Showing posts with label uvumilivu. Show all posts
Showing posts with label uvumilivu. Show all posts
Friday, June 1, 2018
UJUMBE WA LEO IJUMAA YA KWANZA YA MWEZI HUU WA SITA...MAPENZI
Akupendaye atakuvumilia udhaifu wako wote hatakuhesabia makosa yako kwa kukata tamaaa juu yako bali atatafuta njia ya kukusaidia ujione mwenye thamani na kuwa na furaha maishani mwako
IJUMAA NJEMA NA MWANZO MWEMA WA MWEZI!...
Thursday, January 9, 2014
UNAKUMBUKA HABARI/HADITH HII KITABU CHA DARASA LA SITA:- MVUMILIVU HULA MBIVU? KUMBUKUMBU!!
Hapo zamani za kale Sungura na Mbwa Mwitu walioa mabinti wa jamaa mmoja. Mbwa Mwitu alimwoa kifungua mimba na Sungura kitinda mimba. Mbwa Mwitu alikuwa mvivu sana tena mlafi. Sungura alikuwa hodari wa kutega ndege. Kila siku nyumbani kwa Sungura kulikuwa hakukosekani kitoweo kizuri. Mbwa Mwitu akaanza kumwonea wivu Sungua kwa sababu alipendwa na watu wote wote kijijini.
Mwaka fulani njaa ilitokea katika kijiji chao. Mbwa Mwitu na Sungura wakamwendea mkwe wao kuomba ardhi ya kulima. Akawaonyesha mwitu mzuri wenye rutuba nyingi. Sungura hakupenda kufyeka msitu pamoja na Mbwa mwitu. Alikataa kwa sababu aliuelewa sana uvivu wa Mbwa Mwitu.
Kila siku asubuhi Mbwa Mwitu alipokwisha pata kifungua kinywa alikwenda shambani. Alipofika huko alikata mti mmoja, miwili au mitatu, kisha akakaa chini ya mti. Kwenye mti kulikuwa na mtambazi uliotambaa juu na kushikilia matawi imara kabisa. Mbwa Mwitu alitengeza pembea nzuri sana juu ya mtambazi huo. Ikawa kila afikapo shambani kukata miti miwili, mitatu, kisha hurukia pembea yake akijiningíniza.
Kila siku Mbwa Mwitu alirejea nyumbani mapema na kufanya fitina kubwa nyumbani kwa Sungura. Alimwambia shemeji yake kwamba Sungura hafanyi kazi yo yote ya kutayarisha shamba. Kazi anayoifanya ni kutege ndege tu. Kwa kuwa Sungura alikuwa hodari, kila siku alileta ndege aliowanasa kwa mitego yake. Jambo hili lilimfanya mke wa Sungura aamini maneno ya Mbwa Mwitu. Mke wa Sungura alipoona hayo, ugomvi ukazuka kati yake na mumewe. Ugomvi huu ukaendelea siku baada ya siku. Mbwa Mwitu alikuwa ibilisi mbaya sana. Sungura alijua haya yote yalitokana na fitina ya Mbwa mwitu. Hakusema neno. Alivumilia kwa sababu alifahamu kuwa njia ya mwongo ni fupi.
Majira ya kupanda yalipowadia Mbwa Mwitu alimwendea tena mkwewe kuomba aina mbalimbali za mbegu akapande shambani mwake. Akapewa. Mbwa Mwitu alipokwenda shambani, alichukua kigae. Akakoka moto, kisha akakaanga zile mbegu kwenye kigae, akala akashiba , halafu akalala fofofo. Mbegu zilizobaki akaziweka akiba mpaka kesho yake. Asubuhi ya siku iliyofuata aliendelea na mambo yale yale. Kama waswahili wasemavyo, "Chovya chovya humaliza buyu la asali", hivyo Mbwa Mwitu alimaliza mbegu zote.
Sungura hakwenda kwa mkwewe kuomba mbegu. Hii ilimfanya Mbwa Mwitu azidi kutia fitina, hata Sungura akawa anachukiwa sana. Hata hivyo akaendalea kuvumilia. Baada ya kununua mbegu za kila namna kwa fedha alizojiwekea akiba, Sungura alikwenda shambani mwake akapanda. Punde si punde, mvua kubwa ikanyesha na mbegu zote zikaota vizuri sana.
Wakati wa kupalilia ulipotimia, Mbwa Mwitu akaendelea na mchezo wake ule ule wa pembea. Lakini Sungura alifanya bidii mpaka shamba lake likawa safi kabisa. Alifanya kazi hiyo kwa juhudi kubwa, akayafuata mashauri ya wataalamu wa kilimo. Juhudi yako pamoja na maarifa ndivyo vilivyokuwa msingi wa kulipata shamba kubwa lenye mimea mizuri.
Mbwa Mwitu alikwenda kisirisiri kuangalia shamba la Sungura. Uzuri wake ulimshtua sana, naye akazidi kumwonea wivu. Alikata shauri kuliharibu. Akakusanya majani makavu na kueneza katika shamba ya Sungura, ili ayatie moto na kuliunguza shamba. Lakini kwa kudura za Mungu; Sungura aliwahi kugundua hila hiyo. Mbwa mwitu alipotaka kulichoma moto, Sungura aliwahi mapema shambani mwake. Mbwa Mwitu akashindwa kuliharibu shamba la Sungura.
Mbwa mwitu hakuchoka kumfanyia Sungura hila. Baada ya miezi kadhaa alipeleleza habari za shamba la Sungura akafahamu kuwa mazao yalikuwa tayari kuvunwa. Akakusudia kuyaiba mazao ya Sungura. Alijidai kwamba shamba lile lilikuwa lake. Akawaomba mkwe na jamaa wajitayarishe kwenda shambani kuvuna, lakini Sungura akazipata habari hizo.
