Showing posts with label wasichana. Show all posts
Showing posts with label wasichana. Show all posts

Tuesday, May 21, 2013

Wanafunzi waliokatishwa masomo kwa mimba wafunguka



Mmoja wa wanafunzi alyepata mimba akiwa kidato cha tatu

Mada hii imenigusa sana,,,,nimekuwa muda mrefu nikulalamika sana kuhusu hili yaaani kwanini wasichana waachishwe shule na sio wavukana pia. na kwanini wasichana wasipate muda wa kusoma baaada ya kupata watoto. ..soma hapa  china...mada hii nimeiipata http://maendeleonivita.blogspot.se/ soma mwenyewe!!!!
----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
WANAFUNZI wengi wanaosoma katika shule za sekondari wilayani Tunduru mkoani Ruvuma wanakatishwa masomo yao wanapofikia kidato cha pili na cha tatu baada ya kupata mimba na kuolewa wakiwa shuleni.
Hali hiyo inatokana na historia ya wakazi wa wilaya hiyo ambao ni kabila la wayao kutokuwa na mwamko katika elimu hasa kutokana na kutoa kipaumbele kwa desturi na mila za kabila hilo ambazo zinatoa fursa zaidi katika mila potofu za unyago,msondo na jando kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari hali ambayo inaathiri suala zima la elimu.
Takwimu ambazo zimetolewa na mkuu wa wilaya ya Tunduru Chande Nalicho zinaonyesha kuwa mwaka 2012 wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na sekondari mwaka huu walikuwa ni 2788 hata hivyo hadi kufikia mwezi Aprili mwaka huu ni wanafunzi 1710 tu ndiyo walioripoti hali ambayo inakwamisha maendeleo ya elimu.
Flavian Nchimbi kaimu afisa elimu msingi wilaya ya Tunduru anasema tatizo la mimba katika shule za msingi zimepungua ukilinganisha na miaka mitatu nyuma kulikuwa na mimba karibu 250 ambapo takwimu za mwaka jana zinaonyesha kuwa katika shule za msingi zililipotiwa mimba 16 na kwamba kuanzia mwezi Januari hadi Aprili mwaka huu imeripotiwa mimba moja tu.
Hata hivyo afisa elimu sekondari wilaya ya Tunduru Ally Mtamila amekiri tatizo la mimba na ndoa za utotoni kwa wanafunzi wa shule za sekondari kuwa ni kubwa ambapo wanafunzi wa kike wanakatishwa masomo kwa mimba au kuolewa.
Sarah Michael(15) mkazi wa Tunduru alikuwa anasoma katika shule ya sekondari Makita ambapo alipewa ujauzito akiwa kidato cha tatu na mwanaume ambaye alitoroka mara baada ya tukio hilo hali ambayo ilimfanya aishi kwa shida hadi alipojifungua salama mtoto wake wa kiume.
“Baada ya kupata ujauzito niliacha masomo wazazi walinipokea licha ya kupata misukosuko mingi hasa kutoka kwa baba yangu mzazi,nimejifungua naendelea kumlea mwanangu katika mazingira magumu sana kwa kweli nakumbuka shule mwaka huu ningekuwa namaliza kidato cha nne’’,alisema.
Sarah alisema anapenda sana kusoma lakini wazazi wake hawana uwezo wa kumsomesha hivi sasa hivyo endapo atampata mtu wa kumsomesha anaweza kuendelea na masomo ya sekondari na kwamba kitendo cha kupata mimba na kukatisha masomo yake kimetoa fundisho kubwa kwake hivyo hawezi kurudia makosa ambayo yameharibu ndoto za maisha yake.
Hata hivyo anasema baba yake ni mwajiriwa wa serikali anafanya kazi ya uaskari magereza wilayani Mbinga ambaye kitendo cha yeye kukatishwa masomo kilimchukiza na alitaka mtuhumiwa kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria,hata hivyo wazazi wa pande zote mbili waliyamaliza na kufuta kesi.
“Hivi sasa baada ya mwanangu kukua nimemwomba baba anisomesha ili niweze kuendelea na masomo,lakini baba bado ana hasira amekataa na kusema ningoje kwanza nijifunze maisha kwa kuwa mimi niliacha shule na kukimbilia mambo yaliosababisha kupata mimba naendelea kumuomba radhi baba kwamba sitarudia tena nikipata nafasi ya kusoma’’,alisema kwa huruma.
