Showing posts with label dini. Show all posts
Showing posts with label dini. Show all posts

Tuesday, June 24, 2014

KAKA S. ANAMPONGEZA MTOTO WAKE KWA KUPATA KOMONIO YA KWANZA

KILINDA SAMUEL MBOGO
Jumapili  22/6 Kijana Kilinda alipata komonio yake ya kwanza. Bahati mbaya sikupata nafasi kwenda kuhudhuria siku hii. Ila nimehudhuria kwa kuangalia picha kama muonavyo. Nimetumiwa picha nami nimeona niwashirikishe wenzangu maana baadhi yetu tunakumbuka sana siku hii...HONGERA SANA KILINDA SAMUEL MBONGO KWA  SIKU HII...HII NI ZAWADI YANGU KWAKO....SHANGAZI YAKO YASINTA a.k.a Kapulya/kadala.

Sunday, August 11, 2013

JUMAPILI HII TUANGALIA HADITHI YA MAISHA YA YESU KWA KIBENA!!!

UDALIKE uliyerekodi hii kwa kibena. Nimefurahi kweli kusikia LUGHA YA KIBENA kwa mara nyingine nimejisikia kama nipo ubenani. HAYA NAWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA NA UPENDO NA AMANI PIA UTULIVU UTAWALA KATIKA NYUMBA ZENU. KRISTU NI TUMAINI LETU.

Sunday, August 14, 2011

JUMAPILI YA LEO:- IMANI IMEKWISHA/ KWENYE KIFO HAMNA KUJUANA, UNAMKANA HATA MUUMBA WAKO!

Nimeamka nikaona ngoja nifunguo kopo langu na kusoma barua pepe na mara nakutana na ujumbe huu kwa vile sina tabia ya kuwanyima ninyi ndugu zangu chochote nimeona niweke hapa ili wote tupate kuelimika. ujumbe wenyewe ni hivi....Karibuni.

Jamaa mmoja alikwenda msikitini na panga mkononi na kuwauliza waumini: "Nani muislamu kati yenu?"
Watu kimyaa! Akauliza tena kimyaa!! Akamfuata mmoja akamchukua akaenda nae nyumbani kwake akampa mbuzi wake amchinjie.

Kabla ya kumchuna akarudi tena msiktini na kisu chenye damu na kuwauliza tena waumin: "Ni nani muislamu?" wote kimya kwa woga.
Kwa mshangao akawauliza kwa SAUTI kubwa: "Yaani nyie mpo ndani ya msikiti halafu hamumjui Muislamu?"

......Ghafla wote huku wakitetemeka wakasema IMAMU wetu ndie muislamu.


IMAMU kusikia anatajwa akalalamika: "Jamani....jamani! yaani kuwaswalisha siku mbili tu ndo nshakuwa Mwisilamu? Muogopeni Mungu!!"

Kumbe yule jamaa lengo lake lilikuwa kuchinjiwa na kuchuniwa mbuzi wake!

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE!!!


Sunday, November 28, 2010

LEO NI JUMAPILI YA KWANZA YA MAJILIO/IDAG ÄR FÖRSTA ADVENT!!!!!

Jumapili ya kwanza ya majilio/Först Advent!!!

Nimeipenda sala hii ya kaka Baraka Chibiriti na nimeona ni vizuri kuitumia jumapili hii ya leo.Ukizingatia ni jumapili ya kwanza ya majilio haya hebu tusali kwa pamoja.

Nia yangu naileta kwako Bwana Mungu wangu, nakuomba Bwana unisikie ninalia kwa uchungu. Nakuomba uipokee sala yangu, sikiliza na sauti ya kilio changu. Ninajua Bwana siku zote wewe hupatikani kwenye gasia, ninajua siku zote wewe hupatikani kwenye vurugu.
Bwana nijaie utulivu wa moyo na nipe nguvu nimshinde mwovu shetani, shusha roho wako anipe faraja. Bwana niongoze ili nitimize nia yangu ya kuwa mtumishi wako mwema!

