Showing posts with label kufa. Show all posts
Showing posts with label kufa. Show all posts

Wednesday, October 10, 2012

KATARINA KWA NINI ULIKUFA?

Wapendwa wasomaji wa blog hii na wanablog wenzangu nimekuwa nikipokea email nyingi toka kwa wasomaji wa blog hii wa huko nyumbani Tanzania, wengi wakielezea uzoefu wao na wakitaka niziweke hapa ili tujadili kwa pamoja, na mimi sina kinyongo kwa kuwa blog hii inazungumzia Maisha, basi nitakuwa nikiziweka hapa ili wasomaji wengine wapate kujifunza
 Leo nimewaletea kisa cha kusikitisha cha binti aitwae Katarina, naomba muuangane na msimulizi wa kisa hiki.
 **********************************************************************
 Alikuwa ni mtumishi wa nyumbani na alikuwa na umri wa miaka 14 wakati huo, nakumbuka ilikuwa ni mwaka 1993, ndio aliletwa kufanya kazi kwa shemeji yangu.
Nakumbuka nilikuwa naenda kwa shemeji yangu kila baada ya wiki kumjulia hali yeye na wanae.

Huyu Binti ambae alikuwa akijulikana kwa jina la Katarina mwenyeji wa kule Iringa alitokea kunipenda kweli na hakuficha hisia zake, kalikuwa ni kabinti kazuri na kadogo sana na kalikuwa na heshima kweli.

Siku moja shemeji yangu aliniambia kwa utani lakini, kuwa Katarina ananipenda na Kama nikitaka kuoa basi nisitafute mwanamke mwingine bali Katarina angenifaa zaidi.

Sikutilia maanani kauli ya shemeji yangu, na niliichukulia kama utani tu. Nilikuwa kila nikienda kwa huyo shemeji yangu Katarina atahakikisha ananipikia na kuniandalia maji ya moto ya kuoga tena kwa heshima kweli na nikishaoga kama nitalala pale alipenda sana kupiga soga na mimi na alikuwa akivutiwa sana na simulizi zangu za uongo na kweli.

Ilitokea nilipata kazi moja ya muda mfupi ambapo nililazimika kwenda Msolwa Morogoro ambapo nilikaa kwa miezi sita niliporudi nilikaa kama mwezi mmoja kabla sijaenda kwa shemeji yangu ambaye alikuwa akiishi Mbezi kwenye nyumba yake mwenyewe kumjulia hali.

Siku moja nilijikuta nikipata hamu sana ya kwenda kumuona shemeji yangu na nakumbuka ilikuwa ni mwaka 1994 mwishoni. Nilipotoka kibaruani jioni nilikwenda kwa shemeji yangu, lakini nilipofika nilikuta kuna mtumishi mwingine pale nyumbani, nilikaribishwa na kwa bahati mbaya shemeji yangu hakuwepo nyumbani alitoka kidogo kwenda kwa shoga yake aishiye mtaa wa pili.

Kumbuka kwamba kipindi hicho kulikuwa hakuna simu za mkononi, ilibidi nikae pale sebuleni peke yangu kwani hata watoto wa shemeji walikwenda kwa marafiki zao kusoma tuisheni.

Nilikaa pale sebuleni peke yangu kama saa moja na nusu na ndipo shemeji akarudi na aliponiona alifurahi sana. Tulizungumza mambo mengi sana lakini sikumsikia akimzungumzia Katarina, mwishowe ikabidi nimuulize. “Shemeji, tangu nimefika hapa sijamuona Katarina, mchumba wangu, je yuko wapi?” niliuliza kwa utani.

Niliona uso wa shemeji yangu ukisawajika kwa huzuni na alinyamaza kimya kwa sekunde kadhaa, kabla hajasema kitu alimuomba yule binti aliyenipokea ambaye niliambiwa ni mtumishi wa pale nyumbani amletee maji ya kunywa.

Muda wote tukisubiri maji yaletwe tulikaa kimya na alionekana kuwaza sana, hali ile ilinitisha sana. Mara maji ya kunywa yakaletwa, alikunywa funda kadhaa za maji kisha akaweka ile glasi chini na kushusha pumzi ndefu, kisha akasema.

“Shemeji ni jambo la kusikitisha kukujulisha kuwa Katarina alifariki wiki iliyopita na taarifa hizo tumezipata juzi” Alisema shemeji yangu kwa upole, niliposikia taarifa ile kuna kitu kilinichoma moyoni kama msumari wa moto na nilijihisi kama natetemeka na kijasho chembamba kilinitoka.

“Amefia wapi, aliugua nini, na amezikwa wapi?” yalinitoka maswali mengi mfululizo.
Shemeji yangu alinisimulia kuwa, aliamua kumtafutia shamba boy wake wa zamani kibarua katika kiwanda fulani cha wahindi kwa kuwa alitarajia kuoa na kabla ya kuanza kazi alimtuma kwao Singida akamletee shamba boy mwingine ili amfundishe kazi awe ni mrithi wake kabla hajaanza kazi yake mpya.

Alikwenda Singida na akaja na huyo kijana na baada ya kumfundisha alikwenda kuanza kazi na kumuacha yule kijana mpya pale nyumbani.
Kumbe kuna siku yule kijana shamba boy mpya alimbaka Katarina, lakini alimtisha kuwa akisema atamuua na kukimbilia kwao Singida asionekane tena.