Salima Hamad(15) mkazi wa Tunduru anasema alikatishwa masomo yake baada ya kupata mimba akiwa kidato cha tatu mwaka 2012 na kwamba wazazi wake walichukizwa na kitendo hicho ,walifungua kesi ya mwanaume aliyempa mimba,alikamatwa na kutiwa ndani hata hivyo mwanaume huyo ametorokea nchini Msumbuji hadi leo.
“Wazazi walinisakama pamoja na viongozi wa serikali ya kijiji,nilitamani kutoa mimba lakini nilipiga moyo konde,nilivumilia kulea mimba katika mazingira magumu kwa kuwa wazazi wangu ni masikini hadi nikajifungua salama kwa kufanyiwa upasuaji mtoto wa kike,natamani kusoma lakini sina uwezo’’,alisisitiza.
Salima anasema wazazi wake wamekataa kumsomesha na kudai kuwa hawana uwezo wa kumpeleka tena shule na hivi sasa anaishi kwa kujitazamia na kuuguza kidonda ambacho kimetokana na kujifungua kwa upasuaji.
Hemed Ally mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya msingi Frank Weston wilayani Tunduru anasema katika mafunzo ya msondo na unyago wanafunzi wa kike wanaelezwa faida za kuishi na mume lakini hawafundishwi madhara ambayo wanaweza kupata kwa kushiriki katika ndoa wakiwa wadogo hali hiyo ndiyo inawahamasisha wanafunzi kujiingiza kwenye ngono na kushawishika kuolewa na kupata mimba wakiwa wanafunzi.
Rehema Sara mwanafunzi wa kidato cha nne sekondari ya Mgomba anasema mila za unyago na msondo zimesababisha wanafunzi wengi wa kike katika shule hiyo kuacha masomo kwa kupata mimba au kuolewa ambapo hivi sasa katika darasa lao waliofanikiwa kufika kidato cha nne ni wanafunzi 106 tu kati ya wanafunzi zaidi ya 230 walioanza nao kidato cha kwanza mwaka 2010.
Sarah mkombozi wa kidato cha nne sekondari ya Mgomba ambaye alifanyiwa ngoma ya unyago na msondo akiwa darasa la tatu amekiri moja ya mambo ambayo wanafundishwa katika msondo na unyago ni kufanya mapenzi na watu wazima na kwamba kukataa kufanya hivyo ni kuvunja mila na desturi za wayao’’,alidai mwanafunzi huyo.
“wenzangu wengi ambao nilikuwa nao shule ya msingi na wengine ilitakiwa niwe nao sekondari wameacha masomo kwa kuwa wana watoto baada ya kupata mimba na wengine wameolewa na kuachika hivyo wanaangaika na maisha’’,alisisitiza.
Mkuu wa wilaya ya Tunduru Chande Nalicho amekiri mila na desturi za kabila la wayao zinachangia wilaya hiyo kuwa duni kielimu hata hivyo amesema tayari serikali imeunda kikosi kazi cha kuonana na viongozi wa mila, makungwi na manyakanga kuwaelimisha juu ya utoaji wa elimu kwa watoto wa kike kupenda masomo tofauti na sasa ambapo kundi hilo limekuwa likifundishwa kukabiliana na maisha ya ndoa hali iliyosababisha kuwepo kwa matukio mengi ya ndoa za utotoni wakiwa shuleni.
“Mila na desturi za kabila la wayao kuwafanyia unyago wanafunzi ndiyo chanzo kikuu cha tatizo hili,sisi kama serikali ili kukabiliana na tatizo hili tumefanya vikao na viongozi wasiokuwa rasmi lakini wanakubalika katika jamii wakiwemo makungwi, mangariba, masultani,mamwenye,mashehe na maimamu kwa kuzingatia tumejadili kwa pamoja tatizo hili”,anasisitiza.
Kwa mujibu wa Takwimu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, wasichana 8000 kila mwaka huacha shule kutokana na ujauzito. Kati yao 3,000 ni wanafunzi wa shule za msingi.
Kila siku, wanawake 24 hufariki dunia kutokana na mimba au wakati wa kujifungua. Wanawake watano mpaka sita wanaofariki kati ya hao ni watoto wadogo, watoto hao hufariki dunia kwa kuwa miili yao haijakomaa vya kutosha kwa ajili ya kujifungua.
Naibu mwakilishi mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Watoto (UNICEF), Mohamed Safieldin anasema mbali na athari hizo, pia virusi vya ukimwi (VVU), vinavyosambaa kwa kasi kwa wasichana hao. Tanzania kuna watoto yatima milioni 1.3 walioathirika kwa ukimwi.