Ee Bwana upo wapi mimi ninakutafuta, nitazame kwa huruma nateseka Mungu wangu...nakuomba uipokee sala yangu na uisikilize sauti ya kilio changu.
Hata kama nipo kama takataka mbele za watu...lakini mbele yako mimi nina thamani kubwa sana siku zote, kwa hili niajua na ninauhakika kwamba wewe pekee ndiwe wenye kunithamini, nakuomba uipokee sala yangu na uisikilize sauti ya kilio changu.
Ee Bwana wangu nijalie nikabili njia zangu, nimshinde huyu mwovu shetani hanifai kabisa. Bwana Mungu wangu wewe ndiwe tegemeo la maisha yangu yote hapa Duniani, nitausifu na kuku tegemea wewe daima siku zote za maisha yangu!

Sunday, September 5, 2010

Mtu, Kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake!-TAFAKARI

Mathayo 7:15-20
Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali. Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni. Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.

Luka 6:43-45
Kwa maana hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala mti mbaya uzaao matunda mazuri; kwa kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake; maana, katika miiba hawachumi tini, wala katika michongoma hawachumi zabibu. Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo Wave
Habari hii nimeipata nimeipata hapa http://strictlygospel.wordpress.com/ na nikaona si mbaya kama nikiweka katika kibaraba cha Maisha na Mafanikio. JUMAPILI NJEMA KWA WOTE

Saturday, September 4, 2010

Likonde: Jubilei ya miaka 50 ya Seminary ya Likonde

Seminari ya Likonde



Ama kweli miaka inakimbia kweli leo hii ni jubilei ya hii Seminary!!


Sunday, July 4, 2010

NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI HII YA KWANZA YWA MWEZI HUU WA SABA NA/ TAFAKARI YA LEO: IMANI KATIKA NENO TAKATIFU


Nabii Eliya katika maombi

Baada ya kutafakari kwa kina nimepata wazo la kuanzisha kipengele cha Tafakari ya Leo, ambacho kitakuwa kikuzungumzia neno takatifu la Mungu. Kipengele hiki kitakuwa kikiwajia kila siku ya Jumamosi ambapo ni siku yangu ya kupumzika na kumtumikia Mwenye enzi Mungu.

Katika kukumbushana huko, nitaelekeza fikra zangu juu ya maandiko matakatifu na hata nukuu mbalimbali kutoka kwa Wanafilosofia waliowahi kuishi hapa duniani wakiwemo Manabii.

Jana nilishindwa kuweka kipengele hiki kutokana na mtandao kupata kwikwi. Lakini kwa kuwa leo mtandao umetulia ninawaletea kipengele hiki kama ifuatavyo, naomba tutafakari kwa pamoja:

Leo ninaanza na somo la imani, hebu tuangalie 1Wafalme 18:42, nitanukuu,
“Naye Eliya akamwambia Ahabu, Haya! Inuka ule, na unywe; kwani pana sauti ya mvua tele”

Mwisho wa kunukuu.

Kama tulivyosoma fungu hilo hapo juu, Nabii Eliya akimwambia Ahabu ainuke ale na anywe kwani pana sauti ya mvua tele.

Ukweli ni kwamba kulikuwa hakuna mvua, pia mawingu yalikuwa hayaashirii kuwepo kwa mvua, pia hata upepo ulikuwa hauvumi kuashiria kwamba kungenyesha mvua. Lakini Nabii huyu wa Mungu Eliya alisema, “Nasikia sauti ya mvua tele”

Kwa kauli hiyo ya Nabii Eliya inanionyesha kuwa katika swala la imani, kusikia ni dalili muhimu kabla ya kuona kile unachokitarajia.

Tatizo la kwa nini sisi tunakuwa na imani haba kiasi cha kutofanikiwa katika kila tulitendalo ni kutokana na kutaka kuona kile tunachokitarajia kabla ya kusikia kwanza.

Nabii Eliya Alisema kuna sauti ya mvua tele, hebu tuliangalie kwa makini neno “Sauti” kwa sababu neno sauti anazungumzia kelele na matokeo yake.

Pia ni vyema ukijua kwamba sauti aliyokuwa akiisikia sio halisi bali ilikuwa ni ya rohoni.
Katika biblia tunasoma kuwa Nabii Eliya alimwagiza mtumishi wake kwenda kuangalia iwapo kuna dalili ya mvua, na mtumishi huyo alikwenda mara sita kuangalia, lakini alirudi na jibu lile lile kuwa kulikuwa hakuna dalili ya mvua.

Labda wewe unayesoma hapa leo uko katika hali hiyo hiyo, umeshajaribu kila kitu na una imani katika kufikia malengo yako lakini imani yako imekuwa ni bure kabisa.

