MTOTO wa miaka miwili na nusu, (jina linahifadhiwa), anayeishi katika Kijiji cha Buseresere kilichopo Wilaya ya Chato, mkoani Geita, anasadikiwa kubakwa na mjomba wake, Tatizo Lubalaza (20).
Taarifa za awali zinadai tukio hilo lilitokea Julai 5, mwaka huu, saa tatu usiku, baada ya mjomba huyo anayesadikiwa alikuwa amelewa kufika nyumbani hapo na kuingia ndani na kumkuta mtoto huyo akiwa sebuleni, huku mama yake mlezi, Pelesi Lubalaza, akiwa chumbani pamoja na wadogo zake na kisha akambeba na kuanza kumfanyia ukatili huo wa kinyama.
Baada ya kuanza kufanyiwa kitendo hicho, alianza kulia huku akilalamika anaumizwa, ndipo mjomba wake, Tatizo alipomwachia na kutoka nje, huku mtoto huyo akikimbilia chumbani kwa mama yake mlezi akilia.
Akisimulia tukio hilo huku akibubujikwa na machozi, Pelesi, alisema hakuamini kama kaka yake angeweza kufanya kitendo hicho cha kinyama kwa mtoto wao na mtoto huyo, ambaye aliingia chumbani huku akikamata sehemu zake za siri na kulitaja jina la mjomba wake, ndipo alipomkagua na kugundua damu zikitiririka miguuni mwake.
Alisema baada ya kugundua mtoto huyo kafanyiwa kitendo cha kinyama alichukua uamuzi wa kwenda Kituo Kidogo cha Polisi cha Buseresere kwa lengo la kutoa taarifa na kupewa barua ya matibabu ambapo alipelekwa katika Zahanati ya Buseresere kwa ajili ya matibabu kutokana na maumivu makali aliyoyapata.
Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Buseresere, Dk. Joram Nyanza, alithibitisha kumpokea Victoria na kudai alikuwa amechanika sehemu zake za siri na kumpatia matibabu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Leonard Paul, hakupatikana kuzungumzia tukio hilo.
chanzo: MTANZANIA
Showing posts with label mtoto. Show all posts
Showing posts with label mtoto. Show all posts
Tuesday, July 10, 2012
Friday, June 8, 2012
WATU TUMETOKA MBALI/KUJIFUNZA MAISHA!!!
Picha hii imenipeleka mbali sana. Hakika watu tumetoka mbali na changamoto nyingi tumepitia. Binafsi napenda kuwashukuru wazazi/walezi wangu kwa kunilea, kuniongoza vipi jinsi ya kuishi maisha. Je? wewe pia unakumbuka kazi za utotoni?.......IJUMAA NJEMA TENA!!!
Friday, May 4, 2012
CHAGUO LA MAISHA NA MAFANIKIO KUWA PICHA YA WIKI :- JE? HUU NI UBUNIFU AU?
Nimetumiwa picha hii na msomaji wa Maisha na Mafanikio kwanza nikashikwa na butwaa, na pili nikajiuliza ni ubunifu? Na tatu nikajiuliza kukosa mtu wa kumtunza mtoto au chekechea? Nawaachia mwenzangu tusaidiana kujadili hapa...Duh! ila sidhali kama mtoto huyo anapata raha hapo.....MCHANA MWEMA MAJEMANI!!!
Thursday, September 8, 2011
MATITI NI CHAKULA CHA MTOTO AU?
Sijui kwa ajili ya kukosa watoto au Kweli huu ni UUNGWANA kweli kumnyonyesha mbuzi?
Na huyo naye anamnyonyesha mtoto wa ndama kisa? Sijui akimngáta hapo atasema nini?
