Showing posts with label mavazi. Show all posts
Showing posts with label mavazi. Show all posts

Sunday, May 11, 2014

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE!!!

SWALI LA LEO:- Je? unamfahamu mwanadada huyu ?

Monday, April 14, 2014

TUANZE WIKI NA MDADA HUYU NA MIKANDA YAKE /HILI LILIKUWA VAZI LANGU LA JANA JUMAPILI !!

Kwa kukumbuka vizuri ebu fungua hapa kuona huyu mdada/kapulya anayopenda mikando tangu enzi hizo za ujana wake:-) http://ruhuwiko.blogspot.se/2013/02/mwanadada-na-mikanda-yakemwanamtindo-wa.htmlKama umeangalia vizuri katika hiyo picha ya juu ...Je? Umegundua kitu gani kinakosekana?
NAWATAKIENI MWANZO MWEMA WA JUMA/JUMATATU

Thursday, November 28, 2013

MWANAMTINDO WA LEO NA MTOKO WA NYEUSI ....BLACK IS GOOD !!!!

 Hivi ndivyo lilivyokuwa vazi langu leo koti ndefu nyeusi na suruali vimenunuliwa UNIQUE,blauzi/line toka Vila clothes.
 Hapa mdada anaonekana kuwa mbali kweli kimawazo.....
 ....hapa anawaza sijui nibadili kazi na kuwa mwana mtindo....anaendelea kufikiri
Na mwisho inaonekana hajapata jibu bado kwa hiyo anaendelea kufikiri. Je wasomaji mnaonanaje  kuhusu hili na kuhusu vazi la leo?....NAWATAKIENI WOTE KAMA ILIVYO HAPO ULIPO IKIWA ASUBUHI, MCHANA, ALASIRI, JIONI AU USIKU..BINAFSI NI JIONI HAPA NA NAANZA KUJIANDAA KUPIKA MLO WA JIONI.

Thursday, June 20, 2013

MDADA KAONA KUWA MODE KWA SIKU MOJA SI MBAYA..AU SIJUI NIBADILI KAZI:-)

 Hapa sijui ndo madoido/madolido au sijui alikuwa anapigana kareti mweee kaaazi kweli
 Na hapa bonge la poozi na miondoka mwanana..hapa ni Jangwani seabreeze resort Dar es salaam. Ni sehemu nzuri sana kupunga upepo..ilikuwa mwaka huu mwezi wa mbili.
 Mmmmh...hizi nywele za kimasai zinawasha ..maana ndo nilikuwa nimesuka tu hapa:-)
Na hapa sijui anasoma misa maana utafikiri anasema bwana awe nanyiii...ni Jangwani tena ...Jioni njema. Na kwa taarifa fupi ni kwamba mkiona nipo kimya msiwe na shaka nipo lakini nitakuwa likizo na ndiyo muda wa kupumzika na kuwa na familia..TUSITUPANE NDUGU ZANGU.. TUTAONANA TENA PANAPO MAJALIWA...Kapulya

Tuesday, June 11, 2013

HILI NI CHAGUA LA MAISHA NA MAFANIKIO:- WAREMBO WA WIKI NI HAWA!!!

Hili ni chagua la maisha na mafanikio ...nimependa vazi hili la asili..ni utamaduni na pia wanapendeza ebu angalia na useme lako....JUMANNE IWE NJEMA KWA WOTE....KAPULYA

Thursday, May 2, 2013

WANAWAKE NA MIGOROLI ..HAWA NI WAMTINDO/WAREMBO WA WIKI HII...JE UNAWAFAHAMU?

Wanawake/wadada hawa wanaonekana kupenda sana kuvaa mgoroli ..umegundua kitu hapa ni kwamba wote wameachia mkono wa upande mmoja..:-)
Halafu unajua kitu kingine huyo wa juu katabasamu lakini huyu wa chini au mwenye kijani anaonekana yupo mbali kweli kifkra...Unajua ni kitu gani kingine wadada/wanawake hawa wanapenda kufanya?...Karibuni ....

Tuesday, April 23, 2013

KUNA NJIA NYINGI YA KUITANGAZA BENDERA YETU YA TANZANIA...

