Mwenzenu leo nimejikuta kutamani kuandika historia hii ya wangoni kwa kingoni. Naogopa nitasahau lugha yangu ya asili. Haya someni kama mtaambua mawili -matatu nitafurahi.
Vangoni vitama kuSongea-Tanzania. kuZambia na kuMalawi. Kadeni vangoni avo vatamayi kuZululand. Myaka ya 1800 vakawuka kwenuko pamonga na vanduna na vankosi vavi na kuyingila kumulima uwu. Mulugendu lwavi ulo vakapita kutova ngondo nakutola vavanda vamahele na kuvakita vangoni ngita vene, muni vajovayi “mwana wa lihimba nga lihimba mewa”. Pakukomana ngondo, vangoni vanyagayi ngómbi, mene, mamberere, ngúku na kuwuka. Popoha pevatovayi ngondo vavatolayi vandu vavi na kuyonjekesa uvaha wa kabila lawu na kuyendelela kulingolo na kuyingila mavidunda venijovilivo. Vangoni vayingili kuTanzania kwa mabanja gadatu libanja la Vangoni va Zwangendaba, libanja la vangoni va Mputa Maseko na libanja la vangoni va Zulu Gama na Mbonane Tawete. Mabanja aga goha hata ngati galongosini lepi lukumbi lumonga pakuyingila kuTanzania, nambu gapitili mulamula mwe gipitili mabanja gangi na kutola vavanda. Nsava ya naha ukuvavona vangoni vahangasiniki na mahina gavi pamonga na vibongo na mahina vavanda wavi.
Vangoni va Zwengedaba
Zwangendaba au vakumkemela Zongendaba, amanyikini muni na vangoni na vazeyi voha va chingoni. Chibongo cha lukolo lwa Zongendaba chavi Nkosi au Tole. Vibongo voha ivo akavileka na kutola lihina la Jere. Dadi wa Zongedaba na wamkelayi Hlachwayo. Vijova ya kuvya Zongedaba ahumili kuTanzania. Vangoni va Zongendaba vevayingili kuTanzania, vakahamba kuUjiji ya kuTabaora na kutama kuKahama. Kwenuko vimanyikana kwa lihina la Vatuta. Zongendaba afwili kuMapupo (Chipata) –Ufipa mwaka 1858 na wamhilili kukwokwo. Hinu vandu veavayolili Zwangendaba kuyingila kuTanzania nde ava: Waswazi, Wandwandwe, Wathonga, Wakalanga, Wamashona, Wasenga, Wachewa Watumbuka, Wakamanga, Wasukuma.
Vangoni va kwaZulu Gama na va kwa Mbonane Tawete
Lukolo lwa kadeni sana kuyingila kuSongea lwavili lwa mwene Bambu Zulu Gama na Mbonane Tawete. Yiwonekana veneva vavi he pamonga na Zongedaba peayingilayi kuTanzania na kuhamba kuTabora. Zulu Gama na Mbonane vabwelili lukumbi lungi kuhuma kuzululand. Mbonane Tawete avi mwana wa Mshopi, mwana wa Kibovu mwana wa Kisara. Mulugendu lwavi kuhuma kuzululand, Mbonane na dadi waki Mshopi wakakonganeka kunyanja na vangoni wa kwaZulu. Kunyanja kula Zulu Gama na Mbonane wakatemana ukozi. Mbonane akampela Zulu mlumbu waki Ushambazi au wakumkemela Mafunasi (Nasere) kuvya inkosikazi waki. Mbonane Tawete avi mkozi wa Zulu. Pakuhuma kunyanja kula, voha vavili vakayingila pamonga kuTanzania. Ndava ya naha vandu va Zulu na va Zwangendaba vihwanana mahina na cibongo vyavi. Kuhuma kwa kunyanja uko, voha Mbonane na Zulu vakagenda pamonga na kutindila ngita vangoni va Zwangendaba naha, kuhuma kuSwaziland, vakapita kwa vatonga, kwa wakalanga, kwa wasenga na kwa wasukuma, wakavayonjakesa na wachewa. Vangoni va kwaZulu na va kwaMbonane vakonganiki he na vangoni ya Zwangendaba. Ila pevapitayi vazulu na va Mbonane vapilikayi kuvya mulamula apitili Zwangendaba. Zulu na Mbonane vakakupuka mfuleni wa Zambezi kwa mtahu sana ndava mfuleni uwu unyoliki na kutaluka na umemi mang´wina. Pakumala kukupuka, vandu vakam´bongelela na kumyimbila nyimbo Jeru muni avalangisi pahala pabwina pakukupuka. Pakuhuma kwenuku, vakalongolela na kuhika kuMalawi na kuZambia na kuyingila kuMalangali – Tanzania. Njeru dadi wa Zulu na Mshopi dadi wa Zongendaba vene wafwili kuZambia, vayingi he kuTanzania.
Showing posts with label peramiho. Show all posts
Showing posts with label peramiho. Show all posts
Monday, July 20, 2009
Friday, May 8, 2009
TUENDELEE KUANGALIE SURA YA KIJIJI CHA LIKUYU FUSI SEHEMU YA NNE= KUNYUMBA
Nimeona afadhali nimalizie kuhusu Likuyu Fusi leo.
