Showing posts with label kanga. Show all posts
Showing posts with label kanga. Show all posts

Sunday, July 27, 2014

TUIMALIZIE WIKI HII NA MREMBO HUYU...MWANAMKE WA SHOKA DADA MKUU MSAIDIZI WANGU

 Kanga zina matumizi mengi na hasa ukimpata anayeweza kutumia kama dada yetu hapa. Binafsi nimependwazwa sana na alivyopendeza
Hapa pia safi sana. Picha kwa idhini ya da´Mija...mwanamke wa shoka. JUMAPILI IWE NJEMA SANA KWA WOTE.

Friday, April 11, 2014

NAPENDA KWATAKIENI MWISHO WA JUMA KWA USEMI HUU KWENYE KANGA HII!!

Muwe na mwisho wa juma mwema sana wote. Pia kama ulimkosea rafiki, jirani, ndugu, au mtu yoyote sasa ndiyo wakati mwafaka wa kumsamehe maana wikiendi ijayo ni PASAKA. IJUMAA NJEMA!!!

Tuesday, April 16, 2013

KANGA YA VIKOMBE VYA CHAI...NIMEIPENDA HII KANGA!!!!!

Maandishi yanasema ISIKUHADAE RANGI TAMU YA CHAI NI SUKARI...Hivi ni kweli?

Monday, July 30, 2012

SIO LAZIMA UAMBIWE KWA MDOMO....

....hata kwenye kanga ni tosha kabisa...

Wednesday, July 11, 2012

NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMATANO NJEMA NA UJUMBE HUU!!!

HAYA NDUGU ZANGUNI NI ILE JUMATANO YA KIPENGELE CHA MARUDIO YA MATUKIO MBALIMBALI. KWA HIYO LEO NIMEONA NIWEKE PICHA HII AMBAYO NILISHAWAHI KUIWEKA. KARIBUNI....

Macho ya huruma hufurahisha moyo, habari huburudisha mwili. Kuchukiana huendekeza fitina, kupendana husitiri makosa yote. Nilikuwa mgonjwa ukaja kuniona .Nilikuwa na njaa ukanilisha. Kumhudumia mgonjwa ni wito. JUMATANO NJEMA KWA WOTE . NA KUMBUKENI WOTE MNAPENDWA!!! NA PANAPO MAJALIWA BASI TUONANE TENA WAKATI MWINGINE.

Tuesday, May 18, 2010

Swali la leo:- Hivi kwanini kanga mnyama anaitwa kanga na Kanga vazi ni kanga zina uhusiano gani?

Kanga kama mnyama
Kanga kama vazi hasa kwa wanawake!!
Nimekuwa nikijiuliza miaka yote hii leo nimeona niwailize ndugu zangu kwani umoja ni nguvu utengano ni udhifu. Na anayeuliza sana basi anajua mengi...a.k.a KAPULYA MDADISI.