Showing posts with label pendeza. Show all posts
Showing posts with label pendeza. Show all posts

Thursday, November 28, 2013

MWANAMTINDO WA LEO NA MTOKO WA NYEUSI ....BLACK IS GOOD !!!!

 Hivi ndivyo lilivyokuwa vazi langu leo koti ndefu nyeusi na suruali vimenunuliwa UNIQUE,blauzi/line toka Vila clothes.
 Hapa mdada anaonekana kuwa mbali kweli kimawazo.....
 ....hapa anawaza sijui nibadili kazi na kuwa mwana mtindo....anaendelea kufikiri
Na mwisho inaonekana hajapata jibu bado kwa hiyo anaendelea kufikiri. Je wasomaji mnaonanaje  kuhusu hili na kuhusu vazi la leo?....NAWATAKIENI WOTE KAMA ILIVYO HAPO ULIPO IKIWA ASUBUHI, MCHANA, ALASIRI, JIONI AU USIKU..BINAFSI NI JIONI HAPA NA NAANZA KUJIANDAA KUPIKA MLO WA JIONI.

Wednesday, July 10, 2013

BAADA YA MASAA MATANO NA HUU NDIO MWANEKANO MPYA WA KAPULYA!!!

 Hapa ni kichwa kizima, picha imepigwa kwa juu kuonyesha mwonekano wote...masaa matano nimekaa bila kuinuka na matokeo ndio haya..
Na hapa ni kwa mbele...mnaona kapulya alivyochoka si mchezo lakini nimefurahi nimeweza kusukwa maana zile nilisuka mwezi februari:-)..Dada Natalie kutoka Kongo  ni mwepesi ajabu...Sijui hizi nitakaa nazo muda gani:-)
 
 
Haya nawatakieni jioni njema ..Panapo majaliwa tutaonana tena...Kapulya ndani ya poziiii:-)

Monday, February 4, 2013

SARESARE MAUA ASIYEJUA KUCHAGUA KABILA YAKE...au???

 Unaweza kushona shati pia kama kaka Kitururu alivyofanya si unaona kapendeza mwenyewe......
 .....na halafu kama kawaida unaweza kushona gauna kama uonavyo hapa  safi kabisa
aise na hapa pia unaona gauni..kitenge kimoja ila tofauti hasa rangi zake kinapendeza kwa kweli ....Jumatatu njema jamani.

Thursday, September 13, 2012

TUMALIZE SIKU HII KWA PICHA HIZI:- SARESARE MAUA ASIYEJUA KUCHAGUA ....!!!

 Sehemu fulani Jamaica
Je unamjua huyu?
Nimezipenda hizi picha na nimeona ziwe picha za wiki hii. Rangi za mavazi ni rangi ambazo nazipendaaaaaaaa sana. Hakika ukijipenda mwenyewe basi na wengine watakupenda!!

Na sasa ngoja tusikiliza kibao hiki ambacho kinawakilisha ujumbe murwaaaaaaaaaaaaaaaaa.




Tuesday, August 14, 2012

NIMELIPENDA GAUNI HILI JAMANI..!!

Mdada huyu kila nguo anayoivaa inamkaa utafikiri ndo ilitengenezwa kwa ajili yake..Ingekuwa hivi na kwa sisi wengine ingekuwa bambi kweli..Nimelipenda gauni hili jinsi lilivyo hakuna makolombwezo mengi, rangi nzuri na la heshima yaani ndefu.... Ngoja nitaichukua picha hii nikashone hivyo Je? unafikiri nitapendeza kama mdada huyu?

Wednesday, July 11, 2012

KWA VILE NI SIKU YA MARUDIO BASI TUANGALIA NA HAPA...HUYU NI DADA ESTER ULAYA SIJUI HILO NI SHAMBA LAKE TUJE KUCHUMA KISAMVU??!!!

