Showing posts with label tanzania. Show all posts
Showing posts with label tanzania. Show all posts

Tuesday, August 29, 2017

HISTORIA FUPI YA WANGONI WAKIWA KATIKA ARDHI YA WASHONA WAKIJA KATIKA ARDHI YA TANZANIA

Historia ya Afrikas foto.

Mara baada ya kutokea vita vilivyofahamika kwa jina la mfekane kwenye miaka ya 1800, , vilivyokuwa vikihususisha makabila yalikuwa yakipatikana kusiniu mwa Afrika. Wangoni waliamua kuondoka na kusambaa Afrika mashariki na kati wakiwa na Kiongozi wao Zwangendaba. Wakati wanasambaaa Afrika mashariki na kati, Wangoni walipitia sehemu nyingi sana, zipo sehemu walizopokelewa kwa heri na zipo sehemu walizopokelewa kwa shari. Lakini ukweli ni kwamba Wangoni waliondoka Afrika kusini kutokana na vita vilivyotokea. Na sababu kubwa ya vita hivyo ni sera ya upanuzi ya mfalme wa kabila la Wazulu aliyefahamika kwa jina ka Tshaka Zullu. Kutokana na vita hivyo ambavyo pia vilihusisha hata watu wengine ambao hawakuwa Waafrika kama vile Wadachi na Waingereza. Hivyo Wangoni waliamua kuondoka kusini mwa Afrika na kuja Afrika ya mashariki na kati. Sasa wakati wanakuja Afrika ya kati na mashariki Wangoni walipita sehemu nyingi sana. Moja ya sehemu ni ardhi ya Washona . Kwa ufupi ni kwamba Washona ni moja ya jamii zinazopatiakana katika ardhi ya Zimbabwe. Na zaidi jamii ya Washona wanapatikana mashariki mwa jamii za Wakalanga ( hii ilikuwa moja ya sehmu ambayo Wangoni walipita mara baada ya kuvuka mto Limpopo). Washona waliamia maeneo hayo wakiongozwa na mtemi wao aliyefahamika kwa jina la Ska-vunza kwenye karne ya 18. Na ifahamike kuwa Washona ni moja ya kabila ambalo linapatiakna katika kundi hili la Wangoni. 

Monday, February 1, 2016

NI MWEZI MPYA: NA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO IMEONA TUANZA HUU MWEZI KIHIVI:- TUANGALIE MISEMO NA METHALI TOKA TANZANIA NA MAANA YAKE....!

1. Anayetembea huokota, anayekaa huvimba tumbo (Kikerewe)
Maana ya methali hii ni kwamba riziki hupatikana kwa kutafutwa siyo kwa kukaa tu na kusubiri. Methali hii hutumika kwa wale wasiojishughulisha na kwa wale wanaojishughulisha na kufanikiwa kwa kudhihirisha ukweli wa juhudi yao

2. Atembea na moto mgongoni (Kibena)
Maana ya methali hii ni kwamba kama wewe si mkarimu, basi ujitegemee mwenyewe kwa kila kitu popote pale utakapokwenda. Methali hii hutumika kama fundisho kwamba hakuna mtu anayeweza kutenda kila jambo bila msaada wa wenzake Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu.

3. Penye majani makavu mabichi hayawaki (Kizigua na kinguu)
Maana  yake nikuwa penye wazee ni heshima kwa watoto au vijana kuwaachia wazee wakate mashauri; ikiwa vijana watakata shauri mbele ya wazee ni utovu wa adabu. Hutumika kuwaonya watoto wawe na heshima mbele ya wazee hasa katika kusema.

4. Siku hufanana laini hazilingani (Kiha)
Maana ya methali hii ni kuwa kila mtu anayo bahati yake, leo wewe kwsho mwingine. Methali hii hutumika wakati wa kufariji mtu aliyepatwa na maafa.

5. Kichwa cha msitu (Kipare)
Maana yeke, kichwani mwa mtu kuna siri nyingi kama ulivyo msitu mkubwa. Methali hii hutumika wakati wa kuwambia watu kuwa hata kama ukifanya nini, huwezi kuzifahamu siri za mtu. Ni yeye peke yake anayeweza kuzifahamu siri zake mwenyewe. Huweza pia kutumika kwa kuwaonya watu wasiwadharau wengine wanapokuwa kimua kwani huenda wanafikiri mengi kichwani mwao.

6. Kushindwa na kufa ni mapacha (Kimasai)
Ushujaa huheshimiwa sana katika jamii kwa sababu unadumisha ulinzi wa nchi. Ushujaa na ujasiri vikipunguka maadui wa kila aina na dhiki kadha wa kadha husumbua jamii. Mashujaa wakishindwa basi jamii hufadhaika kwani mipango yake yote huvurugika. Methali hii hutumika kama onyo na pia kwa kukaza ujasiri.

7. Leo ni ugali wa kumpigia mbwa kiko cha mkono (Kisukuma)
Maana yake ni kwamba leo tunakula nyama. Mara nyingi Wasukuma hawapendi kumchinja ng`ombe bila sababu maalum. Kwa hivi hutumia mboga za majani kama kitoweo, wapatapo nyama hugawana mikononi wakati wa kula kwa hiyo hutumia kiko cha mkono kumfunza mbwa anayekaribia. Hutumika wakati mtu anapotunukiwa kitu kizuri.

8. Maneno mengi huvunja nyumba (Kichaga)
Maneno mengi nyumbani huvuruga unyumba kwa sababu mwisho wa maneno hayo ni ugomvi uletao mafarakano. Methali hii inatumika kama onyo kwa jamaa, ikiwa kumbusha kwamba maneno mengi ndio chanzo cha kugombana na kukosana.

