Tafiti nyingi zinaonyesha kwamba, ndoa sita katika kila kumi huvunjwa na wanaume au wanawake kutoka nje. Lakini inaonekana pia kwamba, wale wanaotoka nje ya ndoa zao, wengi ndiyo ambao huacha au kuachwa. Ni karibu ndoa nane katika kila kumi, ambazo hufikia ukomo kutokana na kutoka nje.
Wanawake ambao wako chini ya umri wa miaka 30, hutoka nje kwa kiwango karibu sawa na wanaume. Umri huo ndiyo hatari sana kwa wanawake kutoka nje.
Inaonyesha kwamba, bado dini haiogopwi sana linapokuja suala la kutoka nje. Waumini na viongozi wengi wa dini mbalimbali wanadaiwa kutoka nje kwa kiwango kikubwa kuliko inavyodhaniwa.
Karibu wanawake wawili katika kumi na wanaume watatu katika kumi, huwa wametoka nje ya ndoa zao katika maisha yao hapa duniani.
Uhusiano mwingi wa kiuzinzi hudumu kwa miaka mitatu tu na wapenzi huachana au kuachanishwa kwa kufumaniwa. Lakini mwingine hudumu maisha, ingawa na madhara yake nayo hudumu maisha.
Ni mwanamume mmoja kati ya kila kumi, ambao huwaacha wake zao na kuoa nyumba ndogo. Wengi hubaki na wake zao huku wakiwa na nyumba ndogo, au kuwaacha wake zao, lakini hawaoi nyumba ndogo.
Hata hivyo, wanane kati ya kumi miongoni mwa wale wanaowaacha wake zao na kuoa"nyumba ndogo," nao huja kuachana na nyumba ndogo hizo. Kwa hiyo, ni wawili tu kati ya kumi ambao hudumu na "nyumba ndogo" walizozioa baada ya kuachana na wake zao kwa sababu ya "nyumba ndogo" hizo.
Halafu wanane kati ya kumi ya kila aliyevunja au kuvuruga uhusiano wake na mume au mke kwa sababu ya hawara, huja kujuta baadaye. Ni wawili tu kati ya kumi, ambao uvurugaji wa uhusiano wake kwa sababu ya hawara, hawaji kujuta. Hawa ni wale ambao ndoa zao zilikuwa tayari na mashaka makubwa.
Huchukua mwaka mmoja hadi mitatu kwa ndoa ambayo imeingiliwa na fumanizi, wanandoa kuanza kuelewana tena kama awali. Hapo uhusiano huwa imara kuliko awali, au huingia mashaka ya sirisiri.
Chanzo:- kitabu Mapenzi kuchipia na kunyauka na Munga Tahenan.
Showing posts with label mwanaume. Show all posts
Showing posts with label mwanaume. Show all posts
Monday, October 8, 2012
Wednesday, October 6, 2010
WANANDOA NA KAULI HIZI: HATA VIKOMBE KABATINI HUGONGANA, ITAKUWA SIE?
Ndugu wasomaji, Habari hii nilishawahi kuivuka hapa MAISHA NA MAFANIKIO. Binafsi imenivutia sana na nimeona tuirudie tena kwani KURUDIA KITU ni KUJIFUNZA ZAIDI. KARIBUNI UNGANENI NAMI.
------------------------------------------------------------------------------------------------
Je unadhani au kuamini kwamba kuna ndoa ambazo wanandoa wake hawagombani kabisa? Kama unaamini hivyo, basi unajidanganya na labda unaishi katika dunia ya peke yako.
Ni jambo lenye ukweli wa kutosha kabisa kwamba wanandoa wote duniani hutokea kugombana, lakini kugombana huko hutokana na migongano au mizozo ya muda tu ambayo huweza kutatuliwa na pande mbili kama wakiamua kufanya hivyo.
Wewe unayesoma hapa, napenda kukuambia ukweli kwamba usiogope migogoro ya ndoa, kwani hicho ni kitu ambacho kamwe huwezi kukiepuka. Kuna msemo mmoja unatumika sana huko nyumbani usemao, " hata vikombe kabatini hugongana itakuwa wana ndoa?" Hii ina maana gani, ina maana kwamba haiwezekani watu kuishi pamoja halafu msiwe mnatofautiana, na kama ukiona hivyo, jua kwamba hiyo ndoa si salama kwani siku yoyote bomu litapasuka na madhara yake yatakuwa ni makubwa kuliko kawaida.