Baada ya muda mateka hao walipewa ruhusa ya kuoana na kuzaa watoto. Watoto hao wote walikuwa mali ya Mtepa na waliitwa “Gama”. Wakati wote wa maisha yao walikuwa chini ya nyumba ya Mtepa hata baada ya kufa kwake. Kimila hawa wanaitwa “Gama wa Chikopa”. Mfano mwingine, yupo mzee Zawemba Gama, alipokufa aliacha mke Mzinati mwenye watoto wawili. Baada ya kuondoa tanga bibi Mzinati alipewa ruhusa ya kuolewa na mume mwingine. Akaolewa na Kajanja Komba. Kajanja hakutoa mahari ya kumwoa Mzinati badala yake alitoa mbuzi mmoja dume kwa ndugu wa Zawemba kuwaomba kuwa anataka kuishi na bibi Mzinati. Hivyo Kajanja aliruhusiwa kumchukua Mzinati kwa masharti kuwa watoto wote watakaozaliwa watakuwa mali ya “Gama”. Kajanja hakuwa na haki juu ya watoto, ingwa watoto hawa ilikuwa damu yake. Kutokana na tatizo hili, Kajanja Komba aliamua kuacha jina lake na badala yake akachukua jina Kajanja Gama ili awe na haki ya watoto aliowazaa na bibi Mzinati. Kimila hawa wanaitwa “Gama wa mali” Mfano wa tatu, mzee Yombayomba Nungu aliishi na Mtepa Gama kwa muda mrefu toka ujana wao. Kila ilipotokea shida walisaidiana kama ndugu kumbe ni marafiki tu. Wakati wa pombe watu walibonga “Yeo Gama” au “Yeo Nungu” Mzee Yombayomba aliona aliona jina Nungu halina heshima kama jina la Gama. Baada ya kufa Mtepa, Yombayomba Nungu aliingia nyumba ya Mtepa kwa makusudi ya kuwatunza watoto wa Mtepa. Hapakuwa na mtu aliyemzuia au kushangaa maana kila mmoja alifahamu uhusiano wa Mtepa na Yombayomba. Ili kuwaonyesha watu kuwa yeye Yombayomba hakuwa rafiki au jirani tu, bali alijifanya kuwa ndugu ya Mtepa, hivyo Yombayomba aliamua kuacha jina la “Nungu” na badala yake akajiita Yombayomba Gama. Kimila hawa wanaitwa “Gama wa Kugula”. Nduna Laurent alionya kuwa hakuna sababu ya kugombana na watu wa aina hiyo.
Iwapo mtu aliamua kujiita GAMA au TAWETE kwa manufaa yake ni bora kumwacha alivyo ingwa kama watu wengine wanajua yeye si Gama au Tawete. Alionya pia kuwa watu wa aina hiyo ni wabaya sana na ni lazima kuangalia katika kushirikiana nao. Mtu kama huyo huhesabiwa kama mgeni asiyeaminika maana anaweza kufanya kitendo kibaya kwa wenyeji ili yeye apate kutawala. Kufuatana na utaratibu wa Wangoni katika utawala wa jadi, Manduna na Majumbe wengi walitoka katika jamaa zenye asili ya Waswazi, Watonga, Wakalanga, Wasenga na Wasukuma. Manyapara walichaguliwa toka makabila mengine yaliyojulikana kwenye vita vya makabila. Hapa chini imeorodhesha ufafanuzi wa Nduna Laurenti kuhusu Wangoni wa Songea kwa ujumla.
Wangoni wenye asili ya WASWAZI: Gama, Tawete, Chongwe, Magagura, Mswani, Maseko, Nyumoyo, Tole, Jere, Mshanga, Masheula, Nkosi, Mlangeni na Malindisa.
Wangoni wenye asili ya WATONGA: Makukura, Silengi, Ntocheni, Sisa, Ntani, Ngairo, Nguo, Matinga, Nkuna, Gomo na Pili.
Wangoni wenye asili ya WAKALANGA: Mbano, Soko, Moyo, Zenda, Newa, Shonga, Shawa, Chiwambo, Hara, Mapara, Mteka na Nyati.
Wangoni wenye asili ya WASENGA: Miti, Mvula, Sakara, Lungu, Tembo, Njovu, Duwe, Nguruwe, Ngómbe, Mwanja na Mumba.
Wangoni wenye asili ya WASUKUMA: Chisi, Ntara, Mpepo, Satu, Zinyangu, Chawa na Mzila.
Wangoni wenye asili ya WANYAME: Nyanguru.
Wangoni wenye asili ya WANDENDEULE: Ngonyani, Mapunda, Ntini, Milinga, Nyoni, Henjewele, Ponera, Luhuwu, Nungu, Mango, Nyimbo, Humbaro, Kigombe, Wonde, Ndomba, Tindwa, Magingo na Luambano.
Wangoni wenye asili ya WAMATENGO: Nchimbi, Ndunguru, Komba, Nyoni, Kapinga, Kifaru, Pilika, Hyera, Mbele, Mkwera, Ndimbo, Mapunda, Ngongi, Mbunda, Kinyero, Nombo na Kumburu.
Wangoni wenye asili ya WAPANGWA: Mhagama, Kihwili, Nditi, Lugongo, Njombi, Mwingira, Kihaule, Mbawala, Njerekela, Komba, Kayombo, Mselewa, Nandumba, Luoga, Luena, Mbena, Mwagu, Mlimira, Sanga, Kokowo, Miloha, Kihuru, Chali, Mwinuka, Nyilili, Mkuwa, Mhonyo, Mkinga, Ngaponda, Goliama na Ng´wenya.