Naona kwa leo inatosha lakini kama nawe unayo Misemo/methali usisite kuongezea...elimu ni kugawana...TUPO PAMOJA

Saturday, August 23, 2014

Wednesday, July 9, 2014

LEO TUANGALIE BAADHI YA MISEMO NA METHALI TOKA TANZANIA

1. Mtoto wa kwale hapotezi njia yake (Kibena)
2.  Mtoto wa nyoka hukua na sumu yake (Kisambaa)
3. Mtoza ushuru sokoni huvumilia (Kichaga)
4. Mtu hodari husifiwa na watu (Kizigua na kinguu)
5. Mtu si sikio (Kiiraqw)
6. Muwa mmoja haujazi mtungi (Kipare)
7. mvua ya vuli imeanza (Kinyakyusa)
8. Mwanamke ni kambalemamba huamshwa na mkuki  (Kikerewe)
9. Ukiona mishale nyanyo ziko nyuma (Kimasai)
10. Kucheka hakuna majira, chenya majira ni kilimo (Kiha)
11. Tumbo la nguruwe halipasuliwi mbele ya watoto (Kisukuma)
12. Wazee walimtoa nyoka katika pua ya mwene (Kifipa)
KAMA NAWE UNA CHA NYONGEA KARIBU SANA SI MNAJUA  TUPO PAMOJA.....JUMATANO NJEMA SANA KWA WOTE..PANAPO MAJALIWA .  KAPULYA

Thursday, May 8, 2014

WAGONJWA WA DENGUE WAFIKIA 376

Na Hudugu Ng'amilo
Homa ya dengue inaendelea kushika kasi nchini baada ya takwimu za Januari hadi juzi kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, kuonyesha kuwa watu 376 wamekwishagundulika kuugua ugonjwa huo.
Mtaalamu wa Ufuatiliaji wa Magonjwa wa wizara hiyo, Dk Janeth Mugamba alisema hadi jana watu wawili walikuwa wamepoteza maisha, idadi ambayo alisema inaweza kuwa kubwa zaidi endapo upimaji utafanyika katika kila wilaya. "Pengine idadi inaweza kuwa kubwa zaidi kwa sababu wengi hawapimwi, Ijumaa (kesho) tutatoa, taarifa zaidi," alisema.
Alisema Wilaya ya Kinondoni ina wagonjwa wengi zaidi, ikifuatiwa na Ilala na Temeke. Hata hivyo, alisema huenda wilaya zenye idadi ndogo ya wagonjwa hazijaweza kupima na kubaini watu wenye maradhi hayo ikilinganishwa na Kinondoni.
Juzi, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid alisema hali ni mbaya na wananchi wanatakiwa kuchukua hadhari wasipate maambukizi ya ugonjwa huo.
Mtafiti wa malaria, tabia za mbu na mazingira, wa Taasisi ya Afya ya Ifakara, Dk Nicholas Govela alisema tayari wameshatuma maombi ya kufanya utafiti wa kina kuwajua mbu wanaoeneza homa ya dengue nchini. "Utafiti huu utasaidia kujua ni mbu kiasi gani wameathirika na virusi hivyo. Tukifanya hivyo tutajua ukubwa wa tatizo, tutajua wanapatikana wapi zaidi na virusi vyao vimetokea wapi," alisema.
Dk Govela alisema ni lazima utafiti huo ufanyike ili kudhibiti maambukizi zaidi ya homa hiyo akisema zipo sababu kadhaa zinazohisiwa kusababisha maradhi hayo, ikiwamo ya wahamiaji kuleta virusi hivyo vinavyosababisha homa hiyo na kuambukizwa kwa njia ya kuumwa na mbu.
"Ugonjwa huu umeenea zaidi nchi za Amerika ya Kusini na Kusini mwa Bara la Asia. Hapa kwetu mbu hawa walikuwapo lakini ugonjwa wa dengue haukuwapo kwa kiasi hiki, ndiyo maana sababu zinazohisiwa zaweza kuwa ni wahamiaji," alisema.
Alisema maambukizi ya homa ya dengue hutokea baada ya mtu mwenye ugonjwa huo kuumwa na mbu hao aina ya Aedes Egyptiae na mbu hao wakichukua virusi, huvisambaza kwa watu wengine. "Inawezekana tatizo ni kubwa zaidi ya hivi inavyofikiriwa kwa sababu wanaokuja hospitali kupimwa na kugundulika ni wachache, wengi wasiofika hawawezi kujulikana," alisema.
Makazi duni hatarini zaidi
Daktari Kiongozi na Mtaalamu wa homa ya dengue, Mrisho Rupinda alisema watu wanaoishi katika makazi duni wapo hatarini kuathiriwa zaidi kwa sababu ya kuwapo kwa taka nyingi na madimbwi.
Alitoa mfano wa wagonjwa wa kwanza wilayani Kinondoni, akisema walitokea maeneo ya Kambangwa, Mwananyamala Komakoma ambako kulikuwa na madimbwi na bwawa la maji.
"Wagonjwa wengi huonekana zaidi kwenye makazi duni kwa sababu ya mpangilio mbovu na kuzagaa kwa taka. Lakini pia maeneo mengine ambayo watu huhifadhi maji kwenye matenki au ndoo kwa muda mrefu bila kuyafunika," alisema.
CHANZO MWANANCHI

Wednesday, March 12, 2014

SEHEMU FULANI TANZANIA :- TWENDEN WADOGO ZANGU TUTACHELEWA NAMBA....

Picha hii imenikumbusha enzi hizo:Amka, amka kumekucha x2  Twendeni shuleni.  au Panda, panda  panda, panda mlima panda  panda.....hapo mtu ulishaoga na sasa josho linakuvuja tena ...Duh  kaazi kwelikweli....Je? hapa ni mazingira ya wapi katika Tanzania yetu?

Thursday, January 30, 2014

KAMA KAWAIDA NI ALHAMIS LEO...TWENDE MPAKA MBUGA YETU YA RUAHA ILIYOPO KUSINI MWA TANZANIA!!!!!!!