Kuna watu ambao hata kama wamekosewa na wenzi wao hunyamaza kimya na kumeza hasira zao, wengine huogopa kuwakabili wenzi wao na kuzungumzia jambo linalowakera kwa kuhofia kuonekana kama wana kasoro au ghubu. Jambo hili ni hatari sana.
Kumkabili mwenzi wako na kumwambia hisia zako kama amekukosea au amekwenda kinyume na matarajio yako ni jambao la maana sana katika kudumisha uhusiano. Lakini naomba nitahadharishe kwamba, ni vyema kufanya hivyo bila kumshusha, kubeza au kusimanga kwani hiyo sio dalili nzuri ya upendo.
Inashauriwa kwamba wanandoa au wapenzi wanapokwaruzana inabidi wajadili tofauti zao bila kusigishana, kila mmoja akitaka kuwa mshindi, hiyo haitasaidia kuimarisha ndoa bali itaongeza tatizo. Ni vyema upande unaohusika na tatizo, uwajibike na kuomba radhi kwa ustawi wa ndoa, huo ndio ukomavu.
Kutojadili mgogoro kwa wanandoa na kuupatia ufumbuzi wa tatizo huwafanya wandoa kuwa mbali kihisia, na athari zake ni kuwakuta wanandoa wakiwa wageni wa kila mmoja kwa mwenzake, yaani hakuna mawasiliano, kila mtu na lwake.
Jambo la msingi kwa wanandoa ni kujadili tofauti zao pindi linapojitokeza jambo linalomkera mmoja wa wanandoa, kwani hakuna jambo linaloweza kujitatua lenyewe bila kutatuliwa na wandoa husika. Kuacha jambo lolote bila kulitafutia suluhu ni sawa na kutega bomu, ambapo siku likilipuka madhara yake ni makubwa sana.
Unaweza kukuta mwanandoa anakereka na mambo madogo madogo ya mwenzi wake lakini hasemi, ingawa yanamkera kupita kiasi akitegemea huyo mwenzi wake atajua na kuacha, thubutu…..inapotokea siku yeye amekosa jambo dogo tu na huyo mwenzi wake akamsema, basi atatumia fursa hiyo kuanza kujibu mapigo kwa kueleza yale yanayomkera kutoka kwa mwenzi wake, na hapo itakuwa kila mtu anavutia kwake kama mwamba ngoma………na aamini nawaambia kuwa kamwe hawezi kupatikana mshindi katika jambo hilo, kwani mjadala huo unaweza kutoka nje ya mada kila mmoja akijitahidi kutafuta makosa ya mwenzi wake hata yale yaliyotokea wakati wa uchumba wenu ili mradi vurugu tupu.
Inatakiwa wanandoa wajadili kila jambo linalojitokeza hadi kulipatia suluhu, vinginevyo ni kuichimbia ndoa yenu kaburi la mapema. Wakati mwingine unaweza kukuta mwanamke analalamika juu ya kutoridhishwa kwake na matumizi ya mumewe, na hapo mume naye ataanza kukumbusha juu ya matumizi yasiyo ya lazima yaliyofanywa na mke huko nyuma. Mke naye hataridhika atakumbushia jambo lingine na lingine hadi hata mada iliyokuwa ikijadiliwa inasahaulika.
Jambo lingine ni kujumuisha mambo, matumizi ya maneno kama, mara nyingi, kila wakati au mara kwa mara si mazuri sana. Unaweza kukuta mtu mwenzi wake amekosea jambo halafu mwenzie anamwambia “Kila mara huwa unafanya hivi” au mara nyingi huwa unafanya hivyo…..Hii ni hatari kwa ustawi wa wanandoa, kwani kwa kujumuisha ni sawa na kumwambia mwenzi wako kuwa kila mara yeye ndiye mkosaji.
