Showing posts with label chakula akipendacho kapulya. Show all posts
Showing posts with label chakula akipendacho kapulya. Show all posts

Wednesday, May 29, 2019

VYAKULA/MILO AIPENDAYO KAPULYA

Chakula cha asubuhi mayai, soseji na vinginevyo na bila kusahau matunda kama papai, nanasi na  zabibu. Bila kusahau chai(chingambwe) yaani chai isiyo na sukari

Hapa ni samaki mzima mkubwa aliyeokwa kwenye oven na aina nyingine za samaki kama pweza, kamba nk. Karibuni tujumuike wapendwa.
Hapa ni viazi  kwa samaki wa kuchoma/banika  yaani hapa ndo walinikumbusha kwetu LUNDO/NYASA.
PAMOJA DAIMA.

Friday, August 25, 2017

JAMANI MWENZENU BADO NIPO NYASA KWETU NAKULA SAMAKI CHAKULA NIKIPENDACHO KUPITA VYOTE:-)

Yaani ni kwenda tu ziwani na unapata samaki uwapendao...hapomie nimechagua leo MBUFU  ni huyo mkubwa na "sengefu" huku tunawaita hivyo hao samaki wa mbele ya baiskeli .....NAWATAKIENI MWISHO MWEMA WA JUMA.

Wednesday, October 21, 2015

CHAKULA AKIPENDACHO KAPULYA....MAKANDE

Ni chakula am,bacho ukila unashiba na muda mrefu huhitaji kula chakula kwa muda mrefu..leo nimekitamani mno ......nawatakieni wote siku njema...tulage kwa macho haya makande.