Baada ya muda mateka hao walipewa ruhusa ya kuoana na kuzaa watoto. Watoto hao wote walikuwa mali ya Mtepa na waliitwa “Gama”. Wakati wote wa maisha yao walikuwa chini ya nyumba ya Mtepa hata baada ya kufa kwake. Kimila hawa wanaitwa “Gama wa Chikopa”. Mfano mwingine, yupo mzee Zawemba Gama, alipokufa aliacha mke Mzinati mwenye watoto wawili. Baada ya kuondoa tanga bibi Mzinati alipewa ruhusa ya kuolewa na mume mwingine. Akaolewa na Kajanja Komba. Kajanja hakutoa mahari ya kumwoa Mzinati badala yake alitoa mbuzi mmoja dume kwa ndugu wa Zawemba kuwaomba kuwa anataka kuishi na bibi Mzinati. Hivyo Kajanja aliruhusiwa kumchukua Mzinati kwa masharti kuwa watoto wote watakaozaliwa watakuwa mali ya “Gama”. Kajanja hakuwa na haki juu ya watoto, ingwa watoto hawa ilikuwa damu yake. Kutokana na tatizo hili, Kajanja Komba aliamua kuacha jina lake na badala yake akachukua jina Kajanja Gama ili awe na haki ya watoto aliowazaa na bibi Mzinati. Kimila hawa wanaitwa “Gama wa mali” Mfano wa tatu, mzee Yombayomba Nungu aliishi na Mtepa Gama kwa muda mrefu toka ujana wao. Kila ilipotokea shida walisaidiana kama ndugu kumbe ni marafiki tu. Wakati wa pombe watu walibonga “Yeo Gama” au “Yeo Nungu” Mzee Yombayomba aliona aliona jina Nungu halina heshima kama jina la Gama. Baada ya kufa Mtepa, Yombayomba Nungu aliingia nyumba ya Mtepa kwa makusudi ya kuwatunza watoto wa Mtepa. Hapakuwa na mtu aliyemzuia au kushangaa maana kila mmoja alifahamu uhusiano wa Mtepa na Yombayomba. Ili kuwaonyesha watu kuwa yeye Yombayomba hakuwa rafiki au jirani tu, bali alijifanya kuwa ndugu ya Mtepa, hivyo Yombayomba aliamua kuacha jina la “Nungu” na badala yake akajiita Yombayomba Gama. Kimila hawa wanaitwa “Gama wa Kugula”. Nduna Laurent alionya kuwa hakuna sababu ya kugombana na watu wa aina hiyo.
Iwapo mtu aliamua kujiita GAMA au TAWETE kwa manufaa yake ni bora kumwacha alivyo ingwa kama watu wengine wanajua yeye si Gama au Tawete. Alionya pia kuwa watu wa aina hiyo ni wabaya sana na ni lazima kuangalia katika kushirikiana nao. Mtu kama huyo huhesabiwa kama mgeni asiyeaminika maana anaweza kufanya kitendo kibaya kwa wenyeji ili yeye apate kutawala. Kufuatana na utaratibu wa Wangoni katika utawala wa jadi, Manduna na Majumbe wengi walitoka katika jamaa zenye asili ya Waswazi, Watonga, Wakalanga, Wasenga na Wasukuma. Manyapara walichaguliwa toka makabila mengine yaliyojulikana kwenye vita vya makabila. Hapa chini imeorodhesha ufafanuzi wa Nduna Laurenti kuhusu Wangoni wa Songea kwa ujumla.
Wangoni wenye asili ya WASWAZI: Gama, Tawete, Chongwe, Magagura, Mswani, Maseko, Nyumoyo, Tole, Jere, Mshanga, Masheula, Nkosi, Mlangeni na Malindisa.
Wangoni wenye asili ya WATONGA: Makukura, Silengi, Ntocheni, Sisa, Ntani, Ngairo, Nguo, Matinga, Nkuna, Gomo na Pili.
Wangoni wenye asili ya WAKALANGA: Mbano, Soko, Moyo, Zenda, Newa, Shonga, Shawa, Chiwambo, Hara, Mapara, Mteka na Nyati.
Wangoni wenye asili ya WASENGA: Miti, Mvula, Sakara, Lungu, Tembo, Njovu, Duwe, Nguruwe, Ngómbe, Mwanja na Mumba.
Wangoni wenye asili ya WASUKUMA: Chisi, Ntara, Mpepo, Satu, Zinyangu, Chawa na Mzila.
Wangoni wenye asili ya WANYAME: Nyanguru.
Wangoni wenye asili ya WANDENDEULE: Ngonyani, Mapunda, Ntini, Milinga, Nyoni, Henjewele, Ponera, Luhuwu, Nungu, Mango, Nyimbo, Humbaro, Kigombe, Wonde, Ndomba, Tindwa, Magingo na Luambano.
Wangoni wenye asili ya WAMATENGO: Nchimbi, Ndunguru, Komba, Nyoni, Kapinga, Kifaru, Pilika, Hyera, Mbele, Mkwera, Ndimbo, Mapunda, Ngongi, Mbunda, Kinyero, Nombo na Kumburu.
Wangoni wenye asili ya WAPANGWA: Mhagama, Kihwili, Nditi, Lugongo, Njombi, Mwingira, Kihaule, Mbawala, Njerekela, Komba, Kayombo, Mselewa, Nandumba, Luoga, Luena, Mbena, Mwagu, Mlimira, Sanga, Kokowo, Miloha, Kihuru, Chali, Mwinuka, Nyilili, Mkuwa, Mhonyo, Mkinga, Ngaponda, Goliama na Ng´wenya.
Wednesday, May 6, 2009
TUENDELEE KUANGALIE SURA YA KIJIJI CHA LIKUYU FUSI SEHEMU YATATU = KUNYUMBA
Inaendelea toka sehemu ya kwanza ya Kijiji cha Likuyu Fusi.