Kwa haya niliyoyaeleza hapa sina maana kwamba huu ndio muarobaini pekee wa kuimarisha mahusiano kwa wanandoa, bali ni moja ya mambo muhimu kati ya mengi ambayo yakizingatiwa na wanandoa wote basi ndoa yao itakuwa imara Tujadili pamoja………..
Na hapa yalikuwa maoni ya baadhi ya wasomaji......
James Adolwa said...
Kweli unavyosema kuwa maranyingi mzozo ukidhihirika ni kwasababu kuna kero lililo fichika ama kufunikiwa. Swala lingine ambalo watu wanatakikana kuzingatia....wacha nitumie kiingereza kidogo....One needs to consider what one keeps steaming under the lid of the cooking pot. If you spend your time and energy focusing on the weaknesses or faults of another then all that you will see in the other person are weaknesses and faults...and you will end up cooking up a foul tasting broth that will spill over and put out the flame of your relationship.
Instead try and focus on the strengths and virtues of your partner and in the end you will find that you keep seeing more and more good things. This is not to say that all the experiences will be pleasant but rather all the bitter, sweet, sour and salty experiences work out together such that the sum total ; the big picture, the essence of the whole experience works out to be a pleasant experience for both. I am no expert but these are the thoughts that flowed from my soul.
October 12, 2009 8:34 PM
Ramson said...
Dada yangu hapo umenena, kaka James, naona imebidi kuandikwa kwa kiingereza ili kuweka msisistizo....kaaaazi kweli kweli.
Dada Yasinta hili ni darasa tosha kwa wale wanandoa ambao hawakubahatika kujifunza namna ya kutatua migogogro ya ndani katika uwanja ulio sawa. Unajua wazee wetu walipokuwa wakituambia kuwa ndoa ni kuvumiliana wengi walitafsiri vibaya, walijua kuwa ni kumeza hasira zetu pindi tunapokosewa na hii ilitumiwa vibaya zaidi na wanawake, lakini siwalaumu bali mfumo dume ndio uliowafundisha.......
Inaposemwa kuwa ndoa ni kuvumiliana maana yake ni kujadiliana kwa uwazi pale tatizo au kunapozuka kutoelewana juu ya jambo fulani na uzingativu uwekwe kwenye kutatua tatizo sio kubishana kwa ajili ya kumtafuta mkosaji. Tumelelewa katika familia tofauti, kuna baadhi ya wanume wamefundishwa kuwa hawapaswi kuwaomba wake zao radhi hata kama wamekosa,,,,,inabidi mke awe makini kama akishajua kuwa mumewe ni wa aina hiyo.....
Anonymous said...
Darsa hilo Yasinta, safi sana, umemaliza yote hata cha kuongeza sina kwa leo labda kifupi sana wanasema katika maandiko matakatifu kwamba "upendo huvumilia, hauhesabu mabaya na kadhalika..." basi kama tafsiri sahihi ya upendo ikiwepo miongoni mwa wana ndoa basi mchezo umeisha, du ni hivi jioni hii nilikuwa nasikiliza kipindi cha maridhiano kupitia redio Maria Tanzania du, niliyoyasikia huko yanatisha kisa kusaka mtoto sijui ujiko kwa mwanaume! na kisa kingine kilikuwa wiki iliyopita ambapo mwanaume alienda kuazima dume ili limzalishie watoto, huko kote mwanamke alikuwa anashinikizwa lazima afanye mapenzi na hilo beberu!!
SIMON KITURURU said...
Bomba la somo hili Dada Yasinta!
Lakini sijui kwanini huu msemo wa kuwa Vikombe hugongana kabatini huwa na wasiwasi nao kwa kuwa nashindwa kuwa na uhakika kuwa kihalihalisi labda VIKOMBE hugonganishwa na HAVIGONGANI tu kienyeji ndani ya KABATI.
Anonymous said...