Tuesday, September 18, 2012

UJUMBE WANGU WA LEO:- WASICHANA NA WANAWAKE WANA HAKI!!

Watu wote ni sawa, watu wote wana thamani sawa. Hii ina maana kuwa wanawake na wanaume, wasichana na wavulana, wana haki sawa. Lakini katika jamii zetu wanawake na wasichana wananyimwa haki zao.
Hatua ya kwanza kuleta usawa ni kuielewa na kutokuukubali unyanyasaji wa wanawake na wasichana
JUMANNE NJEMA NDUGU ZANGUNI!!!

Wednesday, June 30, 2010

Kinamama Kilindi wakiri kuwakeketa watoto wa kike

WANAWAKE wa jamii ya wamasai wilayani Kilindi mkoani Tanga wameeleza waziwazi kuwa wimbi la ukeketaji wasichana bado linaendelea katika jamii hiyo ya wafugaji, licha ya kampeni mbalimbali zinazofanywa na mashirika mbalimbali kukomesha shughuli hiyo.
Kina mama hao, walisema pamoja na kuendelea na vitendo hivyo vya ukeketaji kwa usiri mkubwa, pia wameeleza wamekuwa wakiwauguza mabinti zao nyumbani wanapopata madhara sehemu za siri kutokana na majeraha baada ya kukeketwa na wakati mwingine kupoteza maisha.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa mkutano wa hadhara ulioshirikisha marika na jinsia zote katika eneo la Shule ya Msingi Mbogoi Kata ya Mkindi wilayani hapa juzi,kina mama hao, walisema wanaendelea na ukeketaji kwa madai kuwa hawajapata elimu ya kujua madhara yake.
Mimi tangu nianze kuwazalisha wazazi tangu miaka mingi iliyopita sijawahi kuona mwanamke ambaye hajakeketwa. Sisi tulifikiri kuwa duniani hakuna mwanamke ambaye hakeketwi na tuliona ni muhimu kwa kuwa ni kudumisha mila zetu. Lakini pia tukielimishwa zaidi tutaacha ukeketaji,†alisema Yosephat Taringo.
Naye Wiliam Tangoro (65) katika mkutano huo, alisema wanashukuru Shirika la AMREF kuchukua jukumu la kuwaelimisha wafugaji ili kuepuka mila hizo, ambazo sasa zimepitwa na wakati.
“Sisi tunalishukuru shirika hili la AMREF kwa kutujali na kutuelimisha ili tuachane na mila hii ambayo sasa elimu hiyo, imeanza kuenea sehemu mbalimbali za makazi yetu wafugaji,†alisema Tangono.
Mafunzo hayo, yanayofanyika usiku kwa njia ya mijadala na sinema na kushirikisha watu wa rika zote na jinsia zote ikiongozwa na Afisa Utamaduni wa wilaya hiyo, Adelina Ndumbaro na yamekuwa yakivutia watu wengi huku wachangiaji wakielezea undani wa maisha yao kwa uwazi zaidi.