Mazao haya yote ni kwa ajili ya chakula chao na kuuza ziada. Baadhi ya wananchi wanalima tumbaku, kwa ajili ya kupata fedha kidogo za matumizi. Wakati wa kiangazi wananchi hulima mboga za aina mbalimbali, kama mchicha, mabogo, nyanya, lipwani, bamia na siku za karibuni wameingiza aina ya mboga za kigeni kama kabeji, saladi, biringanya na aina nyingine. Kwa ujumla kilimo cha mvua za mwaka huwa katika sehemu zalizoinuka na wakati wa kiangazi wananchi hulima mabondeni. Hivyo shughuli za kilimo ni za wakati wote katika mwaka. Mvua za mwaka huanza mwezi Novemba na kumalizika mwezi mei.
Kilimo kimekuwa kwa miaka mingi cha mtu mmoja mmoja au mtu na jamii yake wakishirikiana na jirani wa karibu katika kilimo cha bega kwa bega au “Chama”. Mapato na hali ya maisha ya wakazi kwa ujumla si ya kuridhisha sana. Ingawaje wananchi wanapata chakula kwa wingi cha kuwashibisha lakini kuna uhaba wa vyakula vya aina ya nyama ambayo ni muhimu kujenga miili ya binadamu hasa akina mama wajawazito, watoto na vijana. Vyakula aina ya nyama, samaki, mayai, dagaa, kunde, maharagwe na maziwa ndivyo vinavyojenga miili yetu. Ili watu wajengeke vema kiafya kuna haja ya kuwapa akina mama wajawazito, watoto na vijana vyakula vya aina nilivyotaja kwa wingi.
Kabla ya vita kuu ya pili, wananchi walikuwa na mifugo ya aina mbalimbali, kama ngómbe, mbuzi, kondoo, kuku, njiwa, na bata. Na kwenye mapori kulikuwa na wanyama wa aina mbalimbali kama funo, tambaramba, nguruwe, ngungusi, kwale, kanga, nyani, ngedere, chui na simba na wengineo. Wanyama hawa walikuwa wakiwindwa kwa nyavu, mitego na pengine kwa bunduki za migobole. Hivyo kutokana na mifugo na wanyama wa porini, wananchi waliweza kula nyama mara kwa mara wakati walipotaka. Hivi sasa ufugaji wa wanyama umepungua sana na kadhalika idadi ya wanyama wa porini. Hali hii inaleta shida kubwa ya kupata nyama huko vijijini.
Watu wachache wanofuga wantama hao ni kwa ajili ya posa, misiba, harusi au wakati mwingine kwa ajili ya kuwapata watu kuwalimia mashamba yao ya binafsi. Ufugaji wa kuku na bata nao ni wa kijadi. Kuku huzurura ovyo mashambani wakitafuta panzi, kupelkua mchwa na kutafuta chembe za nafaka mashambani. Hali hiyo hiyo ipo kwenye ufugaji wa bata.
Watu wachache hufuga nguruwe nao pia ni kiasi kidogo sana na matumizi yake makubwa ni kuwalipa watu wanolima wakati wa masika. Kuna uwezekano wa kuongeza ufugaji huu kwani chakula cha nguruwe si vigumu kupatikana.
Kijiji cha Likuyu Fusi kina mafundi wachache wa useremala wenye mashine za kuranda, kupasua mbao, kutengeneza milango, madirisha, meza, viti na madawati nk. Mafundi hawa ambaohupata msaada wa mara kwa mara toka misheni, hufanya kazi zao binafsi ingawaje huwaajiri vijana wa kuwafunza kazi. Siku hizi karibu kila kijiji kilichoandikishwa kimekopeshwa na Benki ya maendeleo vijijini, mashine za kusaga na kukoboa nafaka, matrekta ya kulimia na malori. Hata hivyo ni watu wachache wenye kuzingatia kazi za kilimo, kwani idadi kubwa ya wakazi wa sehemu hizi hutegemea kazi za kuajiriwa na misheni au mahali pengine katika mashirika na Serikali. Katika vijiji nilivyovitaja wapo pia mafundi wa uhunzi wenye kutengeneza mashoka, mikuki, visu, nyengo,vinu n.k. Vitu hivi hutengenezwa kwa kiasi kidogo sana ili kupata fedha za kununua mahitaji na kulipa gharama mbalimbali za maisha. Katika kila kijiji kilichoandikishwa na vile vya asili zimefunguliwa shule moja kutegemea idadi ya watoto walioko. Zaidi ya hayo zipo huduma za madhehebu mbalimbali ya dini katka kila kijiji. Ingawa bado watu wengi hutegemea masoko yaliyoko katika vituo vya misheni, siku hizi kila kijiji kimeanzisha shughuli za soko kama vile uuzaji wa pombe na vyakula, na mazao mbalimbali toka mashambani kwao. Hata hivyo serikali za vijiji zinatakiwa kufanya jitihada kubwa kupunguza tatizo la wizi wa mali za vijiji ambao hutokana na kuwa na majengo hafifu ya kutunzia mali hizo, pamoja na utunzaji mbaya wa mahesabu yake. Wengi wa viongozi wa vijiji hawana ujuzi wa shughuli hizo, na hawapo tayari kutoa nafasi kwa wale wenye uwezo. Hilo ni tatizo la kudumu katika baadhi ya vijiji na limesababisha vijiji hivyo kushindwa kuendelea. Bado ipo haja ya kuwa na msukumo mkubwa sana wa kuwaelimisha wakazi kuhusu uendeshaji wa shughuli za kijiji katika upande wa uchumi.
Jengo la Mahakama lililojengwa wakati wa Nduna Laurent akiwa mtawala wa jadi, bado linaendea kutumika kama mahakama na ofisi ya Mahakama ya Mwanzo.