Kesho yake asubuhi na mapema, Sungura akawahi shambani mwake akiwa na jamaa. Mbwa Mwitu alipogundua kwamba Sungura amewahi, akalazimika kuwapeleka wale aliokuwa nao shambani kwake. Walipowasili mahali Mbwa Mwitu alipopaita shamba lake, hawakuona dalili y yote ya mazao. Mkwe wake alihamaki, akamsaili kwa nini hakukuwa na mazao. Mbwa Mwitu alifedheheka akashindwa kujibu kwa aibu. Karibu na shamba chini ya mti mkubwa, wakaona mahali alipokaangia mbegu. Waligundua maganda ya karanga na mpunga yametapakaa huku na huko. Mkwe wa Mbwa Mwitu na jamaa wakarudi nyumbani wamekasirika sana.
Jioni ileile, Sungura alimwendea mkwe wake akamweleze kwamba angefurahi sana kama yeye pamoja na jamaa wangefika kuliona shamba lake. Mkwewe alikataa shauri hili. Akaeleza jinsi alivyotendewa na Mbwa Mwitu. Sungura akambembeleza sana mkwewe mwishowe akakubali.
Waliondoka asubuhi na mapema kwenda kuliona shamba la Sungura. Walipofika shambani wakaona mazao mengi yaliyostawi vizuri. Sungura akamweleza kwamba hilo ndilo shamba lake. Akawaomba waingie shambani kuvuna. Wote waliofika walifurahi sana. Zaidi ya hayo walishangaa jinsi Sungura alivyokuwa mvumilivu kwa fitina za Mbwa Mwitu. Mkwe wa Sungura akaona ni kweli kwamba matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno. Mbwa Mwitu alikuwa amesema maneno mengi kujisifu na kumfitini Sungura lakini hakuna alilokuwa ametenda.
Jioni ile mkwa wao aliwaita Sungura, Mbwa Mwitu na jamaa wote, akasema, "Leo tumepata fundisho kubwa kwa vijana hawa wawili, Sungura na Mbwa Mwitu. Kwa juhudi na uvumilivu, Sungura amejipatia chakula cha kutosha. Kwa ajili ya fitina, Mbwa Mwitu hakuambulia cho chote. Nataka wote mjifunze kuwa "Juhudi ni Shina la Maendeleo," na ya kuwa kwetu tunayo ahadi isemayo " Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko," Kwa hiyo anamwonya Mbwa Mwitu aache fitina, uchochezi na uvivu. Badala yake afanye kazi ili afaidi matunda ya jasho lake."
Tangu siku ile Mbwa Mwitu alianza kujirekebisha. Akashirikiana na wanakijiji wenzake kuendeleza kijiji chao. Kutokana na hadithi hii twakumbuka maneno ya wahenga wetu yasemayo "Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu."
UJUMBE:- Hii hutokea mara nyingi sana ..Tuache uvuvi, fitina na tufanye kazi ili kuendelea..Akina Sungura wapo wengi sana katika dunia hii.
Mwaka fulani njaa ilitokea katika kijiji chao. Mbwa Mwitu na Sungura wakamwendea mkwe wao kuomba ardhi ya kulima. Akawaonyesha mwitu mzuri wenye rutuba nyingi. Sungura hakupenda kufyeka msitu pamoja na Mbwa mwitu. Alikataa kwa sababu aliuelewa sana uvivu wa Mbwa Mwitu.
Kila siku asubuhi Mbwa Mwitu alipokwisha pata kifungua kinywa alikwenda shambani. Alipofika huko alikata mti mmoja, miwili au mitatu, kisha akakaa chini ya mti. Kwenye mti kulikuwa na mtambazi uliotambaa juu na kushikilia matawi imara kabisa. Mbwa Mwitu alitengeza pembea nzuri sana juu ya mtambazi huo. Ikawa kila afikapo shambani kukata miti miwili, mitatu, kisha hurukia pembea yake akijiningíniza.
Kila siku Mbwa Mwitu alirejea nyumbani mapema na kufanya fitina kubwa nyumbani kwa Sungura. Alimwambia shemeji yake kwamba Sungura hafanyi kazi yo yote ya kutayarisha shamba. Kazi anayoifanya ni kutege ndege tu. Kwa kuwa Sungura alikuwa hodari, kila siku alileta ndege aliowanasa kwa mitego yake. Jambo hili lilimfanya mke wa Sungura aamini maneno ya Mbwa Mwitu. Mke wa Sungura alipoona hayo, ugomvi ukazuka kati yake na mumewe. Ugomvi huu ukaendelea siku baada ya siku. Mbwa Mwitu alikuwa ibilisi mbaya sana. Sungura alijua haya yote yalitokana na fitina ya Mbwa mwitu. Hakusema neno. Alivumilia kwa sababu alifahamu kuwa njia ya mwongo ni fupi.
Majira ya kupanda yalipowadia Mbwa Mwitu alimwendea tena mkwewe kuomba aina mbalimbali za mbegu akapande shambani mwake. Akapewa. Mbwa Mwitu alipokwenda shambani, alichukua kigae. Akakoka moto, kisha akakaanga zile mbegu kwenye kigae, akala akashiba , halafu akalala fofofo. Mbegu zilizobaki akaziweka akiba mpaka kesho yake. Asubuhi ya siku iliyofuata aliendelea na mambo yale yale. Kama waswahili wasemavyo, "Chovya chovya humaliza buyu la asali", hivyo Mbwa Mwitu alimaliza mbegu zote.
Sungura hakwenda kwa mkwewe kuomba mbegu. Hii ilimfanya Mbwa Mwitu azidi kutia fitina, hata Sungura akawa anachukiwa sana. Hata hivyo akaendalea kuvumilia. Baada ya kununua mbegu za kila namna kwa fedha alizojiwekea akiba, Sungura alikwenda shambani mwake akapanda. Punde si punde, mvua kubwa ikanyesha na mbegu zote zikaota vizuri sana.
Wakati wa kupalilia ulipotimia, Mbwa Mwitu akaendelea na mchezo wake ule ule wa pembea. Lakini Sungura alifanya bidii mpaka shamba lake likawa safi kabisa. Alifanya kazi hiyo kwa juhudi kubwa, akayafuata mashauri ya wataalamu wa kilimo. Juhudi yako pamoja na maarifa ndivyo vilivyokuwa msingi wa kulipata shamba kubwa lenye mimea mizuri.
