Showing posts with label ujasiri. Show all posts
Showing posts with label ujasiri. Show all posts

Thursday, October 13, 2016

JIPE MOYO KAMWE USIKATE TAMAA KWA MUNGU YOTE YANAWEZEKANA

"Nilikuwa naangalia mpira wa miguu katika uwanja wa shule. Nilipokaa, nilimuuliza kijana mmoja juu ya matokeo ya mchezo. Kwa tabasamu, alijibu "Wako mbele yetu 3-0"! Nikasema, Kweli!! Mbona huonekani kukata tamaa.
"Kukata tamaa? "Yule mvulana aliuliza kwa mshangao.... Kwanini nikate tamaa wakati bado refa hajapuliza kipenga cha mwisho? Nina imani na timu yangu na meneja wa timu; Nina hakika tutashinda! Na kweli, mchezo uliisha 5-4 timu ya kijana ikiwa mbele! Alinipungia mkono taratibu, na tabasamu zuri akiondoka uwanjani; nilishangaa,mdomo wazi, ujasiri mkuu kiasi hiki; nilipenda alivyojiamini ;  Nilipofika nyumbani usiku ule, swali lake lilizidi kuja kwangu zaidi.
"Kwanini niogope wakati refa hajapuliza kipenga cha mwisho?" Maisha ni kama mchezo. Kwanini ukate tamaa wakati Mwenyezi Mungu ndiye meneja wako? Kwanini ukate tamaa wakati kungalipo uhai ndani yako? Kwanini ukate tamaa wakati kipenga chako cha mwisho bado hakijapigwa? Ukweli ni kwamba watu wengi hujipulizia wenyewe vipenga vyao vya mwisho. Lakini madamu ungalipo uhai, hakuna kisichowezekana muda haujakuacha. 
Nusu kipindi si kipindi kizima na ratiba ya Mungu kwa mwanadamu si ratiba ya mwanadamu kwa Mungu.
Usijipulizie kipenga chako cha mwisho wewe mwenyewe.
UJUMBE- Maisha ni changamoto  ambapo pia ni kama mchezo...twapaswa kuwa jasiri na kujiamini.

Thursday, October 27, 2011

UJUMBE WA LEO UKUTOKAO KWA KAPULYA NI HUU HAPA!!!

Ndoto zetu zote zinaweza kutimizwa ikiwa tutakuwa na ujasiri wa kutimizwa.

Ngoja Kaka Sam amalizie na wimbo huuu...


ALHAMIS NJEMA JAMANI NA TUSISAHAU KUMSHUKURU MUNGU KWA KILA JEMA NA KILA SEKUNDE ATUPAYE NA KILA ATUJALIALO.

Tuesday, October 14, 2008

KUMBUKUMBU YA MANENO ALIYOSEMA HAYATI BABA WA TAIFA JULIUS K. NYERERE

"Uongozi unaweza ukwa mzuriau mbaya, au usijali, lakini kama watu wameamka na wanajitambua wenyewe, kutoshirikishwa kwa mawaza na tabia ya jamii hakutaendelea kwa muda mrefu".

NYERERE:- BORA NINGEKUWA MHUBIRI WA DINI KULIKO KUWA RAIS WA NCHI!

Baadhi ya maneno ya hayati Mwalimu, alipofikisha umri wa miaka 50"..Wakati nikiwa Makerere, niligundua kwamba serikali ya nchi yangu ilikuwa ikinilipia kiasi cha paundi 80 kila mwaka kwa ajili ya elimu yangu. Lakini hio haikuwa na maana kubwa sana kwangu, isitoshe paundi 80 ni chembe ndogo tu ya kiasi cha jumnla ya pesa zinazokusanywa na kutoka kwa walipa kodi wa nchi yangu, yaani wa-Afrika. Leo hii, paundi 80 ziimeongezeka thamani yake na kuwa na maana kubwa kwangu. Siyo kwamba ni zawadi muhimu tu na tunu kwangu, lakini pia ni deni ambalo kamwe sitaweza kulilipa.""Sina uhakika kama wengi wetu wamepata kufikiria kwamba wakati paundi 80 zilikuwa zinatyumika kunitunza mimi kule Makerere, hela hizo zingeweza kujenga Zahanati angalau mbili katika kijiji changu au chochote kingine Tanzania."".. Inawezekana kabisa kuwa wananchi walikuwa wanakufa kwa ukosefu wa dawa kwa sababu tu ya kukosa paundi zile 80 zilizokuwa zikilipwa kwa ajili yangu. Kwa hiyo kuwapo kwangu chuoni kuliinyima jamii huduma ya wale wote ambao wangeweza kusomeshwa kwenye shule chini ya miti, na kuwaandaa kina Aggreys na Booker Washingtons, Je nitawezaje kamwe kutolilipa hilo deni kwa jamii yangu hii?.""Jamii inatumia fedha zote hizo kwa ajili yetu kwa sababu inataka tuwe nyenzo za kuiinua jamii hiyo. Kwa hiyo lazima siku zote tubakie chini ya jamii hiyo na kuhimili uzito wote wa wananchi ambao wanahitaji kuinuliwa, na lazima tusaidie kuifanya hiyo kazi ya kuwainua wananchi wasiojiweza"Wakati nikisoma matukio yaliyojiri kuelekea kifo cha Babu (Sokoro) kama tulivyozoea kumuita, machozi yamenidondoka sio tu kwa sababu ya kuondokewa na mtu muhimu kwangu na Taifa, bali pia kwa kukosa nafasi ya kutimiza nadhiri yangu ya kumpa shukrani japo ya ahsante kwa mema aliyonitendea mimi pamoja na mafanikio aliyonitabiria tarehe 2.1.1987. Pia nalia kwa sababu baada ya kuonana naye wakati alipotembelea maonesho ya Sabasaba mwaka 1999, sikumuona tena zaidi ya alipokuwa ndani ya jeneza pale Msasani na Butiama.Lakini nalia zaidi ninapokumbuka kuwa baada ya kifo chake, watu wengi wamikuwa victimized kwa sababu ya misimamo ya kiuadilifu. Wazalendo wamekuwa wakitemewa mate na kupewa majina ya huyo siyo MWENZETU (katika ufisadi) n.k. Waovu katika jamii wamepewa majina ya Huyo mjanja n.k. Nitaendelea......... machozi yamelowanisha Key Board mpaka imestark.