Nimependa magauni haya nafikiri safati ijayo nami nitashona maana duh nimepeata hamu kweli--kama tusemavyo ni rangi nzuri na kila moja ina maana yake..tukianzia na..
1. Nyeusi- Huonyesha watu wa Jamuhuri ya Tanzania.
2. Kijani - Huonyesha mimea na ardhi ya Tanzania
3. Njano - Huonyesha utajiri wa mali ya asili.
4. Bluu - Huonyesha bahari inayoziunganisha sehemu za Jamuhuri ya Muungano
Haya ni maelezo  ya Bendera yetu ya Jamuhuri ya Tanzania....Si mnakumbuka tulijifunza darasa la tatu-nne vile au?......Nawatakieni wote JUMANNE NJEMA!!!!

Friday, February 8, 2013

MWANADADA NA MIKANDA YAKE..MWANAMTINDO WA WIKI!!

 Hapa alianza na mkanda wa kipepeo mwaka 1992 hakika zilipendwa haswaaaaaa.................
 .....................akaona ngoja ajaribu na mkanda wa kitaifa  si mbaya au??? 2011
,,,,na leo 2013 yupo na mkanda mwingine, inaonekana anapenda sana mikanda huyo dada...ni kweli:-)
nawatakieni IJUMAA NJEMA NA MWISHO WA WIKI UWE MWENYE FURAHA NA UPENDO KWENU PAMOJA NA MAJIRANI ZENU. TUPO PAMOJA.

Wednesday, June 27, 2012

KWELI ZILIPENDWA HASWA!!!!

NI KILE KIPENGELE CHETU CHA JUMATANO YA MARUDIO NA LEO NIMEONA TUWA HAPA HAPA YAANI NDANI YA BLOG HII KWA KURUDIA NA PICHA HII NILISHAWAHI KUIWEKA  KWA KUKUMBUSHA ANGALIA HAPA KAPULYA. KARIBUNI SANA.....
Kitu kimoja nasikitika sina picha ambayo nilikuwa kabinti kadogo sana. Najiuliza sijui nilionekana vipi lakini sipati jibu. Panapo majaliwa tuonane tena JUMATANO IJAYO....Kaaaazi kweli naipenda zamani/zilipendwa kwa kweli..inaonekana niliupenda huo mpapai au sijui ndo ulikuwa mtindo kusimama kwenye miti..LOL

Monday, May 7, 2012

KISA CHA WANYASA NA SUTI!!!


Habari za jioni jamani!
Baada ya kuweka hiyo picha ya suti leo, nimetumiwa hiki kisa cha suti cha wanyasa na msomaji pia kaka yangu wa hiari Che Jiah. Nimecheka kweli nikaona si vizuri kucheka peke yangu. Nimeona niweke hapa ili tuvunje mbavu pamoja.Tusinyimane uhondo ..Haya karibuni
-------------------------------------------------------------------------------------------------------
HAPO ZAMANI WANYASA WALIKUWA HAWAPENDI KUVAA SUTI LAKINI KILA SIKU WALIKUWA WANAMWONA RAIS WAO ENZI HIZO KAMUZU BANDA YEYE ALIPENDA SANA KUVAA SURUALI YAANI KAPTULA YEUPE NA SHATI JEUPE. SIKU MOJA ALIVAA SUTI, SIKU  ALIPOTEMBELEWA NA MALKIA WA UINGEREZA. ENZI HIZO BASI NAE ALIVAA SUTI AKAPENDEZA SANA. HIVYO TOKA SIKU HIYO WANYASA WALIKUWA TAYARI KUVAA SHATI LAZIMA TAI NA SUTI. IKIBIDI HATA KAMA SUTI IMECHANIKA, LAIZIMA ATINGE TAI TUU. NA MPAKA LEO UKIENDA MALAWI HUU NDIYO MVAO WAO
KWAHERI!
CHE JIAH.

TUIANZE JUMATATU HII KIHIVI:- KAPULYA AKIWA NDANI YA SUTI KWA MARA YA KWANZAKATIKA MAISHA YAKE!!!

Vipi mbona umenuna mama au hupendi ?
Ah! wewe nawe haya ngoja basi nitabasamu kidogo:-)
Kama wasemavyo watu MTU UNAISHI MARA MOJA basi jana jioni nikaona kwanini nisijaribu kuvaa suti na kuina naonekana vipi ndani ya suti.  Hakika ilikuwa kichekesho kwelikweli kama uonavyo katika picha ilikuwa mara ya kwanza na mara ya mwisho...Au? HAYA JUMATATU NJEMA JAMANI.