Habari hii imeandikwa na Hussein Semdoe,Kilindi iliandikwa 25/3/2010 nimeona si vibaya kama wengi tukiisoma kupitia kibaraza hiki cha Maisha na Mafanikio.

Thursday, September 17, 2009

HATUA SITA ZA KUSAIDIA KUDHIBITI MIMBA SHULENI

MAANDALIZI ya safari yangu kwa ajili ya kumpeleka mtoto wa dada yangu kujiunga na masomo ya sekondari Morogoro yalikwenda vizuri na asubuhi yake nilijona mtu mwenye bahati.

Tulifika mapema kwenye kituo kikuu cha mabasi, Ubungo na tulipokuwa tunaelekea kwenye basi moja ambalo tulitaka kukata tiketi, tuliwaona wasichana kadhaa walioonekana kuwa ni wanafunzi, ni kweli nao walikuwa wanakwenda katika shule hiyo. Alikuwepo mwanamume mmoja aliyevalia vizuri ambaye alijitambulisha kuwa mwalimu wa shule hiyo.
Mwalimu huyo, ambaye alikuwa na vitambulisho vya kazi aliwaambia wazazi waliokuwa wanawasindikiza watoto wao wasisumbuke kwani yeye ametumwa kwa ajili hiyo. Hivyo, wazazi, walezi na sisi wengine tuliotumwa tulimkabidhi mwalimu huyo watoto nasi tukarudi nyumbani.

Kwa haiba aliyokuwa nayo mwalimu yule, kwa umri wake na hata upole alioonyesha, alivyokuwa anazungumza taratibu na alivyotuaminishia usalama, haraka tulinong’onezana kuwa ni mlokole. Niliporudi nyumbani asubuhi ile niliwachekesha wazazi wake kwamba 'nimekbidhi binti yao kwa mwalimu mlokole'.
Hilo lilikuwa kosa kubwa. Utaratibu ule ulikuwa tofauti na fikra zake moyoni, alikuwa mbwa mwitu. Mwalimu huyo ambaye, nahifadhi jina lake, ndiye alikuja kutupa pigo kubwa kwa kumkatisha masomo binti yetu baada ya kumpa ujauzito. Tumefungua kesi kortini.

Pamoja na kuchukua hatua hizo, tumekuwa tukijiuliza nini ki kifanyike ili, siyo tu kwa sisi kupata haki kutokana na binti yetu kupewa ujauzito na mwalimu anayepaswa kuwa mlezi wake, bali pia kuwadhibiti walimu wengine wa kiume wenye tabia ya kuwarubuni wanafunzi wa kike na kuwapa mimba.
Hii ni kwa sababu tuliokumbwa na kero siyo sisi tu bali wazazi wengi, na kumekuwa na malalamiko kila kona unayopita, kuhusu wanafunzi wa kike kukatishwa masomo baada ya kugundulika wamepata ujauzito shuleni.
Japokuwa baadhi ya wasichana hupewa mimba shuleni na wanafunzi wenzao wa kiume, watu wa mitaani pamoja na wafanyakazi, ukweli ni kwamba wengi wao hukatishwa masomo kwa kupewa mimba na walimu wao.
Taarifa mbalimbali na uchunguzi uliofanywa katika maeneo mengi, walimu wanahusika kwa kiasi kikubwa. Walimu hao huwapata wanafunzi kwa urahisi kwa vishawishi kadha wa kadhaa vikiwemo vya kuongezewa alama, kupewa maswali ya ziada (twisheni) na kupangiwa kazi nyepesi.

