili kukwepa
kulifanya vibaya.

2 comments:

Unknown said...

Kweli dada mambo vp? Umenikumbusha mambo mengi hapo,hongera sister.

Yasinta Ngonyani said...

Nilifanya hivyo ili tusisahu methali zetu kwani ni moja ya utamaduni