Showing posts with label majonzi. Show all posts
Showing posts with label majonzi. Show all posts

Friday, December 6, 2013

AFRIKA TUMEPATWA NA MSIBA BABU YETU NELSON ROLIHLAHLA MANDELA HATUNAYE TENA.

Nelson Mandela wakati wa uhai wake
 
1918-2013....ni pengo kubwa umeacha. Utakumbukwa daima. Mwenyezi Mungu ailaze roho yako mahali pema. Amina.


TUTAKUKUMBUKA DAIMA MKOMBOZI WETU. AMINA

Thursday, September 10, 2009

LEO NI MAZISHI YA BABY D

Ndiyo tunakubali kuwa Mungu alitoa na Mungu anachukua lakini inapokuja kwa mtoto huwa inaumiza kidogo nahasa mtoto huyo hata hajaishi kama inavyotakiwa. Na pengine hata hajabebwa na waliompenda. Mtoto D amekuwa katika dunia hii kwa muda wa siku 18 tu. Naomba wote tuchukua angalao dakika na tumwombe mtoto D. Mama, baba, wajomba, shangazi na ndugu wote watakuwa wanakukumbuka kila siku, ustarehe kwa amani peponi. Amina. Zaidi soma hapa. http://changamotoyetu.blogspot.com/ mada aliyoandika jumapili 6/9 na mada yenye kichwa cha habari Rest in peace baby D.

Friday, March 6, 2009

SITASAHAU MWAKA 2004­-2005

Sitasahau:- Ghafla 18/8 2004 niletewa habari kuwa sina mama tena. Ilikuwa kama ndoto, kwani sikuletewa habari kuwa anaumwa. Kwa hiyo sikuamini kabisa. Kwa kweli ni pigo kubwa sana kuondokewa na mama. Huku mbali ugenini sikujua nifanye nini, kwenda nyumbani ni mbali. Maisha yangu yanazidi kuwa magumu;- ningebaki nyumbani NINGE. Kwani kuna mambo mengi watu wanahitaji kuongea /kupata ushauri wa mama, sasa nitaenda wapi. Kila nikifikiria hili jambo nakosa raha kabisa. Pole mama yangu hajawafaidi /hajacheza na wajukuu wake. Na pia pole mimi sijamfaidi mama. Namshukuru mume wangu pamoja na marafiki wote kwa kunifariji wakati nilipokuwa na majonzi. Naweza kusema ilikuwa si mbali sana ningechanganyikiwa kabisa. Kwani kidogo nilichanganyikiwa niliacha kula nilikataa kwenda kazini pia shuleni nilichotaka ni kulia tu kwa kweli ilikuwa hatari. Ukizingatia pia sikuweza kuhudhuria mazishi kwa maana hiyo inakuwa vigumu sana kuamini. Mwaka huu mzima ulikuwa mwaka wa majonzi na mateso makubwa sana nilipungua/ kilo 10 hivi. Ila kwa maana nyingine nasi tulihudhuria mazishi yake. Tuliwaombe wapige picha (video) lakini hata hivyo sio sawa na kuwa pale. Kwa hiyo mpaka sasa kichwani/akilini mwangu mnaniambia mama bado yupo. Nimesahau kusema mama alitutoka trehe 17/8-04 saa mbili usiku hii siku ilikuwa si siku nzuri kwani pia binti yangu ilikuwa siku yake ya kwanza kuanza shule. Mama alizikwa 19/8-04

Mapema 2005 mwanzoni tukafunga safari kwenda nyumbani Tanzania. Ilikuwa taabu sana nilibadilika, sikutaka kutoka pale nyumbani kwenda mbali. Kama vile kusalimia marafiki Wino-Matetereka. Nilikuwa naogopa, nilikuwanamsubiri mama. Kwani ilionekena kama tu, ameondoka kidogo. Au yupo safarini. Nadhani maisha yangu hayatakuwa kama yalivyokuwa. Wakati mwingine siwezi kuamini eti mama hayupo. Wengi waliumia sana siku ile, ila kwa kuwa mbinafsi nataka kusema mimi niliumia zaidi. Naletewa habari mama hayupo, lakini siwezi kwenda kwenye mazishi pia wala kumwona mama yangu kwa mara ya mwishoyaani ile (BURIANI). Hii ndio maana siwezi/sitaki kuamini pia kusema hili neno marehemu. Kwa sababu kwa mimi mama yupo nami si marehemu.HILI SITASAHAU.

Sunday, August 17, 2008

AGOSTI 17, 2008 KUMBUKUMBU,KUTOWEKA KWA MAMA YANGU

Mpaka leo ni miaka minne (4) imepita tangu mama yangu mpendwa Alana magnus Ngonyani aiage dunia hii. Ila kwa mimi inaonekana kama ilikuwa jana tu. Napenda kukuombea mama kwa sara hii:-


Salamu, Maria, umejaa neema,
Bwana yu nawe,
umebarikiwakuliko wanawake wote,
Na Yesu, mzao wa tumbo lako amebarikiwa.

Maria mtakatifu, Mama wa Mungu,
Utuombee sisi wakosefu,
Sasa na saa ya kufa kwetu,
Amina.


Marehemu astarehe kwa amani, Amina.