Wakazi wa vijiji nilivyotaja wanahudumiwa na hospitali kubwa ya Peramiho na Songea. Hata hivyo katika kila kijiji lipo sanduku la huduma ya kwanza ambayo huangaliwa na Serikali ya Kijiji. Zipo barabara kubwa zinazopita katika maeneo ya baadhi ya vijiji lakini hali ya vijiji hivyo bado havijafikia hatua ya kujitegemea katika huduma za usafiri kwa wakazi wake. Malori ya mikopo na matrekta hutumika kwa muda mfupi kutokana na kuharibika mara kwa mara kwa kukosa uangalizi mzuri.
Kama nilivyoeleza hapo juu kuwa eneo la Likuyu Fusi limebahatika kuwa na mito ya kudumu kwa hiyo hakuna tatizo la kukosa maji. Hata hivyo kwa msaada wa Serikali na Misheni baadhi ya vijiji vimepelekewa maji kwa mabomba. Mipango hiyo inaendelea katika vijiji vilivyobaki.
Wakazi wa Likuyu Fusi ni Wangoni wenye asili mbalimbali. Nduna Laurent alikuwa mjuzi wa kupambanua asili zao. Alikuwa anasimulia kuwa siyo kila mtu ni Mngoni wa asili. Watu wengine wanaitwa Wangoni kwa sababu zao mbalimbali. Mathalani, yapo makabila yaliyokuwepo katika nchi hii kabla ya Wangoni wageni hawajaingia Wilaya ya Songea. Makabila hayo ni Wandendeule, Wamatengo,Wamwera,Wahyao, Wamatumbi na Wapangwa, Baadhi ya watu toka katika makabila haya walipewa Ungoni kwa ajili ya kutekwa katika vita vya makabila, na wengine kwa ajili ya kuzaliwa katika mali ya mtu, na wengine walinunua kabila. Mathalani, Mtepa Gama alipokuwa vitani aliteka watumwa wanne, wawili wanawake na wawili wanaume, Hawa wote kila mmoja wao alikuwa na jina lake la ukoo, kama Komba, Hyera, Ngonyani, Kihaule n.k. Watumwa hawa baada ya kutekwa waliruhusiwa kuendelea kutumia majina yao au walitaka waweze kutumia jina la mtu aliyewateka. Ili kulinda usalama wao watumwa hao waliamua kutumia jina la ukoo wa Mtepa ambaye aliwateka na hivyo walijulikana kuwa ni watu wa Mtepa. ITAENDELEA.......
Mazao haya yote ni kwa ajili ya chakula chao na kuuza ziada. Baadhi ya wananchi wanalima tumbaku, kwa ajili ya kupata fedha kidogo za matumizi. Wakati wa kiangazi wananchi hulima mboga za aina mbalimbali, kama mchicha, mabogo, nyanya, lipwani, bamia na siku za karibuni wameingiza aina ya mboga za kigeni kama kabeji, saladi, biringanya na aina nyingine. Kwa ujumla kilimo cha mvua za mwaka huwa katika sehemu zalizoinuka na wakati wa kiangazi wananchi hulima mabondeni. Hivyo shughuli za kilimo ni za wakati wote katika mwaka. Mvua za mwaka huanza mwezi Novemba na kumalizika mwezi mei.
Kilimo kimekuwa kwa miaka mingi cha mtu mmoja mmoja au mtu na jamii yake wakishirikiana na jirani wa karibu katika kilimo cha bega kwa bega au “Chama”. Mapato na hali ya maisha ya wakazi kwa ujumla si ya kuridhisha sana. Ingawaje wananchi wanapata chakula kwa wingi cha kuwashibisha lakini kuna uhaba wa vyakula vya aina ya nyama ambayo ni muhimu kujenga miili ya binadamu hasa akina mama wajawazito, watoto na vijana. Vyakula aina ya nyama, samaki, mayai, dagaa, kunde, maharagwe na maziwa ndivyo vinavyojenga miili yetu. Ili watu wajengeke vema kiafya kuna haja ya kuwapa akina mama wajawazito, watoto na vijana vyakula vya aina nilivyotaja kwa wingi.
Kabla ya vita kuu ya pili, wananchi walikuwa na mifugo ya aina mbalimbali, kama ngómbe, mbuzi, kondoo, kuku, njiwa, na bata. Na kwenye mapori kulikuwa na wanyama wa aina mbalimbali kama funo, tambaramba, nguruwe, ngungusi, kwale, kanga, nyani, ngedere, chui na simba na wengineo. Wanyama hawa walikuwa wakiwindwa kwa nyavu, mitego na pengine kwa bunduki za migobole. Hivyo kutokana na mifugo na wanyama wa porini, wananchi waliweza kula nyama mara kwa mara wakati walipotaka. Hivi sasa ufugaji wa wanyama umepungua sana na kadhalika idadi ya wanyama wa porini. Hali hii inaleta shida kubwa ya kupata nyama huko vijijini.
Watu wachache wanofuga wantama hao ni kwa ajili ya posa, misiba, harusi au wakati mwingine kwa ajili ya kuwapata watu kuwalimia mashamba yao ya binafsi. Ufugaji wa kuku na bata nao ni wa kijadi. Kuku huzurura ovyo mashambani wakitafuta panzi, kupelkua mchwa na kutafuta chembe za nafaka mashambani. Hali hiyo hiyo ipo kwenye ufugaji wa bata.
Watu wachache hufuga nguruwe nao pia ni kiasi kidogo sana na matumizi yake makubwa ni kuwalipa watu wanolima wakati wa masika. Kuna uwezekano wa kuongeza ufugaji huu kwani chakula cha nguruwe si vigumu kupatikana.