Hapa sawa, mama akimpa mtoto chakula ambacho ndicho chakula bora sana kwa watoto wachanga. Ila kuna simulizi nimeisikia kuwa, wanaume wengi huwa wanaona WIVU sana wakati mama/mke wake amnyonyeshapo mtoto. Hasa mtoto wa kiume. Sijui wenzangu nanyi mmewahi kusikia? Na kama kweli kwanini sio anyonyeshwapo mtoto wa kike?Friday, February 11, 2011
BREAKING NEWS: LITTLE MAKULILO AZALIWA
On February 10th, 2011 at 5:42pm, Pacific Time, Marie Makulilo has delivered our cute little Makulilo named BENEDIKT FULBRIGHT MAKULILO. Benedikt has 8.8lbs (weight) and 21 inches (length)
The logic behind the names (Benedikt Fulbright Makulilo)
The logic behind the names (Benedikt Fulbright Makulilo)
The name Benedikt (with letter "K" instead of "C" because of Kiswahili and Germany spelling of Benedikt), which comes from the Latin word meaning "the blessed", in honour of both Saint Bendict of Nursia and Pope Benedict XVI. And the name Fulbright is in honour of the prestigious FULBRIGHT scholarship. Fulbright Scholarship is the scholarship which has been named after William James Fulbright, and it has lot of meaning in realizing my dreams today, and MAKULILO is the honor of unsung hero Boniface Makulilo, my father
Thank you all for your prayers and encouragement.
The Makulilos (Marie, Ernest and Benedikt)
Blog www.makulilo.blogspot.com
www.scholarshipnetwork.ning.com
Thank you all for your prayers and encouragement.
The Makulilos (Marie, Ernest and Benedikt)
Blog www.makulilo.blogspot.com
www.scholarshipnetwork.ning.com
Thursday, June 3, 2010
HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA KWAKO ERIK!!
Thursday, February 18, 2010
HADITHI YA MWANA MPOTEVU
Hiii hadithi inanikumbusha mambo mengi sana sijui wenzangu mnasemaje?
Kulikuwa na baba mmoja aliyekuwa na watoto wawili wa kiume. Siku moja yule wa mwisho akamwambia baba yake : baba mimi sasa ni mkubwa naomba haki yangu nataka kuondoka kwenda mbali kutafuta maisha. Baba yake akampa pesa nyingi tu. Akaondoka akaenda zake na pesa zote.
Muda si mrefu akapata marafiki wengi tu. akawa anakula na kunywa nao pamoja na yeye ndiye aliyekuwa analipa kila kitu.
Lakini muda si mrefu pesa zote zikamwishia. Akawa hana kitu cha kula. Marafiki zake wote hawakumpa wala kumsaidia chochote isipokuwa walimtupa barabarani.
Siku moja akaondoka akaenda kwa mkulima mmoja na kusema ya kwamba anaomba chakula, aina yoyote ile, na halafu atafanya kazi kwake. Mkulima akamhurumia akampa chakula na akamwambia kazi yake ni kuchunga nguruwe wake.
Hata hiyo kijana bado alikuwa ana njaa. Akaanza kuwaza: kwa nini napata taabu hapa wakati baba yangu ana chakula kingi tu. Narudi nyumbani kwa baba tena. Nataka kufanya kazi kwa baba kuliko hapa.
Mara akaanza safari ya kurudi kwa baba yake. Na kusema baba, naomba radhi nimekosa. Ilibidi nisirudi na wala usinipokee tena hapa nyumbani kwako. Lakini baba kwa uchungu wa furaha akamkumbatia na kumpokea. Kwa furaha kubwa baba akamfanyia kijana wake sherehe kubwa kwa kufurahia kwa sababu kijana wake alikuwa amerudi tena kwake.
Kaka mtu akawa anarudi toka kazini(shambani) akakutana na babake asemaye. Mdogo wako amerudi tena nyumbani njoo tumsherehekee. Alipotea sasa amerudi tena.
Swali: Je? Hadithihii wewe inakufundisha nini?
Na je? ungekuwa wewe ni yule kaka mkubwa ungefanyaje?