Kuna ukweli pia kwamba baadhi ya wasichana hupata ujauzito kutokana na kutokuwa na maadili mazuri, papara au ulibukeni wa maisha lakini wengine hulazimika kujenga mahusiano ya kimapenzi na walimu wao kwa kufundishwa masomo ya ziada ili wafaulu mitihani yake.
Kwa mfano, hivi karibuni, tulisikia katika baadhi ya vyombo vya habari vikiripoti kuwa mwalimu mkuu wa shule moja iliyoko Kusini mwa Tanzania amepandishwa kizimbani akikabiliwa na shtaka la kumpa mimba mwanafunzi wake.

Katika tukio kama hili, kwa hali ya kawaida unaweza usiamini wala kupata picha inakuwaje, lakini ndiyo hali halisi ya maisha yalivyo katika ulimwengu wa sasa. Kama mzazi wa kiume anaweza kujenga uhusiano wa kimapenzi na mtoto aliyemzaa sembuse mwalimu?.
Ukichunguza kwa makini utagundua chanzo cha tatizo hili ni tamaa ya walimu na ukiukwaji mkubwa wa kanuni za maadili kazini. Walimu hupaswa kuwa walinzi wa wanafunzi na waongoza maadili kinyume cha hivyo ni utovu wa nidhamu.

Mapendekezo yangu.

Kwanza wazazi wote wenye wanafunzi wa kike wahakikishe wanafungua kesi dhidi ya wahusika ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Endapo binti atadai hajui, kwa lengo la kumficha mhusika, basi binti huyo ashitakiwe binafsi.

Pili, wazazi tusikubali vishawishi vya wavulana au walimu au watu wengine weyote walihusika kwamba wasishtakiwe ila waachiwe wawatunze mabinti na ujauzito walionao. Imebainika hufanya hivyo kwa muda tu, baada ya miezi michache huwapa talaka na huo unakuwa mwisho wao.

Tatu, napendekeza serikali iweke uzito kwa upande wa walimu kwamba watakaobainika kuhusishwa tu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanafunzi waachishwe kazi. Nina uhakika hakuna anayependa kuachishwa kazi hivyo wataachana na tamaa yao kwa wanafunzi.
Hatua hizo zinaweza kuchangia kupunguza kuwepo kwa matukio kama haya na walimu watajitahidi kuishi juu ya tuhuma za kimapenzi.

Nne, uwepo utaratibu wa kuwapima wanafunzi wa kike kila mara na kuwapa ushauri nasaha kwamba wajifunze na wazoee kusema "hapana" wanapofuatwa na walimu wao kimapenzi.

Tano, iko haja ya kuweka sheria kuzuia wanafunzi kufika kwa walimu kama hawana uhusiano wa kidugu. Shule za seminari na zinazoendeshwa na masista zimeweza, kwa nini ishindikane katika shule za serikali?

Sita ni kwamba chanzo kingine cha matukio ya mamba ni kushiriki starehe. Wazazi wawazuie watoto wao; wavulana kwa wasichana kujiingiza kupita kiasi kwenye burudani kwani ni nchimbuko kubwa la maasi ya maadili na mwishowe kupeana mimba.

Hii ilitoka mwananchi la tarehe 23/6/2009 na mwandishi Elizabeth Suleyman.

Wednesday, September 16, 2009

WANAFUNZI WA KIKE WAPATAO MIMBA KABLA YA KUMALIZA SHULE WARUHUSIWA KUFANYA MTIHANI

Nimezoea sana kusikiliza habari za BBC, kwa hiyo wakati nasikiliza habari hii, nikaona sio mbaya kama nikiiweka hapa kibarazani kwangu ili wengi msome na tuweze kujadiliana.