My sista unanikuna jamani hilo ni kweli my sista kwani kila mtu kalelea kivyake na malezi yake just meet with her /him ukubwani ni lazima kuwe na migongano ya hapa na pale nduguyo tu mwajibizana sembuse mtu baki ooh please Kaka Simon Kitururu kwani utakuta wewe ukisusa wenzio wanakula food yote lkn familia nyingine ukisusa watu hawali mpaka ujongee mezani,Kuna wengine hata hajui kumheshimu dadaake or kakaake yote ni malezi hp umeelewa brother from anaother mother meanz ya vikombe kugongana ni misemo ya mafumbo ya mababu zetu soo Open ya Eyes oky!!!!
chib said...
Big up Kitururu, huwa naupinga msemo huo wa vikombe kabatini kugongangana, ukweli kama kabati imetulia, vitagongana vipi, ni wale wenye mafujo tu ndio huvigonganisha, au kama unakaa Sumatra ambako matetemeko ya ardhi hayaishi, hapo ndio vitagonganishwa na tetemeko. Ypte kwa yote, somo hilo ni zuri kabisa kwa watu wote wenye ndoa na watarajiwa.
SIMON KITURURU said...
@Anony: nankunukuuu ``ooh please Kaka Simon Kitururu kwani utakuta wewe ukisusa wenzio wanakula food yote......''
Hapo si kunauwezekano kiwagonganishacho ni FUDI?:-)
Nimekuelewa lakini MKUU na pointi yako nimeipata.
@MKUU CHIB: Hapo kwa mtazamo wangu umemaliza NUKTA
Markus Mpangala said...
Ni MSARAGAMBO hapo
Yasinta Ngonyani said...
Nachukua nafasi hii kuwashukuruni wote kwa maoni yenu kwani huku ndio kujifunza. Maana kila mtu anajifunza toka kwa mwingine. Ila sifungi mjadala karibuni kujadili zaidi
------------------------------------------------------------------------------------------------
Je unadhani au kuamini kwamba kuna ndoa ambazo wanandoa wake hawagombani kabisa? Kama unaamini hivyo, basi unajidanganya na labda unaishi katika dunia ya peke yako.
Ni jambo lenye ukweli wa kutosha kabisa kwamba wanandoa wote duniani hutokea kugombana, lakini kugombana huko hutokana na migongano au mizozo ya muda tu ambayo huweza kutatuliwa na pande mbili kama wakiamua kufanya hivyo.
Wewe unayesoma hapa, napenda kukuambia ukweli kwamba usiogope migogoro ya ndoa, kwani hicho ni kitu ambacho kamwe huwezi kukiepuka. Kuna msemo mmoja unatumika sana huko nyumbani usemao, " hata vikombe kabatini hugongana itakuwa wana ndoa?" Hii ina maana gani, ina maana kwamba haiwezekani watu kuishi pamoja halafu msiwe mnatofautiana, na kama ukiona hivyo, jua kwamba hiyo ndoa si salama kwani siku yoyote bomu litapasuka na madhara yake yatakuwa ni makubwa kuliko kawaida.
Kuna watu ambao hata kama wamekosewa na wenzi wao hunyamaza kimya na kumeza hasira zao, wengine huogopa kuwakabili wenzi wao na kuzungumzia jambo linalowakera kwa kuhofia kuonekana kama wana kasoro au ghubu. Jambo hili ni hatari sana.
Kumkabili mwenzi wako na kumwambia hisia zako kama amekukosea au amekwenda kinyume na matarajio yako ni jambao la maana sana katika kudumisha uhusiano. Lakini naomba nitahadharishe kwamba, ni vyema kufanya hivyo bila kumshusha, kubeza au kusimanga kwani hiyo sio dalili nzuri ya upendo.
Inashauriwa kwamba wanandoa au wapenzi wanapokwaruzana inabidi wajadili tofauti zao bila kusigishana, kila mmoja akitaka kuwa mshindi, hiyo haitasaidia kuimarisha ndoa bali itaongeza tatizo. Ni vyema upande unaohusika na tatizo, uwajibike na kuomba radhi kwa ustawi wa ndoa, huo ndio ukomavu.
Kutojadili mgogoro kwa wanandoa na kuupatia ufumbuzi wa tatizo huwafanya wandoa kuwa mbali kihisia, na athari zake ni kuwakuta wanandoa wakiwa wageni wa kila mmoja kwa mwenzake, yaani hakuna mawasiliano, kila mtu na lwake.
