Monday, November 29, 2021

NARUDI NYUMBANI:- LAKINI KWA MUDA TU!

NI RAHA ILIOJE KUWENDA NYUMBANI KULA LIKOLO LA NANYUNGU! TUTAONANA SI MUDA MREFU

Wednesday, October 6, 2021

VYAKULA VYA ASILI NI MUHIMU SANA

Tusisahau vyakula vyetu vya asili. Maana hapo utakuwa umesahau ulikotoka.

Friday, September 3, 2021

UJUMBE WA WIKI HII!

Watu watano wanaostahili muda wako:- 1. Familia 2. Rafiki(bora) wa karibu 3. Mshauri/mlezi wako 4. Wanaohitaji msaada wako 5. Wewe mwenyewe yapaswa:- Ujipende na utumie muda wako kutafakari na kujiboresha.

Saturday, August 21, 2021

Wednesday, June 9, 2021

LEO MWENZENINIMEKUMBUKA NYASA KWETU NA KITU HII LIKUNGU..NI MBOGA TAMU SANA

KATI YA VYAKULA NIVIPENDAVYO MOJAWAPO NI LIKUNGU HASA LIKIWA MADAFU

Monday, May 10, 2021

MKE ASIYE NA MUME, AKAMCHUMBIE NANI?

Niolewe na nani mie! Isingekuwa vigeni, mwanamke kuchumbia Ningepita mitaani, mume kujitafutia, Nisimuudhi Manani, ndio nimejizuia. Mke asiye na mume akamchumbie nani? Ndege maingainga, si jambo la kujitakia, Mume mwema natamani, vipi tajitafutia? Na mwanamume haini, sitaki kunichumbia, Mke asiye na mume akamchumbie nani? Nimetulia nyumbani, sina mume kunioa, Wanifuatao ndani, si wachumba wa kuoa, Hutaka kunirubuni, maasini kunitia, Mke asiye na mume akamchumbie nani? Ndege maingainga, si kosa langu sikia, Niliolewa zamani na mume mwenye udhia, Kanitia kilabuni, pombe kumchuuzia Mke asiye na mume akamchumbie nani? Mimi nikamuamini, huku machozi nalia, Mume hii kazi gani, alokataza jalia? Kheri tukate kuni, mimi nitakuuzia. Mke asiye na mume akamchumbie nani? Akapanda hasirani, na maneno akafyoa: Mke wee mke gani, dini lini ulijua! Alipozidisha kani, ndoaye nikajivua. Mke asiye na mume akamchumbie nani? Wako mabwana wa shani, ningependa kunioa, Hawamtii shetani, Munguamewaongoa, Nao wamomashakani, kwa mabibi walooa, Mke asiye na mume akamchumbie nani? Tu wema hatujuani, wake na waume pia, Twaingia mashakani, kwa wenzi waso murua, Namlilia Manani, mume mwema kunioa, Mke asiye na mume akamchumbie nani? Nawe muombe, ndoa yenu kutulia, Tusikuone mwakani, viragoumepania, Mke na mume nyumbani, mumche Mola Jalia. Mke asiye na mume akamchumbie nani? Shairi hili limetungwa na Sheikh Amri Abedi, nami limenivutia nikaona niliweke hapa ili tujifunze kwa pamoja

Thursday, May 6, 2021

MAHINDI YA KUCHOMA NI BORA KULIKO POP CORN!

Hivi kwa nini tusile mahindi ya kuchoma tuingiapo sinema kama ilivyo utamaduni wetu badala ya kula pop corn?

Friday, April 16, 2021

LEO NIMETAMANI KWELI HII KITU...EMBE

JAMANI MWENZENU JIONI HII NIMETAMANI SANA EMBE:-( NI MIMI KAPULYA WENU!

Thursday, March 25, 2021

TUMALIZE MWEZI HUU WA TATU KWA UJUMBE HUU UFUATAO:-

UHURU WA NCHI NI SAWA NA AFYA YA MWILI/MWILINI. NAPENDA KUWATAKIENI AFYA NJEMA NA TUUMALIZE MWEZI HUU SALAMA. PAMOJA DAIMA! KAPULYA WENU.