Yaani hapa nimetamani hicho kisamvu halafu nimeangalia nimeona pia kama kuna mlenda pori vile. Najigamba sikuchukua mbegu za mihogo. Eti hata ule wa kutafuna tu hakuna. Safari ijayo ntajitahidi..LOL..  Ukitaka kufaidi mambo mengine afanyayo mdada huyu basi gonga hapa. Haya niwatakieni mwendelezo wa siku mwema...

Thursday, June 21, 2012

TUMALIZE SIKU HII KWA KUANGALIA:- UREMBO HUU WA KIASILI!!!

Hakuna kiti  nikipendacho kma hizi bangili ....Ebu angalia kwanza rangi zake zilivyokaa kaa ...Hivi ni waMasai tu ndio wanaoweza kutengeneza vitu hivi. Hakika kama ni wao tu nawapa hongera sana kwa kudumisha utamaduni hii mwanana. Ipo kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kutupa mikono pia ubunifu. Bado nasikitika bangili yanmgu ilikataka :-) Je wewe pia ni mdhaifu vya vitu kama hivi vya asili?

Tuesday, May 8, 2012

TUMEPUMZIKA SONGEA KIDOGO INATOSHA! SASA NAONA TUENDELEE NA SAFARI YETU !TUNAELEKEA KULE ALIKOZALIWA KAPULYA!!!

 Sio kwingine tena ni hapa:- katika  pichani ni moja ya fukwe bora katika ziwa Nyasa eneo la Lundo. Na ndio alikozaliwa mdada huyu. Ni sehemu nzuri sana kwa kutalii ukitembelea maeneo haya siku moja usikose kutembelea na hapa.
Pomonda jiwe la ajabu lililopo ziwa nyasa.
Hili ni jiwe la Pomonda, moja ya vivutio adimu vya utalii ziwa Nyasa ..Kuna mambo mengi katika nchi yetu ambaye ni mazuri na ya kuvutia ebuliangalia jiwe hili  halafu angalia huo ufukwe hapo juu. Mweee mpaka raha kweli. 

Thursday, May 3, 2012

MTU NA MAZINGIRA:- MAMBO AMBAYO NIYAPENDAYO KATIKA MSIMU HUU NI BUSTANI YA MAUA NA BUSTANI YA MBOGAMBOGA!!!

 Kwa hiyo mkiona sionekani hapa basi nipo nje naongea na maua yangu. maua haya leo nimeyapatia kulikuwa na jua kwa hiyo mchana yanachanua ikifika jiona/jua lizamapo nayo hufifia. Jina sijui ...nitatafuta nikijua nitawajuza....
 Hapa napo hili ua rangi zake nazipenda sana ila nalo jina sijui kwa kiswahili ila kiswidi ni (RÖDVIVA/GULLVIVA)
Na haya hapa nilipanda mwaka jana mwezi wa kumi na sasa yapo hivi ni yanaitwa(Tulpaner) mmmhh itabidi nijifunze kwa kiswahili...Bustani ya mboga bado sijaanza kwani bado ni baridi kweny udongo....Mija, Rachel, Edna Simon, Kaka S, aahh! na wengine wote nitawajuza itakapokaribia si mnakumbuka  huwa kuna ushirika wa kulima/chama  na baada ya kulima kupiga UGIMBI au mmesahau?...:-)...
.Halafu mwenzenu nina UDHAIFU SANA WA MAWE kuna mawe mengine ni kutoka TZ na sehemu mbalimbali niendako:-) JIONI NJEMA SANA JAMANI NGOJA MIE NIENDELEE kuongea NA MAUA YANGU......pia MAWE.....

IMETOKEA TU KWAMBA NAPENDA SANA MAMBO YA ASILI KAMA UTAMADUNI HUU!!


 Katika ukuaji wangu nimekuwa nikipenda sana kuva urembo uliotengenezwa kiasili  NAPENDA MNO juzi juzi tu tamaduni yangu ya mkononi imekatika nimelia kweli :-(....

