Showing posts with label tangazo. Show all posts
Showing posts with label tangazo. Show all posts

Monday, July 14, 2014

TUANZE JUMATATU HII NA TANGAZO:- CITE SUMMER CONFERENCE 2014

HABARI HII NIMETUMIWA NA DADA RACHEL NAMI NIMEONA SI MBAYA KAMA NIKIIWEKA HAPA  SIKU HII YA LEO.  MWANZO MWEMA WA JUMA.

Wednesday, February 20, 2013

TANGAZO: MABINGWA WA KILIMO CHA MITI YA MBAO NA NGUZO WAMEREJEA. .....


Habari za jioni wandugu...nimetumiwa habari/tangazo hili na mzee wa Mzee wa LUNDUNYASA karibuni tuwe pamoja-------------------------------------------
Kampuni ya Anesa Co.,Ltd kupitia biashara yake tanzu ya Fresh Farms(T); kwa kushirikiana na kikundi cha “Rudisha Uumbaji wa Mungu kwa Kupanda Miti (RUMM)-Kilolo;” tukiwa mkoani Iringa, tumezindua programu maalumu iliyolenga kuwawezesha watanzania wengi kuwekeza na kumiliki mashamba ya miti ya mbao na nguzo kwa urahisi kabisa.
 1.  Progamu hii inaitwa “GREEN THE WORLD and BECOME RICH” ambapo tunauza mashamba yenye miti (miti pamoja na ardhi) kwa utaratibu wa mtu kulipa kidogo kidogo kwa kadiri ya kipato chake. Kiwango cha chini cha kununua ni ekari tano, ambapo utatakiwa kulipa walau asilimia 50% ya bei yote; kisha fedha inayobaki utaendelea kuilipa kwa awamu kwa kadiri utakavyokubaliana na kampuni
 2.  Tupo Iringa mjini na Kilolo (kijiji cha Mwatasi), na mashamba yapo maeneo mbalimbali katika wilaya za Mufindi na Kilolo. Yapo mashamba yenye miti kuanzia ya mwaka mmoja hadi minne, na bei zake ni kuanzia tsh. 700,000(laki saba) hadi 2,000,000 (milioni mbili) kutegemeana na umri wa miti husika. Bei zote zinajumuisha (miti pamoja na ardhi)
 3.  Miti ya mbao inachukua miaka kati ya 7 hadi 10 tangu kupandwa hadi kuvunwa. Wastani wa faida unayoweza kupata kwa ekari moja ya miti iliyokomaa ni tsh milioni tisa hadi kumi na tano (kama ungekuwa unauza leo). Gharama ya kuhudumia ekari moja kwa mwaka haizidi laki mbili. NOTE KWA WALE WAGENI KUHUSU KILIMO HIKI CHA MITI: Pamoja na taarifa hizi, kampuni inahamasisha watu ambao ni wageni kabisa na taarifa zihusuzo miti; kutafuta taarifa zaidi na zaidi kutoka vyanzo mbalimbali kuhusu kilimo-biashara hiki; ili kujiridhisha kabla ya kufanya maamuzi ya kiuwekezaji.
 4.  Mnunuzi akishafika na kuyatazama mashamba (au kama anayafahamu mazingira yalipo mashamba); akishajiridhisha, atasaini mkataba wa makubaliano ya kimalipo kati yake na kampuni, kisha ataanza malipo mara moja. Baada ya kukamilisha malipo yake, utafanyika utaratibu wa kupata hati za kimila/mikataba ya kiumiliki kutoka mamlaka ya baraza la ardhi la kata/kijiji kwa mujibu wa sheria ya umiliki wa ardhi ya vijiji ya mwaka 1999.
 5.  Fresh Farms(T) tukiwa na falsafa ya “Greening the world and Feeding People”; lengo letu ni kuhakikisha tunawasaidia mamia ya watanzania kutumia fursa ya uboreshaji mazingira; kwa kuwekeza vitega uchumi vya mashamba vinavyowahakikishia kipato kikubwa sasa na siku za usoni.
 6   Kampuni itaendelea kutoa usaidizi wa uangalizi na utunzaji wa mashamba yote yanayonunuliwa kutoka kwetu kwa utaratibu rahisi na nafuu kabisa. Nia yetu ni kuona kuwa kila anayewekeza; avune faida ya uwekezaji wake. Hivyo, hauhitaji kuhofu juu ya usalama wa shamba utakalonunua, popote utakapokuwepo utajihakikishia kuwa “investment” yako inafanyiwa juhudi kubwa kuhakikisha inakua.
 7.  Programu na ofa hii ni ya muda maalumu, imeanza tarehe 15, Februari, 2013 na itamalizika, Aprili, 14, 2013. Programu hii inaweza kukoma kabla ya tarehe ya ukomo, ikiwa ekari zilizotengwa zitaisha mapema. Hivyo kwa yeyote anayehitaji tunashauri kuwasiliana nasi mapema.
 Mawasiliano:
Iringa:Mkurugenzi, Albert Sanga (0719 127 901,  0766 742 414),albertnyaluke@yahoo.com
Dar es Salaam: Meneja Masoko, Markus Mpangala (0764936655),mwanazuoni27@gmail.com

Wednesday, January 4, 2012

Nafasi ya Kazi...

Blogger Mwenza.
Ninatafuta blogger mwenza kwa ajili ya kushirikiana kuiandikia na kuiendeleza Kona Ya Waungwana.Sifa zifuatazo zahitajika:
1. Awe ni msomaji na mfuatiliaji wa blog mbalimbali hapa nchini Tanzania
2. Awe ni mkazi wa jijini Dar
3. Awe na background ya uandishi wa habari (si lazima sana)
4. Anaweza kuwa mwanafunzi katika chuo chochote Dar na hasa chuo cha Uandishi wa habari
5. Awe na ujuzi katika kublog na ufahamu wa blogger.com
6. Awe na nafasi ya angalau masaa matatu kwa siku kwa ajili ya kutafiti habari na kupost
7. Awe ni mmiliki wa Laptop yenye uwezo wa kuunganisha internet, na digital camera
8. Awe na uwezo wa kuongea kwa ufasaha lugha ya Kiswahili na Kiingereza
Mafao ni maelewano. Kama una sifa hizo hapo juu niandikie lacford.media@gmail.com au SMS +1301 222 7739 Ahsante, Mfalme MropeJe Huu Ni Uungwana