Idadi ya wanafunzi wa kike wanaoacha shule kwa sababu ya mimba isiotarajiwa inazidi kupanda

IDADI ya wasichana wanaokatisha masomo yao na kuacha shule wilayani Kericho, kwa sababu ya kupachikwa mimba wasiotarajia imewashangaza maafisa wa Elimu na wadau wengine.

Katika kisa ambacho kimezua mjadala mkubwa juu ya Elimu na mimba miongoni mwa wanafunzi wa kike, imeibuka kuwa toka kwa idadi ya wasichana 25 waliojiunga katika kidato cha kwanza katika shule moja katika eneo hilo, 24 waliacha shule baada ya kutwikwa mimba.

Katika makala ya wiki hii tunahoji nini kinachopelekea hali kama hii ya mimba za mapema miongoni mwa wanafunzi???? Mwalimu mkuu alizungumzia umbali wa shule kuoka kwa makao ya wanafunzi ambao wanalazimika kupitia katika misitu ya chai jambo amabalo linawaweka katika hatari ya mahusiano ya kimapenzi na hata ubakaji.

Mwalimu huyo mkuu alisema ni jambo la kushangaza sana. Aliongezea kuwa idadi ya waichana katika shule hio sasa ni ishirini pekee. Wengi wa wasichana waliokuwa wakifanya vyema katika masomo wameacha shule baada ya wanafunzi wenzao na baadhi ya wafanyakazi katika mashamba ya chai kuwatwika mimba.

Elimu ya watoto wa kike inaendelea kuwa ndoto isioweza kutimika katika eneo hili la Afrika. Wasichana wengi wanadanganywa na wanaume na kujitosa katika tabia na mahusiano ya kingono yanayopelekea mimba isiotarajiwa. Jambo ambalo huwafanya wasichana hawa kuacha shule na kuanza maisha ya uzazi wakiwa wao wenyewe bado wachanga.

Wengine wanakumbwa na vizingiti vya kitamaduni kama vile tohara ya wanawake, ndoa za mapema, kazi za nyumbani, magonjwa na umasikini. Kumekuwa na mjadala iwapo kuratibishwa kwa masomo ya afya ya uzazi katika silabasi za shule kutaksaidia kudhibiti mimba isiotarajiwa na magonjwa ya zinaa miongoni mwa wanafunzi.

Inchini Tanzania serikali, kwa mara ya kwanza, imewaruhusu wale waliopata mimba wakiwa shuleni kufanya mitihani. Hapo awali wanafunzi waja wazito walikuwa wakikatazwa kufanya hivyo.

Je, nini mchango wako kuhusu yote haya??????

Habari zaidi sikiliza hapa katika kipengele cha kimasomaso. http://www.bbc.co.uk/swahili/

Tuesday, March 24, 2009

MILA NA DESTURI/JE? KUTAHIRI WASICHANA NI HAKI?

Ni jambo la kutatanisha kidogo kwangu: Labda nianze hivi katika Tanzania tupo makabila tofauti. Na ni mengi na kila moja lina mila na desturi zake. Makabila 129 (130). Kwa hiyo hapa ninachotaka kusema ni kwamba hili jambo la kutahiri wasichana hasa wenzetu wamasai (pia nchi yenzetu jirani Somalia) lina maana gani? Kwa sababu wao wanadai wakishawatahiri ndo wanakuwa wanawake kamili na pia wanakuwa safi. Lakini papo hapo hawajui kama ni hatari sana :-

Tukianza na vyombo wanavyotumia, Je? Ni visafi au je wanabadili kwa kila mtoto hapana. Halafu kubwa zaidi je wanawapa ganzi? Hapana. Kwa sababu baada ya hapo inasemekana wanawashona na kuacha shimo ndogo sana kwa ajili ya kukojoa mkojo tu.