Mbuga ya Ruaha :- Mbuga hii ni nzuri na ndogo ambayo haijulikani sana kana SERENGETI au NGORONGORO. Ipo kusini wa Tanzania, kama uonavyo kuna simba, tembo, nyati, twiga na wanyama wengine wengi wa pori ambao wanaipendezesha Mbuga hii kwa ukamilifu mazingira yetu ya Afrika/Tanzani....ALHAMIS IJIYO NA MBUGA MPYA...

Thursday, January 23, 2014

LEO TWENDE KUTEMBELEA MBUGA YA NGORONGORO...KARIBU TANZANIA YETU


Kama nilivyosema ALHAMIS ya wiki iliyopita nimeanzisha kipindi kipya kila Alhamis tutakuwa karibu na Mbuga moja kutoka nyumbani TANZANIA na leo tupo NGORONGORO .....TUONANE TENA ALHAMIS IJAYO  KATIKA MBUGA NYINGINE.

Wednesday, October 2, 2013

TUBAKI HAPA TANZANIA.......NA KWINGINE TENA BALI NI MKOANI RUVUMA KWETU!!!


MKOA WA RUVUMA -TANZANIA
MKOA WA RUVUMA:- Ni kati ya mikoa 26 ya nchi yetu Tanzania.
Mkoa wa Ruvuma umepewa jina kutokana na mto RUVUMA ambao ni mpaka wake wa kusini na Msumbiji. Mkoa wa Ruvuma unapakana na Ziwa la Nyasa na Mkoa wa Morogoro upande wa magharibi, mikoa ya Iringa na Lindi upande wa kaskazini na Mkoa wa Mtwara upande wa Mashariki. Kuna mikoa mitano ambayo ni (idadi ya wakazi katika mabano) Songea Mjini (131,336), Songea Vijijini (147924), Tunduru (247,976), Mbinga 404,799), na Namtumbo ni (185,131). Makao makuu ya mkoa ndipo Songea. Jumla ya wakazi wote katika Mkoa wa Ruvuma ni 1,117,166 (sensa 2002).
Makabila makuu katika Mkoa huu wa Ruvuma ni Wangoni, Wanyao, Wamatengo, Wandendeule na Wandengereko.
Karibu na Songea iko monasteri/Seminari kubwa ya Peramiho ya watawa wa Wabenedikto kama wengi mjuavyo.
Sehemu ya mashariki ya mkoa kuna barabara ya lami kutoka Dar es Salaam kupitia Makambako na Njombe hadi Songea. Barabara kuu kwenda Lindi ipo katika hali mbaya..
YATAKUJA MENGI KUHUSU MKOA HUU WA RUVUMA WENYE KUVUMA:-)
NA KAPULYA WENGU YUPO KINAMNA  ....MCHANA/JIONI NJEMA KWA WOTE.

Tuesday, September 3, 2013

TUSISAHAU METHELI ZETU ZA KISWAHILI....!!!!!

1. Yaliyopita si ndwele, tugange yajayo.
2. Yote yangáayo usidhani ni dhahabu.
3. Ungelijua alacho nyuki, usingelionja asali.
4. Radhi ni bora kuliko mali.
5. Ndugu wakigombana, chukua jembe ukalime, wakipatana chukua kapu ukavune.
NAWATAKIENI JUMANNE NJEMA WOTE NA KAMA UNA METHALI PIA ONGEZEA:-)

Thursday, June 20, 2013

MDADA KAONA KUWA MODE KWA SIKU MOJA SI MBAYA..AU SIJUI NIBADILI KAZI:-)

 Hapa sijui ndo madoido/madolido au sijui alikuwa anapigana kareti mweee kaaazi kweli
 Na hapa bonge la poozi na miondoka mwanana..hapa ni Jangwani seabreeze resort Dar es salaam. Ni sehemu nzuri sana kupunga upepo..ilikuwa mwaka huu mwezi wa mbili.
 Mmmmh...hizi nywele za kimasai zinawasha ..maana ndo nilikuwa nimesuka tu hapa:-)
Na hapa sijui anasoma misa maana utafikiri anasema bwana awe nanyiii...ni Jangwani tena ...Jioni njema. Na kwa taarifa fupi ni kwamba mkiona nipo kimya msiwe na shaka nipo lakini nitakuwa likizo na ndiyo muda wa kupumzika na kuwa na familia..TUSITUPANE NDUGU ZANGU.. TUTAONANA TENA PANAPO MAJALIWA...Kapulya

Saturday, June 15, 2013

JUMAMOSI YA LEO TUTEMBELEE MJI WA IRINGA..NA WIMBO HUU...

JUMAMOSI IWE NJEMA KWENU WOTE...UJUMBE:- Tumaini huzaa Furaha, Furaha huzaa Amani

Saturday, June 8, 2013

KILIMANJARO IONEKANAVYO TOKA ANGANI PICHA KAKA ERIK 2013 JANUARI

 mlima wetu Kilimanjaro
Hakika unapendeza na tuna haki ya kuutangaza mlima wetu Kilimanjaro...
nawatakieni wote JUMAMOSI NJEMA. UJUMBE WA LEO:- Vitu muhimu katika maisha sio vitu.

Saturday, May 25, 2013

TUSISAHAU NGOMA ZETU ZA ASILI ..NGOMA YA MGANDA HAPA KARIBUNI


 
Hay moja pili tatu uhuuuuuuuu, uhhhhh sikiliza hizo ngoma wangoni hao aaaaah eeeh yaani hapa nipo hoi kabisa...JUMAMOSI NJEMA JAMANI....