Mbwa Mwitu alikwenda kisirisiri kuangalia shamba la Sungura. Uzuri wake ulimshtua sana, naye akazidi kumwonea wivu. Alikata shauri kuliharibu. Akakusanya majani makavu na kueneza katika shamba ya Sungura, ili ayatie moto na kuliunguza shamba. Lakini kwa kudura za Mungu; Sungura aliwahi kugundua hila hiyo. Mbwa mwitu alipotaka kulichoma moto, Sungura aliwahi mapema shambani mwake. Mbwa Mwitu akashindwa kuliharibu shamba la Sungura.
Mbwa mwitu hakuchoka kumfanyia Sungura hila. Baada ya miezi kadhaa alipeleleza habari za shamba la Sungura akafahamu kuwa mazao yalikuwa tayari kuvunwa. Akakusudia kuyaiba mazao ya Sungura. Alijidai kwamba shamba lile lilikuwa lake. Akawaomba mkwe na jamaa wajitayarishe kwenda shambani kuvuna, lakini Sungura akazipata habari hizo.
Kesho yake asubuhi na mapema, Sungura akawahi shambani mwake akiwa na jamaa. Mbwa Mwitu alipogundua kwamba Sungura amewahi, akalazimika kuwapeleka wale aliokuwa nao shambani kwake. Walipowasili mahali Mbwa Mwitu alipopaita shamba lake, hawakuona dalili y yote ya mazao. Mkwe wake alihamaki, akamsaili kwa nini hakukuwa na mazao. Mbwa Mwitu alifedheheka akashindwa kujibu kwa aibu. Karibu na shamba chini ya mti mkubwa, wakaona mahali alipokaangia mbegu. Waligundua maganda ya karanga na mpunga yametapakaa huku na huko. Mkwe wa Mbwa Mwitu na jamaa wakarudi nyumbani wamekasirika sana.
Jioni ileile, Sungura alimwendea mkwe wake akamweleze kwamba angefurahi sana kama yeye pamoja na jamaa wangefika kuliona shamba lake. Mkwewe alikataa shauri hili. Akaeleza jinsi alivyotendewa na Mbwa Mwitu. Sungura akambembeleza sana mkwewe mwishowe akakubali.
Waliondoka asubuhi na mapema kwenda kuliona shamba la Sungura. Walipofika shambani wakaona mazao mengi yaliyostawi vizuri. Sungura akamweleza kwamba hilo ndilo shamba lake. Akawaomba waingie shambani kuvuna. Wote waliofika walifurahi sana. Zaidi ya hayo walishangaa jinsi Sungura alivyokuwa mvumilivu kwa fitina za Mbwa Mwitu. Mkwe wa Sungura akaona ni kweli kwamba matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno. Mbwa Mwitu alikuwa amesema maneno mengi kujisifu na kumfitini Sungura lakini hakuna alilokuwa ametenda.
Jioni ile mkwa wao aliwaita Sungura, Mbwa Mwitu na jamaa wote, akasema, "Leo tumepata fundisho kubwa kwa vijana hawa wawili, Sungura na Mbwa Mwitu. Kwa juhudi na uvumilivu, Sungura amejipatia chakula cha kutosha. Kwa ajili ya fitina, Mbwa Mwitu hakuambulia cho chote. Nataka wote mjifunze kuwa "Juhudi ni Shina la Maendeleo," na ya kuwa kwetu tunayo ahadi isemayo " Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko," Kwa hiyo anamwonya Mbwa Mwitu aache fitina, uchochezi na uvivu. Badala yake afanye kazi ili afaidi matunda ya jasho lake."
Tangu siku ile Mbwa Mwitu alianza kujirekebisha. Akashirikiana na wanakijiji wenzake kuendeleza kijiji chao. Kutokana na hadithi hii twakumbuka maneno ya wahenga wetu yasemayo "Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu."
UJUMBE:- Hii hutokea mara nyingi sana ..Tuache uvuvi, fitina na tufanye kazi ili kuendelea..Akina Sungura wapo wengi sana katika dunia hii.
Friday, October 18, 2013
IJUMAA YA LEO NA UJUMBE HUU MWANZO WA MAISHA NI MGUMU LAKINI UVUMULIVU NDIO KINGA!!!
Uvumilivu ni Msingi wa maisha ya kila binadamu..Mwanzo ni mgumu...IJIMAA NJEMA KWA KILA ATAKAYEPITA HAPA.....KAPULYA WENU.
Friday, January 25, 2013
NAWATAKIENI WOTE IJUMAA NJEMA KWA WIMBO HUU:- MOYO WA SUBIRA NA LINEX!!!!
IJUMAA NJEMA JAMANI ...TUWE NA MOYO WA SUBIRA HATA KAMA TUMEUMIA/UMIZWA....KAPULYA
Wednesday, January 11, 2012
Ndoa ni ninyi wenyewe, Siyo watu wa nje
TULIKUWA TUMEPUMZIKA KIDOGO NA KIPENGELE CHETU CHA MARUDIO KILA SIKU KAMA HII YA JUMATANO. NA LEO KATIKA UPEKUZI WA KAPULYA AMEKUTANA NA MAKALA HII NA AMEONA SI MBAYA KAMA WENGI TUKIJUA KWANI KAMA NISEMAVYO KURUDIA SOMA NDIO MTU UNAPOELEWA ZAIDI. MAKALA HII NIMEIKUTA HAPA. KARIBUNI.
---------------------------------------------------------------------------------------------
SIRI moja kubwa ya kuwa na ndoa nzuri ni wanandoa wenyewe kujitambua kuwa wao ndiyo wenye deni la kuimarisha uhusiano walionao.
Ndiyo kusema kuwa kila siku katika maisha yako, unapaswa kutafuta mbinu za kufanya ili uhusiano wenu uendelee kuwa mzuri.
Siku moja nilikuwa napita Sinza (Dar es Salaam), nikamsikia dada mmoja akijibizana na mwenzi wake kwenye simu; Aah! kwani wewe unataka muda huu niwe wapi? Haya basi niko chooni.