Kijiji cha Likuyu Fusi kina mafundi wachache wa useremala wenye mashine za kuranda, kupasua mbao, kutengeneza milango, madirisha, meza, viti na madawati nk. Mafundi hawa ambaohupata msaada wa mara kwa mara toka misheni, hufanya kazi zao binafsi ingawaje huwaajiri vijana wa kuwafunza kazi. Siku hizi karibu kila kijiji kilichoandikishwa kimekopeshwa na Benki ya maendeleo vijijini, mashine za kusaga na kukoboa nafaka, matrekta ya kulimia na malori. Hata hivyo ni watu wachache wenye kuzingatia kazi za kilimo, kwani idadi kubwa ya wakazi wa sehemu hizi hutegemea kazi za kuajiriwa na misheni au mahali pengine katika mashirika na Serikali. Katika vijiji nilivyovitaja wapo pia mafundi wa uhunzi wenye kutengeneza mashoka, mikuki, visu, nyengo,vinu n.k. Vitu hivi hutengenezwa kwa kiasi kidogo sana ili kupata fedha za kununua mahitaji na kulipa gharama mbalimbali za maisha. Katika kila kijiji kilichoandikishwa na vile vya asili zimefunguliwa shule moja kutegemea idadi ya watoto walioko. Zaidi ya hayo zipo huduma za madhehebu mbalimbali ya dini katka kila kijiji. Ingawa bado watu wengi hutegemea masoko yaliyoko katika vituo vya misheni, siku hizi kila kijiji kimeanzisha shughuli za soko kama vile uuzaji wa pombe na vyakula, na mazao mbalimbali toka mashambani kwao. Hata hivyo serikali za vijiji zinatakiwa kufanya jitihada kubwa kupunguza tatizo la wizi wa mali za vijiji ambao hutokana na kuwa na majengo hafifu ya kutunzia mali hizo, pamoja na utunzaji mbaya wa mahesabu yake. Wengi wa viongozi wa vijiji hawana ujuzi wa shughuli hizo, na hawapo tayari kutoa nafasi kwa wale wenye uwezo. Hilo ni tatizo la kudumu katika baadhi ya vijiji na limesababisha vijiji hivyo kushindwa kuendelea. Bado ipo haja ya kuwa na msukumo mkubwa sana wa kuwaelimisha wakazi kuhusu uendeshaji wa shughuli za kijiji katika upande wa uchumi.
Jengo la Mahakama lililojengwa wakati wa Nduna Laurent akiwa mtawala wa jadi, bado linaendea kutumika kama mahakama na ofisi ya Mahakama ya Mwanzo.
Wakazi wa vijiji nilivyotaja wanahudumiwa na hospitali kubwa ya Peramiho na Songea. Hata hivyo katika kila kijiji lipo sanduku la huduma ya kwanza ambayo huangaliwa na Serikali ya Kijiji. Zipo barabara kubwa zinazopita katika maeneo ya baadhi ya vijiji lakini hali ya vijiji hivyo bado havijafikia hatua ya kujitegemea katika huduma za usafiri kwa wakazi wake. Malori ya mikopo na matrekta hutumika kwa muda mfupi kutokana na kuharibika mara kwa mara kwa kukosa uangalizi mzuri.
Kama nilivyoeleza hapo juu kuwa eneo la Likuyu Fusi limebahatika kuwa na mito ya kudumu kwa hiyo hakuna tatizo la kukosa maji. Hata hivyo kwa msaada wa Serikali na Misheni baadhi ya vijiji vimepelekewa maji kwa mabomba. Mipango hiyo inaendelea katika vijiji vilivyobaki.
Wakazi wa Likuyu Fusi ni Wangoni wenye asili mbalimbali. Nduna Laurent alikuwa mjuzi wa kupambanua asili zao. Alikuwa anasimulia kuwa siyo kila mtu ni Mngoni wa asili. Watu wengine wanaitwa Wangoni kwa sababu zao mbalimbali. Mathalani, yapo makabila yaliyokuwepo katika nchi hii kabla ya Wangoni wageni hawajaingia Wilaya ya Songea. Makabila hayo ni Wandendeule, Wamatengo,Wamwera,Wahyao, Wamatumbi na Wapangwa, Baadhi ya watu toka katika makabila haya walipewa Ungoni kwa ajili ya kutekwa katika vita vya makabila, na wengine kwa ajili ya kuzaliwa katika mali ya mtu, na wengine walinunua kabila. Mathalani, Mtepa Gama alipokuwa vitani aliteka watumwa wanne, wawili wanawake na wawili wanaume, Hawa wote kila mmoja wao alikuwa na jina lake la ukoo, kama Komba, Hyera, Ngonyani, Kihaule n.k. Watumwa hawa baada ya kutekwa waliruhusiwa kuendelea kutumia majina yao au walitaka waweze kutumia jina la mtu aliyewateka. Ili kulinda usalama wao watumwa hao waliamua kutumia jina la ukoo wa Mtepa ambaye aliwateka na hivyo walijulikana kuwa ni watu wa Mtepa. ITAENDELEA.......
lebo:
afrika,
historia,
Kumbukumbu,
likuyu fusi,
peramiho
Tuesday, May 5, 2009
NGOJA LEO NIWAPELEKE NA TUANGALIE SURA YA KIJIJI CHA LIKUYU FUSI SEHEMU YA KWANZA= KUNYUMBA
Kijiji cha Likuyu Fusi ni kijiji cha asili cha muda mrefu kilichoanzishwa na kundi la Wangoni wa Luyangweni ya malawi miaka michache baada ya vita vya Majimaji. Kabla ya kuanzisha kijiji hiki wakazi wake waliishi katika eneo la kijiji cha Kilawalawa-Luyangweni ya Mpitimbi, mahali ambapo Bambo Fusi, bin Zulu alihamia na kundi lake toka Malawi.