Tuesday, May 21, 2013

Wanafunzi waliokatishwa masomo kwa mimba wafunguka



Mmoja wa wanafunzi alyepata mimba akiwa kidato cha tatu

Mada hii imenigusa sana,,,,nimekuwa muda mrefu nikulalamika sana kuhusu hili yaaani kwanini wasichana waachishwe shule na sio wavukana pia. na kwanini wasichana wasipate muda wa kusoma baaada ya kupata watoto. ..soma hapa  china...mada hii nimeiipata http://maendeleonivita.blogspot.se/ soma mwenyewe!!!!
----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
WANAFUNZI wengi wanaosoma katika shule za sekondari wilayani Tunduru mkoani Ruvuma wanakatishwa masomo yao wanapofikia kidato cha pili na cha tatu baada ya kupata mimba na kuolewa wakiwa shuleni.
Hali hiyo inatokana na historia ya wakazi wa wilaya hiyo ambao ni kabila la wayao kutokuwa na mwamko katika elimu hasa kutokana na kutoa kipaumbele kwa desturi na mila za kabila hilo ambazo zinatoa fursa zaidi katika mila potofu za unyago,msondo na jando kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari hali ambayo inaathiri suala zima la elimu.
Takwimu ambazo zimetolewa na mkuu wa wilaya ya Tunduru Chande Nalicho zinaonyesha kuwa mwaka 2012 wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na sekondari mwaka huu walikuwa ni 2788 hata hivyo hadi kufikia mwezi Aprili mwaka huu ni wanafunzi 1710 tu ndiyo walioripoti hali ambayo inakwamisha maendeleo ya elimu.
Flavian Nchimbi kaimu afisa elimu msingi wilaya ya Tunduru anasema tatizo la mimba katika shule za msingi zimepungua ukilinganisha na miaka mitatu nyuma kulikuwa na mimba karibu 250 ambapo takwimu za mwaka jana zinaonyesha kuwa katika shule za msingi zililipotiwa mimba 16 na kwamba kuanzia mwezi Januari hadi Aprili mwaka huu imeripotiwa mimba moja tu.
Hata hivyo afisa elimu sekondari wilaya ya Tunduru Ally Mtamila amekiri tatizo la mimba na ndoa za utotoni kwa wanafunzi wa shule za sekondari kuwa ni kubwa ambapo wanafunzi wa kike wanakatishwa masomo kwa mimba au kuolewa.
Sarah Michael(15) mkazi wa Tunduru alikuwa anasoma katika shule ya sekondari Makita ambapo alipewa ujauzito akiwa kidato cha tatu na mwanaume ambaye alitoroka mara baada ya tukio hilo hali ambayo ilimfanya aishi kwa shida hadi alipojifungua salama mtoto wake wa kiume.
“Baada ya kupata ujauzito niliacha masomo wazazi walinipokea licha ya kupata misukosuko mingi hasa kutoka kwa baba yangu mzazi,nimejifungua naendelea kumlea mwanangu katika mazingira magumu sana kwa kweli nakumbuka shule mwaka huu ningekuwa namaliza kidato cha nne’’,alisema.
Sarah alisema anapenda sana kusoma lakini wazazi wake hawana uwezo wa kumsomesha hivi sasa hivyo endapo atampata mtu wa kumsomesha anaweza kuendelea na masomo ya sekondari na kwamba kitendo cha kupata mimba na kukatisha masomo yake kimetoa fundisho kubwa kwake hivyo hawezi kurudia makosa ambayo yameharibu ndoto za maisha yake.
Hata hivyo anasema baba yake ni mwajiriwa wa serikali anafanya kazi ya uaskari magereza wilayani Mbinga ambaye kitendo cha yeye kukatishwa masomo kilimchukiza na alitaka mtuhumiwa kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria,hata hivyo wazazi wa pande zote mbili waliyamaliza na kufuta kesi.
“Hivi sasa baada ya mwanangu kukua nimemwomba baba anisomesha ili niweze kuendelea na masomo,lakini baba bado ana hasira amekataa na kusema ningoje kwanza nijifunze maisha kwa kuwa mimi niliacha shule na kukimbilia mambo yaliosababisha kupata mimba naendelea kumuomba radhi baba kwamba sitarudia tena nikipata nafasi ya kusoma’’,alisema kwa huruma.
Salima Hamad(15) mkazi wa Tunduru anasema alikatishwa masomo yake baada ya kupata mimba akiwa kidato cha tatu mwaka 2012 na kwamba wazazi wake walichukizwa na kitendo hicho ,walifungua kesi ya mwanaume aliyempa mimba,alikamatwa na kutiwa ndani hata hivyo mwanaume huyo ametorokea nchini Msumbuji hadi leo.
“Wazazi walinisakama pamoja na viongozi wa serikali ya kijiji,nilitamani kutoa mimba lakini nilipiga moyo konde,nilivumilia kulea mimba katika mazingira magumu kwa kuwa wazazi wangu ni masikini hadi nikajifungua salama kwa kufanyiwa upasuaji mtoto wa kike,natamani kusoma lakini sina uwezo’’,alisisitiza.
Salima anasema wazazi wake wamekataa kumsomesha na kudai kuwa hawana uwezo wa kumpeleka tena shule na hivi sasa anaishi kwa kujitazamia na kuuguza kidonda ambacho kimetokana na kujifungua kwa upasuaji.
Hemed Ally mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya msingi Frank Weston wilayani Tunduru anasema katika mafunzo ya msondo na unyago wanafunzi wa kike wanaelezwa faida za kuishi na mume lakini hawafundishwi madhara ambayo wanaweza kupata kwa kushiriki katika ndoa wakiwa wadogo hali hiyo ndiyo inawahamasisha wanafunzi kujiingiza kwenye ngono na kushawishika kuolewa na kupata mimba wakiwa wanafunzi.
Rehema Sara mwanafunzi wa kidato cha nne sekondari ya Mgomba anasema mila za unyago na msondo zimesababisha wanafunzi wengi wa kike katika shule hiyo kuacha masomo kwa kupata mimba au kuolewa ambapo hivi sasa katika darasa lao waliofanikiwa kufika kidato cha nne ni wanafunzi 106 tu kati ya wanafunzi zaidi ya 230 walioanza nao kidato cha kwanza mwaka 2010.
Sarah mkombozi wa kidato cha nne sekondari ya Mgomba ambaye alifanyiwa ngoma ya unyago na msondo akiwa darasa la tatu amekiri moja ya mambo ambayo wanafundishwa katika msondo na unyago ni kufanya mapenzi na watu wazima na kwamba kukataa kufanya hivyo ni kuvunja mila na desturi za wayao’’,alidai mwanafunzi huyo.
“wenzangu wengi ambao nilikuwa nao shule ya msingi na wengine ilitakiwa niwe nao sekondari wameacha masomo kwa kuwa wana watoto baada ya kupata mimba na wengine wameolewa na kuachika hivyo wanaangaika na maisha’’,alisisitiza.
Mkuu wa wilaya ya Tunduru Chande Nalicho amekiri mila na desturi za kabila la wayao zinachangia wilaya hiyo kuwa duni kielimu hata hivyo amesema tayari serikali imeunda kikosi kazi cha kuonana na viongozi wa mila, makungwi na manyakanga kuwaelimisha juu ya utoaji wa elimu kwa watoto wa kike kupenda masomo tofauti na sasa ambapo kundi hilo limekuwa likifundishwa kukabiliana na maisha ya ndoa hali iliyosababisha kuwepo kwa matukio mengi ya ndoa za utotoni wakiwa shuleni.
“Mila na desturi za kabila la wayao kuwafanyia unyago wanafunzi ndiyo chanzo kikuu cha tatizo hili,sisi kama serikali ili kukabiliana na tatizo hili tumefanya vikao na viongozi wasiokuwa rasmi lakini wanakubalika katika jamii wakiwemo makungwi, mangariba, masultani,mamwenye,mashehe na maimamu kwa kuzingatia tumejadili kwa pamoja tatizo hili”,anasisitiza.
Kwa mujibu wa Takwimu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, wasichana 8000 kila mwaka huacha shule kutokana na ujauzito. Kati yao 3,000 ni wanafunzi wa shule za msingi.
Kila siku, wanawake 24 hufariki dunia kutokana na mimba au wakati wa kujifungua. Wanawake watano mpaka sita wanaofariki kati ya hao ni watoto wadogo, watoto hao hufariki dunia kwa kuwa miili yao haijakomaa vya kutosha kwa ajili ya kujifungua.
Naibu mwakilishi mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Watoto (UNICEF), Mohamed Safieldin anasema mbali na athari hizo, pia virusi vya ukimwi (VVU), vinavyosambaa kwa kasi kwa wasichana hao. Tanzania kuna watoto yatima milioni 1.3 walioathirika kwa ukimwi.