Katarina aliogopa kusema na akabaki kimya akiugulia maumivu baada ya kitendo kile. Haikupita muda , yule binti alianza kuumwa umwa na kutapika kusikoisha, ikawa kila anachokula anatapika. Utendaji wa kazi ukapungua na akawa anatumia muda mwingi sana kulala. Shemeji yangu akajenga wasiwasi ikabidi amdadisi kama ana mimba.

Awali Katarina alikataa katakata kuwa si mjamzito, lakini shemeji alimtishia kuwa atampleke Hospitali kesho yake akapime ili kujiridhisha Katarina alikiri kuwa ni mjamzito. Sasa Shughuli ikawa kwenye kumtaja mhusika, Katarina alikataa kabisa kumtaja mhusika shemeji ilibidi atumie mbinu ya kumtisha kuwa atampeleka Polisi na ndio akamtaja yule kijana lakini alisema kuwa alitishwa sana kuwa akimtaja atamuua ilibidi shemeji amfuate yule kijana chumbani kwake ili kumdadisi lakini kumbe yule kijana alikuwa akifuatilia ule mzozo kupitia dirishani na aliposikia jina lake likitajwa kuhusika na ile mimba alitoweka haraka sana asijulikane alipokwenda.

Ilibidi shemeji abaki na ule mzigo, kwanza alikuwa ni mjane pili hakuwa na mfanya kazi wa Ng’ombe maana yule kijana katoweka na pia mtumishi wake wa ndani yaani Katarina ndio huyo ni mjamzito, na yeye ni mtumishi serikalini, ilikuwa ni kaazi kweli kweli.
 Ilibidi afanye mawasiliano na marafiki zake na kwa kushirikiana na yule boy shamba wake wa zamani alifanikiwa kupata mfanyakazi wa ng’ombe mwingine, na baada ya wiki akapata House girl mwingine.

Baadae alimshauri Katarina arudi kwao Iringa na alimuahidi kumpa pesa ya kutosha ili imsaidie kujifungua na akijifungua alimtaka arudi kwake ili aendelee na kazi.
Ni kweli Katarina alikubali japo shingo upande na alikuwa na wasiwasi jinsi atakavyopokelewa nyumbani kwao na wazazi wake.
 Baada ya wiki moja Katarina alipakiwa ndani ya basi na kurudishwa Iringa na yule Shamba Boy wa zamani. Shemeji aliandika barua ndefu kueleza mkasa uliompata Katarina ili wazazi wake wasije kumuadhibu.

Aliporudi kutoka Iringa yule shamba boy aliyempeleka Katarina alisimulia kuwa walipokelewa lakini kwa wasiwasi kutokana na hali aliyokuwa nayo Katarina. Na kama si ile barua alioandika shemeji, basi yule shamba boy angelipishwa mahari na kuozeshwa yule binti, lakini ile barua iliposomwa ndio wakaamini japokuwa wapo walioitilia mashaka kuwa huenda imetengenezwa makusudi ili kumnasua yule kijana. Hata hivyo yule binti alikanusha kuwa yule kijana aliyefuatana naye hahusiki.
 Baada ya kupita mwezi mmoja shemeji yangu alipokea taarifa kuwa Katarina alifariki wiki moja iliyopita baada ya jaribio la kutoa mimba kushindikana.
Taarifa zaidi zilisema kuwa alipata manyanyaso pale nyumbani kwao kwa wazazi wake kutokana na kwamba walikuwa wanamtegemea na baada ya kurudi pale nyumbani wakawa wana hali ngumu na hivyo kumtupia Katarina lawama kuwa amekuwa mzembe kaharibu kazi kwa umalaya.

Katarina alikusudia kuitoa mimba ile ambayo ilishatimiza miezi sita na ndipo ikashindikana na akapoteza maisha yeye na kiumbe kilichokuwa ndani.
Nilishikwa na butwaa wakati wote shemeji yangu alipokuwa akinisimulia mkasa huo wa Katarina.
Ni miaka 15 sasa tangu binti huyu afariki Dunia, lakini leo katika hali ya kushangaza nimetokea kumkumbuka, sijui ni kwanini.

Dada Yasinta nakuomba uuweke mkasa wa binti huyu katika blog yako kama Dedicationa kwa binti huyu ambaye alifariki mwezi huu wa Oktoba japo tarehe siikumbuki.
Ni mimi msomaji wa blog yako Miki Malissa

Friday, March 11, 2011

MAISHA/MILA,UTAMADUNI NA DESTURI:- SIKU YANGU ILIVYAKUWA LEO....MAZISHI!!!

Sijui nianzia wapi??
Ok ni hivi:- Jana Alhamisi nilikuwa kazini, na baada ya kazi kama kawaida ya watu wote huwa wana hangaika na mihangaiko au kuridi nyumbani na kupumzika. Kwa hiyo nami nilifanya hivyo jana nilikuwa na mihangaiko yangu na baadaye nikarudi nyumbani. Ile kuingia tu ndani nikakumbana na mlio wa simu, kuangalia sioni jina yaani limefichwa, hata hivyo sikusita nikapokea.