Je? Huyu msichana atapoolewa mnafikiri atapata maumivu kiasi gani wakati anatarajia kufanya tendo la ndoa kama sio mateso makali. Ambayo badala ya kuifurahia ndoa yake inakuwa kuijutia. Na itakuaje atapotarajia kuzaa. Kwa kweli na mateso makubwa sana atayapata. Ambayo atatamani hata asingeishi.

Kwa nini? Na je? ni safi kwa nani?. Kwa sababu msichana wa miaka mitano hawazi kuelewa ni nini kuwa mwanamke.
Na watoto wengi wamepoteza maisha yao wakati wa tendo hili, wengine wanapata tetanus, wengine wanapata mshtuko pia maambukizo mbalimbali. Tukiendelea hivi tutamaliza wasichana!!.

Saturday, September 27, 2008

Matatizo ya uzeeni, Mila na desturi za kubagua watoto wa kike

........................................................

Wazee mara nyingi hupoteza uwezo wa kukumbuka vitu kwa hiyo huwa wasahaulifu sana. Huwa rahisi kuvurugikiwa akili zaidi hasa pale wanapopatwa na homa kali. Mara nyingi wazee wanapata shida ya kukabiliana na mazingira mapya au yanayobadilika. Kijadi mara nyingi wazee ni watu ambao walikuwa wakiheshimiwa sana na kutunzwa vizuri. Heshima hii iliwafanya wajione kuwa ni watu wanaothaminiwa na jamii, na kuwaongezea furaha ya maisha. Siku hizi vijana wengi wanashindwa kuzingatia mila za zamani za kuwaenzi na kuwaheshimu wazee na hivyo kushindwa kuwapa nafasi yao katika jamii. Wazee wa mijini na hata vijijini wanakuwa wapweke bila watu wa kuwasaidia. Sehemu nyingine wazee wanasakwa na kupigwa hadi kufa kwa kuhofia kwamba wao ni wachawi. Hali hii ya kuwatenga wazee na kuwasingizia uchawi ni mojawapo ya matatizo ambayo yanaathiri sana afya yao ya akili.Sijui mila ipi ni nzuri kwani mimi kwa sasa nina mila "mbili" wenzetu ughaibuni wazee wao wanatunzwa kwenye nyumba maalum hii mara nyingi inasumbua akili yangu na nataka nitakapokuwa mzee sitaki kutunzwa na mtu zaidi ya familia yangu je nakosea? semeni ninyi.
. .


Nilizani ubaguzi utapungua lakini, naona hadi leo kuna baadhi ya wazazi ambao wanapuuza elimu ya watoto wa kike na kutoa kipaumbele kwa watoto wa kiume. Mfumo dume huu unachangia kuathiri afya ya akili ya kina mama. Nyumbani watoto wa kike wanatakiwa wasaidie kazi za jikoni na za ndani wakati wa kiume wanasoma au kwenda kutembelea marafiki. Hata katika maamuzi ya familia mawazo ya watoto wa kiume yanapewa uzito zaidi kuliko yale ya watoto wa kike. Waalimu nao mara nyingine wanawajengea watoto wa kike imani potofu kwamba wao hawawezi masomo ya sayansi.

Wasichana na vijana wanawake daima hujikuta wapo kati ya mila za zamani na mila za kisasa, kwa mfano, anapotaka kwenda shule hupambana na mila za zamani, zikiwa za dini au za kikabila.
Hili limekuwa ni tatizo kwani wasichana wa siku hizi hupenda kusoma ili baadaye waweze kupata kazi kabla ya kuolewa. Kwa hiyo wanapolazimishwa kufuata huo utamaduni wanapata mvurugiko wa akili.

Wednesday, September 24, 2008

MJADALA WA LEO

Hili swali limekuwa likinikereketa sana miaka yote ambayo nimeishi hapa duniani kwa hiyo sasa naomba mwenzangu tujadiliana au mnipe jibu.

SWALI NDIO HILI:- Je? Kuna sheria Tanzania isemayo kama msichana akipata mimba asiendelee na masomo?