Thursday, March 15, 2012

NIMELIPENDA GAUNI HILI MNO....

.......ebu angalia hizo rangi na jinsi lilivyorembwa, nimelipenda mno . Swali sijui nami nitapendaza kama lilivyompendeza huyu dada?:-)

Tuesday, March 6, 2012

J's JOY: Mavazi ya Kiafrika. Tujivunie. Tuunge mkono!!!!!

Ladies and Gentlemen,
I would like to take this great opportunity to introduce you to my niece, Karungi Mukurasi who has a renown business in Dar for making nguo za wakina mama na mashati ya wakina baba and some very interesting stylish African suits for men.
She is the one in the photos in the attachment.
From the time she was born she showed artistic proficiency and when school was done, she embarked into this voyage which has brought her to the heights of the design of premier African dressing. She gets her materials from West Africa where the best fabrics are woven and has dress-makers to her designs both in West Africa and in Tanzania.
Her dresses have been worn by prominent women in Tanzania and some international circles, as well as some shirts which some Wabunge have found very fashionable as they mingle in public circles.
Just as the advertisement on Mwananchi Newspaper shows (photo above, click to enlarge), these are African dresses with an African style which eclipse what you may see at a Hollywood movie premier or the Oscar's red carpet runway.
Please feel free to contact her for any additional info, specially for you who are abroad and would like to show the international community that African dressing is second to none!
Her email address is: kmukurasi@hotmail.com or k_mukurasi@yahoo.com Duka lipo Kinondoni Road, Kinondoni Muslim, Duka namba 37, jina la duka ni J's JOY. Namba ya simu ni +255 784 95 95 51
We hope to have a website soon!
Thanks,
Ben K.

Saturday, October 15, 2011

MAJIBU KWA NDUGU MANGI NA KAKA SIMON KITURURU!!!

Kutokana na maoni ya ndugu zangu Mangi na kaka Simon Kitururu ambayo yanatoka katika picha hizi nimeona niweke hii picha labda itasaidia. Maoni yenye yalisema hivi:Ndugu Mangi anasema "Akina msitudanganye kabisa!Tuonyesheni kitu kipya na kamili kwa kuvaa mavazi ya wanawake katika picha kamili kuanzia juu kwenda chini mkionyesha uwakilishi wa kitanzania." Na kaka Simon naye anasema "Ghafla naamia upande wa mtani wangu MANGI ,...... nahisi kuna kitu hamjatuonyesha. Na neno la MANGI liheshimiwe nanyi. Amen.
JUMAMOSI NJEMA WAPENDWA!!!!!

Saturday, October 8, 2011

UNAMFAHAMU MWANAMTINDO HUYU WA JUMAMOSI HII!!!





Kaka Sam upo? au bado unataka nivae LOL.......hapo kwenye deshi jaza wewe LOL... mdada huyu ni mpezi sana wa sketi ndefu. Sketi ya kitenge hii imeshonwa Songea, top nyeusi imenunuliwa Vila, blauzi kijana /maji ya bahari imenunuliwa H&M. Na nyuma yake nadhani mnaona baiskeli nyekundu hiyo ndiyo inayomfikisha kila aendako...ni usafiri wa haraka sana...


Hapa pia yupo kakaa chini na sketi yake imetanda kama gauni la bibi harusi... LOL.

Swali je? unafikiri ni mpiga picha ni mmoja au ni tofauti? kama ni tofauti hiyo picha ya kwanza nani kapiga na hii ya pili nani kapiga?


JUMAMOSI NJEMA KWA WOTE NA KUMBUKENI MNAPENDWA SANA!!!

Wednesday, September 14, 2011

JUMATANO YA KIPENGELE CHA MARUDIO LEO HII TUWE NA HUYU DADA NA MITINDO YAKE:- UKIJIPENDA MWENYWE NA WENGINE WATAKUPENDA=MAISHA

Ndiyo, ndiyo! Ndugu wasomaji wa blog ya Maisha na Mafanikio kile KIPENGELE chetu cha marudio ya mada, picha, au nisema MATUKIO MBALIMBALI ambayo huwa kila JUMATANO...leo nimeona tuangalie picha hizi za huyo madada. Ambazo tulishawahi kuziona hapa. Ila leo ana swali moja maana si mnajua huyu ni Kapulya...Je ni picha gani wewe imekupendeza? unaweza kutoa sababu pia.:-)

Hapa mwanadada ametinga kimgolole/kimasai.