Oh! Kumbe wewe Mariana, ndiyo mimi Yasinta, hali yako? Salama tu......tukaendelea maneno mawili matatu...Oh, nilisahau Mariana ni rafiki yangu anatoka Angola. Basi pale tukawa tunapeana habari za hapa na pale na mara akaniambia kuwa rafiki yetu mwingine kutoka Serbien kafiwa na mamamkwe wake na mazishi ni kesho yaani leo.

Hapo nikawa hoi, ingwa huyo mama mkwe wa rafiki yetu Saida sijawahi kumwona hata siku moja. Nikashikwa na uchungu sana. Kwa hiyo nikakata shauri kwenda kwenye mazishi yake ambayo yalikuwa leo. Mamamkwe wa Saida anaitwa Maria amefariki akiwa na miaka 82.

Tulikuwa na misa na baadaye tukaunganika na kumsindikiza mamamkwe Maria kwa safari yake ya mwisho. Kulikuwa na watu 23 na Padre 24. Nasikitika sana kuwa sijaweza kupiga picha nilisahau kamera yangu nyumbani. Mamamkwe Maria na Ustarehe kwa Amani Peponi Amina!!

Monday, March 22, 2010

Aliyedaiwa kufa na kuzikwa aibuka hai!!!

MKAZI wa mjini Mafinga ambaye alidaiwa kufa na kuzikwa mwezi Oktoba mwaka jana, amerejea kwao akiwa hai na kusema"sikumbuki kama niliwahi kufa".
Kijana huyo, Nickson Kabonge, 23, aliwasili nyumbani kwao juzi mchana akitokea msitu wa Kihanga ulio Mafinga ambako amedai alikuwa akifanya shughuli za kupakia mbao na magogo kwenye magari.
Wakati familia yake, na hasa baba ikiamini kuwa alishafariki na ilishiriki kumzika, kijana huyo aliiambia Mwananchi kuwa aliamua kurejea kwao baada ya kuota kila mara kuwa baba yake amefariki.
Kurejea kwa kijana huyo kulizua yaharuki kwa wakazi wa mjini hapa ambao walifurika nyumbani kwao kumshangaa, wakionekana kutoamini kuwa aliyerejea ni kijana waliyemzika na badala yake kumchukulia kuwa ni msukule.
Pamoja na kurejea kwao, baba wa kijana huyo, Boniface Kabonge alisema kuwa mwanaye Nickson alifariki dunia Oktoba 6 mwaka jana na kuzikwa kwenye makaburi ya Mufindi.
"Nilishtuka mwanangu alipobisha hodi na kuingia ndani wakati najua alishakufa na tulimzika, sijui imekuwaje hadi aliyekufa arejee nyumbani,"alisema
Alisema kabla ya kifo chake kijana huyo alikuwa akifanya kazi ya kupasua mbao kwenye msitu huo wa Kihanga, lakini alifariki baada ya kuangukiwa na gogo ambalo lilimjeruhi vibaya kichwani.
Alisema mwili wa kijana huyo ulipelekwa Hospitali ya Wilaya ya Mufindi na kuhifadhiwa katika chumba cha maiti hadi siku ya pili ulipopelekwa nyumbani kwao kwa ajili ya kuagwa.
"Mimi ndiye niliyemuosha mwanangu kutokana na mila zetu, tulimpeleka nyumbani watu waliaga kama kawaida na baadaye tulimzika kwa sababu kila mmoja alijiridhisha na kifo chake," alisema
Akizungumza na Mwananchi kijana huyo alisema hafahamu habari za kifo chake.
"Nashangaa wanaponikimbia ila sikumbuki kama niliwahi kufa, nachojua nilikuwa nikiishi na wenzangu kumi katika msitu wa Kihanga ambako tulikuwa tukila pumba na maji,"alisema
Alisema kuwa kilichomrejesha nyumbani kwao ni ndoto alizokuwa akiota kuwa baba yake amefariki hali iliyomlazimu arudi kuhani msiba.
"Kila nikikaa mwili wa baba yangu ulikuwa ukipita mbele yangu kwenye jeneza huku ukiwa umefunikwa kitambaa chekundu, ndio maana nikaamua kuja kumzika.
Nashangaa nilipofika hapa nikaambiwa kuwa mimi ndio nilikuwa nimekufa,†"alisema.
Kijana huyo alishangaa zaidi baada ya kuonyeshwa kaburi ambalo mwili wake umezikwa na akataka lifukuliwe kukujua ulizikwa mwili gani.
Jeshi la polisi limethibitisha kupokea taarifa za kurejea kwa kijana huyo ambaye mwili wake ulihifadhiwa katika Hospitali ya Mufindi kabla ya kuzikwa.
Mganga msaidi wa hospitali hiyo, Meshack Mlyapatali alisema wapo tayari kufanya uchunguzi wa kisayansi wa tukio hilo, lakini wanasubiri agizo kutoka serikalini au Jeshi la Polisi.
Baba yake alisema kija huyo amebadilika kwa kuwa siku hizi anazubaa na kujikunyata na kuwa wakati mwingine amekuwa akiweweseka kuwa anaona jeneza likipita mbele.