Wednesday, April 17, 2013

BIBI KIDUDE AMEFARIKI DUNIA MAPEMA ALFAJIRI LEO..UTAKUKUMBUKWA DAIMA!!

Hapa ni Bi Kiduka katika uhai wake akipiga ngoma..
Upumzike kwa amani utakumbukwa daima.

Monday, April 1, 2013

MWEZI WA NNE(APRILI) NI MWEZI KUKUMBUKWA NA MUHIMU KWA HISTORIA YA NCHI YETU

Kwa watanzania wengi ambao wanafuatailia historia na kukumbuka masuala muhimu ya nchi hii mwezi huu una mambo muhimu ya kukumbukwa kutokana na matukio makuu yasiyopungua manne.
Kama ifuatavyo hapa chini.
Ø Baba wa Taifa hayati mwalimu Nyerere alizaliwa mwezi hu wa nne 13/04/19922.
Ø Muungano kati ya iliyokuwa Tanganyika na Zanzibar kuzaliwa kwa Tanzania Ulizaliwa mwezi wa nne 26/04/1964.
Ø Rais wa kwanza wa Zanzibar hayati shekh Abeid Aman Karume aliuwawa mwezi huu wa Nne tarehe 07/04/1972
Ø Aliyekuwa Waziri mkuu wa tatu wa Tanzania Hayati Edward Moringe Sokoine alifariki mwezi hu wa nne tarehe 12/04/1984.
Ø Na kwa mwaka 2013,unaongeza tukio lingine la kuanza utaratibu mpya wa kujadili na kupitisha bajeti ya Serikali kuanzia tarehe 9/4/2013.
Ø Mwaka 2014 utakuwa na tukio muhimu na nyeti litaongezeka katika mwezi huu kutokana na kuendelea kwa mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya ya Tanzania ambayo inatarajiwa kuzinduliwa tarehe 26/04/2014,wakati muungano utakapokuwa unatimiza miaka 50.
Kutokana na matukio manne ya awali tunatakiwa kuwaenzi mzee wetu hayati Abeid Karume, Julius K Nyerere na Edward M. Sokoine ,kuna umuhimu kwa Watanzania kupewa au kukumbushwa kuhusu historia ya Viongozi hawa na tukio la muungano, viongozi hao wana michango ya aina yake katika historia ya nchi hii na kutokana na hilo tunatakiwa kujiuliza nini kama jamii tunaweza kujifunza na kuiga kutoka kwao kwa faida ya kizazi hiki na kijacho.

07/04/1972-KUUWA KWA HAYATI KARUME KWA KUPIGWA RISASI.
Mambo ya kukumbukwa aliyasimamia hayati karume.
Hayati karume aliweza kuwaongoza wazanzibar kuwaondoa watawala wa kisultani
Historia inatuonyesha kuwa karume alikuwa baharia/mvuvi. Karume alisoma mpaka darasa la nne. Kwa kusoma na kuishi darasa la nne na pia kwa kuwa baharia inamaanisha kuwa kiongozi bora na jasiri hakuhitaji kwenda shule kubwa,Uongozi ni kipaji/kujitolea na kujituma. Kiongozi anatakiwa kuongozwa na Uzalendo na siyo ubinafsi kama ilivyo kwa viongozi wengi.