Hayakuwa majibu mazuri, kiasi dada mwingine aliyekuwa karibu, akamsihi mwenzake asizungumze vile.Watu wengi wanapenda kuwa na ndoa nzuri, lakini wao hawajui kuwafanyia mazuri wenzao. Utakuwaje na ndoa nzuri wakati kauli zako ni chafu?
Jitahidi kuwa na kauli nzuri kwa mwenzi wako. Hata pale mwenziyo anapokukosea, zungumza naye kwa njia ya kuondoa kasoro, si kutukanana. Siku zote waza namna ya kuujenga uhusiano wenu. Usidhani ndoa nzuri za wenzio ni jambo linaloshindikana kwako, hapana. Ndoa haijengwi kwa matofali, bali kauli njema na matendo mema.
Kumbuka hakuna mtu aliyezaliwa aje kuiimarisha ndoa yako, ni wewe mwenyewe unapaswa kufanya kazi hiyo. Anza leo kuchukua hatua kama ndoa yako ina walakini huo, utashangaa utakavyokuwa na ndoa nzuri. Katika maisha hakuna lisilowezekana. Kwanza weka lengo, kisha chukua hatua, utafanikiwa.
Ni muhimu kujifunza masuala haya kwani elimu haina mwisho. Wengi wakishaingia kwenye ndoa, basi hudhani wameshamaliza kila kitu. Ni makosa makubwa, unapaswa kuendelea kutafuta mbinu mpya kila siku ili mfaidi raha za ndoa.
Kuna mengi ya kujifunza:
Katika ndoa kuna mengi ya kujifunza, mojawapo ni kujua mwenzi wako anapenda nini. Kwa mfano wanaume wengi wanapenda wake zao wawe na utayari katika mahusiano.Unaweza kushangaa, lakini ni ukweli. Tafiti zinaonyesha watu wasio kwenye ndoa hukutana kimwili mara nyingi zaidi kuliko walio kwenye ndoa, licha ya kuwa wanalala kitanda kimoja.
Watu wakishaingia kwenye ndoa, hufanya tendo hilo kwa muda mfupi zaidi kuliko ilivyokuwa kabla hawajaoana, unajua ni kwa nini? Utayari huwa matatizoni. Sababu ziko nyingi, lakini mojawapo ni wanaume wengi kurudi majumbani wamelewa chakari, wananuka pombe na wake zao wanalazimika tu, wafanyeje.
Lakini wakati wa uchumba, wanaume hao huenda kwa wapenzi wao wakiwa hawajalewa.
Ndiyo ukweli. Kimsingi wanandoa kila mmoja anatarajia kuona mwenzi wake anamjali na anamsikiliza. Kufanikiwa hili, lazima kutumia akili.
Kuna ambao licha ya kuwa tayari kaingia kwenye ndoa, lakini kwa upumbavu, anazungumzia habari za mpenzi wa zamani.
Pia kuna walio kwenye ndoa, lakini wanajali zaidi watu wengine wa nje au kuwasikiliza zaidi wazazi ambao mara kadhaa wamekuwa chanzo cha ndoa kuvunjika.
Jamani hata Biblia imeandika;
Mtu atawaacha wazazi wake na kuandamana na mkewe, hao wawili watakuwa mwili mmoja.
Wengine wako katika ndoa lakini wana lundo la wapenzi nje. Hapo ndoa yako ikiyumba utamlaumu nani? Fanya jitihada kuipa uhai ndoa yako, iwe paradiso ya kweli.Kuna ambao badala ya kutamani kurudi nyumbani, wao hutamani kuchelewa, maana nyumbani hakukaliki.Yaani hakuna mapenzi, hakuna kinachovutia. Mume au mke hapendi kujifunza mambo zaidi.
Ndugu yangu rekebisha ndoa yako, uishi kwa furaha.
Dismas Lyassa ni mtaalam wa mahusiano, wasiliana naye kwa simu 0754 498972 au 0786 148105.
TUKUTANE TENA WAKATI UJAO AU NISEME JUMATANO IJAYO.
---------------------------------------------------------------------------------------------
SIRI moja kubwa ya kuwa na ndoa nzuri ni wanandoa wenyewe kujitambua kuwa wao ndiyo wenye deni la kuimarisha uhusiano walionao.
Ndiyo kusema kuwa kila siku katika maisha yako, unapaswa kutafuta mbinu za kufanya ili uhusiano wenu uendelee kuwa mzuri.
Siku moja nilikuwa napita Sinza (Dar es Salaam), nikamsikia dada mmoja akijibizana na mwenzi wake kwenye simu; Aah! kwani wewe unataka muda huu niwe wapi? Haya basi niko chooni.
Hayakuwa majibu mazuri, kiasi dada mwingine aliyekuwa karibu, akamsihi mwenzake asizungumze vile.Watu wengi wanapenda kuwa na ndoa nzuri, lakini wao hawajui kuwafanyia mazuri wenzao. Utakuwaje na ndoa nzuri wakati kauli zako ni chafu?
Jitahidi kuwa na kauli nzuri kwa mwenzi wako. Hata pale mwenziyo anapokukosea, zungumza naye kwa njia ya kuondoa kasoro, si kutukanana. Siku zote waza namna ya kuujenga uhusiano wenu. Usidhani ndoa nzuri za wenzio ni jambo linaloshindikana kwako, hapana. Ndoa haijengwi kwa matofali, bali kauli njema na matendo mema.
Kumbuka hakuna mtu aliyezaliwa aje kuiimarisha ndoa yako, ni wewe mwenyewe unapaswa kufanya kazi hiyo. Anza leo kuchukua hatua kama ndoa yako ina walakini huo, utashangaa utakavyokuwa na ndoa nzuri. Katika maisha hakuna lisilowezekana. Kwanza weka lengo, kisha chukua hatua, utafanikiwa.
Ni muhimu kujifunza masuala haya kwani elimu haina mwisho. Wengi wakishaingia kwenye ndoa, basi hudhani wameshamaliza kila kitu. Ni makosa makubwa, unapaswa kuendelea kutafuta mbinu mpya kila siku ili mfaidi raha za ndoa.