Nimeona si vibaya nikiweka habari hii hapa kibarazani kwangu kwani wote tuna nia moja ya kuhabarisha jamii.
Imeandikwa na Tumaini Msowoya, Mufindi


Thursday, February 4, 2010

SAYANSI YAKIRI BINADAMU HAFI, HUBADILIKA.

Kwa zaidi ya miongo miwili sasa, wanasayansi wamekuwa wakijitahidi kutafuta jibu la swali la, je binadamu anaendelea kuishi baada ya kupoteza mwili wake? Kuna wanaoonesha kwamba wanakubaliana na hilo na kuna wale ambao wanasema huenda hakuna kitu kama hicho.
Kwa mfano kuna wale wanasayansi ambao wanakiri kwamba, watoto wanaofahamika kwa jina la Indigo, ni watoto ambao wana akili kubwa kuliko zile za binadamu wa kawaida. Tafiti zinaonesha kwamba, watoto hawa walianza kuzaliwa hapa duniani kuanzia mwaka 1975. Ni watoto ambao uwezo wao katika kuelewa mambo ni mkubwa kuliko tulivyozoea kuona.

Baadhi ya watoto hawa, kutokana na uwezo mkubwa, wamekuwa wakikumbuka maisha yao ya nyuma, kabla hawajafa. Watoto hao wamekuwa wakisema waliishi zamani sana na kufa au kupoteza miili yao na kuja tena kuzaliwa mahali pengine.

Hakuna idadi maalum ya watoto hawa hapa duniani, lakini inadaiwa kwamba, wako wengi kiasi cha kufikia elfu kadhaa. Wanatofautiana pia kiuelewa, wengine wakiwa na kumbukumbu kali na uwezo mkubwa sana kiakili, kuliko wengine, ingawa wote wana ufahamu wa kiajabu.
Kwa nini wameanza kuzaliwa miaka ya 1975? Kuna nadharia nyingi zenye kujibu swali hilo. Moja kubwa ni ile inayohusisha ukuaji wa dunia na ulimwengu kwa ujumla. Kwamba itafika mahali, maarifa mengi yaliyojificha yataibuliwa. Kizazi cha watoto hawa kinadaiwa kwamba, kimekuja kumwonesha binadamu kwamba, amekuwa akiuchukulia ulimwengu na maisha, ndivyo sivyo.

Hivi karibuni mwanasayansi mmoja nchini India, amekiri kwamba binadamu anapokufa, huja kuzaliwa tena na kupewa mwili mwingine . Hii ina maana kwamba, sisi pia tumeshawahi kuishi huko nyuma kabla hatujafa na kurejea tena tukiwa na miili mipya, tuliyo nayo hivi sasa.
Mwanasayansi huyu Vikram Raj Singh Chauhan, amesema ana uhakika ataweza kuthibitisha hilo baada ya kukutana na mtoto wa umri wa miaka sita ambaye anakumbuka maisha yake ya nyuma kwa kiwango kikubwa sana. Mtoto huyo wa kiume, Taranjijt Singh anasema aliwahi kuishi miaka michache nyuma, ambapo alifariki kwa ajali ya pikipiki akiwa bado mdogo.

Mtoto huyo akiwa na umri wa miaka miwili alianza kusema kuhusu maisha yake ya nyuma na alikuwa akitoroka sana nyumbani . Alikuwa akiwaambia wazazi wake kwamba anakumbuka kijiji alichokuwa akiishi na hata jina la shule aliyokuwa akisoma.

Alikumbuka pia jina la baba yake wa zamani {kabla hajafa}. Awali ilionekana kama aina fulani ya kisirani cha mtoto, lakini ilibidi wazazi wake waanze kuwa na wasiwasi kwa kadiri alivyokuwa akiongezeka kiumri.

Mtoto huyo alikumbuka pia siku aliyokufa . Aliwaambia wazazi wake kwamba, alikufa September 10,1992. Alikufa baada ya kugongwa na pikipiki wakati akiwa kwenye baiskeli akiwa anakwenda shuleni asubuhi. Baada ya ajali hiyo alipata majeraha kichwani na alifariki siku ya pili baada ya ajali.

Baba yake wa sasa hivi, Ranjit Singh, anasema, mtoto wake alipozidi kusisitiza kuhusu maisha yake ya zamani, waliamua na mkewe kumpeleka huko kijijini anakodai kwamba, ndiko alikoishi kabla hajafa. Awali hawakuweza kumpata mtu ambaye alikuwa anafanana na maelezo ya mtoto huyu. Mkazi mmoja wa kijiji hicho aliwaomba waende kijiji cha jirani kinachofuata.

Kwenye kijiji hicho walikwenda kwenye shule ya kijiji ambapo mwalimu mkuu wa shule hiyo alithibitisha kamba, September 10, 1992 alikufa mwanafunzi wa shule hiyo kwa ajali ya pikipiki. Kupitia shuleni hapo, walibaini mahali wazazi wa mtoto yule aliyekufa kwa ajali ya pikipiki, walipokuwa wakiishi.

Ni kweli waliwakuta wazazi ambao walithibitisha kufiwa na mtoto katika tarehe na njia iliyoelezwa. Baba wa sasa wa mtoto huyu, Tanjit Singh alieleza kwamba, mtoto wao aliwaambia kwamba madaftari aliyokuwa nayo wakati wa ajali yalilowa damu baada ya ajali ile na alitaja kiwango cha fedha ambazo zilikuwa kwenye mkoba wake wa shule.

