Showing posts with label mazoezi kukimbia. Show all posts
Showing posts with label mazoezi kukimbia. Show all posts
Tuesday, July 23, 2013
SWALI LILILONISUMBUA SIKU YA LEO...!!!!
Nimeamka asubuhi hii na nimemshukuru Mungu kwa kunilinda. Nikaona ngoja ninyooshe viungo:- Yaani nikaende nje kama kawaida yangu kukimbia, nimekimbia, nimekimbia mara nikakutana na mkimbaji mwingine naye kawaza kama mimi anakimbia. Sasa hapa kitu kilichonipa swali ni kwamba mdada huyu alikuwa akikimbia na mbwa wake ambaye amemfunga kamba shingoni. Swali likanijia huyu dada ana uhakika kama huyu mbwa/kambwa anataka kukimbia? Maana niliona kama mbwa mwenyewe hata hakufurahia. Nikataka kusimama na kumuuliza.....lakini nikaacha. Muda wote nilipokuwa nakimbia swali lilizidi kunisumbua hivi kweli yule mbwa alipenda kukimbia? Na pia nikazidi kuwaza....Nikaona niwape na wenzangu haka kakisa....TUSITENGANE TUWA TUNAKUMBUKANA. PAMOJA DAIMA SIKU NJEMA. KAPULYA!!
Tuesday, March 5, 2013
PICHA YA/ZA WIKI MAZOEZI NI MUHIMU KATIKA AFYA ZETU TUZINGATIE!!!!
Mchaka mchaka chinja....aaah ebu tuchukue wimbo huu Idi amini akifa mimi siwezi kulia nitamtupa Kagera awe chakula cha mamba....
Dada mkuu msaidizi naye hayuko nyuma kabisa ..Haya dada mkuu msaidizi msimu wa kuanza mazoezi unakaribia ,,wewe endelea usitazame nyuma ..haya alisema, alisema, alisema Nyerere alisema vijana wangu wote mwalegea sharti tuanze mchakamchaka....mmmmhhh ngoja niwaachie na wengine waanzishe kuimba maaana mapumzi hapa yanasumbua kweli....Sijui mnawafahau wadada hawa?:-) JUMANNE IWE NJEMA SANA KWA KILA MMOJA!!!!!
Dada mkuu msaidizi naye hayuko nyuma kabisa ..Haya dada mkuu msaidizi msimu wa kuanza mazoezi unakaribia ,,wewe endelea usitazame nyuma ..haya alisema, alisema, alisema Nyerere alisema vijana wangu wote mwalegea sharti tuanze mchakamchaka....mmmmhhh ngoja niwaachie na wengine waanzishe kuimba maaana mapumzi hapa yanasumbua kweli....Sijui mnawafahau wadada hawa?:-) JUMANNE IWE NJEMA SANA KWA KILA MMOJA!!!!!
Tuesday, August 7, 2012
HAYA TWENDEE, TWENDE,TWENDE USICHOKE...!!!!
Huyoooo anakuja, huyooo anakuja..anakuja anakuja....
.....na hapa ndiyo nimefika golini...hii ilikuwa leo asubuhi...nimepanga kupata dhahabu ya olimpiki ..LOLmazoezi tu kwa ajili ya afya ..ngoja nikapalilie bustani yangu sasa...
Tuesday, October 4, 2011
PICHA YA WIKI...MAZOEZI NI MAHIMU KWA AFYA YAKO!!!
Sunday, September 14, 2008
Friday, August 22, 2008
AGOSTI 22,2008 ERIK NA YASINTA KATIKA MAZOEZI YA KUKIMBIA
Subscribe to:
Posts (Atom)