Kuna mengi ya kujifunza:
Katika ndoa kuna mengi ya kujifunza, mojawapo ni kujua mwenzi wako anapenda nini. Kwa mfano wanaume wengi wanapenda wake zao wawe na utayari katika mahusiano.Unaweza kushangaa, lakini ni ukweli. Tafiti zinaonyesha watu wasio kwenye ndoa hukutana kimwili mara nyingi zaidi kuliko walio kwenye ndoa, licha ya kuwa wanalala kitanda kimoja.
Watu wakishaingia kwenye ndoa, hufanya tendo hilo kwa muda mfupi zaidi kuliko ilivyokuwa kabla hawajaoana, unajua ni kwa nini? Utayari huwa matatizoni. Sababu ziko nyingi, lakini mojawapo ni wanaume wengi kurudi majumbani wamelewa chakari, wananuka pombe na wake zao wanalazimika tu, wafanyeje.
Lakini wakati wa uchumba, wanaume hao huenda kwa wapenzi wao wakiwa hawajalewa.
Ndiyo ukweli. Kimsingi wanandoa kila mmoja anatarajia kuona mwenzi wake anamjali na anamsikiliza. Kufanikiwa hili, lazima kutumia akili.
Kuna ambao licha ya kuwa tayari kaingia kwenye ndoa, lakini kwa upumbavu, anazungumzia habari za mpenzi wa zamani.
Pia kuna walio kwenye ndoa, lakini wanajali zaidi watu wengine wa nje au kuwasikiliza zaidi wazazi ambao mara kadhaa wamekuwa chanzo cha ndoa kuvunjika.
Jamani hata Biblia imeandika;
Mtu atawaacha wazazi wake na kuandamana na mkewe, hao wawili watakuwa mwili mmoja.
Wengine wako katika ndoa lakini wana lundo la wapenzi nje. Hapo ndoa yako ikiyumba utamlaumu nani? Fanya jitihada kuipa uhai ndoa yako, iwe paradiso ya kweli.Kuna ambao badala ya kutamani kurudi nyumbani, wao hutamani kuchelewa, maana nyumbani hakukaliki.Yaani hakuna mapenzi, hakuna kinachovutia. Mume au mke hapendi kujifunza mambo zaidi.
Ndugu yangu rekebisha ndoa yako, uishi kwa furaha.
Dismas Lyassa ni mtaalam wa mahusiano, wasiliana naye kwa simu 0754 498972 au 0786 148105.
TUKUTANE TENA WAKATI UJAO AU NISEME JUMATANO IJAYO.
Thursday, October 27, 2011
UJUMBE WA LEO UKUTOKAO KWA KAPULYA NI HUU HAPA!!!
Ndoto zetu zote zinaweza kutimizwa ikiwa tutakuwa na ujasiri wa kutimizwa.
Ngoja Kaka Sam amalizie na wimbo huuu...
ALHAMIS NJEMA JAMANI NA TUSISAHAU KUMSHUKURU MUNGU KWA KILA JEMA NA KILA SEKUNDE ATUPAYE NA KILA ATUJALIALO.
Ngoja Kaka Sam amalizie na wimbo huuu...
ALHAMIS NJEMA JAMANI NA TUSISAHAU KUMSHUKURU MUNGU KWA KILA JEMA NA KILA SEKUNDE ATUPAYE NA KILA ATUJALIALO.
ELIMU:- EBU TUSIKILIZE SIMULIZI YA DADA YACINTA, HAKUNA KISICHOWEZEKANA!!
Kila la kheri Yacinta...hakuna kabisa lisilowezekana kama unapenda. Mvumilivu hula mbivu.
Thursday, October 15, 2009
LAITI KAMA NINGEKUFAHAMU KABLA.........HADITHI YA KUFIKIRIKA
Miaka mitano iliyopita nilikuwa natafuta mke wa kumuoa ambaye angekuwa na sifa nizitakazo. Nilikuwa natafuta msichana mzuri wa wastani maana sikutaka kuoa mke mzuri kupindukia asije niua bure kwa presha na jakamoyo. Nilikuwa natafuta binti atakanikubali kama nilivyo na mapungufu yangu na mimi niliahidi kumkubali na mapungufu yake ili mradi asiwe ni mwenye tamaa ya kupenda sana pesa na mfujaji.
Awe na staha na anayeweza kukabiliana na hali yoyote, niwe nacho, nisiwe nacho au kwa kifupi tupendane kwa shida na raha.
Pamoja na sifa nyingine ndogo ndogo, lakini muhimu ni upendo na amani vitawale nyumbani kwangu.
Hatimaye nilimpata Binti Yasinaty, na kukutana kwetu kulikuwa ni kama muujiza, nakumbuka siku hiyo nilipanda daladala nikielekea kazini na kwa bahati kiti nilichokalia kilikuwa ni cha mwisho upande wa dirishani. Wakati nakaa nikahisi kukalia kitu kigumu, nilipopapasa ilikuwa ni simu mpya kabisa tena ya bei mbaya kama sikosei wakati huo ilikuwa inauzwa shilingi laki nne kwa wakati huo, kumbuka kwamba hapa nazungumzia habari ya miaka mitano iliyopita.
Kwa bahati mbaya simu ile ilikuwa imezimwa, na nilipojaribu kuiwasha iliwaka na kuzima kuashiria kwamba betri yake iliisha chaji. Niliiweka mfukoni na kujiuliza kuwa ile simu ilikuwa ni ya nani, sikusikia mtu kulalamika kwamba amepoteza simu na niliogopa kuuliza maana nilichelea mtu kujitokeza na kusema kwamba ni yake ilihali sio yakwake.
Nilifika ofisini na kuanza kazi, baadae nilimuita katibu muhtasi wangu na kumwomba anisaidie kutafuta chaji ya ile simu kwa kuwauliza wafanyakazi pale ofisini, nilikuwa na shauku ya kumfahamu mwenye simu ile ili nimrudishie, kwani nilikuwa namuoana dhahiri akisikitika kwa kupotelewa na simu yake, kwa jinsi ilivyoonekana ilikuwa bado ilikuwa ni mpya kabisa na ilikuwa haijatumika zaidi ya wiki.