Mama wa zamani wa mtoto huyu ambaye kwa maana hiyo ni mama wa mtoto aliyefariki mwaka 1992 aliposikia hivyo aliangua kilio kikubwa , kwani maelezo hayo yalikuwa sahihi bila doa la kosa. Alisema vitabu na fedha hizo bado vipo, kwani aliviweka kwa kumbukumbu ya kifo cha mwanaye .

Baadae mtoto huyu alirudi na wazazi wake wa sasa nyumbani kukiwa na maswali yasiyo na majibu. Wazazi wake wa zamani pamoja na ndugu zake, walikwenda kumtembelea kwao baadae. Mtoto huyu aliibaini picha ya siku ya ndoa ya wazazi wake, ambayo walikuja nayo wakati walipokwenda kumtembelea kwa wazazi wake wapya.

Awali mwanasayansi, Vikram Chauhan, alikataa kukubaliana na maelezo kuhusu mtoto huyu , lakini baadae alijipa moyo wa kuanza uchunguzi. Alitembelea vijiji vyote viwili , cha zamani alikozaliwa na kufa na hiki cha sasa alipozaliwa.

Alizungumza na wazazi wote na kupata maelezo ambayo yalimfanya kuona kuna jambo la maana kuhusiana na kifo na ‘kufufuka’ kwa mtoto huyu. Kwenye kijiji alichozaliwa na kufa mtoto huyu, muuza duka mmoja alikiri kwamba ni kweli , mtoto kama huyo alikuwepo na yeye alimkopesha madaftari jana yake na alipogongwa alikuwa akielekea dukani kwake kumlipa madaftari hayo.

Chauhan alichukua sampuli ya mwandiko wa mtoto huyu na ule wa kwenye madaftari ya marehemu. Ilipokwenda kupimwa na wataalamu wa mwandiko, ilibainika kwamba, ilikuwa ni ya mtu mmoja.
Kumbuka kwamba mwandiko wangu hauwezi kuwa sawa na wa mtu yeyote, kama ilivyo alama za vidole. Kila mwandiko una sifa zake maalum ambazo haziwezi kupatikana kwenye mwandiko wa mtu mwingine.

Wataalamu wana uwezo wa kubaini mwandiko wa kughushi hata kama umefanywa na mtaalamu wa kiasi gani wa kughushi miandiko.
Kubwa zaidi ni kwamba mtoto huyu ambaye alishaanza kusoma kwenye maisha yake ya kabla ya kifo, hivi sasa hajapelekwa shule, kwa sababu familia yake ya sasa ni maskini. Hata hivyo katika jambo la kushangaza zaidi alipotakiwa kuandika alifabeti za kiingereza na ki-punjabi aliweza kufanya hivyo bila tatizo. Kama hajasoma ingewezekana vipi kufanya hivyo? Anatumia akili ya zamani ya kabla hajafa.

Familia yake ya zamani imeomba kukabidhiwa mtoto wao, lakini familia yake ya sasa imesema hapana, huyo ni mtoto wao. Kisheria, bila shaka, familia yake ya sasa ambayo ni maskini sana, wakati ile ya zamani ilikuwa na uwezo, ndiyo yenye uhalali wa kuishi na mtoto huyu.
Huenda baada ya sayansi kuthibitisha kwamba watu hufa na baadae kurudi wakiwa wanamiliki miilia tofauti, familia kama hii ya zamani ya mtoto huyu, ndipo itakapoweza kupata haki.

Hata hivyo, bila shaka kila familia kati ya hizo mbili, itakayoishi naye, itakuwa na mashaka ya aina fulani.

Mwanasayansi kama Chauhan na wengine wanaamni kwamba, kama roho ikihama kutoka mwili mmoja na kwenda mwili mwingine, huenda huko na akili au mawazo na hisia pia. Kinachoachwa ni mwili unaoonekana, lakini hiyo miili mingine huwa pamoja. Hii ina maana kwamba, hata mwandiko utabaki kuwa uleule kama ilivyokuwa.
Chauhan anasema, hivi sasa anao ushahidi wa kisayansi kuthibitisha kwamba, binadamu anapokufa, huja kuzaliwa tena, lakini hutumia mwili mwingine. Hata hivyo anasema anahitaji muda zaidi kuthibitisha jambo hili.

Bila shaka, ushahidi wa wazi kabisa kuhusu watoto hawa wa indigo, unaweza kutuonesha kwamba, tunapokufa, maana yake tumepoteza mwili , lakini bado hisia, akili, na roho ambavyo huja kuingia kwenye mwili mwingine ambao utatengenezwa na wazazi wengine wawili au wale wale, vinakuwepo.

Ni vigumu kupingana na maelezo ya mtoto huyu, ambaye tangu akiwa na umri wa miaka miwili, alikuwa akizungumzia kuhusu kumbukumbu alizonazo juu ya maisha yake ya nyuma. Ugumu wa kupinga unatokana na ukweli kwamba, hatimaye maelezo yake yalithibitika.
Kama ingekuwa Chauhan sio mwanasayansi, tungeweza kusema, suala hili bado, halijatazamwa kisayansi na hivyo, haliwezi kuelezewa kama jambo halisi.