Jambo la msingi kwa wanandoa ni kujadili tofauti zao pindi linapojitokeza jambo linalomkera mmoja wa wanandoa, kwani hakuna jambo linaloweza kujitatua lenyewe bila kutatuliwa na wandoa husika. Kuacha jambo lolote bila kulitafutia suluhu ni sawa na kutega bomu, ambapo siku likilipuka madhara yake ni makubwa sana.
Unaweza kukuta mwanandoa anakereka na mambo madogo madogo ya mwenzi wake lakini hasemi, ingawa yanamkera kupita kiasi akitegemea huyo mwenzi wake atajua na kuacha, thubutu…..inapotokea siku yeye amekosa jambo dogo tu na huyo mwenzi wake akamsema, basi atatumia fursa hiyo kuanza kujibu mapigo kwa kueleza yale yanayomkera kutoka kwa mwenzi wake, na hapo itakuwa kila mtu anavutia kwake kama mwamba ngoma………na aamini nawaambia kuwa kamwe hawezi kupatikana mshindi katika jambo hilo, kwani mjadala huo unaweza kutoka nje ya mada kila mmoja akijitahidi kutafuta makosa ya mwenzi wake hata yale yaliyotokea wakati wa uchumba wenu ili mradi vurugu tupu.
Inatakiwa wanandoa wajadili kila jambo linalojitokeza hadi kulipatia suluhu, vinginevyo ni kuichimbia ndoa yenu kaburi la mapema. Wakati mwingine unaweza kukuta mwanamke analalamika juu ya kutoridhishwa kwake na matumizi ya mumewe, na hapo mume naye ataanza kukumbusha juu ya matumizi yasiyo ya lazima yaliyofanywa na mke huko nyuma. Mke naye hataridhika atakumbushia jambo lingine na lingine hadi hata mada iliyokuwa ikijadiliwa inasahaulika.
Jambo lingine ni kujumuisha mambo, matumizi ya maneno kama, mara nyingi, kila wakati au mara kwa mara si mazuri sana. Unaweza kukuta mtu mwenzi wake amekosea jambo halafu mwenzie anamwambia “Kila mara huwa unafanya hivi” au mara nyingi huwa unafanya hivyo…..Hii ni hatari kwa ustawi wa wanandoa, kwani kwa kujumuisha ni sawa na kumwambia mwenzi wako kuwa kila mara yeye ndiye mkosaji.
Kwa haya niliyoyaeleza hapa sina maana kwamba huu ndio muarobaini pekee wa kuimarisha mahusiano kwa wanandoa, bali ni moja ya mambo muhimu kati ya mengi ambayo yakizingatiwa na wanandoa wote basi ndoa yao itakuwa imara Tujadili pamoja………..
Na hapa yalikuwa maoni ya baadhi ya wasomaji......
James Adolwa said...
Kweli unavyosema kuwa maranyingi mzozo ukidhihirika ni kwasababu kuna kero lililo fichika ama kufunikiwa. Swala lingine ambalo watu wanatakikana kuzingatia....wacha nitumie kiingereza kidogo....One needs to consider what one keeps steaming under the lid of the cooking pot. If you spend your time and energy focusing on the weaknesses or faults of another then all that you will see in the other person are weaknesses and faults...and you will end up cooking up a foul tasting broth that will spill over and put out the flame of your relationship.
Instead try and focus on the strengths and virtues of your partner and in the end you will find that you keep seeing more and more good things. This is not to say that all the experiences will be pleasant but rather all the bitter, sweet, sour and salty experiences work out together such that the sum total ; the big picture, the essence of the whole experience works out to be a pleasant experience for both. I am no expert but these are the thoughts that flowed from my soul.
October 12, 2009 8:34 PM
Ramson said...
Dada yangu hapo umenena, kaka James, naona imebidi kuandikwa kwa kiingereza ili kuweka msisistizo....kaaaazi kweli kweli.