Katibu wangu muhtasi hakufanikiwa kuipata ile chaja ya ile simu. Niliweka ile simu kwenye droo ya ofisini kwangu ili jioni nikitoka nipitie nayo kariakoo ninunue chaja yake.
Ilipofika jioni alikuja mchumba wangu ambaye tulitofautiana wiki iliyopita na kuamua kutengana naye. Sikutaka kuonana naye na nilimwambia katibu wangu muhtasi amwambie kuwa niko bize na sitaki afike tena pale ofisini kwangu.
Ukweli ni kwamba nilimpenda sana lakini kitendo chake cha kukuta mwanaume mwingine chumbani kwake tena akiwa amelala kitandani kwake halafu anajidai kunidanganya kuwa eti ni binamu yake hakikunifurahisha kabisa. Nakumbuka nilisafiri kikazi kwenda Mbeya, na ilikuwa nikae kule kwa wiki moja, lakini ilitokea dharura huku Makao makuu Dar ikabidi nirudi baada ya siku mbili tu na nilipofika kwa kuwa ilikuwa ni usiku kama saa mbili niliamua kupitia kwa mchumba wangu ambaye alikuwa akiishi Mwengeili kupata chakula cha jioni kabla sijaenda kwangu Maeneo ya Sinza. Nilipofika nilimkuta akiwa nje akipika, lakini aliponiona alishtuka sana akabaki kinywa wazi, hakunipokea alibaki ameduwaa, nikahisi kuna jambo. Nilimsalimia alijibu kwa wasiwasi nilipotaka kuingia ndani, alinizuia, na huku akiongea kwa sauti yenye kutetemeka aliniambia eti ndani kuna binamu yake kaja na amejipumzisha kitandani kwake, nilishtuka. Niliiingia ndani moja kwa moja na kumkuta kijana amelala kitandani nilipomuhoji kuwa yeye ni nani na anafanya nini pale akaniambia kuwa yuko pale kwa girlfriend wake na alitaka kujua eti mimi ni nani..Sikutaka kuzua ugomvi, nilimwambia kuwa pale ni kwa dada yangu na nilifika kumsalimia, nilimuomba radhi kwa kuingia bila hodi, ila nilimshauri aharakishe kulipa mahari ili tujue kuwa dada yetu anaye mtu, ili wakati mwingine tubishe hodi, niliongea kwa utani, yule kijana alimsifia sana mchumba wangu kuwa ni mzuri hasa na anajua kupenda, alibwabwaja mambo mengi na upuuzi wao wanaofanya nikiwa sipo, niliongea naye kwa utani mwingi na kuaga na kuondoka, lakini moyoni roho ilikuwa ikiniuma kweli. Nilikuwa nampa yule binti karibu kila kitu alichohitaji, lakini kumbe hakuridhika bado akawa na mwanaume mwingine.
Nilitoka na nilimkuta kajiinamia pale nje, sikumuaga nikaondoka zangu. Nilipofika nyumbani nilimtumia ujumbe mfupi wa simu ya kiganjani nikimwambia kuwa kuanzia siku hiyo ilikuwa ni mwisho wa uhusiano wetu. Hakijibu na siku iliyofuata alipiga simu lakini sikupokea, alibadilisha namba na nilipopokea na kugundua kuwa ni yeye nilikata simu, baadae zilifuata ujumbe kadhaa wa simu yake ya kiganjani akitaka tuonane ili tuyamalize. Sikumjibu. Na ndio akaamua kuja ofisini.
Nilimpigia simu katibu muhtasi wangu na kumuamuru amwambie yule binti aondoke pale ofisini. Niliambiwa kuwa amekataa, nilimpigia simu dereva wangu na kumuuliza kama gari limeshatoka gereji, akanijibu kuwa gari litatoka baadae kidogo, nikamwambia akitoka gereji aende nalo nyumbani kisha kesho asubuhi anifuate. Gari langu liliharibika siku mbili zilizopita, hivyo nililazimika kupanda daladala au taxi kama nikiwa na dharura. Niliondoka pale ofisini nikimuacha akiongea na katibu wangu muhtasi na kuondoka zangu. Nilikodi taxi na wakati niko njiani nikakumbuka kuhusu ile simu, lakini niliisahau ofisini, kwa hiyo sikupitia kariakoo tena. Nilikwenda moja kwa moja hadi kwa rafiki yangu anayeishi maeneo ya kijitonyama na kupoteza muda huko hadi usiku ndio nikarudi nyumbani.
Siku iliyofuata dereva alinifuata na kunipeleka ofisini, nilipofika nilimpa ile simu na kumtuma akanitafutie chaja ya ile simu. Baadae alirudi akiwa na chaja ya simu ile na kunikabidhi. Niliichaji na ilipojaa niliiwasha ziliingia ujumbe kadhaa kutoka kwa watu waliokuwa wakimtafuta mwenye simu ile, nilipozisoma niligundua mwenye simu ile alikuwa anaitwa Yasinaty, nilikata shauri nimpigie mmoja wa watu waliokuwa wametuma ujumbe ambaye alionekana kuwa ni mama yake. Nilipompigia simu na kuuliza kama anamjua mwenye simu kwanza alitaka kujua mimi ni nani na kwa nini simu ya mwanaye ninayo mimi. Nilimsimulia kila kitu na nilimuomba ampe mwanae namba yangu ya simu na kumuomba amwambie awasiliane na mimi ili nimpe simu yake. Yule mama alifurahi sana na kunishukuru sana, kumbe ile simu Yasinaty alitumiwa na kaka yake aishie Ughaibuni.
Mchana nilipigiwa simu na Yasinaty na tuliongea mengi na alionekana ni binti mchangamfu kweli, alinimbia kuwa anafanya kazi kwenye Hoteli moja ya kitalii maarufu iliyoko katikati ya jiji, nilimuahidi kumpitia kazini kwake jioni nikitoka ofisini.
