Malaria ni moja ya magonjwa hatari yanayoambukizwa kwa haraka sana. Gonjwa hili linaenea zaidi kwenye nchi za tropiki na (subtropical) juu zaidi kwenye joto duniani, zaidi ya yote Afrika. Dalili kubwa kujua una malaria ni joto la kupita kiasi(homa), baridi ya nguvu, maumivu ya kichwa, maumivu ya mwili, kutokwa na jasho. Pia kinyaa, kutapika na kuhara inaweza kutokea pia.
Wasiliana na daktari kama umepata joto baada ya kusafiri nchi za joto ambazo kuna uwezekano wa kuambukizwa na malaria, hata kama ulikuwa unatumia kinga. Mimi na familia yangu hapa juzi tulipokuwa TZ wote tumeumwa malaria na wakati huo huo tulikuwa tunatumia kinga. Kwa hiyo kula/kunywa kinga si kuwa hutapata malaria.
Watu zaidi ya milioni 300 kila mwaka huambukizwa na malaria. Zaidi ya milioni moja wanakufa na vifo vingi ni watoto hasa Afrika. Hapa Sweden kuna ripoti watu kama 100 husumbuliwa na malaria kwa mwaka. Wengi wao wameambukizwa Afrika
Ugonjwa huu husababishwa na protozo ambazo ni seli moja kutoka mnyama/mdudu ambaye ni familia moja na plasmodium na kuingia ndani ya mwili wa binadamu kwa kuumwa na mbu wa malaria. Vimelea(parasiter) vinaingia ndani ya seli za maini na humu wanagawana kabla maambukizo ya seli za dawa nyekundu(corpuscle)
Dalili nyingine
Muda kutoka maambukizo mpaka homa kwa kawaida ni kati ya wiki mbili mpaka wiki nne. Lakini inawezekana ikachukua miezi mingi kwa yale malaria ambayo si hatari sana, au muda mrefu zaidi.
Kuna ile aina hatari ya malaria ambayo dalili zake ni ngumu na maambukizi yake hajatibiki kwa hiyo watu wengi wanaweza kuzimia au kufa.
Aina ya pili ya malaria ina dalili ambazo zinaweza kuzuilika ila zinarudiarudia “baada ya siku mbili” au baada ya siku tatu.
Kupinga/kuzuia
Kama unasafiri katika sehemu za malaria jaribu kujiepusha kuumwa na mbu kwa kutumia dawa (anti-mosquito), vaa nguo mbazo unajua zinafunika mwili mzima hasa wakati wa jioni na usiku na tumia chandalua.
Mbu mara nyingi wanauma jioni na wakati wa usiku. Kama unajua sehemu uendayo kuna mbu wa malaria ni lazima uwe na dawa kwa nia ya kuzuia malaria.
Hata kama matibabu ya kuzuia sio 100% yanakinga, ni muhimu kuzuia kwa kunywa dawa kwa sababu ukiacha inaweza kuhatarisha na kusabisha ugonjwa mwingine zidi ya malaria.
Uchunguzi
Utambuzi wa malaria unafanyika kwa kupima damu kwenye darubini.Lakini hapa nilipokuwa nyumbani nilishangaa sana nilipojisikia vibaya nilienda kupima. Nilikwenda kwenye kliniki ya mchina mmoja yeye hatoi damu anatumia komputa tu anaweka vifaa kwenye vidole na inachukua nusu dakika kugundua kuwa una wadudu wa malaria au sio.
Matibabu
Inasemekana kuna dawa nyingi zenye nguvu ambazo zinaweza kutibu malaria.
Kwa urahisi inabidi kunywa dawa mara mbili mpaka mara tatu kwa siku (usiku na mchana). Kama hali inakuwa mbaya sana ni lazima upewe dawa moja kwa moja kwenye mishipa ya damu.
Wengi wanaweza kutibiwa muda mrefu, wakati huohuo mgonjwa mwingine wa malaria anaweza kuhitaji matibabu ya uangalizi makini (intensive care) Muhimu ni kwamba matibabu yaanze mara moja uonapo dalili.
Showing posts with label ugonjwa hatari. Show all posts
Showing posts with label ugonjwa hatari. Show all posts
Friday, April 3, 2009
Wednesday, October 22, 2008
MALARIA NI UGONJWA HATARI
Habari za ziku mbili hizi nilikuwa katika harakati za kuitafuta picha hii. Ngoja tuiangalie kidogo nadhani wote mmegundua ni nini. Hata hivvyo nitawaeleza kidogo.

Hapa ni mnaona jinsi malaria yanavyoharibu chembechembe za damu(blood cell) katika miili yetu. Malaria aina hii yanaitwa malaria malaria. Ilikuwa mwaka 2001 wakati tulipokuwa Tanzania, nilitaka kumpoteza mume wangu kwa homa hii ya malaria. Nina maana vidudu hivi vya malaria mnavyoviona vilikuwa mwilini mwake.

Hapa ni mnaona jinsi malaria yanavyoharibu chembechembe za damu(blood cell) katika miili yetu. Malaria aina hii yanaitwa malaria malaria. Ilikuwa mwaka 2001 wakati tulipokuwa Tanzania, nilitaka kumpoteza mume wangu kwa homa hii ya malaria. Nina maana vidudu hivi vya malaria mnavyoviona vilikuwa mwilini mwake.
Subscribe to:
Posts (Atom)