Kwa mwanasayansi kuvutiwa na jambo hili na kuanza kulifanyia utafiti huku akikiri kwamba, kuna mambo yenye kutanza, ni hatua kubwa katika binadamu kuingia mahali ambapo atabaini ukweli wa kuwepo maisha baada ya kifo.

Lakini sio maisha baada ya kifo peke yake bali pia kukubali kwamba huenda binadamu ataendelea kuwepo, kwa sababu uwepo {being} haujapotea na hauwezi kupotea. Mwili wako utaharibika, lakini uwepo wa binadamu hauwezi kupotea.

Habari hii nimeipata katika gazeti la Jitambue la huko nyumbani Tanzania, ambalo siku hizi halichapishwi tena baada mmiliki wake Munga Tehenan kufariki dunia.

Sunday, December 27, 2009

KATARINA KWA NINI ULIKUFA?

Wapendwa wasomaji wa blog hii na wanablog wenzangu nimekuwa nikipokea email nyingi toka kwa wasomaji wa blog hii wa huko nyumbani Tanzania, wengi wakielezea uzoefu wao na wakitaka niziweke hapa ili tujadili kwa pamoja, na mimi sina kinyongo kwa kuwa blog hii inazungumzia Maisha, basi nitakuwa nikiziweka hapa ili wasomaji wengine wapate kujifunza

Leo nimewaletea kisa cha kusikitisha cha binti aitwae Katarina, naomba muuangane na msimulizi wa kisa hiki.

**********************************************************************

Alikuwa ni mtumishi wa nyumbani na alikuwa na umri wa miaka 14 wakati huo, nakumbuka ilikuwa ni mwaka 1993, ndio aliletwa kufanya kazi kwa shemeji yangu.
Nakumbuka nilikuwa naenda kwa shemeji yangu kila baada ya wiki kumjulia hali yeye na wanae.

Huyu Binti ambae alikuwa akijulikana kwa jina la Katarina mwenyeji wa kule Iringa alitokea kunipenda kweli na hakuficha hisia zake, kalikuwa ni kabinti kazuri na kadogo sana na kalikuwa na heshima kweli.

Siku moja shemeji yangu aliniambia kwa utani lakini, kuwa Katarina ananipenda na Kama nikitaka kuoa basi nisitafute mwanamke mwingine bali Katarina angenifaa zaidi.

Sikutilia maanani kauli ya shemeji yangu, na niliichukulia kama utani tu. Nilikuwa kila nikienda kwa huyo shemeji yangu Katarina atahakikisha ananipikia na kuniandalia maji ya moto ya kuoga tena kwa heshima kweli na nikishaoga kama nitalala pale alipenda sana kupiga soga na mimi na alikuwa akivutiwa sana na simulizi zangu za uongo na kweli.

Ilitokea nilipata kazi moja ya muda mfupi ambapo nililazimika kwenda Msolwa Morogoro ambapo nilikaa kwa miezi sita niliporudi nilikaa kama mwezi mmoja kabla sijaenda kwa shemeji yangu ambaye alikuwa akiishi Mbezi kwenye nyumba yake mwenyewe kumjulia hali.

Siku moja nilijikuta nikipata hamu sana ya kwenda kumuona shemeji yangu na nakumbuka ilikuwa ni mwaka 1994 mwishoni. Nilipotoka kibaruani jioni nilikwenda kwa shemeji yangu, lakini nilipofika nilikuta kuna mtumishi mwingine pale nyumbani, nilikaribishwa na kwa bahati mbaya shemeji yangu hakuwepo nyumbani alitoka kidogo kwenda kwa shoga yake aishiye mtaa wa pili.

Kumbuka kwamba kipindi hicho kulikuwa hakuna simu za mkononi, ilibidi nikae pale sebuleni peke yangu kwani hata watoto wa shemeji walikwenda kwa marafiki zao kusoma tuisheni.

Nilikaa pale sebuleni peke yangu kama saa moja na nusu na ndipo shemeji akarudi na aliponiona alifurahi sana. Tulizungumza mambo mengi sana lakini sikumsikia akimzungumzia Katarina, mwishowe ikabidi nimuulize. “Shemeji, tangu nimefika hapa sijamuona Katarina, mchumba wangu, je yuko wapi?” niliuliza kwa utani.

Niliona uso wa shemeji yangu ukisawajika kwa huzuni na alinyamaza kimya kwa sekunde kadhaa, kabla hajasema kitu alimuomba yule binti aliyenipokea ambaye niliambiwa ni mtumishi wa pale nyumbani amletee maji ya kunywa.

Muda wote tukisubiri maji yaletwe tulikaa kimya na alionekana kuwaza sana, hali ile ilinitisha sana. Mara maji ya kunywa yakaletwa, alikunywa funda kadhaa za maji kisha akaweka ile glasi chini na kushusha pumzi ndefu, kisha akasema.

“Shemeji ni jambo la kusikitisha kukujulisha kuwa Katarina alifariki wiki iliyopita na taarifa hizo tumezipata juzi” Alisema shemeji yangu kwa upole, niliposikia taarifa ile kuna kitu kilinichoma moyoni kama msumari wa moto na nilijihisi kama natetemeka na kijasho chembamba kilinitoka.