Nilimpitia jioni na kama alivyonielekeza kuwa yuko reception nilimkuta pale akimalizia kazi na aliniomba nimsubiri kweye kijimgahawa kilichopo pale ndani, kwa kuwa mimi sio mnywaji wa pombe niliagiza juisi ili kumsubiri. Baadae alinipitia pale nilipokaa na kunimbia kuwa anatoka hivyo tukutane nje kwani anakwenda kubadili sare za kazini. Alitoka na kunikuta nje nikimsubiri, alipanda kwenye gari na nilimuomba dereva wangu atupeleke Hoteli nyingine ya kitalii maarufu pale hapa jijini ili tupate kahawa na Yasinaty. Tulifika pale tuliagiza vinywaji. Nilitumia wasaa ule kumtazama vizuri Yasinaty, alikuwa ni binti mrembo sana, na mchangamfu hasa, naamini alistahili kufanya kazi reception.
Nilimkabidhi simu yake na yakafuata maongezi mengine ya kujuana na simulizi za hapa na pale. Huo ndio ukawa mwanzo wa kujuana na Yasinaty, ambaye baadae alikuja kuwa mke wangu mpenzi.
Laiti kama ningekufahamu kabla Yasinaty………………….
Habari hii nimetumiwa na msomaji wa blog hii ya MAISHA ambaye anasheherekea ndoa yake kutimiza miaka mitano leo. Na nimeona si vibaya kama nikiweka hapa.
Awe na staha na anayeweza kukabiliana na hali yoyote, niwe nacho, nisiwe nacho au kwa kifupi tupendane kwa shida na raha.
Pamoja na sifa nyingine ndogo ndogo, lakini muhimu ni upendo na amani vitawale nyumbani kwangu.
Hatimaye nilimpata Binti Yasinaty, na kukutana kwetu kulikuwa ni kama muujiza, nakumbuka siku hiyo nilipanda daladala nikielekea kazini na kwa bahati kiti nilichokalia kilikuwa ni cha mwisho upande wa dirishani. Wakati nakaa nikahisi kukalia kitu kigumu, nilipopapasa ilikuwa ni simu mpya kabisa tena ya bei mbaya kama sikosei wakati huo ilikuwa inauzwa shilingi laki nne kwa wakati huo, kumbuka kwamba hapa nazungumzia habari ya miaka mitano iliyopita.
Kwa bahati mbaya simu ile ilikuwa imezimwa, na nilipojaribu kuiwasha iliwaka na kuzima kuashiria kwamba betri yake iliisha chaji. Niliiweka mfukoni na kujiuliza kuwa ile simu ilikuwa ni ya nani, sikusikia mtu kulalamika kwamba amepoteza simu na niliogopa kuuliza maana nilichelea mtu kujitokeza na kusema kwamba ni yake ilihali sio yakwake.
Nilifika ofisini na kuanza kazi, baadae nilimuita katibu muhtasi wangu na kumwomba anisaidie kutafuta chaji ya ile simu kwa kuwauliza wafanyakazi pale ofisini, nilikuwa na shauku ya kumfahamu mwenye simu ile ili nimrudishie, kwani nilikuwa namuoana dhahiri akisikitika kwa kupotelewa na simu yake, kwa jinsi ilivyoonekana ilikuwa bado ilikuwa ni mpya kabisa na ilikuwa haijatumika zaidi ya wiki.
Katibu wangu muhtasi hakufanikiwa kuipata ile chaja ya ile simu. Niliweka ile simu kwenye droo ya ofisini kwangu ili jioni nikitoka nipitie nayo kariakoo ninunue chaja yake.
Ilipofika jioni alikuja mchumba wangu ambaye tulitofautiana wiki iliyopita na kuamua kutengana naye. Sikutaka kuonana naye na nilimwambia katibu wangu muhtasi amwambie kuwa niko bize na sitaki afike tena pale ofisini kwangu.
Ukweli ni kwamba nilimpenda sana lakini kitendo chake cha kukuta mwanaume mwingine chumbani kwake tena akiwa amelala kitandani kwake halafu anajidai kunidanganya kuwa eti ni binamu yake hakikunifurahisha kabisa. Nakumbuka nilisafiri kikazi kwenda Mbeya, na ilikuwa nikae kule kwa wiki moja, lakini ilitokea dharura huku Makao makuu Dar ikabidi nirudi baada ya siku mbili tu na nilipofika kwa kuwa ilikuwa ni usiku kama saa mbili niliamua kupitia kwa mchumba wangu ambaye alikuwa akiishi Mwengeili kupata chakula cha jioni kabla sijaenda kwangu Maeneo ya Sinza. Nilipofika nilimkuta akiwa nje akipika, lakini aliponiona alishtuka sana akabaki kinywa wazi, hakunipokea alibaki ameduwaa, nikahisi kuna jambo. Nilimsalimia alijibu kwa wasiwasi nilipotaka kuingia ndani, alinizuia, na huku akiongea kwa sauti yenye kutetemeka aliniambia eti ndani kuna binamu yake kaja na amejipumzisha kitandani kwake, nilishtuka. Niliiingia ndani moja kwa moja na kumkuta kijana amelala kitandani nilipomuhoji kuwa yeye ni nani na anafanya nini pale akaniambia kuwa yuko pale kwa girlfriend wake na alitaka kujua eti mimi ni nani..Sikutaka kuzua ugomvi, nilimwambia kuwa pale ni kwa dada yangu na nilifika kumsalimia, nilimuomba radhi kwa kuingia bila hodi, ila nilimshauri aharakishe kulipa mahari ili tujue kuwa dada yetu anaye mtu, ili wakati mwingine tubishe hodi, niliongea kwa utani, yule kijana alimsifia sana mchumba wangu kuwa ni mzuri hasa na anajua kupenda, alibwabwaja mambo mengi na upuuzi wao wanaofanya nikiwa sipo, niliongea naye kwa utani mwingi na kuaga na kuondoka, lakini moyoni roho ilikuwa ikiniuma kweli. Nilikuwa nampa yule binti karibu kila kitu alichohitaji, lakini kumbe hakuridhika bado akawa na mwanaume mwingine.
Nilitoka na nilimkuta kajiinamia pale nje, sikumuaga nikaondoka zangu. Nilipofika nyumbani nilimtumia ujumbe mfupi wa simu ya kiganjani nikimwambia kuwa kuanzia siku hiyo ilikuwa ni mwisho wa uhusiano wetu. Hakijibu na siku iliyofuata alipiga simu lakini sikupokea, alibadilisha namba na nilipopokea na kugundua kuwa ni yeye nilikata simu, baadae zilifuata ujumbe kadhaa wa simu yake ya kiganjani akitaka tuonane ili tuyamalize. Sikumjibu. Na ndio akaamua kuja ofisini.