Hebu sikiliza hapa lugha ya mwenzetu wasukuma mimi nimeipenda kwani nimeelewa neno moja moja hata hivyo najivunia lugha zetu za asili zinasikika.
Au kama hujaelewa hapo basi sikiliza hapa lugha yetu ya kiswahili
Kulikuwa na baba mmoja aliyekuwa na watoto wawili wa kiume. Siku moja yule wa mwisho akamwambia baba yake : baba mimi sasa ni mkubwa naomba haki yangu nataka kuondoka kwenda mbali kutafuta maisha. Baba yake akampa pesa nyingi tu. Akaondoka akaenda zake na pesa zote.
Muda si mrefu akapata marafiki wengi tu. akawa anakula na kunywa nao pamoja na yeye ndiye aliyekuwa analipa kila kitu.
Lakini muda si mrefu pesa zote zikamwishia. Akawa hana kitu cha kula. Marafiki zake wote hawakumpa wala kumsaidia chochote isipokuwa walimtupa barabarani.
Siku moja akaondoka akaenda kwa mkulima mmoja na kusema ya kwamba anaomba chakula, aina yoyote ile, na halafu atafanya kazi kwake. Mkulima akamhurumia akampa chakula na akamwambia kazi yake ni kuchunga nguruwe wake.
Hata hiyo kijana bado alikuwa ana njaa. Akaanza kuwaza: kwa nini napata taabu hapa wakati baba yangu ana chakula kingi tu. Narudi nyumbani kwa baba tena. Nataka kufanya kazi kwa baba kuliko hapa.
Mara akaanza safari ya kurudi kwa baba yake. Na kusema baba, naomba radhi nimekosa. Ilibidi nisirudi na wala usinipokee tena hapa nyumbani kwako. Lakini baba kwa uchungu wa furaha akamkumbatia na kumpokea. Kwa furaha kubwa baba akamfanyia kijana wake sherehe kubwa kwa kufurahia kwa sababu kijana wake alikuwa amerudi tena kwake.
Kaka mtu akawa anarudi toka kazini(shambani) akakutana na babake asemaye. Mdogo wako amerudi tena nyumbani njoo tumsherehekee. Alipotea sasa amerudi tena.
Swali: Je? Hadithihii wewe inakufundisha nini?
Na je? ungekuwa wewe ni yule kaka mkubwa ungefanyaje?
Hebu sikiliza hapa lugha ya mwenzetu wasukuma mimi nimeipenda kwani nimeelewa neno moja moja hata hivyo najivunia lugha zetu za asili zinasikika.
Au kama hujaelewa hapo basi sikiliza hapa lugha yetu ya kiswahili
Tuesday, January 19, 2010
PIACHA YA LEO:- NAKUMBUKA ZAMANI NILIPOKUWA MDOGO!!!
Leo nimekumbuka nilipokuwa mdogo kwenda mstuni kuokota kuni, na hapo ujue ukirudi inabidi uende mtoni/kisimani kuchota maji. Wakati huo huo maharage yapo jikoni inabidi uchochee na kisha inabidi kutwanga mihogo. Ama kweli tumetoka mbali!!! Haya ndio maisha tuliopitia wengi huwa najiuliza sijui ni muda gani nilisoma?....!!Sunday, December 27, 2009
LEO NI JUMAPILI YA MWISHO YA MWAKA HUU NA NI JUMAPILI YA FAMILIA TAKATIFU!!! NAWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA!!
Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako,
Wala usiyapuuze mafundisho ya mama yako.
Maisha ya kila binadamu huanza na hatua ya utoto. Mafanikio ya kila mtoto hutegemea malezi na makuzi ya wazazi au walezi.Thursday, October 8, 2009
MTOTO AJIFUNGUA MTOTO MWENZIE!!!!!