Kijiji cha Likuyu Fusi kipo upande wa kusini wa kanisa la Misheni Peramiho, umbali wa maili tatu na kipo kusini ya mji wa Songea umbali wa maili kumi na tatu kuelekea barabara iendayo Mbambabay.
Jina la Likuyi Fusi linatokana na mti uitwao “mkuyu” ambao unapendelea kuota katika bonde la mto Likuyu. Tunda la mti huo huitwa “Likuyu” na hupendwa sana kuliwa na baadhi ya ndege. Mto Likuyu unaanzia mlima wa Liwanganjahi na kupeleka maji yake hadi mto Ruwawazi. Urefu wake ni maili nne. Kabla ya kuvuka mto huu katika barabara itokayo Songea kuelekea Mbambabay ulikuwepo mti mkubwa wa mkuyu wenye kivuli kizuri chini yake. Wasafiri wengi walizoea kupumzika na kupika chakula chao chini ya mti huo. Kituo hiki kilikuwa kikubwa na kilijulikana kwa wasafiri wengi waliokitumia. Wasafiri hao walipita mahali hapo “Likuyu” kutokana na matunda ya mti wake. Toka muda huo jina la Likuyu limeendelea kutumika hadi sasa.
Jina la Fusi ni jina la baba mzazi wa Nduna Laurent. Kwa kuwa mto wa Likuyu ulikuwepo katika eneo la utawala wake, wasafiri waliamua kuita mto huo Likuyu Fusi kutofautisha na Likuyu nyingine iliyoko katika sehemu ya Undendeule, katika wilwya ya Songea, ambayo ilitawaliwa na Nduna Sekamaganga.
Kijiji cha Likuyu Fusi kimekuwa ni makao makuu ya utawala wa Nduna Laurent Fusi. Makao haya kwanza yalikuwa kijiji cha Luyangweni ya Mpitimbi na hatimaye yalihamishiwa Likuyu miaka michache baada ya vita vya majimaji.
Utawala wa Nduna Laurent Fusi ulijumlisha wakazi wa vijiji vya asili ya Parangu, Lihongo, Likuyu, Mkurumo, Ruwawazi, Mangúa, Chimbembe, Mlahimonga, Liboma, Mbatamira, Mapera, Litapwasi, Halali Magomera, Halali Fusi, Mhangazi, Matomondo, Kikole na Kilawalawa.
Kijiji cha Likuyu Fusi kina milima miwili na yote ipo upande wa kusini ya kijiji. Mlima Livánganjali upo karibu zaidi na nyuma yake unafuata mlima wa Namakinga. Pia katika eneo la kijiji ipo mito; Lihongo, Likuyu, Litapwasi, Chimbembe, Liboma, Mhangazi, Ruwawazi na Ruvuma. Mito hiyo ina mabonde mazuri kando yake yenye maji ya kutosha kwa wakati wote wa mwaka. Ardhi yake ni kidongo chekundu katika sehemu kubwa na mabonde yake yana udongo wa aina ya mfinyanzi wenye rutuba nzuri. Vilevile vya milima vina mawe mazuri yenye kuzuia mmongónyoko wa ardhi.
Katika maeneo ya vijiji nilivyovitaja ipo miti ya aina mbalimbali, kama miyombo, misuku, miwanga na aina nyingine ya miti midogo midogo. Kwa vile maeneo haya yalikaliwa na watu kwa muda mrefu sehemu nyingi zilizolimwa zamani sasa zimeota manyasi marefu na vichaka vya miti midogo midogo. Mitelemko ya milima na kando kando ya mabonde ya mito bado kuna miti mikubwa kiasi ya aina niliyoitaja hapo juu. Kabla ya matumizi ya mbolea ya chumvichumvi kuenezwa wananchi walikuwa wanafanya kilimo cha kuhamahama wakikata “matema” kila baada ya miaka mitatu au minne. Tabia hii imesababisha kupungua kwa miti katika sehemu zote za tambarare na kuwalazimu wananchi kuanzisha mashamba mapya kwenye mitemko ya milima na hata kwenye vilele vya milima. Mabonde ya mito iliyotajwa hapo juu ina sehemu nzuri ya kilimo cha kiangazi “madimba”. Manyasi, magugu na matete na mimea ya asili ambayo sehemu nyingi hufyekwa wakati wa kiangazi ili kulima mashamba ya madimba.
Wananchi katika sehemu za vijiji nilivyovitaja hulima mahindi, maharagwe,ulezi, mtama, mihogo, viazi vitamu, viazi vikuu mpunga na aina mbali mbali za kunde, kama mbaazi, nandala, fiwi, mangatungu, pia hulima karanga, ufuta, mazomba, aina mbalimbali za matunda kama mapapai, mapera na miembe.Inaendelea........
Kijiji cha Likuyu Fusi kipo upande wa kusini wa kanisa la Misheni Peramiho, umbali wa maili tatu na kipo kusini ya mji wa Songea umbali wa maili kumi na tatu kuelekea barabara iendayo Mbambabay.