Nilimpigia simu katibu muhtasi wangu na kumuamuru amwambie yule binti aondoke pale ofisini. Niliambiwa kuwa amekataa, nilimpigia simu dereva wangu na kumuuliza kama gari limeshatoka gereji, akanijibu kuwa gari litatoka baadae kidogo, nikamwambia akitoka gereji aende nalo nyumbani kisha kesho asubuhi anifuate. Gari langu liliharibika siku mbili zilizopita, hivyo nililazimika kupanda daladala au taxi kama nikiwa na dharura. Niliondoka pale ofisini nikimuacha akiongea na katibu wangu muhtasi na kuondoka zangu. Nilikodi taxi na wakati niko njiani nikakumbuka kuhusu ile simu, lakini niliisahau ofisini, kwa hiyo sikupitia kariakoo tena. Nilikwenda moja kwa moja hadi kwa rafiki yangu anayeishi maeneo ya kijitonyama na kupoteza muda huko hadi usiku ndio nikarudi nyumbani.
Siku iliyofuata dereva alinifuata na kunipeleka ofisini, nilipofika nilimpa ile simu na kumtuma akanitafutie chaja ya ile simu. Baadae alirudi akiwa na chaja ya simu ile na kunikabidhi. Niliichaji na ilipojaa niliiwasha ziliingia ujumbe kadhaa kutoka kwa watu waliokuwa wakimtafuta mwenye simu ile, nilipozisoma niligundua mwenye simu ile alikuwa anaitwa Yasinaty, nilikata shauri nimpigie mmoja wa watu waliokuwa wametuma ujumbe ambaye alionekana kuwa ni mama yake. Nilipompigia simu na kuuliza kama anamjua mwenye simu kwanza alitaka kujua mimi ni nani na kwa nini simu ya mwanaye ninayo mimi. Nilimsimulia kila kitu na nilimuomba ampe mwanae namba yangu ya simu na kumuomba amwambie awasiliane na mimi ili nimpe simu yake. Yule mama alifurahi sana na kunishukuru sana, kumbe ile simu Yasinaty alitumiwa na kaka yake aishie Ughaibuni.
Mchana nilipigiwa simu na Yasinaty na tuliongea mengi na alionekana ni binti mchangamfu kweli, alinimbia kuwa anafanya kazi kwenye Hoteli moja ya kitalii maarufu iliyoko katikati ya jiji, nilimuahidi kumpitia kazini kwake jioni nikitoka ofisini.
Nilimpitia jioni na kama alivyonielekeza kuwa yuko reception nilimkuta pale akimalizia kazi na aliniomba nimsubiri kweye kijimgahawa kilichopo pale ndani, kwa kuwa mimi sio mnywaji wa pombe niliagiza juisi ili kumsubiri. Baadae alinipitia pale nilipokaa na kunimbia kuwa anatoka hivyo tukutane nje kwani anakwenda kubadili sare za kazini. Alitoka na kunikuta nje nikimsubiri, alipanda kwenye gari na nilimuomba dereva wangu atupeleke Hoteli nyingine ya kitalii maarufu pale hapa jijini ili tupate kahawa na Yasinaty. Tulifika pale tuliagiza vinywaji. Nilitumia wasaa ule kumtazama vizuri Yasinaty, alikuwa ni binti mrembo sana, na mchangamfu hasa, naamini alistahili kufanya kazi reception.
Nilimkabidhi simu yake na yakafuata maongezi mengine ya kujuana na simulizi za hapa na pale. Huo ndio ukawa mwanzo wa kujuana na Yasinaty, ambaye baadae alikuja kuwa mke wangu mpenzi.
Laiti kama ningekufahamu kabla Yasinaty………………….
Habari hii nimetumiwa na msomaji wa blog hii ya MAISHA ambaye anasheherekea ndoa yake kutimiza miaka mitano leo. Na nimeona si vibaya kama nikiweka hapa.
Wednesday, October 15, 2008
KUMBUKUMBU+HISTORIA
Leo nimekumbuka kweli mika ya tisini; wakati nilipokuwa nasoma Songea. Familia yangu walikuwa wanaishi kijiji kimoja kiitwacho Kingoli. Sijui nisemeje ili mnielewe kwani wengine msije mkasema ni kudeka tu. Haya semeni mtakavyo. Yaani nilikuwa natembea toka Kingoli mpaka Peramiho kwa miguu kulikuwa hakuna magari. Pale kijijini kulikuwa na lori moja tu lilikuwa linasafiri kwa wiki mara moja.
Baina ya Kingoli mpaka Peramiho kuna vijiji kama vitano hivi, hivi safari hiyo ilikuwa inachukua siku moja – mbili nilikuwa nalala katika kijiji kimoja kiitwacho Mgazini. Wakati mwingine sikuwa na maji wala chakula, na kama nilikuwa na chakula basi nilikuwa na (CHIMBONDI) = karanga zilizokaangwa na kutwangwa pamoja na chumvi. Au kama ni ule msimu wa maembe basi kuzitwanga kweli embe. Kwani wengine wana maisha ya raha, wengine ya kuteseka, ndugu zangu hivyo ndivyo maisha yalivyo.--
Baina ya Kingoli mpaka Peramiho kuna vijiji kama vitano hivi, hivi safari hiyo ilikuwa inachukua siku moja – mbili nilikuwa nalala katika kijiji kimoja kiitwacho Mgazini. Wakati mwingine sikuwa na maji wala chakula, na kama nilikuwa na chakula basi nilikuwa na (CHIMBONDI) = karanga zilizokaangwa na kutwangwa pamoja na chumvi. Au kama ni ule msimu wa maembe basi kuzitwanga kweli embe. Kwani wengine wana maisha ya raha, wengine ya kuteseka, ndugu zangu hivyo ndivyo maisha yalivyo.--
Subscribe to:
Posts (Atom)