Hapa nilikuwa nafikiria nifunge mtindo upi? Kabla sijaamua picha ikapigwa...kaaziii kwelikweli!!!
Hapa nikaona nikumbuke nilipokuwa mdogo maana nilikuwa napenda sana kufunga nguo (Lubega) shingoni. Lubega na ndala si mbaya au mnasemaje.... Ahsanteni wote TUONANE TENA JUMATANO NYINGI /IJAYO KATIKA KIPENGELE CHETU HIKI CHA MARUDIO YA MATUKIO MBALIMBALI!!!!!

Wednesday, May 11, 2011

WANAMITINDO WA WIKI HII NI HAWA HAPA!!

Huwa nafurahi sana nionapo utamaduni wetu wa KIAFRIKA unaendelezwa yaani kuvaa kama vile kanga na vitenge. Na sasa naona KANGA zinakuja juu kwa kushona magauni, mashati, mikoba nk. UTAMADUNI WA KIAFRIKA UDUMU!!!

Ebu angalia hapa, yaani kuangalia tu unaona jinsi UAFRIKA HALISI na mavazi yako unavyopendeza. BINAFSI NIMEPENDA/NINAYAPENDA SANA MAVAZI KAMA HAYA. Je? wewe unapenda mavazi ya aina gani?



Friday, January 14, 2011

MAVAZI YA WANAWAKE

Nimelipenda shairi hili kwani linasema ukweli limeandikwa na Katekista Rafael Mlelwa katika gazeti la Mwenge:-

Natembea natazama, ni hali ya kushangaza,
Mitaani akina mama, mambo wanayoigiza,
Wengine watuwazima, inakuwaje nawaza,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.

Vazi la Mtanzania, tangu kale heshima,
Watu walijivunia, wa lika zote nasema,
Haya nawasimulia, walivaa akina mama,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.

Suruali mwavalia, mfanane na wazungu,
Asili mwaikimbia, mnanitia uchungu,
Watu wote angalia, mnamdharau Mungu,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.

Vimini mwajibalia, mwana kama vikatuni,
Nyingine mnapasua, makusudi mapajani,
Mapaja twaangalia, pia na nguo za ndani,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.

Siketi taiti pia, mitaani mwavalia,
Hiyoni ya kulalia, maungo yaoneshea,
Mitaani mwatembea, watu kwa kuangalia,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.

Kweli mwatia karaha, moyoni nasononeka,
Singerendi mwavalia, maziwa yanaonekana,
Mitaani mnahaha, kutwa nzima mwazunguka,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.

Kwa umbo mmeumbika, kwa uzuri asilia,
Uarabu mwautaka, tena kwa kujichubua,
Kama Mungu angetaka, mngekuwa Saudia,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.

Wengine watu wazima, tena ni wake za watu,
Watoto wenu lazima, watawaigeni tu,
Malazi yao lazima yatakuwa yenye kutu,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.

Hapa mimi nasimama, naomba mnisikie,
Wanamama wenye hekima, hali hii tukemee,
Hakika mimi nasema, tena isiendelee,
Mavazi mnayovaa, ya aibu kinamama.

Thursday, October 7, 2010

Wanamitindo na warembo wa wiki hii ni hawa:- kumbe tupo wengi tunaopenda kutinga mgololi!!!


Yasinta Ngonyani na Salma Kikwete

Mama wa Maisha na Mafanikio na vazi lake la asili la mgololi na halafu hapo si mwingine tena ni mama Salma Kikwete akiwa naye ametinga vazi la asili aina ya mgololi. Ebu angalia ni kitu gani unaona ni tofauti au sawa katika picha hii:-) TUTAONANA WAKATI UJAO!!!

Friday, September 3, 2010

Huyu ni mrembo wa wiki hii, Je? unamfahamu huyu??

Napenda kuwatakieni wote Ijumaa njema. Picha hii nimeipenda na nimeona iwe ni picha ya wiki hii. Jipende kwanza mwenyewe na wengine watakupenda!!! Juma ndio linaisha sasa, kwa wengi ni wakati wa kumpumzika, na wengine kazi kama kawaida. Basi nasema tena nawatakieni wote muwe na wakati mzuri. IJUMAA NJEMA!!