Hakuna kinachotokea na maisha yako yamekuwa ni yale yale, kama vile ilivyokuwa kwa mtumishi wa Nabii Eliya alivyokwenda kuangalia dalili ya mvua mara sita lakini akirudi na jibu lile lile la hakuna dalili ya mvua.

Labda kwa upande wako imekutokea katika kazi yako, biashara zako, ujuzi wako, elimu yako, na unaanza kupoteza imani kwa mungu au unafikiria kuachana na mungu na kutomwamini.

Nataka nikwambie leo hii kuwa kama imani yako ikisema ndio, hakika hata mungu hawezi kusema hapana.

Nabii Eliya alisema,… “Nasikia…” na hakusema….. “Naona….” Hii inaonyesha kuwa Nabii Eliya alikuwa anajua kanuni ya kuwa na imani.

Kwa hiyo na wewe ili dalili ya imani yako kufanya kazi ni lazima kwanza usikie ile dalili ya kupata majibu kutoka kwa mungu ni lazima ujiandae kuisikia dalili hiyo kutoka kwa mungu.

Lakini tatizo walilo nalo waumini wengi ni la kusikia. Katika biblia tunasoma katika Warumi 10:17 “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo”

Biblia haikusema kuwa “imani huja kwa kusikia neno” Kiasi gani utasikia inategemea na umbali unaoweza kuona.

Hebu tuangalie nyuma kidogo kwenye historia ya Abrahamu katika kitabu cha mwanzo 15:1. Mungu alimwambia Abrahamu “Usiogope Abrahamu, mimi ni ngao yako na thawabu yako kubwa sana”.

Lakini Abrahamu akamwambia mungu, “utanipa nini il hali sina hata mtoto”
Naamini kuwa tunafahamu kuwa hatimaye Abrahamu alikuja kupata mtoto.

Lakini hata hivyo kabla ya kupata mtoto, tuliona jinsi mungu alivyomchukuwa Abrahamu hadi ufukweni kuhesabu mchanga na pia alivyomchukuwa hadi nje wakati wa usiku na kumwambia ahesabu nyota. Unaweza kujiuliza kwa nini afanye yote hayo?

Naamini ni kwa sababu Mungu alitaka kubadili picha aliyokuwa nayo Abrahamu ya kutokuwa na mtoto.

Kwa somo hili naamini wote tumeona ni jinsi gani imani inavyoweza kufanya kazi iwapo tutafuata kanuni kama nilivyoeleza.

Tukutane Jumamosi ijayo……………

Mada hii nimeichukua kutoka kwenye kibaraza cha VUKANI, cha mdogo wangu Koero, nami nimevutiwa nayo nikaona sio vibaya kuirejea ili kujikumbusha. jumapili njema kwa wote.

Sunday, January 24, 2010

SALA YA LEO NI KUWAOMBEA WATU WOTE DUNIANI!!!

Salam Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Maria Mtakatifu mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

Je? unajua hapa chini ni lugha gani??? zawadi nono itatolewa.

Yethi Maria ogcwele igrasiya, iNkosi inawe, ubusisiwe wena esifazaneni, ibusisiwe nenzalo yesisu sakho uJesu. Maria ocwebileyo, Nina kaNkulunkulu, mawusikhulekele thina zoni, kalokhu nasesikhathini sokufa kwethu. Amen.


Var hälsad Maria, full av nåd.
Herren är med dig.
Välsignad är du bland kvinnor
och välsignad är din livsfrukt Jesus.
Heliga Maria, Guds Moder,
be för oss syndare
nu och i vår dödsstund.
Amen

NAPENDA KUWATAKIENI JUMAPILI HII YA NNE IWE NJEMA KWA WOTE!!!!

Saturday, August 22, 2009

KUANZA KWA MWEZI MTUKUFU WA MFUNGO WA RAMADHANI

Napenda kuwatakia ramadhani njema waislamu wote duniani!!!

Friday, April 10, 2009

UJUMBE WA LEO IJUMAA KUU NI:-

Yesu Kristo mwenyewe alichukua dhambi zetu katika mwili wake msalabani, tupate kufa kuhusu dhambi, na kuishi kwa ajili ya uadilifu. Kwa majeraha yake niny mmeponywa (1 Pet 2:24)

Na pia tukumbuke kuwa:-
Kuna mungu mmoja na baba wa wote ambaye yuko juu ya wote, afanya kazi katika yote na yuko katika yote. Waefeso 4:6