Karume kutokana na kuongozwa na kanuni ya maadili ya asili aliweza kufanya maamuzi ya kijasiri bila ya kujifikiria yeye kwanza pale alipokubali kuunganisha Zanzibar na Tanganyika na kuzaliwa Tanzania,Inasadikiwa kuwa kabla ya Tanganyika kuungana na Zanzibar Mwalimu hayati JK Nyerere alitaka tuungane na Kenya Kenyatta akakataa. Kwa kukubali kwake kuungana na Tanganyika alipoteza sifa ya Ukuu wa Nchi na kuwa Makamu wa Rais kitu ambacho kama hakuwa anaongozwa na uzalendo asingekubali pamoja na kuwa kulikuwa na sababu zingine za kiusalama na za kuharakisha uhuru wa nchi zingine za kiafrika bado kwa uamuzi wake anaingia katika viongozi waliotanguliza uzalendo kwanza kabla ya ubinafsi.

Kutokana na kukubali kwake kuungana na Tanganyika Muungano huu umekuwa wa kuigwa na unaendelea kudumu pamoja na kasoro za hapa na pale. Kuna nchi nyingi za Afrika zilijaribu kuungana lakini kutokana na ubinafsi wa viongozi wa nchi hizo muungano wao haukudumu mfano Senegambia muungano kati Senegal na Gambia.

Karume alikuwa mtu wa vitendo kiongozi anayeonyesha kwa mifano halisi na hai ya kuwatumika wananchi alianzisha wazo la kujenga nyumba za kuishi watu wa maisha ya kawaida Michenzani.

Karume pia aliweza kutoa maamuzi ambayo yanaweza kufananishwa na mzazi katika familia kwa kumteua Dkt Salim A.Salim kuwa balozi mdogo wa Tanzania nchini Misri akiwa na umri wa miaka 22,ambapo katika hali ya kawaida Dkt Salim alikuwa anaonekana mchanga na mdogo na kwa mazoea ya viongozi hata katika ngazi ya familia angeweza kusema huyo ni Taifa la kesho au kiongozi wa kesho. Kwa kumteua Dkt Salimu karume alidhihirisha kuwa ni kiongozi ambaye anaamini kuwa hata vijana wanaweza kusimamia majukumu katika ngazi mbalimbali pale watakapokabidhiwa madaraka hayo kwa nia njema. Kudhihirisha kuwa chaguo lake halikuwa la kubahatisha Dkt Salim alipanda hadi kufikia kutaka kuwa katibu mkuu wa Umoja wa mataifa kama kusingekuwa na mizengwe ya mataifa makubwa. Ikubukwe kuwa dkt Salim ni mmoja kati ya makatibu wakuu wa uliokuwa umoja wa nchi huru za Afrika OAU kwa sasa AU ambaye ametumikia cheo cha ukatibu Mkuu kwa muda mrefu..

Hayati karume anatufundisha kuwa wazazi na viongozi wanatakiwa kuwaamini na kuwajengea moyo wa kujiamini na kujitumia vijana watoto wao ili waweze kusimamia na kutekeleza masuala mbalimbali. Fundisho kubwa tunalolipata kutokana na suala la KARUME kumteua Dkt salim kwa umri wa miaka 22,kuwa kuna umuhimu wa kuwaandaa vijana kuwa viongozi na wasimamizi katika ngazi ya kuanzia katika familia. Mfano tunatakiwa kuhakikisha kuwa tunawashirikisha vijana katika masuala ya utunzaji wa mali na rasimali katika ngazi ya familia na jamii.

Karume ametuachia changamoto kubwa ya kuifanyia kazi katika masuala yanayohusiana na pale tunapotakiwa kufanya maamuzi yanayohusiana na masilahi ya umma na kwa manufaa ya walio wengi. Swali wewe kama kiongozi unajilinganishaje na Mzee huyu ambaye hatuko naye kimwili lakini ambaye anaonekana bado yu hai na ataendelea kuwa hai.

Unajengaje uzima wa milele wa jina lako katika ngazi ya familia na jamii kama viongozi waliotangulia mbele ya haki?

TAREHE 12/04/2008
SOKOINE.
Historia inaonyesha kuwa Sokoine alikuwa ni waziri Mkuu wa tatu wa Tanzania alitanguliwa Nyerere,Kawawa. Alikuwa waziri Mkuu kwa vipindi viwili 1977-1981 na 1982-1984.
Sokoine alikuwa jasiri na alifanya kwa vitendo/alithubutu na aliweza. Kwa kifupi Sokoine alikuwa ana mtazamo wa kufanya kwa mkabala wa kuweza.

Kutokana na ujasiri aliweza kuthubutu na kutenda,Sokoine aliweza kuthubutu na kumshawishi mwalimu nyerere kupunguza baraza la mawaziri wakati huu baraza la mawaziri lilikuwa na mawaziri wapatao 26,alilipunguza na kuwa na mawaziri 13.

Sokoine ndiye muasisi wa kitu kinachoitwa daladala katika miaka ya 1980 lilikuwa shirika la usafiri Dar lilielemewa na idadi ya wakazi jijini Dar na kushindwa kuhimili wimbi hilo sokoine akaamuru kuanzishwa kwa usafiri wa watu binafsi ikumbukwe kuwa wakati huo suala la makapuni na biashara binafsi hazikuwa zinaruhusiwa daladala za mwanzo kabisa zilikuwa canter na zilijulikana kwa jina maarufu (Chai maharage) kutokana na kuwa na viti vya mbao mabenchi ambayo yalikuwa yanatumika sana katika migahawa na ambayo watu wa kipato cha chini hasa kwa jiji la Dar asubuhi walikuwa wanapata kifungua kinywa chai kuchanganya na maharage na maandazi au kitumbua na mkate.