Jina la Likuyi Fusi linatokana na mti uitwao “mkuyu” ambao unapendelea kuota katika bonde la mto Likuyu. Tunda la mti huo huitwa “Likuyu” na hupendwa sana kuliwa na baadhi ya ndege. Mto Likuyu unaanzia mlima wa Liwanganjahi na kupeleka maji yake hadi mto Ruwawazi. Urefu wake ni maili nne. Kabla ya kuvuka mto huu katika barabara itokayo Songea kuelekea Mbambabay ulikuwepo mti mkubwa wa mkuyu wenye kivuli kizuri chini yake. Wasafiri wengi walizoea kupumzika na kupika chakula chao chini ya mti huo. Kituo hiki kilikuwa kikubwa na kilijulikana kwa wasafiri wengi waliokitumia. Wasafiri hao walipita mahali hapo “Likuyu” kutokana na matunda ya mti wake. Toka muda huo jina la Likuyu limeendelea kutumika hadi sasa.
Jina la Fusi ni jina la baba mzazi wa Nduna Laurent. Kwa kuwa mto wa Likuyu ulikuwepo katika eneo la utawala wake, wasafiri waliamua kuita mto huo Likuyu Fusi kutofautisha na Likuyu nyingine iliyoko katika sehemu ya Undendeule, katika wilwya ya Songea, ambayo ilitawaliwa na Nduna Sekamaganga.
Kijiji cha Likuyu Fusi kimekuwa ni makao makuu ya utawala wa Nduna Laurent Fusi. Makao haya kwanza yalikuwa kijiji cha Luyangweni ya Mpitimbi na hatimaye yalihamishiwa Likuyu miaka michache baada ya vita vya majimaji.
Utawala wa Nduna Laurent Fusi ulijumlisha wakazi wa vijiji vya asili ya Parangu, Lihongo, Likuyu, Mkurumo, Ruwawazi, Mangúa, Chimbembe, Mlahimonga, Liboma, Mbatamira, Mapera, Litapwasi, Halali Magomera, Halali Fusi, Mhangazi, Matomondo, Kikole na Kilawalawa.
Kijiji cha Likuyu Fusi kina milima miwili na yote ipo upande wa kusini ya kijiji. Mlima Livánganjali upo karibu zaidi na nyuma yake unafuata mlima wa Namakinga. Pia katika eneo la kijiji ipo mito; Lihongo, Likuyu, Litapwasi, Chimbembe, Liboma, Mhangazi, Ruwawazi na Ruvuma. Mito hiyo ina mabonde mazuri kando yake yenye maji ya kutosha kwa wakati wote wa mwaka. Ardhi yake ni kidongo chekundu katika sehemu kubwa na mabonde yake yana udongo wa aina ya mfinyanzi wenye rutuba nzuri. Vilevile vya milima vina mawe mazuri yenye kuzuia mmongónyoko wa ardhi.
Katika maeneo ya vijiji nilivyovitaja ipo miti ya aina mbalimbali, kama miyombo, misuku, miwanga na aina nyingine ya miti midogo midogo. Kwa vile maeneo haya yalikaliwa na watu kwa muda mrefu sehemu nyingi zilizolimwa zamani sasa zimeota manyasi marefu na vichaka vya miti midogo midogo. Mitelemko ya milima na kando kando ya mabonde ya mito bado kuna miti mikubwa kiasi ya aina niliyoitaja hapo juu. Kabla ya matumizi ya mbolea ya chumvichumvi kuenezwa wananchi walikuwa wanafanya kilimo cha kuhamahama wakikata “matema” kila baada ya miaka mitatu au minne. Tabia hii imesababisha kupungua kwa miti katika sehemu zote za tambarare na kuwalazimu wananchi kuanzisha mashamba mapya kwenye mitemko ya milima na hata kwenye vilele vya milima. Mabonde ya mito iliyotajwa hapo juu ina sehemu nzuri ya kilimo cha kiangazi “madimba”. Manyasi, magugu na matete na mimea ya asili ambayo sehemu nyingi hufyekwa wakati wa kiangazi ili kulima mashamba ya madimba.
Wananchi katika sehemu za vijiji nilivyovitaja hulima mahindi, maharagwe,ulezi, mtama, mihogo, viazi vitamu, viazi vikuu mpunga na aina mbali mbali za kunde, kama mbaazi, nandala, fiwi, mangatungu, pia hulima karanga, ufuta, mazomba, aina mbalimbali za matunda kama mapapai, mapera na miembe.Inaendelea........
lebo:
kijiji,
Kumbukumbu,
likuyu fusi,
nyumbani,
peramiho,
tanzania
Saturday, December 27, 2008
BLOG MAISHA SAFARINI = YASINTA
Blog Maisha, nimeona ni vema niage sitakuwa hewani kwa muda kidogo NASAFIRI. Nakwenda Peramiho, nakwenda ungonini. Nakwenda kula likolo la nanyungu na malombi (mahindi ya kuchoma) Wangoni wote myumwike?
Walongo Vangu!!!!
Tutaonana karibuni tena. KWA HERINI KWA MUDA. NAWATAKIENI WOOOOTEEE MWAKA MPYA 2009.
Friday, November 28, 2008
BOOKSHOP PERAMIHO
Sunday, November 23, 2008
MDUNDUWALO/PERAMIHO 2005
Sunday, August 17, 2008
AGOSTI 17, 2008 KUMBUKUMBU,KUTOWEKA KWA MAMA YANGU
Mpaka leo ni miaka minne (4) imepita tangu mama yangu mpendwa Alana magnus Ngonyani aiage dunia hii. Ila kwa mimi inaonekana kama ilikuwa jana tu. Napenda kukuombea mama kwa sara hii:-Salamu, Maria, umejaa neema,
Bwana yu nawe,
umebarikiwakuliko wanawake wote,
Na Yesu, mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Maria mtakatifu, Mama wa Mungu,
Utuombee sisi wakosefu,
Sasa na saa ya kufa kwetu,
Amina.
Marehemu astarehe kwa amani, Amina.
Subscribe to:
Posts (Atom)