Dunia hii sasa ni hatari kweli. Mtu na akili zake kabisa anathubutu kumfanyia unyama mtoto wa mwenzie. Kiasi cha kumpa mimba na kuzaa mtoto mapema. Kabla ya wakati wake wa kuzaa haujafika. Inaonekana huku tunakoelekea sasa ni hatari tupu au ni kweli labda ni mwisho wa dunia.
Monday, August 24, 2009
Monday, June 22, 2009
Tuesday, June 9, 2009
Thursday, June 4, 2009
KUMUAHIDI MTOTO ZAWADI NI KUMFUNDISHA AU KUMUHARIBU?
Kuna tabia ya sisi wazazi kuwaahidi watoto kwamba tutawapa zawadi fulani kama watafanya kitu fulani. Tatizo la kwanza linalojitokeza hapa ni kwa mtoto kushindwa kujua kwamba anapaswa kufanya mambo mazuri hata kama hakuna zawadi.
Kila wakati mtoto atakuwa akifanya jambo au mambo mazuri kwa matarajio ya zawadi na endapo kutakuwa hakuna zawadi hataona sababu ya kufanya hivyo
Mtoto anapoambiwa kwa mfano kwamba akiwa wa kwanza darasani atapatiwa viatu, anakuwa anajengewa dhana kwamba viatu sio haki yake bali ni mpaka afikie matarajio fulani ya mzazi wake ili aweze kupata viatu.
Kuna wazazi ambao huwaahidi watoto wao zawadi kama nguo, midoli, baskeli na vitu vingine vinavyofanana na hivyo, ambavyo kimsingi ni haki yake.
Wengi wetu tumelelewa katika mazingira ya aina hii. Tulipokuwa wadogo wazazi wetu walishindwa kujua kwamba viatu, nguo, midoli na kadhalika ni haki yetu, bila kujali kama tumefanya vizuri darasani au tumefanya jambo lolote tulilopaswa kulifanya kwa ustadi mkubwa, kama walivyotarajia.
Kwa mtindo huo wa malezi wametufanya tuamini kwamba ili tupate haki zetu ni lazima tufikie matarajio ya wazazi.
Na sisi tumejikuta tunatumia mbinu hiyo hiyo katika kuwalea watoto wetu.
Je? malezi ya aina hii yana athari gani katika ustawi wa watoto wetu?
Labda hilo niwaachie wasomaji mtoe maoni yenu, kwani mimi hili linanitatiza….
Kila wakati mtoto atakuwa akifanya jambo au mambo mazuri kwa matarajio ya zawadi na endapo kutakuwa hakuna zawadi hataona sababu ya kufanya hivyo
Mtoto anapoambiwa kwa mfano kwamba akiwa wa kwanza darasani atapatiwa viatu, anakuwa anajengewa dhana kwamba viatu sio haki yake bali ni mpaka afikie matarajio fulani ya mzazi wake ili aweze kupata viatu.
Kuna wazazi ambao huwaahidi watoto wao zawadi kama nguo, midoli, baskeli na vitu vingine vinavyofanana na hivyo, ambavyo kimsingi ni haki yake.
Wengi wetu tumelelewa katika mazingira ya aina hii. Tulipokuwa wadogo wazazi wetu walishindwa kujua kwamba viatu, nguo, midoli na kadhalika ni haki yetu, bila kujali kama tumefanya vizuri darasani au tumefanya jambo lolote tulilopaswa kulifanya kwa ustadi mkubwa, kama walivyotarajia.
Kwa mtindo huo wa malezi wametufanya tuamini kwamba ili tupate haki zetu ni lazima tufikie matarajio ya wazazi.
Na sisi tumejikuta tunatumia mbinu hiyo hiyo katika kuwalea watoto wetu.
Je? malezi ya aina hii yana athari gani katika ustawi wa watoto wetu?
Labda hilo niwaachie wasomaji mtoe maoni yenu, kwani mimi hili linanitatiza….
Subscribe to:
Posts (Atom)