Sokoine ndiye muasisi wa sheria ya nguvu kazi ambayo iliwezesha nchi hii kuwa na uzalishaji wa chakula cha kutosha kutokana na kuisimamia sheria hiyo ya nguvu kazi,Chanzo cha kijiji maarufu cha GEZA ULOLE.
Sokoine kam kiongozi wa kusimamia shughuli za Serikali aliongoza na kusimamia vita dhidi ya wahujumu uchumi (Tunaweza kusema yeye ndiye muasisi wa kweli wa kupiga vita hiki kitu kinachoitwa ufisadi.) pamoja na kuwa katika vita hiyo imeacha makovu lakini funzo tunalolipata ni kuwa Sokoine alijitolea kuwahudumia wanyonge wananchi waliowengi ambao kutokana na matokeo ya vita ya kagera makovu na machungu ya vita hiyo ilisababisha uchumi wa nchi kuyumba na baadhi ya wafanyabiashara kuitumia nafasi hiyo kwa manufaa yao kwa kuamua kuficha bidhaa muhimu ili ziuzwe kwa bei ya kulangua ( Kuliibuka biashara ya ulanguzi kurusha/Sukari, sabuni, hata sigara kwa wanaokumbuka vizuri kipindi cha miaka ya 1980) Vijana wengi wa wakati huo waliacha kusoma(shule za Msingi na sekondari) na kujiingiza katika biashara ya ulanguzi kurusha vitu muhimu ili kujitajirisha. Katika vita hiyo ya wahujumu uchumi Tanzania kwa mara ya kwanza iliweza kushuhudia wafanyabiashara wanatupa mali zao ikiwemo fedha kutokana na jinsi Sokoine alivyosimamia zoezi hilo. Historia inaonyesha kuwa wafanyabiashara wengi wanaongozwa na ubinafsi na kwa maana hiyo hawako tayari kupoteza hata senti tano,lakini waliweza kutupa mali zao.

Tunatakiwa kumkumbuka SOKOINE kwa kuangalia na kusoma yale yote aliyataka kuyafanyia kazi. Mfano hata wazo la kuwa na Usafiri wa treni Dar, (Maarufu treni ya Mwakyembe) ni moja ya masuala aliyokua anafikiria k uyafanyia kazi

SOKOINE KAMA KIONGOZI
Aliongoza kwa maslahi ya wengi wananchi aliokuwa anawatumikia
Alikuwa na sifa ya UJASIRI,KUJITUMA KUWAJIBIKA kwa vitendo.
Wewe kama kiongozi wa kisiasa au mtumishi wa umma unajipima vipi na Hayati SOKOINE jikague ili uone kama unaweza kuvaa viatu vya marehemu sokoine hata kama au kukubana?

13/04/1922-KUMBUKUMBU YA KUZALIWA KWA HAYATI BABA WA TAIFA.
Historia inatuambia kuwa mwl alizaliwa mwaka 1922 kijiji butiama katika wilaya ya musoma Mkoani mara,alianza shule akiwa na miaka 11,baada ya kuwa mchungaji wa mifugo hasa ng
ombe. Mwalim alisoma shule ya msingi inayoitwa mwishenge na baada ye kuendelea na masomo ya sekondari katika shule ya sekondari Tabora ,mahali alikoanza kuonyesha au kujipambanua kuwa yeye ana sifa za kuwa kiongozi kwa kuwa kiongozi wa serikali ya wanafunzi na alikuwa anasifa ya kutetea wanafunzi wake, sifa nyingine alikuwa na mtazamo wa kimapinduzi/ukombozi hasa katika michango yake aliyokuwa anaitoa katika debeti (Mijadala iliyokuwa inaendeshwa katika shule enzi hizo ambayo ilikuwa inahusisha na kuchambua mada mbalimbali hasa katika masomo ya historia na kiingereza.

Mwalimu aliendelea na harakati za masuala ya ukombozi hata alipokuwa katika chuo Makerere nchi Uganda.
Baada ya kumaliza masomo ya chuo kikuu mwalimu aliaajiriwa kama mwalimu katika shule ya sekondari pugu na kuendelea na harakati za ukombozi kwa kushiriki katika kuasisi uanzishaji wa chama cha Tanu Mwaka 1954 kutoka TAA. Ili kuonyesha kuwa mwalimu alikuwa amejipambanua kuwa ni mwalimu na mwalimu ni kioo cha jamii alikubali kuacha kazi ya ualimu na kuendelea na masuala ya ukombozi wa watanganyika (Kuthamini maslahi ya wengi na siyo ubinafsi). Mwalimu wakati anajikita katika masuala ya siasa ili kupigania uhuru alikuwa na miaka 32 tu,umri ambao katika hali ya kawaida katika miaka ya sasa hivi unachukuliwa kama kijana hajakomaa kuwa katika masuala ya uongozi wa kitaifa wakati si kweli.

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ni nani katika historia ya Tanzania,Afrika na Dunia kwa ujumla?
Mfano:-  Mwl.  Nyerere alikuwa kama taasisi ya kutuwezesha kupata viongozi kwa mfumo aliuenzi-Mwinyi na Mkapa ni matokeo ya mwalimu kuwa kama taasisi.
Mwalimu alikuwa kiongozi anayeongozwa na UTU na kujali maslahi ya wengi,alikuwa Muasisi na kukubali DSM kuwa makao makuu ya kamati ukombuzi wa Nchi za kusini mwa Afrika na yeye kuwa kiongozi wa Nch zilizokuwa mstari wa mbele katika mapambano ya ukombozi wa Nchi za kusini mwa Afrika, Msumbiji, Angola, Namimbia, Zimbabwe na Afrika ya Kusini.
Mwalimu alikuwa kiongozi wa wanyonge kumbuka mwalimu alikuwa Mwenyekiti wa kamati ya SOUTH SOUTH Commision,Kamati iliyoundwa na Nchi zinazoendelea kuangalia na kupendekeza mfumo wa Uchumi mara baada ya kwisha kwa vita baridi iliyokuwa inaongozwa na Nchi za Urusi na Marekani.