....ni hapa chini kulia ila hicho kidani/cha shingoni bado ninacho...ila nitajitahidi kutengeneza au kutafuta mpya:-)

Thursday, April 12, 2012

PICHA YA WIKI HIII:-NYWELE


Baada ya wiki kadha mdada huyu kufikiria afanye nini na nywele zake, leo amepata msusi na sasa anajiandaa kwenda kusuka........

....baada ya masaa tisa anaonekana hivi...bahati mbaya msusi wangu hakutaka kuwa katika picha ni mdada kutoka Kongo....Nimesuka rasta (tena) ila si za wamasai ..hahahaha...Oh! halafu nimesahau kusema bei yake ni 500 kr. Maana nimesoma maoni ya Da´Mija ameuliza ni shiling ngani kusuka hivi?

Tuesday, March 27, 2012

RANGI NA UZURI WAKE!!!!!!!!!

Nimependa mchanganyiko huo wa rangi … kwa kutazama pia kuvaa … . ni ubunifu mzuri sana. Hivi hizi ni rangi za taifa fulani au ni kwamba imetokea tu mbunifu akabuni namna hiyo?
Pamoja Daima...

Thursday, March 15, 2012

NIMELIPENDA GAUNI HILI MNO....

.......ebu angalia hizo rangi na jinsi lilivyorembwa, nimelipenda mno . Swali sijui nami nitapendaza kama lilivyompendeza huyu dada?:-)

Thursday, August 25, 2011

PICHA ZA WIKI HII:- MAMA NA MWANA!!!


CAMILLA NA MAMA YAKE YASINTA (mwaka jana 2010 mwezi wa saba)




NA HAPA NI MALIA NA MAMA YAKE MICHELLE

Ni ujumbe tu mfupi ambao unaweza kukufanya utafakari kitu fulani....PAMOJA DAIMA!!!



Tuesday, January 25, 2011

UNAKUMBUKA MICHEZO KAMA HII?

Nimekumbuka michezo kama hii nilipokuwa mdogo, maana katika familia yetu watoto wa kiume ni wengi zaidi kwa hiyo tulikuwa hawanibagui katika michezo....haya wewe je uliwahi kusafiri na gari kama hili????:-) brrrrrrrrrrrrrrr kanyonyonyooooooo twendeeee....

Friday, December 3, 2010

PICHA YA WIKI HII:- MTINDO WA NYWELE!!!!

SIJUI ANAFANYA NINI?
Wiki hii tuangalie mtindo wa nywele. Ebu angalia wanadada hawa ni wanandugu au? labda marafiki? au labda imetokea tu kuwa hivyo? Maana wanafanana hadi jinsi ya kuweka nywele.
IJUMAA NJEMA WANDUGU!!!

Friday, November 26, 2010

Je umewahi kuona Maajabu haya hapa ni Njombe: Mwamba Wenye Ramani ya Afrika

Mwamba huu wenye ramani ya bara la Afrika unaitwa Lwivala, upo katika pori la hifadhi ya msitu Lwivala kijiji cha Igodivaha Wilaya ya Njombe, inaweza isiwe rahisi kuamini lakini huo ndio ukweli wenyewe. Picha kutoka Mjengwa.

Friday, July 16, 2010

HATIMAYE JANA NIMESUKWA TENA BAADA YA MIEZI SITA, KAAZI KWELIKWELI!!

Mtaka cha uvungoni sharti ainame

Masaa sita na nusu baadaye nilikuwa hivi. Kuchoka pia :-)
Ijumaa njema tutaonana wakati mwingine!!!!!!!


Sunday, August 23, 2009

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE

Kupenda kazi hurahisisha kazi

Si kwamba tuishi tu mahali, bali tuishi mahali pazuri. Kwa juhudi zetu tunaweza kupendezesha mahali pa kuishi, miji na vijiji vyetu.

Saturday, November 15, 2008

JE? HAPA NAPENDEZA?




Hapa mwenzenu nilikuwa Saudi Arabia, wanawake wote wanavaa hivi kazi kweli kweli