Dada Yasinta hili ni darasa tosha kwa wale wanandoa ambao hawakubahatika kujifunza namna ya kutatua migogogro ya ndani katika uwanja ulio sawa. Unajua wazee wetu walipokuwa wakituambia kuwa ndoa ni kuvumiliana wengi walitafsiri vibaya, walijua kuwa ni kumeza hasira zetu pindi tunapokosewa na hii ilitumiwa vibaya zaidi na wanawake, lakini siwalaumu bali mfumo dume ndio uliowafundisha.......
Inaposemwa kuwa ndoa ni kuvumiliana maana yake ni kujadiliana kwa uwazi pale tatizo au kunapozuka kutoelewana juu ya jambo fulani na uzingativu uwekwe kwenye kutatua tatizo sio kubishana kwa ajili ya kumtafuta mkosaji. Tumelelewa katika familia tofauti, kuna baadhi ya wanume wamefundishwa kuwa hawapaswi kuwaomba wake zao radhi hata kama wamekosa,,,,,inabidi mke awe makini kama akishajua kuwa mumewe ni wa aina hiyo.....
Anonymous said...
Darsa hilo Yasinta, safi sana, umemaliza yote hata cha kuongeza sina kwa leo labda kifupi sana wanasema katika maandiko matakatifu kwamba "upendo huvumilia, hauhesabu mabaya na kadhalika..." basi kama tafsiri sahihi ya upendo ikiwepo miongoni mwa wana ndoa basi mchezo umeisha, du ni hivi jioni hii nilikuwa nasikiliza kipindi cha maridhiano kupitia redio Maria Tanzania du, niliyoyasikia huko yanatisha kisa kusaka mtoto sijui ujiko kwa mwanaume! na kisa kingine kilikuwa wiki iliyopita ambapo mwanaume alienda kuazima dume ili limzalishie watoto, huko kote mwanamke alikuwa anashinikizwa lazima afanye mapenzi na hilo beberu!!
SIMON KITURURU said...
Bomba la somo hili Dada Yasinta!
Lakini sijui kwanini huu msemo wa kuwa Vikombe hugongana kabatini huwa na wasiwasi nao kwa kuwa nashindwa kuwa na uhakika kuwa kihalihalisi labda VIKOMBE hugonganishwa na HAVIGONGANI tu kienyeji ndani ya KABATI.
Anonymous said...
My sista unanikuna jamani hilo ni kweli my sista kwani kila mtu kalelea kivyake na malezi yake just meet with her /him ukubwani ni lazima kuwe na migongano ya hapa na pale nduguyo tu mwajibizana sembuse mtu baki ooh please Kaka Simon Kitururu kwani utakuta wewe ukisusa wenzio wanakula food yote lkn familia nyingine ukisusa watu hawali mpaka ujongee mezani,Kuna wengine hata hajui kumheshimu dadaake or kakaake yote ni malezi hp umeelewa brother from anaother mother meanz ya vikombe kugongana ni misemo ya mafumbo ya mababu zetu soo Open ya Eyes oky!!!!
chib said...
Big up Kitururu, huwa naupinga msemo huo wa vikombe kabatini kugongangana, ukweli kama kabati imetulia, vitagongana vipi, ni wale wenye mafujo tu ndio huvigonganisha, au kama unakaa Sumatra ambako matetemeko ya ardhi hayaishi, hapo ndio vitagonganishwa na tetemeko. Ypte kwa yote, somo hilo ni zuri kabisa kwa watu wote wenye ndoa na watarajiwa.
SIMON KITURURU said...
@Anony: nankunukuuu ``ooh please Kaka Simon Kitururu kwani utakuta wewe ukisusa wenzio wanakula food yote......''
Hapo si kunauwezekano kiwagonganishacho ni FUDI?:-)
Nimekuelewa lakini MKUU na pointi yako nimeipata.
@MKUU CHIB: Hapo kwa mtazamo wangu umemaliza NUKTA
Markus Mpangala said...
Ni MSARAGAMBO hapo
Yasinta Ngonyani said...
Nachukua nafasi hii kuwashukuruni wote kwa maoni yenu kwani huku ndio kujifunza. Maana kila mtu anajifunza toka kwa mwingine. Ila sifungi mjadala karibuni kujadili zaidi
Subscribe to:
Posts (Atom)