Showing posts with label MIAKA 11 HAUPO NASI MAMA. Show all posts
Showing posts with label MIAKA 11 HAUPO NASI MAMA. Show all posts

Monday, August 17, 2015

KUMBUKUMBU:- LEO NI MIAKA KUMI NA MOJA (11) KAMILI TANGU MAMA YETU ALANA NGONYANI ATUTOKE!!

MAMA! ANAWEZA KUCHUKUA  NAFASI ZA WENGINE LAKINI NAFASI YAKE HAIWEZI KUCHUKULIWA NA YEYOTE YULE
 
KUZALIWA 2/10/1952-KUFA 17/8/2004
Mama ni miaka kumi na moja  sasa tangu ututoke. Umetuacha na majonzi pia maumivu moyoni mwetu. Tunaukumbuka sana uwepo wako, tukiamini Mungu angekuacha japo kwa miaka michache. Midomo yetu haiwezi kuelezea jinsi tulivyokupenda. Lakini Mwenyezi Mungu anajua ni jinsi gani tulivyokupenda. Na jinsi gani tunakukumbuka, mapenzi yako, wema wako. Pia kama mama kwa mwongozo wako katika nyumba yetu, ambayo sasa ni upweke mtupu bila wewe.
Tunakukumbuka sana, sisi wanafamilia wote pamoja na ndugu wote na pia marafiki. KIMWILI HAUPO NASI, BALI KIROHO UPO NASI DAIMA. MWENYEZI MUNGU AIPUMZISHE ROHO YAKO MAHALA PEMA PEPONI. AMINA!!!