“Amefia wapi, aliugua nini, na amezikwa wapi?” yalinitoka maswali mengi mfululizo.
Shemeji yangu alinisimulia kuwa, aliamua kumtafutia shamba boy wake wa zamani kibarua katika kiwanda fulani cha wahindi kwa kuwa alitarajia kuoa na kabla ya kuanza kazi alimtuma kwao Singida akamletee shamba boy mwingine ili amfundishe kazi awe ni mrithi wake kabla hajaanza kazi yake mpya.

Alikwenda Singida na akaja na huyo kijana na baada ya kumfundisha alikwenda kuanza kazi na kumuacha yule kijana mpya pale nyumbani.

Kumbe kuna siku yule kijana shamba boy mpya alimbaka Katarina, lakini alimtisha kuwa akisema atamuua na kukimbilia kwao Singida asionekane tena.

Katarina aliogopa kusema na akabaki kimya akiugulia maumivu baada ya kitendo kile. Haikupita muda , yule binti alianza kuumwa umwa na kutapika kusikoisha, ikawa kila anachokula anatapika. Utendaji wa kazi ukapungua na akawa anatumia muda mwingi sana kulala. Shemeji yangu akajenga wasiwasi ikabidi amdadisi kama ana mimba.

Awali Katarina alikataa katakata kuwa ni mjamzito, lakini shemeji alimtishia kuwa atampleke Hospitali kesho yake akapime ili kujiridhisha Katarina alikiri kuwa ni mjamzito. Sasa Shughuli ikawa kwenye kumtaja mhusika, Katarina alikataa kabisa kumtaja mhusika shemeji ilibidi atumie mbinu ya kumtisha kuwa atampeleka Polisi na ndio akamtaja yule kijana lakini alisema kuwa alitishwa sana kuwa akimtaja atamuua ilibidi shemeji amfuate yule kijana chumbani kwake ili kumdadisi lakini kumbe yule kijana alikuwa akifuatilia ule mzozo kupitia dirishani na aliposikia jina lake likitajwa kuhusika na ile mimba alitoweka haraka sana asijulikane alipokwenda.

Ilibidi shemeji abaki na ule mzigo, kwanza alikuwa ni mjane pili hakuwa na mfanya kazi wa Ng’ombe maana yule kijana katoweka na pia mtumishi wake wa ndani yaani Katarina ndio huyo ni mjamzito, na yeye ni mtumishi serikalini, ilikuwa ni kaazi kweli kweli.

Ilibidi afanye mawasiliano na marafiki zake na kwa kushirikiana na yule boy shamba wake wa zamani alifanikiwa kupata mfanyakazi wa ng’ombe mwingine, na baada ya wiki akapata House girl mwingine.

Baadae alimshauri Katarina arudi kwao Iringa na alimuahidi kumpa pesa ya kutosha ili imsaidie kujifungua na akijifungua alimtaka arudi kwake ili aendelee na kazi.
Ni kweli Katarina alikubali japo shingo upande na alikuwa na wasiwasi jinsi atakavyopokelewa nyumbani kwao na wazazi wake.

Baada ya wiki moja Katarina alipakiwa ndani ya basi na kurudishwa Iringa na yule Shamba Boy wa zamani. Shemeji aliandika barua ndefu kueleza mkasa uliompata Katarina ili wazazi wake wasije kumuadhibu.

Aliporudi kutoka Iringa yule shamba boy aliyempeleka Katarina alisimulia kuwa walipokelewa lakini kwa wasiwasi kutokana na hali aliyokuwa nayo Katarina. Na kama si ile barua alioandika shemeji, basi yule shamba boy angelipishwa mahari na kuozeshwa yule binti, lakini ile barua iliposomwa ndio wakaamini japokuwa wapo walioitilia mashaka kuwa huenda imetengenezwa makusudi ili kumnasua yule kijana. Hata hivyo yule binti alikanusha kuwa yule kijana aliyefuatana naye hahusiki.

Baada ya kupita mwezi mmoja shemeji yangu alipokea taarifa kuwa Katarina alifariki wiki moja iliyopita baada ya jaribio la kutoa mimba kushindikana.
Taarifa zaidi zilisema kuwa alipata manyanyaso pale nyumbani kwao kwa wazazi wake kutokana na kwamba walikuwa wanamtegemea na baada ya kurudi pale nyumbani wakawa wana hali ngumu na hivyo kumtupia Katarina lawama kuwa amekuwa mzembe kaharibu kazi kwa umalaya.

Katarina alikusudia kuitoa mimba ile ambayo ilishatimiza miezi sita na ndipo ikashindikana na akapoteza maisha yeye na kiumbe kilichokuwa ndani.

Nilishikwa na butwaa wakati wote shemeji yangu alipokuwa akinisimulia mkasa huo wa Katarina.

Ni miaka 15 sasa tangu binti huyu afariki Dunia, lakini leo katika hali ya kushangaza nimetokea kumkumbuka, sijui ni kwanini.

Dada Yasinta nakuomba uuweke mkasa wa binti huyu katika blog yako kama Dedicationa kwa binti huyu ambaye alifariki mwezi huu wa Disemba japo tarehe siikumbuki.

