Showing posts with label Wino/madaba. Show all posts
Showing posts with label Wino/madaba. Show all posts

Monday, June 17, 2013

LEO TUANZE JUMATATU NA KUANGALIA SHULE HIZI ZA KATA YA WINO TARAFA YA MADABA WILAYANI SONGEA!!!

Ifinga ni kijiji ambacho kipo kata ya Wino kutoka barabara kubwa kama inavyoonyesha kwenye kibao ni km 48. Kijiji hiki kinajulikana sana kwa kilimo cha mpunga na machungwa...Mwaka 1992 tulifanya safari mpaka Ifinga tulichukua chumvi nasi tulipata machungwa mengi sana . Kijiji hiki wanakula sana wali hakuna ugali. Ninachoshangaa mwaka ule kulikuwa hakuna hata shule sasa leo napita hapa naona kibao Ifinga Matumbi Secondary school..nikaona ni lazima nipige picha..najiuliza sijui ni maendeleo au ili mradi kila kijiji kiwe na shule?
Kwa sababu mwanzo kulikuwa na shule yetu hii  Wilima ndiyo ilikuwa ya kata. Lakini nayo sasa imeendelea na kuwa High school. Nakumbuka mengi sana kuhusu shule hii....Wilima Sekondari. Kuna nyingi kumbukumbu zinazowahusu watu wengi...Jumatata njema....