Pamoja na mapungufu yake kama binaadmau bado anabaki kuwa kiongozii wa mfano aliyepata kutokea katika Nchi yetu, Bara la Afrika na Dunia.
Mwalimu anatuonyesha kuwa Uongozi ni suala la kujitolea kwa maslahi ya walio wengi na si suala la kujinufaisha. Kiongozi unatakiwa kuwa na msimamo thabiti na usio yumba,kumbuka mwalimu alipewa jina la utani la HAAMBILIKI kutokana na kusimamia katika kile anachoamini.
Mwalimu alikuwa kiongozi mwenye maono,SIASA YA UJAMAA NA KUJITEGEMEA,pamoja na mapungufu yaliyojitokeza katika utekelezaji wa siasa ya Ujamaa na kujitegemea ,suala la kujitegemea katika familia na kama taifa halina mjadala, na kuamini kuwa binaadamu wote ni sawa kwa maana katika hali ya kawaida sisi binaadamu thamani yetu ni huo UBINAADAMU na si kile unachomiliki.

 26/04/1964 NI SIKU YA MUUNGANO WA ILIYOKUWA TANGANYIKA NA VISIWA VYA UGUNJA NA PEMBA(ZANZIBAR NA KUZAA TANZANIA)
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar pamoja na sababu nyingi zinazotolewa za masuala ya kiulinzi na usalama na undugu wa asili kutokana na watu wa kutoka Tanganyika wengi kulowea katika visiwa vya ugunja na pemba kufanya kazi za manamba katika mashamba ya mikarafuu,kazi za ulinzi na uvuvi. Sababu kubwa ni kutaka kurudisha udungu huo na pia kuhakikisha kuwa wazo la kuwa na Afrika moja linatimia kwa kuunganisha nchi na kanda na baadae kuwa na muungano wa Afrika ambao utakuwa umejengwa kwa misingi ya kueleweka miongoni mwa mataifa ya Afrika na ikumbukwe kuwa huu ndio ulikuwa mtazamo wa baba wa taifa katika suala la kuwa na muungano wa Nchi za Afrika kwa lengo la kuwa na Sauti ya pamoja katika masuala mbalimabali ya kiuchumi kijamii,kisiasa na kiutamaduni. Nini kimetokea na nini kinaendelea ni suala la kulijadili na kuliangalia kwa mapana bila ya kuwa na mtazamo wa nani anapata nini na nani anakosa nini. Je muungano huo unaweza kuwa soma kwetu katika kufikiria mustakabali wetu kama Taifa na hasa katika kipindi hiki cha viguvugu la katiba mpya. Wewe unasemaje.
Vipi suala la muungano katika familia zetu linadumishwa au ndo kila siku migogoro. Tujadili kwa pamoja.

 

Friday, March 29, 2013

JENGO LA GHOROFA 12 LAPOROMOKA TANZANIA ..

Inaarifiwa takriban watu zaidi ya kumi wamefarriki na wengine bado wamenaswa kwa vifusi
 
Takriban watu watatu wamethibitishwa kufariki baada ya jengo lenye ghorofa zaidi ya kumi kuporomoka mjini Dar es Salaam, Tanzania.
Waokozi wanaendelea na shughuli ya kuwatafuta na kuwaokoa manusura na wanasema kuwa hadi sasa watu kumi na watatu waliokuwa wamenaswa wameokolewa.
Zaidi ya wengine arobaini wangali wamenaswa chini ya vifusi.
Shughuli ya ujenzi ilikuwa inaendelea kwenye jengo hilo wakati lilipoporomoka katikati mwa mji wa Dar es Salaam.
Miongoni mwa watu ambao wangali kupatikana ni wafanyakazi wa mjengo na watoto kutoka shule jirani ya mafunzo ya dini ya kiisilamu.
Kulingana na walioshuhudia ajali hiyo, watu walisikika wakipiga mayowe kutaka msaada.
"nilidhani lilikuwa tetemeko la ardhi, na kisha nikasikia mayowe,'' alisema shahidi mmoja.
Jengo hilo liko katikati mwa Dar es Salaam na liliporomoka saa tatu kasorobo asubuhi kwa saa za Afrika mashariki.
Mamia ya watu wanaaminika kuwa ndani ya jengo hilo huku wengine wakiwa nje wakati wa ajali hiyo . Hata hivyo idadi kamili ya watu hao bado haujulikani.
Habari na picha BBC

Wednesday, March 20, 2013

TANZANIA NCHI YANGU ...NAKUPENDA TANZANIA

Nitakutangaza nchi yangu tanzania,nakupenda Tanzania nchi yangu Tanzani na najivuna kuwa mTanzania.JUMATANO NJEMA KWA WOTE...

Monday, March 18, 2013

MSONGAMANO WA MAGARI/FOLENI KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM!!!

Nimekuwa nikijiuliza muda mrefu sasa kuhusu foleni katika Jiji letu la Dar es salaam. Nianze hivi hivi kwanini watu wanaishi nyumba moja na kila mtu anakuwa na gari lake? Kwanini wasitumie gari moja?
Kwanini tusiwekeane zamu kutumia gari moja kwa wiki na hata mwezi..kwa mfano mfanyakazi mwenzako au jirani..hii ingepunguza sana gharama za mafuta pia foleni zingepungua kwa kiasi fulani. Haya ni mawazo yangu..karibuni sana tujadili kwa pamoja...Kapulya