Ni mimi msomaji wa blog yako Miki Malissa

Wednesday, August 19, 2009

KUFA NA KUZIKANA

Sijui nianze vipi?:- Mila na desturi, kweli kila watu wana zao. Nimeishi hapa Sweden sasa miaka mingi kidogo. Lakini bado sielewi pale panapotokea msiba (mtu kufa)

Nina maana hapa Sweden mtu akifa basi wahusika watatangaza kwenye gazeti na pia wanaandika lini mazishi yatakuwa. Sasa hapo ndipo nisipoelewa mimi, yaani hapa sasa sio kwamba kila mtu kuhudhuria msiba huo? la hasha. Ni lazima ualikwe na unapoalikwa ni lazima utoe taarifa kuwa utafika. Sababu kubwa ya kufanya hivyo wanataka wajue kwamba waandae chakula cha watu wangapi.

Sio kama nyumbani TZ mtu ana safari zake au alikuwa shambani, mara akasikia kwa fulani kuna msiba, basi ni kuataacha kila kitu na kwenda huko na kuungana na wafiwa. Kusema kweli mila za huku hasa kuhusiana na misiba inanichanganya sana.
Kuna siku niliwakuta watu wanazika na walikuwa watu watano tu yaani hata ndugu akisikia ndugu yake amekufa haendi kwenye msiba anasubiri kualikwa. Huku mtu hawezi kwenda msibani au kuzika ni mpaka awe rafiki au ndugu na hapo pia mpaka aalikwe. Yaani hata awe jirani hakuna mtu anaenda kila mtu na lwake .

Kitu kingine tena ambacho ni ajabu kidogo kwa mimi sijui wenzangu mnalijua hili. Ni hiki kitendo cha watu wakiwemo ndugu wa karibu wa marehemu kuondoka kanisani na kurejea majumbani mwao baada ya misa na kuuacha mwili wa marehemu hapo, yaani kwao huko ndio kuzika, baada ya hapo shughuli ya mazishi hufanywa na wazikaji wa kukodi ambao hulipwa kwa kazi hiyo, tena hakuna hata kulala matanga, shughuli inakuwa inaishia kanisani. Tofauti na TZ, nadhani wote tunajua nyumbani tunafanya nini. Kwa sababu kama unaenda kuzika ni lazima kuzika kwa maana kuhudhuria mpaka makaburuini na kuhakikisha mwili unafukiwa sio kuuacha mwili kanisana, halafu? Naamini mazishi ni wajibu wa wote waliofika pale kumsindikiza mwenzao katika safari yake ya mwisho yaani katika shamba la Mungu (makaburini) na sio kukabidhi mwili kwa watu wa kulipwa na nyie kuondoka na hamsini zenu.

Pia hapa kuna mtindo wa kuchoma mwili na halafu yale majivu kwenda kuyamwaga sehemu ambayo marehemu alikuwa anaipenda kama vile ziwani au mlimani. Na wengine wanazika au wanaweka kwenye chupa na kuhifadhi kwenye nyumba maalumu (minneslund) sehemu ya makumbusho.

Saturday, November 1, 2008

LEO NI SIKUKUU YA MAREHEMU


Leo hapa Sweden ni sikuuu ya marehemu labda sehemu nyingine pia ila sina uhakika. Kwa hiyo napenda kuwakumbuka Marehemu wote kwa sala hii:-

Salamu, Maria, umejaa neema,
Bwana yu nawe,umebarikiwakuliko wanawake wote,
Na Yesu, mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Maria mtakatifu, Mama wa Mungu,
Utuombee sisi wakosefu,
Sasa na saa ya kufa kwetu,Amina.
Marehemu wote wastarehe kwa amani, Amina.

Na hapa sala yangu:


Bikikira Maria mama wa msaada,
Na uwabariki watu wote wa dunia hii,
Uwaokoe katika dhambi. Amina.

Tuesday, September 16, 2008

KUFA

Kwa nini watu kwanza tunazaliwa halafu tunakufa. Wengine wanaishi dakika, saa, siku, miezi, mwaka, miaka na miaka. Mara nyingi nimekuwa nikiwaza neno KUFA lazima itakuwa ni pumziko la amani sana kulala kwenye lile sanduku giza na hali tulivu hakuna anayekusumbua peke yako.



Unajua kama una ndugu, jamaa na marafiki ambao hawakujali kwa nini kuishi peke yako hapa duniani wakati kuna uwezo wa kuwa upweke Kaburini. Afadhali kabisa kufa. Haya ni mawazo yangu.



Kama ilivyoandikwa: Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi akampulizia puani PUMZI YA UHAI na mtu yule akawa NAFSI hai.

Kufa ni kama kulala usingizi usio na ndoto. Yesu alifundisha hivyo.

Baada ya kufa ubongo unaharibika hauwezi kujua , wala kukumbuka kitu chochote. Hisia zote za moyo za kibinadamu hukoma kabisa mtu anapoishi.

"Kama mimi niishivyo, atangaza Bwana Mungu,..... kila ROHO ILIYO HAI(LIVING SOUL) ni mali yangu....... ROHO YULE ATENDAYE DHAMBI NDIYE ATAKAYEKUFA." Ezekieli 18;3-4.

Swali:- Kwa nini yesu alikufa na akafufuka na sio sisi wengine "wanadamu"?